Serikali sasa ijifunze toka Tigo kwa wanaovujisha siri zake nje

Mleta thread nafikiri ana matatizo ya ku-analyse issues na ndio maana anachukua vitu na kuviweka pamoja kiasi kwamba the story sounds vague. Utakapotaka kuandika tena tro any to be objective in your presentation. Lakini jambo linahusu utesaji wa mtu mpaka katika hali ya kufa sio la kuwekea propaganda, ushabiki na upenzi uliopitiliza. Umetanguliza mambo hayo ambayo ni kinyume cha uandishi wa aina yoyote and hence to any sensible man your barbaric, uncounth, inhuman, tragic and a killer not worthy living in the community of human beings but in the hyenas. Kama umetumwa kuandika madudu watafute maana wataaalamu wakufundishe namana ya kuandika na nenda kajifunze utu maana huna cha kupoteza isipokuwa uhayawani
 
Uzi umeandikwa kwa mpangilio mzuri na hata lugha imekaa vizuri lakini tatizo ni maudhui yake. Naona yamekaa kiutumbotumbo tu. Mtu yeyote anayeweza kumsifia mtumiaji wa sheria kandamizi kama ya habari lazima awe na mtindio wa aina fulani kwenye ubongo. Si bure!
 
security guard: Wanafanya hivyo kwa kutaka kuivuruga serikali ili ishindwe kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kile ambacho katika ujumla wao wanapenda kiondoshwe madarakani mwaka 2015 huku chaguo lao hivi sasa likiwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachotaka kuleta ushoga nchini!
Hapo umechemka, kama taarifa ya mwananchi ilikuwa ya uongo hata tigo wasinge fukuza watumishi wao, inaonekana kumekuwepo pressure toka serikalini..!

Kimsingi serikali yenyewe ndio inahatarisha usalama wake, uharamia kama ul;e na mbinu za kizamani kiasi kile ni ujinga ulipuitiliza, japo siungi mkono matukio yote yale ila naishangaa serikali na vyombo vya usalama kwa matumizi yua mbinu za kitoto namna ile.

Kupata taarifa kama zile na kuziweka hadharani ni sahihi kabisa kwa ulimwengu wa sasa, cha msingi ni mbinu za upataji taarifa, serikali katika mambo yake yote wanapaswa kuhakikisha system iko secure sasa walishindwa ku-secure system matokeo yake wanaishia kulifunga gazeti na kufukuzisha watumishi kazi..
 
kama kuvunja sheria ww mwenyewe tayari umeisha vunja makala yako inalenga kutukana
 
Kuwachukulia hatua maofisa 31 wa tigo inaonyesha habari ya mwanahalisi ni kweli.Sasa wahusika ambao namba za simu zao zilitajwa wakamatwe kwa maojiano
 
Kutoa siri za mteja ni kitu hatari nadhani kama ni kweli Tigo wamefanya sahihi.

VIjana wasio waaminifu kama hao wanaweza hata kuvunja ndoa za watu bora wafukuzwe tu.
 
kutoa siri kutoka mahali unapofanya kazi panakuja tu pindi mambo hayaendani na sheria ya kazi kwa mujibu wa katiba
kwa hiyo wanatoa siri ni baada ya kuchoka na uongozi uliopo madarakani kwenda ndivyo sivyo na kutokujali kabisa maslahi ya waliowachagua.
kwa sasa siri nyingi kila wizara zinatolewa na wao wenyewe baada ya kuchoka jinsi serikali inavyoendesha mambo kuwa ndivyo sivyo na taarifa zinazotolewa zile ukweli mtupu ndani yake mfano swala DR Uli kwa kuwa amerudi tutajua zaidi na zaidi
jaribu kuangalia taarifa za mawizara zinavyotolewa na mawaziri wenyewe ama kujichanganya wao kwa wao kitu ambacho kinaonyesha mawaziri hawapo pamoja mfano swala la Ufisadi wa richmond Waziri Samweli sitta hakukubaliana na serikali ,kuandikwa katiba mpya waziri aliyekuwepo na AG walikataa lakini rais akapitisha ,waziri aliyejiuzulu kwa hashfa sasa wanamwita waziri mkuu mstaafu wakati hatuna waziri mkuu mstaafu na mengine mengi ambayo sisi raia wa kawaida tunaona wasiwasi sasa tunajiuliza hawa usalama wa taifa nini kazi yao

kwa hiyo uliyetoa mada angalia unatetea nini na wakati gani maana ufahamu wa watanzania wa leo wanajua vizuri sana sio kama zamani walikuwa wanadanganywa tu na kukubali
 
