Serikali Iko Mbioni Kujenga Uwanja wa Ndege Zenye Uwezo wa Kubeba Abiria 50 Mkoani Singida

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,897
941
Katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni jijini Dodoma, Mhe. Martha Nehemia Gwau aliuliza swali lililojibiwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile na kusema kuwa Serikali iko mbioni kujenga uwanja wa ndege wa daraja 2C

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Mhe. Martha Nehemia Gwau alitaka kufahamu ni lini Serikali itajenga uwanja wa ndege wa Singida. Ambapo Naibu Waziri Kihenzile amemuhakikikishia kwamba eneo lililopo kwa sasa ni hekta 49.1 na tunahitaji kuongeza hekta 97.8.

"Tunaendelea kushirikiana na Kamishina wa ardhi Singida kutwaa ardhi hiyo. Katika Mwaka wa fedha 2024/2025 tutatenga fedha kwa ajili ya uhuishaji wa usanifu wa kina ili kuwa na mahitaji ya kiufundi na mara baada ya hatua hii kukamilika serikali itatenga fedha kuanza utekelezaji wa mradi" Kihenzile

Mhe. David Kihenzile amesema kuwa lengo pia ni kuhakikisha kiwanja hiki kiwe na daraja la 2C ili kuongeza uwezo wa kubeba ndege kubwa pia zenye abiria 50.

maxresdefaultqaswe.jpg
IMG-20230905-WA0006.jpg
 
Serikali Iko Mbioni Kujenga Uwanja wa Ndege Zenye Uwezo wa Kubeba Abiria 50 Mkoani Singida

Katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni jijini Dodoma, Mhe. Martha Nehemia Gwau aliuliza swali lililojibiwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile na kusema kuwa Serikali iko mbioni kujenga uwanja wa ndege wa daraja 2C

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Mhe. Martha Nehemia Gwau alitaka kufahamu ni lini Serikali itajenga uwanja wa ndege wa Singida. Ambapo Naibu Waziri Kihenzile amemuhakikikishia kwamba eneo lililopo kwa sasa ni hekta 49.1 na tunahitaji kuongeza hekta 97.8.

"Tunaendelea kushirikiana na Kamishina wa ardhi Singida kutwaa ardhi hiyo. Katika Mwaka wa fedha 2024/2025 tutatenga fedha kwa ajili ya uhuishaji wa usanifu wa kina ili kuwa na mahitaji ya kiufundi na mara baada ya hatua hii kukamilika serikali itatenga fedha kuanza utekelezaji wa mradi" Kihenzile

Mhe. David Kihenzile amesema kuwa lengo pia ni kuhakikisha kiwanja hiki kiwe na daraja la 2C ili kuongeza uwezo wa kubeba ndege kubwa pia zenye abiria 50.
Kumbe Singapore hakuna Uwanja wa Ndege!!!!!
 
tusichoshane bwana hapo kahama kwenye uwanja wa kutua ngenge umewashinda sawa na kuweka jengo la watu sio uwezo wa ndege kuingia wala kutoka
 
Wakati mwingine sio uwanja wa ndege, bali wasafiri wenyewe wapo au ndio tunajengea kunguru.

kwasasa Singida Kuna investments za kuwafanya watu wapande ndege kuwahi biashara zao? Kuna wakati tuache kuchezea hela.

Mwanza pale Kuna biashara kwasababu ya migodi kuanzia Geita, Musoma, Mwadui, kahama nk, migodi mikubwa na wachimbaji wadogo wadogo pia.
 
Wakati mwingine sio uwanja wa ndege, bali wasafiri wenyewe wapo au ndio tunajengea kunguru.

kwasasa Singida Kuna investments za kuwafanya watu wapande ndege kuwahi biashara zao? Kuna wakati tuache kuchezea hela.

Mwanza pale Kuna biashara kwasababu ya migodi kuanzia Geita, Musoma, Mwadui, kahama nk, migodi mikubwa na wachimbaji wadogo wadogo pia.
Biashara ipi ipo Geita? Uwanja wa chato sasa wanatua ndege aina ya popo na bundi
 
Back
Top Bottom