Serikali imeona wabunge wamepuyanga bungeni imerudi kukusanya maoni kwa wenye akili timamu

Nafikiri kwa sasa kuna umuhimu wa kigezo cha elimu kuzingatiwa wakati wa kupata wabunge, hawa wa darasa la nne na saba waishie 2025, sisemi wenye elimu kwa binge hili tunaona tija yao,hapana, angalau wanaweza fanya mambo wanayojua athari zake kwa kuchambua na kutafuta sehemu tofauti tofauti. Wabunge wenyekusaidiwa na uwezo wao wa kupanua midomo nafikiri tuondokane nao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin
Anaweza kuvuka, lakini akiwa amelemaa.!!
Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!
Kwa Tanganyika sio daraja la pili tu bali la nne kabisa. Hawastahili wala hawana haki kufanya maamuzi Kwa mambo yanatuhusu Watanganyika!

Na kwa taarifa yako, huyu ndiye atakuwa raia wa mwisho toka Zanzibar kushika madaraka ya U - Rais wa Tanzania..!
Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...
Hili☝️☝️umesema wewe na halina ubishi wowote. Lakini kwanini uwezo wao ni mdogo? Jibu lake ni wewe kufanya utafiti na uje na jibu!
HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!
Huwa wana maamuzi lakini ya hovyo na ya kijinga kama anavyofanya huyu mama yako sasa, alivyofanya Ally H. Mwinyi na J. M. Kikwete..!
Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hakuna Ubaguzi hapa..

Kilichopo hapa ni Watanganyika kupiga kelele kukataa kutawaliwa na raia wa nchi nyingine ya kigeni..

✓ Samia Suluhu Hassan ni raia wa Zanzibar...

✓ Prof. Makame Mbarawa ni raia wa Zanzibar...

✓ Katibu Mkuu wizara ya ujenzi na uchukuzi ni raia wa Zanzibar

##Hii ndiyo sababu ya kelele zetu...

##Wanauza rasrimali za Tanganyika kwa sababu wao ni Wazanzibari. Watoe wapi uchungu hawa????

#This is not about racism or Bigotry dude!!
 
Uchambuzi kuntu sana! Hongera.

Hakuna Bunge pale.

Hopefully, Mh Rais ameona mwenyewe; sasa mpira uko kwake.
 
Tuliona walichofanya wabunge Dodoma; tumeona wanachofanya wanazuoni kutoka kwenye dini na fani mbalimbali nchini. Wanajadili mule mule alipopita Mzee Mbowe na Lissu, tofauti ni kwamba wanazuoni wanawapiga shule mawaziri wakati wabunge waliwapigia makofi mawaziri bila kuwapa maarifa mapya.

Hiki kinachoendelea ni fedheha kwa bunge na wabunge; kwamba pamoja na kupitisha kumbe wao siyo final bali kazi yao ilikuwa rubber stamp au kukamilisha ratiba.

Goma limekuwa gumu na endapo Mbowe na Safu yao wataingia uwanjani kwenye mikutano ya adhara kwa agenda hii upo uwezekano pakatokea mmomonyoko mkubwa na makundi kuhusu bandari.

Changamoto kubwa ya Watanzania ni wanafiki wazuri; wakiona unataka kusikia habari hoja fulani nao wanakupigia makofi ila moyoni wana ukweli na wewe ukijiongezea unagundua huna watu nyuma yako.

Magufuli alisifika ila waliokuwa wanamsifu angewaruhusi wapige kura ya siri angelalamika kaibiwa kura kwa sababu baada ya kuondoka tu watu walewale waliokuwa mgongoni mwake walijitokeza kumkataa.

Kama walimkataa hadharani akiwa ameondoka je, walimpigia kura sirini? Kwa kuwa alifahamu fika kwamba amewakosea Watanzani aidha akiwa na nia nzuri au mbaya ndipo akaona njia sahihi ni kuchafua uchaguzi.

