Serikali isikie kilio cha Barabara ya Goba Mpakani, ruti zinabadilishwa, wanapandisha nauli kiholela

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
4fa5db40-eb12-42b5-b571-a50e8e74a666.jpg
Jamii Forums naomba mtusaidie kupaza sauti kuhusu Barabara ya Goba Mpakani hadi Tegeta A hapa Dar es Salaam, ni mbovu sana na inatugharimu sisi raia wa kawaida.

Mfano mvua iliyonyesha jana tarehe 5 Mei, 2023 eti imesababisha tubadilishiwe ruti na nauli ipande, je hii ni sawa?

Mwezi uliopita Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikuja akiwa katika ziara kuzindua mradi wa maji, wakampitisha Njia Nne ambapo kuna lami.

Hivyo hakuona uhalisia wa njia yetu ya huku Goba Mpakani.

Huku daladala ni chache na wakati wa mzua zinabaki chache zaidi au wakati mwingine hazipo kabisa, hivyo tunakuwa tunategemea usafiri wa Bajaj ambapo kutoka Mbezi Mwisho nauli huwa ni shilingi 1,000.

Mtu unatoka na bajeti zako umepanga, unakuta nauli wanakwambia shilingi 1,500 na wakati mwingine hadi shi;ingi 2,000 hii si sawa, kwani hata ukisema utembee ni mbali na si salama.

Shida ni barabara haichongwi mara kwa mara na ina madimbwi mengi sana yanayosababisha mvua kubwa ikinyesha kunakuwa na ugumu wa kupitika kwa sababu yanajaa sana maji.


Pia soma>> Baada ya Mdau wa Jamii Forums kulalamika, Serikali yaanza kuboresho ya Barabara ya Goba - Mpakani
 
Ungeeleza njia yake rasmi ni kutoka wapi kwenda wapi.

Nauli halali ni kiasi gani na wanapandisha kiasi gani.

Wanakatisha ruti wakifika eneo gani nk ili iwe rahisi kwa wapaza sauti kupata pa kuanzia.
 
Ki ukweli hii barabara ni kama haipo nchi ya Tanzania maana sio kawaida kukuta njia mbovu kiasi hiki ishindikane japo kupitisha greda tu hali ni mbaya Sana hakuna viongozi upande huo wangekua washalifanyia kazi
 
Ki ukweli hii barabara ni kama haipo nchi ya Tanzania maana sio kawaida kukuta njia mbovu kiasi hiki ishindikane japo kupitisha greda tu hali ni mbaya Sana hakuna viongozi upande huo wangekua washalifanyia kazi
Nauliza tena mbunge wenu ni nani? Ni Kitila, Mtemvu au Gwajima?
 
Hii njia panda ya Tegeta A kuelekea kwa Bedui hapafai kwakweli, juz hapa kuna kidaraja kimekatika karibu na kibao cha shule ya jerusalemu magari yakawa hayapiti

Naona wanatengeneza hilo daraja ila kwa kiwango cha chini sana ,mvua kubwa zikinyesha tena hilo daraja litaharibika tena
 
Back
Top Bottom