Ilipotolewa sheria ya ku register namba za simu sababu kubwa iliyotolewa ni ili kuwatambua wahalifu. Tigo imetumia mwanya huo kuwatambua wahuni na WAHALIFU waliomteka Dr. Ulimboka tatitizo liko wapi hapo?. Hiv Tigo ingesaidia kuwatambua wezi say waliovunja benki na wakapatikana je ingewafukuza hao wafanyakazi wake?

Lakini pia ikumbukwe simu zilizokuwa tracked ni za kweli na ni wahusika wa kweli katika hilo tukio wao tigo kwani ndo waliwatuma wakafanye shughuli za kijangili kutaka kuua watu? Ilikuwa sahihi kabisa tigo kusaidia kuwakamata kwani hata Kova alisema atakayefanikisha taarifa za kukamatwa kwao atatoa support. mi nafikiri hawa wafanyakazi wasingefukuzwa bali kupewa zawadi kwa kitendo cha ujasiri.
 
Mleta thread hukuhariri habari yako kwani unazidi kuthibitisha kuwa watendaji wa serikali ni watuhumiwa no.1. Bora usingepost hii habari.
 
KUFUNGIWA kwa gazeti la MwanaHalisi, Jumatatu ya wiki iliyopita kumekwenda sambamba na kuwatambua na kufukuzwa kazi kwa maofisa 31 wa kampuni ya simu za mikononi ya Tigo Tanzania jijini Dar es Salaam.

Katika toleo lake la mwisho wiki mbili zilizopita, gazeti hilo linatuhumiwa kuandika habari ya uchochezi dhidi ya serikali kwa kuichafua Idara ya Usalama wa Taifa, uchonganishi na ugombanishi kwa watu huku pia likihatarisha maisha kati yao kwa kuwatuhumu kuhusika na utekaji nyara, utesaji wa kikatili na jaribio la kutaka kumuua Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Stephen Ulimboka Juni 26, mwaka huu.

Sitaki kurejea habari hiyo wala kukumbushia machungu ya unyama aliofanyiwa daktari huyo hasa kwa vile suala hilo lenyewe linashughulikiwa na vyombo vya dola, halafu kuna kesi inaendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, baada ya mmoja kati ya watu wanaodaiwa kufanya ukatili huo kutiwa mbaroni mwezi uliopita.

Ninachotaka kuzungumzia hapa ni hatua iliyochukuliwa na kampuni ya Tigo ya kuwatimua kazi mara moja baadhi ya maofisa wake, wale ambao wanadaiwa kutoa nje siri za wateja wa mwajiri huyo kinyume cha sheria na kanuni za utumishi.

Wanatuhumiwa kuvujisha siri za mawasiliano yaliyofanywa na baadhi ya wateja wake na Ulimboka kwa gazeti hilo ikiwemo kutoa namba za simu zao, muda waliowasiliana naye kwa namna moja ama nyingine na majina yao, kisha wakahusishwa na madai ya kumteka, kumtesa, kujaribu kumuua na kumtelekeza katika Msitu wa Pande uliopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Tumesikia kelele nyingi zilizopigwa kijinga na baadhi ya watu wakiishutumu serikali kwa kulifungia gazeti hilo. Tumeona baadhi yao wanavyokwenda mbali zaidi kwa kutaka ilifungulie, wengine wakisema ifanye hivyo “mara moja na bila masharti yoyote” kwa madai kuwa adhabu hiyo ni ukandamizaji dhidi ya vyombo vya habari nchini.

Wanazungumza kipuuzi kwa kauli za kijinga dhidi ya mamlaka halali iliyopo madarakani kwa mujibu wa sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanajifanya eti hawafahamu kuwa vyombo vyote vya habari vinaendesha majukumu yake siyo kwa ridhaa zake vyenyewe isipokuwa kwa matakwa ya kisheria bila ya kujali kama ni mbovu kama wanavyodai na hata vinginevyo.

