Serikali yazidi kuandama CHADEMA:yawafungulia mashtaka madiwani na viongozi wa chama Mbeya

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), David Mwambigija, maarufu kama Mzee wa Upako na Katibu Mwenezi wa chama hicho Wilaya ya Mbeya Mjini, Lucas Mwampiki, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mwakibete, wamekamatwa na kusafirishwa hadi wilayani Chunya kisha kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kufanya mkutano bila kibali na kutoa maneno ya uchochezi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, alithibitisha kukamatwa kwa viongozi hao na kusema kuwa walikamatwa juzi katika eneo la Inyara, wakiwa ndani ya basi kuelekea Dodoma.

Alisema kuwa viongozi hao walisafirishwa hadi Chunya ambako waliunganishwa na wenzao wawili kabla ya kupelekwa mahakamani na kusomewa mashtaka yanayowakabili.

Kamanda Diwani aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Katibu wa CHADEMA Kata ya Makongorosi, Erick Luvanda na Katibu Mwenezi wa kata hiyo, Dominick Chaula.

Alisema baada ya kusomewa mashtaka yao mahakamani, watuhumiwa walipewa dhamana na kutakiwa kurudi tena mahakamani hapo Agosti 16, mwaka huu kwa ajili ya kuendelea kwa kesi hiyo.

Hivi karibuni viongozi hao kwa kushirikiana na viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Chunya walifanya mikutano mbalimbali kwa siku 10 wilayani humo ikiwa ni sehemu ya operesheni iliyopewa jina la ‘CHADEMA Twanga Kotekote' yenye lengo la kutoa elimu kwa wananchi na kukijenga chama hicho.

Source:Tanzania Daima
 
hii kesi ndiyo itakayo wapatia jina hawa wakuu wa chama na kukiuza/kukitangaza chama kizuri zaidi kesi inafanyikia huko huko Chunya
 
Duu hawa jamaa kwel cdm kikojuu tumeshazoe kes laa wala hatuogopi tunasonga mbele..
 
Haya ni maandalizi tu, 2015 yataisha, halafu tutawfundisha jinsi ya kutawala bila hila na visasi. Hata wao watafurahi.
 
Dalili za kuanguka kwa hiyo wanatapatapa lakini hawawezi kuzuia mabadiliko.Imekwisha amuriwe CHADEMA iwe na inakuwa.
 
nguvu ya dola haiwezi kuwanyamazisha wananchi walokata tamaa hata siku moja,UKWELI NA HAKI HUSHINDA DHIDI YA DHULUMA
 
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), David Mwambigija, maarufu kama Mzee wa Upako na Katibu Mwenezi wa chama hicho Wilaya ya Mbeya Mjini, Lucas Mwampiki, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mwakibete, wamekamatwa na kusafirishwa hadi wilayani Chunya kisha kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kufanya mkutano bila kibali na kutoa maneno ya uchochezi. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, alithibitisha kukamatwa kwa viongozi hao na kusema kuwa walikamatwa juzi katika eneo la Inyara, wakiwa ndani ya basi kuelekea Dodoma. Alisema kuwa viongozi hao walisafirishwa hadi Chunya ambako waliunganishwa na wenzao wawili kabla ya kupelekwa mahakamani na kusomewa mashtaka yanayowakabili. Kamanda Diwani aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Katibu wa CHADEMA Kata ya Makongorosi, Erick Luvanda na Katibu Mwenezi wa kata hiyo, Dominick Chaula. Alisema baada ya kusomewa mashtaka yao mahakamani, watuhumiwa walipewa dhamana na kutakiwa kurudi tena mahakamani hapo Agosti 16, mwaka huu kwa ajili ya kuendelea kwa kesi hiyo. Hivi karibuni viongozi hao kwa kushirikiana na viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Chunya walifanya mikutano mbalimbali kwa siku 10 wilayani humo ikiwa ni sehemu ya operesheni iliyopewa jina la ‘CHADEMA Twanga Kotekote’ yenye lengo la kutoa elimu kwa wananchi na kukijenga chama hicho.
 
Hayo ni mapito kuelekea tanzania tuitakayo, makamanda lazma tuteseke kwa ajil ya huyu mkolon mweusi.
 
Hivi hizi kesi huwa zinaishia wapi? Maana siha uhakika kama kuna hata moja imewahi kumalizika tukasikia hukumu yake ilikuwaje!
 
Hivi hizi kesi huwa zinaishia wapi? Maana siha uhakika kama kuna hata moja imewahi kumalizika tukasikia hukumu yake ilikuwaje!

Mara nyingi huwa wanasamehewa na kuambiwa wasirudie tena.
 
Mara nyingi huwa wanasamehewa na kuambiwa wasirudie tena.

Ok. Polisi wangekuwa wanatangaza basi kama wanavyotangaza kuwakamata na kuwafikisha mahakamani. Mara nyingine huwa nadhani kazi ya polisi ni kukamata na kufikisha watu mahakamani, kinachoendelea si juu yao. Sijui wanapimaje mafanikio ya kazi zao.
 
Laiti hawa watu wetu wanaosimamia haki wangekuwa wanawapeleka mahakamani mafisadi na weizi wa fedha za wananchi kwa spidi kama hiyo, nchi yetu ingekuwa pepo.
 
Back
Top Bottom