Mr George Francis
Senior Member
- Jun 27, 2022
- 186
- 212
FAHAMU kuhusu TALAKA na taratibu zake katika UISLAMU.
Sehemu Ya 1
اَلسَلامُ عَلَيْكُم وَرَحْمَةُ اَللهِ وَبَرَكاتُهُ)
As-salāmu alaikum wa-rahmatullahi wabarakātuh.
Peace be upon you as well as God's mercy and blessings.
Amani iwe juu yako pamoja na rehema na baraka za Mwenyezi Mungu.
Ndugu yangu mpendwa,
Kwa majina naitwa Mr George Francis, kwa taaluma ni mwanasheria.
Ahsante kwa kuendelea kufuatilia mada mbalimbali Mwenyezi Mungu alizonifunulia kuziandaa na kukuletea.
Leo naomba tuwe pamoja, tukienda kuaangazia kuhusu TALAKA na taratibu zake kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
Ndoa iliyofungwa kwa mujibu wa dini ya kiislamu inaweza kuvunjwa kwa kufuata taratibu za kisheria ka mujibu wa dini ya kiislamu.
Ndoa ya kiislamu ni miongoni mwa ndoa zinazotambulika kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa.
Ndoa ya kiislamu ni ile inayofungwa kwa kufuata taratibu zinazokubalika katika dini ya kiislamu.
⚖️Kifungu cha 25(3)(b) cha Sheria ya Ndoa.
Ndoa inatokana na makubaliano ya hiyari kati ya mwanamume na mwanamke bila kushinikizwa na mtu yeyote.
Katika uislamu, Mwanamume anaruhusiwa kuoa wake zaidi ya mmoja hadi wanne.
Muhimu ni kuwa na uwezo wa kuwapa matunzo na huduma zote kwa kuzingatia haki na usawa bila ya upendeleo.
Kama ilivyo katika ndoa nyingine, uislamu pia unaruhusu mume na mke kuachana kwa TALAKA kwa kuzingatia utaratibu.
TALAKA kutoka neno la kiarabu طلاق) au talaaq ni utaratibu wa kuvunja ndoa baina ya mume na mke kabla mume au mke kufariki.
Sheria ya ndoa imeweka utaratibu au masharti ya kuvunja ndoa iliyofungwa kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
Mahakama ni lazima ijirizishe kuwa,
(i).Ndoa ilifungwa kwa mujibu wa dini ya kiislamu.
⚖️ Kifungu cha 107(3)(a) cha Sheria ya Ndoa.
(ii). Bodi ya usuluhishi ya ndoa imethibitisha kuwa imeshindwa kusuluhisha na imetoa hati kwamba imeshindwa kusuluhisha wanandoa hao.
⚖️ Kifungu cha 107(3)(b) cha Sheria ya Ndoa.
(iii). Mmoja kati ya wanandoa amefanya kitendo kinachoonesha kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
⚖️ Kifungu cha 107(3)(c) cha Sheria ya Ndoa.
Mfano: Mwanaume amempa mkewe talaka kwa mujibu wa dini kama vile talaka ya kwanza, talaka ya pili na ya tatu kabla ya amri ya TALAKA ya Mahakama kutolewa.
Inaendelea....
#No_learnig_No_earning
So we have to Learn.
Prepared By
George G Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Sehemu Ya 1
اَلسَلامُ عَلَيْكُم وَرَحْمَةُ اَللهِ وَبَرَكاتُهُ)
As-salāmu alaikum wa-rahmatullahi wabarakātuh.
Peace be upon you as well as God's mercy and blessings.
Amani iwe juu yako pamoja na rehema na baraka za Mwenyezi Mungu.
Ndugu yangu mpendwa,
Kwa majina naitwa Mr George Francis, kwa taaluma ni mwanasheria.
Ahsante kwa kuendelea kufuatilia mada mbalimbali Mwenyezi Mungu alizonifunulia kuziandaa na kukuletea.
Leo naomba tuwe pamoja, tukienda kuaangazia kuhusu TALAKA na taratibu zake kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
Ndoa iliyofungwa kwa mujibu wa dini ya kiislamu inaweza kuvunjwa kwa kufuata taratibu za kisheria ka mujibu wa dini ya kiislamu.
Ndoa ya kiislamu ni miongoni mwa ndoa zinazotambulika kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa.
Ndoa ya kiislamu ni ile inayofungwa kwa kufuata taratibu zinazokubalika katika dini ya kiislamu.
⚖️Kifungu cha 25(3)(b) cha Sheria ya Ndoa.
Ndoa inatokana na makubaliano ya hiyari kati ya mwanamume na mwanamke bila kushinikizwa na mtu yeyote.
Katika uislamu, Mwanamume anaruhusiwa kuoa wake zaidi ya mmoja hadi wanne.
Muhimu ni kuwa na uwezo wa kuwapa matunzo na huduma zote kwa kuzingatia haki na usawa bila ya upendeleo.
Kama ilivyo katika ndoa nyingine, uislamu pia unaruhusu mume na mke kuachana kwa TALAKA kwa kuzingatia utaratibu.
TALAKA kutoka neno la kiarabu طلاق) au talaaq ni utaratibu wa kuvunja ndoa baina ya mume na mke kabla mume au mke kufariki.
Sheria ya ndoa imeweka utaratibu au masharti ya kuvunja ndoa iliyofungwa kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
Mahakama ni lazima ijirizishe kuwa,
(i).Ndoa ilifungwa kwa mujibu wa dini ya kiislamu.
⚖️ Kifungu cha 107(3)(a) cha Sheria ya Ndoa.
(ii). Bodi ya usuluhishi ya ndoa imethibitisha kuwa imeshindwa kusuluhisha na imetoa hati kwamba imeshindwa kusuluhisha wanandoa hao.
⚖️ Kifungu cha 107(3)(b) cha Sheria ya Ndoa.
(iii). Mmoja kati ya wanandoa amefanya kitendo kinachoonesha kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
⚖️ Kifungu cha 107(3)(c) cha Sheria ya Ndoa.
Mfano: Mwanaume amempa mkewe talaka kwa mujibu wa dini kama vile talaka ya kwanza, talaka ya pili na ya tatu kabla ya amri ya TALAKA ya Mahakama kutolewa.
Inaendelea....
#No_learnig_No_earning
So we have to Learn.
Prepared By
George G Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com