Magazeti yote nchini yanasajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976, ileile inayopigiwa kelele nyingi ikisemwa imeshapitwa na wakati na kandamizi, lakini ileile na vilevile inapotumika kusajilia magazeti hakuna anayedai au kusema kuwa ni kandamizi ama kwamba inatakiwa ibadilishwe.

Udikteta wa sheria hiyo na maneno mengine ya shutuma dhidi yake unakuja tu wakati gazeti linapochukuliwa hatua zote halali za kisheria na serikali ikiwemo kuonywa, kufungiwa au kufutwa kabisa kutoka kwenye orodha ya magazeti pindi linapokwenda kinyume cha weledi pamoja na maadili ya uandishi wa habari.

Hapo ndipo kelele zinapoanza kutoka midomoni mwa baadhi ya watu wakiongozwa zaidi na wanasiasa na wanaharakati nchini, wote wakifanya hivyo siyo kwa nia njema isipokuwa kwa ujinga wa kutumiwa na magenge yanayoitwa wahisani na wafadhili kutoka nje ya nchi.

Wanafanya hivyo kwa kutaka kuivuruga serikali ili ishindwe kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kile ambacho katika ujumla wao wanapenda kiondoshwe madarakani mwaka 2015 huku chaguo lao hivi sasa likiwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachotaka kuleta ushoga nchini!

Nikirudi katika maudhui hasa ya makala yangu hii, napenda kuipongeza kampuni ya Tigo Tanzania ilivyochukua hatua za haraka kuwawajibisha watumishi wake kwa kuvujisha nje siri za wateja wake, jambo linaloweza kusababisha watu wengi waikimbie na kujiunga na mitandao mingine ya simu maana ipo mingi na tayari ushindani miongoni mwa makampuni hayo ni mkubwa kupindukia.

Tayari kuna kampuni mbalimbali zikiwemo kubwa za Vodacom, Airtel na Zantel huku nyingine zikianzishwa na kuingia sokoni, jambo ambalo litaongeza ushindani ambao ni pamoja na uaminifu, uadilifu, unyenyekevu; nafuu ya gharama za kupiga, kupokea ama kutumia ujumbe mfupi wa maneno na ubora wa mawasiliano kwa wateja wake.

Haiwezekani mwajiri aendelee kuwakumbatia watumishi waliokosa uaminifu na kufikia mpaka hatua ya kutoa nje siri za wateja wake ambao kimsingi uwepo wao ndio maisha yao ya kila siku, familia zao na ndugu zao wenyewe, lakini wanakuwa na ujinga wa kutumiwa na waandishi wa habari, wanasiasa na wanaharakati kutenda kinyume cha sheria na kanuni za utumishi.

Sifahamu endapo kampuni hiyo ina utaratibu wa kuapisha watumishi wake iwe kwa mdomo au maandishi na kumbukumbu hizo kuhifadhiwa, lakini hata iweje ni ujinga na kinyume cha utumishi mahali popote duniani kwa mfanyakazi awe wa ndani au shambani kutangaza kitu chochote kinachofanywa na mwajiri mahali popote bila idhini yake mwenyewe.

Kama jambo hilo lingekuwa halina tatizo hakika wafanyakazi wenye mchezo huo wa ovyo wangekuwa wanavujisha kwanza siri zao wenyewe na wake zao nyumbani, waume zao au wapenzi wao, vinginevyo wangekuwa wanaeleza wanavyokiuka sheria na kanuni za ajira zao kwa hujuma zote wanazofanya.

Kila wakivujisha nyaraka zisizotakiwa kutoka nje ya ofisi au kwa watu wasiotakiwa siku zote wangekuwa wanatangaza walichofanya, lakini hawafanyi hivyo kwa vile wanaelewa kuwa hairuhusiwi katika hali zote na hilo ni kosa la jinai kwa sheria zote za kazi.

