Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,140
- 144,641
Nchi hii ukiona media au watu maarufu (wanasiasa, wasomi, wanazuoni, n.k) wanaongelea jambo fulani kwa uhuru, jambo ambalo mwanzoni walikuwa hawezi kuliongelea au kuliuunga mkono, ujue teyari jambo husika lina baraka za watawala na liko mbioni kutumia au kutokea.
Kwa misingi huo, naiona serikali ya mseto kwa upande wa Tanzania Bara ikienda kuundwa siku za mbeleni ambapo mabadiliko ya katiba au katiba mpya itaruhusu kuundwa kwa serikali ya aina hiyo nchini kwetu.
Swali ni je, CHADEMA watakubali kushiriki katika serikali hiyo?
NB: Mbowe anaweza kuwa teyari kuridhia kuundwa kwa Serikali ya aina hii huku yeye akiweza kupewa hata uwaziri mkuu, ila namshauri awe makini na asitumie vibaya nafasi yake kama mwenyekiti kutaka kufanikisha jambo hili(in case ana dhamira hiyo) kwani anaweza kukigawa na kukivuruga vibaya chama.
Kwasababu naamini Mbowe hahitaji kuhongwa cheo na wala hana njaa, ila atataka tu kufanikisha hilo kwa masilahi ya Taifa , namshauri asikubali nafasi hiyo ya uwaziri mkuu(in case atapewa) bali aongoze wenzake kumpendekeza kiongozi mwingine apewe hiyo nafasi iwapo CHADEMA wataridhia kuundwa serikali ya mseto huko mbeleni.
Mbowe akikubali nafasi hiyo itakuwa ni mwanzo wa propaganda chafu dhidi yake na chama chake kwa ujumla na hivyo chama watakidhoofisha.
Wengine tulishatabiri kuundwa kwa serikali ya aina hii katika zama hizi:
Pia soma hapa:
Kwa misingi huo, naiona serikali ya mseto kwa upande wa Tanzania Bara ikienda kuundwa siku za mbeleni ambapo mabadiliko ya katiba au katiba mpya itaruhusu kuundwa kwa serikali ya aina hiyo nchini kwetu.
Swali ni je, CHADEMA watakubali kushiriki katika serikali hiyo?
NB: Mbowe anaweza kuwa teyari kuridhia kuundwa kwa Serikali ya aina hii huku yeye akiweza kupewa hata uwaziri mkuu, ila namshauri awe makini na asitumie vibaya nafasi yake kama mwenyekiti kutaka kufanikisha jambo hili(in case ana dhamira hiyo) kwani anaweza kukigawa na kukivuruga vibaya chama.
Kwasababu naamini Mbowe hahitaji kuhongwa cheo na wala hana njaa, ila atataka tu kufanikisha hilo kwa masilahi ya Taifa , namshauri asikubali nafasi hiyo ya uwaziri mkuu(in case atapewa) bali aongoze wenzake kumpendekeza kiongozi mwingine apewe hiyo nafasi iwapo CHADEMA wataridhia kuundwa serikali ya mseto huko mbeleni.
Mbowe akikubali nafasi hiyo itakuwa ni mwanzo wa propaganda chafu dhidi yake na chama chake kwa ujumla na hivyo chama watakidhoofisha.
Wengine tulishatabiri kuundwa kwa serikali ya aina hii katika zama hizi:
If you can't beat them, join them: Naziona dalili za CCM kuja na wazo la Serikali ya mseto huko mbeleni
Upinzani nchi hii umekomaa na kuota mizizi kiasi kwamba ni vigumu kufuta upinzani hapa nchini na ndio maana Mwendazake alifeli vibaya katika adhma yake ya kutaka kuua upinzani(kafa yeye kaacha upinzani ukiwa imara kuliko jana). Kwasababu CCM hawako tayari na pia hawawezi kushindana na upinzani...
www.jamiiforums.com
Pia soma hapa: