Serikali Nayo!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
Serikali Nayo!

Serikali zingine hazina dini! SERIKALI NA TALAKA
Mtazamo wa serikali kuhusiana na talaka umewekwa kutokana na kile raia wake wanataka (desires).
Kama raia wake watataka kuwa na sheria zinawapa au kuruhusu talaka kirahisi, serikali huwapa.
Tatizo kubwa ni kwamba binadamu mahali popote walipo kawaida huwa wanapenda uhuru wa kufanya wanavyotaka na hawataki kuishi katika standards za kibiblia au katika uadilifu ambao Mungu ameuweka
.

Mungu ameweka institution mbili duniani ambazo ni serikali na ndoa na hizi zinawafunga wanaoamini (waliokoka) na wasioamini).
Wote wanahitaji kutii serikali kama vile kulipa kodi haijalishi umeokoka au la kwani bila kulipa kodi kuna adhabu yake tena ya uhakika.
Hata kwenye ndoa uwe umeokoka au hujaokoka lazima utii standards za ndoa na kinyume chake ni penalty.

Serikali nyingi (English speaking) zinaweza kutoa talaka hata kwa kuwepo kwa tofauti katika ya mke na mume (differences and disagreements) .
Hata kama serikali inatoa talaka hii haina maana kwamba talaka zinaruhusiwa. Serikali haina common sense linapokuja suala la uadilifu (God’s morality standards). Hata kama serikali inauza pombe (liquor) hii haina maana pombe ni kitu sahihi.

Serikali haiwezi kutatua tatizo lolote la uadilifu wa binadamu kufuata standards ambazo Mungu ameweka.
Suala la talaka haliwezi kutatuliwa na binadamu yeyote aliye na hekima wala mahakama.

Mke na mume wanapoenda mahakamani ili kupeana mahakama jaji huwaeleza ukweli kwamba wao kama mahakama hawahusiki na suala la kiroho, sheria za Mungu, au sakramenti au kiapo chochote cha dini kuhusiana na kuachana kwani hilo ninyi wahusika mtatatua wenyewe na kwamba sheria za serikali au mahakama hazina uwezo wa kuamua kile mliahidiana mbele za Mungu.

Hii ina maana ninyi mnaopeana talaka mtahusika na Kipengele cha “Hadi kifo kitakapo tutenganisha” na kwamba mahakama haiwezi kutengenisha kile kilichounganishwa na Mungu.

Jaji William J. Gainer wa New York Marekani ameeleza wazi kwamba pamoja na kwamba mahakama ina uwezo wa kutoa talaka bado suala la kiroho linabaki mikono mwa wahusika (Plaintiff na Defendant) kwani mahakama haiingilii sheria za Mungu.
Maana yake unaenda mahakamani na kupeana talaka hata hivyo conditions zote za kuwa mke na mume bado zinabaki palepale untouched.
Bado ninyi ni mke na mume na kila anayeoa au kuolewa anazini
 
Back
Top Bottom