Ndiyo maana naipongeza kampuni hiyo kwa kuwachukulia hatua za haraka kuwang’oa na kuachana nao mara moja. Naishukuru kwa sababu imetimiza wajibu wake halali unaopaswa kufanywa na waajiri wote duniani kuanzia sekta binafsi hadi za umma ikiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mchezo wa kuvujisha siri za ofisi sehemu za kazi umegeuzwa kuwa mchezo wa kawaida kuanzia wizarani hadi bungeni, taasisi za fedha na idara takribani zote za serikali.

Leo utasikia “nyaraka tulizonazo” au “habari za ndani zilizopatikana kutoka” wizara hiyo, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya na kadhalika.

Huko ndiko zinakotoka siri nyingi za serikali na kuangukia mikononi mwa wanaharakati wa masuala ya kijamii ingawa ukweli ni wanaharakati wa kisiasa, viongozi wa vyama vya siasa na makundi mengine yakiwemo haramu.

Ndiyo maana kwa mfano haishangazi kusikia Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Peter Slaa au Mwenyekiti wake, Freeman Aikaeli Mbowe wakitamba kukamata nyaraka za serikali na kuongeza uongo na uzushi juu yake.

Wanadai nyaraka hizo ni maelekezo maalum ya serikali kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya au Wakurugenzi wa Halmashauri za Manispaa, Miji na Wilaya ya kuwashughulikia wapinzani huku wakijua ni uongo ila wanafanya hivyo kwa malengo ya kisiasa na kupotosha ukweli.

Wanatumia nyaraka hizo kufanya uchochezi kwa nia ovu, uchonganishi na ugombanishi ili wananchi waichukie serikali yao na CCM kwa kuwapandikizia majungu, uzushi na fitina zote wanazoweza kuzifanya wakati wowote na mahali popote.

Bila kujifunza kutoka kampuni ya Tigo na kuanza kuwafuatilia watumishi wote wa serikali na taasisi zake wanaovujisha nje siri za ndani ikiwemo kudurufu nyaraka, kuwakabidhi wanasiasa au watu wengine kinyume cha sheria na kanuni za ajira, kisha kuwatimua kazi na tena kwa haraka na kupoteza haki zao zote kamwe hawawezi kukoma.

Hiyo ndiyo kazi inayopaswa ianze sasa na kusimamiwa moja kwa moja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda.


This means that what was written by Mwanahalisi is true, sasa kwanini lifungiwe(sheria kandamizi kwa serikali dhaifu ya kidhalimu)? Kweli kichaa kapewa panga. but no long at easy the day is coming soon ambapo watanzania tutajikomboa kutoka mikononi mwa jangili, dhaifu, dhalimu, jambazi, gamba chichiem.
 
Moja tunataka toka kwako je wamwsema ukweli? Kama ni kweli basi ni kawaida ukisema ukweli utakuwa kama yesu. Hao vijana wa tigo wamenipa raha sanaaaaaaaaaaaaaa. Walio kama hao ni wengi ndo maaana kuwafukuza haisaidii. Iko siku hata hiyo tigo itafungiwa
 
Ilipotolewa sheria ya ku register namba za simu sababu kubwa iliyotolewa ni ili kuwatambua wahalifu. Tigo imetumia mwanya huo kuwatambua wahuni na WAHALIFU waliomteka Dr. Ulimboka tatitizo liko wapi hapo?. Hiv Tigo ingesaidia kuwatambua wezi say waliovunja benki na wakapatikana je ingewafukuza hao wafanyakazi wake?

Lakini pia ikumbukwe simu zilizokuwa tracked ni za kweli na ni wahusika wa kweli katika hilo tukio wao tigo kwani ndo waliwatuma wakafanye shughuli za kijangili kutaka kuua watu? Ilikuwa sahihi kabisa tigo kusaidia kuwakamata kwani hata Kova alisema atakayefanikisha taarifa za kukamatwa kwao atatoa support. mi nafikiri hawa wafanyakazi wasingefukuzwa bali kupewa zawadi kwa kitendo cha ujasiri.