Kwa mantiki hii, hakuna mwenye uhakika wa nani ambaye anamkubali kiongozi wa CCM sirini. Wote tumebaki kusikia uungwaji mkono wa majukwaani ila unapokuja sirini hakuna mwenye uhakika wa kutoboa. Hii inatokana na ukweli kwamba tumewaweka makovu Watanzania kwa muda mrefu kwa kuwaaminisha tunafanya uwekezaji wenye tija matokeo yake hakuna tija.

Kwa hatua za awali Mhe. Rais ameona walipokosea wasaidizi wake, amejifunza kwa ndani nini jamii inataka, amewasikia viongozi wa kijamii na imani wanasimamia nini, lakini amewasikia wale wasaidizi wake bungeni walichangia nini; obviously amebaini wanaompotosha na kumchonganisha na jamii siyo wapinzani bali wasaidizi wake.

Inatia hasira unapodhani una wataalam wazuri kisha unagundua kazi waliyofanya inapigwa vita na kila msomi; swali la kujiuliza, hao wasomi walioteuliwa kukusaidia wameelimika? Wana exposure au wapo kwa sababu wapo?

Naamini soon Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake watapisha ofisi kwa kilichotokea, vinginevyo ikibainika mkataba haukuwa shirikishi, pamoja na kiburi cha kibinadamu bora tuchelewe kufika kuliko tufike tukiwa siyo wamoja.

Padri Kutima ametueleza Somalia na Sudan, mimi nataka niongeze Loliondo na Tarime mgodini, je, tunadhani ni nia zote nzuri ni nia nzuri?
Tatizo ni waliowaweka hao wabunge

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
 
Mibunge ya ccm ni bonge la mipuyangaji ,ona Sasa imeuza na nchi,nitakushangaa Sana mtanzania wewe unayeshobokea mijitu ya kuvaa minguo ya kijani isiyokuwa na chembe ya utu hata kidogo kwenye Raslimali za nchi mijitu hii yenyewe ni kuuza uza tu Kila kitu hakuna chembe ya uwajibikaji ovyo Sana hii
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin

Maswali fikirishi.

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Wangeuza na bandari za Zanzibar watu wasingelalamika
 


Kwa hiyo mtu aliyetoka taifa DOGO hawezi KUSIMAMIA ya taifa kubwa?!!!

Mathalani "Mjapani aliyechukua uraia" hawezi kuwa kiongozi mzuri URUSI ,BRAZIL NA MAREKANI ?!!!

Dr.Salim Ahmed Salim si MZANZIBARI??!

Alichemka alipokuwa waziri wetu mkuu ?!!!

Alichemka akiwa balozi ?!!!

Alichemka akiwa katibu mkuu (OAU) kisa tu ametokea nchi ndogo na isiyo na wasomi wengi kama Tanzania bara ?!!!!

Hivi mnakwenda kweli kusoma huko mashuleni ?!!

Na kabisaaa hayo mashule hayawafundishi "ungese wa fikra na tafakuri" ?!!!mmmh

#SIEMPRE JMT

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Siempre maana yake Nini?
 
..daraja la pili ni sisi Watanganyika ambao tumenyimwa kuwa na serikali yetu.

..pia tumenyimwa kuwa na vitambulisho vya Tanganyika, lakini Zanzibar wana vitambulisho vyao.

..Mtanganyika hata uwe msomi kiasi gani huwezi kuajiriwa au kuteuliwa ktk serikali ya Zanzibar, ingawa tunaambiwa ni nchi moja.
Kwani serikali yenu nyinyi watanganyika sio ndio hiyo ya Muungano au vipi
 
..kuwe na usawa ktk muungano.

..kama ni sahihi kuwa na kitambulisho cha Mzanzibari basi Watanganyika na sisi tupewe haki hiyo.

..kama Zanzibar wana serikali na Raisi wao, Watanganyika nao wapewe serikali na Raisi wao.
Tanganyika imeva koti la muungano serikali yenu ya tanganyika imo humo humo kwenye serikali ya Muungano wewe angalia vizuri tu utaiyona
 
Back
Top Bottom