Serikali yazidi kuandama CHADEMA:yawafungulia mashtaka madiwani na viongozi wa chama Mbeya

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), David Mwambigija, maarufu kama Mzee wa Upako na Katibu Mwenezi wa chama hicho Wilaya ya Mbeya Mjini, Lucas Mwampiki, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mwakibete, wamekamatwa na kusafirishwa hadi wilayani Chunya kisha kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kufanya mkutano bila kibali na kutoa maneno ya uchochezi. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, alithibitisha kukamatwa kwa viongozi hao na kusema kuwa walikamatwa juzi katika eneo la Inyara, wakiwa ndani ya basi kuelekea Dodoma.
Hapo kwenye red. Ni nani anayetoa vibali vya kufanya mikutano ya vyama vya siasa vilivyosajiliwa na Tendwa? Hilo kosa liko kinyume na kifungu kipi cha Katiba au sheria ipi? Ninavyofahamu mimi ni kuwa vyama vya siasa vinaweza lakini havilazimishwi kuitaarifu polisi kwa ajili ya taarifa tu juu ya uwepo wao eneo fulani, na sio kuomba hicho "kibali".
 
Safi sana, lazime walipie, kupata uongozi ni gharama, wananchi tutawapima kwa uvumilivu wao dhidi ya huu uonevu.Yeyote atakayeshindwa kuvumilia mateso,uonevu,dhiaka,manyanyaso, na hila zote ze serikali ya chama cha Mapinduzi itakuwa ni kwa manufaa ya UMA sababu tutakuwa tumepunguziwa viongozi waoga. Asante CCM na serikali yako kwa kutupitishia watu hawa kwenye tanuru la joto.
 
Kamata kamata achia hii ndo inawapa nguvu makamanda na wanazidi kusonga mbele mpaka mkoloni mweusi aachie nchi.
 
Mwanzo wa ukombozi unaonekanaga hv hv!

Mwanzo mgumu!

Kazi ya polisi siyo usalama wa raia tena. Ndiyo maana Mheshimiwa Deo Haule Filkujombe, Mbunge wa Ludewa alisema kwamba kazi ya virungu vya polisi sasa ni kuwapiga CHADEMA..
 
Hapo kwenye red. Ni nani anayetoa vibali vya kufanya mikutano ya vyama vya siasa vilivyosajiliwa na Tendwa? Hilo kosa liko kinyume na kifungu kipi cha Katiba au sheria ipi? Ninavyofahamu mimi ni kuwa vyama vya siasa vinaweza lakini havilazimishwi kuitaarifu polisi kwa ajili ya taarifa tu juu ya uwepo wao eneo fulani, na sio kuomba hicho "kibali".
Uko sahihi,,cjui ni katiba/shreria ipi,,CPA ama Penal code kifungu gani?pengine ndo maana nyingiwazo zinaishia hewani tu
 
Safi sana, lazime walipie, kupata uongozi ni gharama, wananchi tutawapima kwa uvumilivu wao dhidi ya huu uonevu.Yeyote atakayeshindwa kuvumilia mateso,uonevu,dhiaka,manyanyaso, na hila zote ze serikali ya chama cha Mapinduzi itakuwa ni kwa manufaa ya UMA sababu tutakuwa tumepunguziwa viongozi waoga. Asante CCM na serikali yako kwa kutupitishia watu hawa kwenye tanuru la joto.

nimeipenda hii ila simu haina kitufe cha LIKE. Thanks
 
Embu hawa PoloCCM wajipange kutatua matatizo ya ulinzi na wala sio umaarufu kupitia CDM
 
Hawa makamanda wa Polisi katika maeneo mbali mbali hapa nchini naona wameagizwa wafanye kazi ya ziada kuzuia hii M4C na wakifanikiwa watapandishwa vyeo ndoo maana wanakamata tu hata kama makosa yenyewe sio ya msingi lakini mwisho wa ubaya ni AIBU
 
Soma Historia wakati wa ukoloni viongozi wanana mapinduzi kama akina Mandela, Nyerere, Nkuruma, Lumumba, na wegine wengi sana walifunguliwa kesi za aina hii na wengine waliuawa kama Solomon Mhalangu n.k Ila saa ya ukombozi ilipofika kulikuwa hakuna namna!!CCM wajidanganye kama walivojidanganya wakoloni but time is not their best friend !!!
 
Back
Top Bottom