ninachoshanga hapa mimi ni kuwa hawa jama wa tigo wamevumjisha siri hebu tujiulize hiyo siri iliyovujishwa ni ya nani ? na nani kalalamika kuwa siri zake zimevujishwa?
hapa tunazungumzia simu ya ulimboka ndiyo iliyofichuliwa siri zake fine hakuwepo nchini wakati huo nawalitegemea kazi imekwisha Je kwa sasa dr Ulimboga analalamika kwa kuvujishwa kwa sili za simu yake? na je Dr akiomba hizo data sasa na kuziweka hadharani atanyimwa? au atakuwa amevijisha siri za simu yake ????
hi imeka vibaya kwa kwa tigo na serikali kwa ujumla.
 
kila serikali au makampuni duniani kuanzia marekani mpaka china...kunakuaga na vyanzo vya habari vya ndani hilo ni kitu cha kawaida...sasa sijui mnachoshangaa ni nini...america na intelligence yake yote ile lakini bado habari kutoka CIA FBI na WHITE HOUSE zinavuja...ndio itakuja kua TIGO/USALAMA MBOVU WA TAIFA?
 
Ninatatizwa na mambo machache naomba msaada wako mtoa hoja.
1. Kwanin tulisajili namba zetu za sim je ulikuwa upuuzi pia?

2. Kama alieteswa angekuwa mwanao je kuupata ukweli wewe kama baba/mama ni upuuzi? Kumbuka binadamu wote nisawa na wanahitaji haki ya kuishi.

3. Wanao iyumbisha ccm ni nani kati ya hawa

a) waliompiga nakutaka kumuua ulimboka akipigania haki ya madakitari?

a) waliotoa habari za watesaji wa ulimboka

b) Serikali kushindwa kutekeleza matakwa ya madakitari

c) mwanahalisi kwa kuandika habari za kiuchunguzi kwa kuweka ushahidi hadhalani?


Tumepotoka kwa muda mrefu na kufunga mikataba mingi ya kifisadi kwa upuuzi wa neno siri.

Tunarudia kukalili neno siri kwa upuuzi uleuke ulotufanya maskini. Mtu anapigwa auwawe kwa upumvu eti wawetoa siri wamefukuzwa,

Kama ukweli upo au uwongo, mahakama imeshirikishwa kubain makosa ya mwanahalisi? au wafanyakazi wa tigo?

Nilikuwa mteja wa tigo nimeitupa chooni line yao, hawana msaada kwangu kwao fedha ni bora kuliko uhai wangu.
 
Kama tigo wanafukuza wafanyakazi wanaosema ukweli kulinda uhai wetu NAPENDEKEZA TUISUSIE IBAKI NA CCM YAKE.

Kwa kila mpenda haki na aman tigo ni adui mkubwa hatufai.

Kila mmoja wetu angependa uhai wake ulindwe kwa nin tigo iwalinde wauwaji?
 
Ccm hoyeeeeeeeee.......
Hakuna kitu hapa vyeo vyote vimeisha....... Bado zile nafasi za wabunge 10 subiriiii
 
Kama mtu anavujisha siri ili haki ipatikane kwangu mimi nawaunga mkono watu hao, sio wakati wote sheria itatusaidia kutupeleka kweny haki! Unaonekana story nzima ya gazeti la mwanahalisi unaijua lakini umemtaja mhusika mkuu mmoja tu wakati mhusika mwenza hujamtaja!Tulishasamehewa watu waliokwapua mabilion ya EPA..... Tigo kitu gani kwanza wanadaiwa na Tanesco madeni kibao na sijui kwanini hawakatiwi umeme!
 
Mwenye kuleta hii habari anaumwa ugonjwa wa mtikisiko wa ubongo. Nenda kajikombe kwa waliokutuma ila post za UDC zimeshatoka labda usubiri atakaye retire au kupanda daraja ili ukabe nafasi yake. Kweli punguani tupo wengi, Mungu pitisha mbali. Wewe ndiyo wale wale mkiugua mnatibiwa high class hospitals nje ya nchi. Hujui makali ya hospitali za serikali ambazo 90% ya watanzania wanazitumia na 10% ndiyo nyie wenye hela ambao mmetumwa kuchafua hali ya hewa hapa. Pole sana. Wapigie simu waliokutuma waambie tayari umeshaposti ***** hapa JF. Uliishia darasa la pili a la kwanza?
 
Back
Top Bottom