Heparin
Senior Member
- Sep 24, 2021
- 128
- 421
Chama cha ACT Wazalendo kinaitaka mamlaka ya uteuzi kumwajibisha waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro kwa kauli ya kuweka marufuku kwa mashabiki wa timu pinzani zinazotoka nje ya nchi kuvaa jezi za timu zao zitakapocheza dhidi ya timu za Yanga na Simba katika hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika 29 na 30 Machi, 2024.
Kauli hiyo iliyolalamikiwa sana mtandaoni na kuripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya Tanzania inaeleza kuwa "atakayevaa jezi ya Mamelod Sundown au Al Ahly atatakiwa kuonesha pasi ya kusafiria ili kuonesha uraia wake na kwamba Serikali haitanii juu ya jambo hilo la Uzalendo".
Tumeona Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) na Msemaji wa Serikali kwa nyakati tofauti tofauti wamejitokeza kujitenga na kauli hizo na kwa lugha zingine kuwataka wapenzi wa soka kupuuza kauli hiyo ya Waziri. TFF walienda mbali kwamba mchezo huo utaongozwa na kanuni ambazo pasi ya kusafiria sio kigezo cha kuingilia uwanjani.
Hata hivyo Msemaji wa Serikali Ndg. Mubale Matinyi alipoulizwa na waandishi wa habari amejibu kuwa kuwa kauli hiyo ni "utani" hailisaidii taifa. Jibu hili dhihaka na hatari kwa wapenzi wa soka letu. ACT Wazalendo tunaona kauli hizi za Msemaji wa Serikali na TFF hazitoshi kabisa.
Kauli hiyo iliyolalamikiwa sana mtandaoni na kuripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya Tanzania inaeleza kuwa "atakayevaa jezi ya Mamelod Sundown au Al Ahly atatakiwa kuonesha pasi ya kusafiria ili kuonesha uraia wake na kwamba Serikali haitanii juu ya jambo hilo la Uzalendo".
Tumeona Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) na Msemaji wa Serikali kwa nyakati tofauti tofauti wamejitokeza kujitenga na kauli hizo na kwa lugha zingine kuwataka wapenzi wa soka kupuuza kauli hiyo ya Waziri. TFF walienda mbali kwamba mchezo huo utaongozwa na kanuni ambazo pasi ya kusafiria sio kigezo cha kuingilia uwanjani.
Hata hivyo Msemaji wa Serikali Ndg. Mubale Matinyi alipoulizwa na waandishi wa habari amejibu kuwa kuwa kauli hiyo ni "utani" hailisaidii taifa. Jibu hili dhihaka na hatari kwa wapenzi wa soka letu. ACT Wazalendo tunaona kauli hizi za Msemaji wa Serikali na TFF hazitoshi kabisa.