SERIKALI (CoET, UDSM): MSIPOLIFANYIA KAZI HILI MAPEMA....

Hao walimu kuna wakati huwa wanakuja kuwatembelea wanafunzi wakati wa field. Mwalimu anafika field na wengi ni hao vijana anashanga tu naye haelewi chochote, mwisho wa siku anauza sura anaondoka zake. Wakati mwingine hata hawaji.

Wapo ambao ni wazuri, angalau walipata bahati ya kufanya kazi labda muda mfupi au walipata sehemu ya field nzuri. Lakini ukweli ni kwamba wanahitaji muda wa kutosha kushiriki kwenye projects mbalimbali ili waje kuwa walimu wazuri.

Serikali itambue kwamba kwa level ya university mwanafunzi anaandaliwa kufanya kazi, sasa kama wanaowafundisha hawajawahi kufanya hizo kazi tutakuwa tunacheza makidamakida.

Labda na suala lingine ni haya makampuni yaliyopo sababu ndio wanaoajili vijana wanapomaliza chuo, watuambie uwezo wa hao wanafunzi, na kama uwezo hawana wamechukua hatua gani. Sababu kuna makampuni mengi ambayo yamekuwa yakilalamika uwezo wa hao freshers lakini hawajaribu kusaidia kusolve hilo tatizo au kusaidia kutafuta kiini cha tatizo.

Tukumbuke kazi za Engineering zinacheza sana na maisha ya watu. Tusipokuwa na maandalizi ya msingi kwa vijana wetu tutakuja kupata madhara makubwa sana huko baadae. Serikali iache kufikiria siasa za kila siku badala yake iinvest kwenye Elimu.
inaumaa sana we are the victimof the system
bila wahandisi imara kweli bongo itaendelea

do politician hear this?
 
Yaani mimi nakubaliana na wewe mia kwa mia,kwa kweli experience inahusu,there is a lot to learn n relate with class,nina uhakika ukimuweka engineer wa civil aliyekaa field kwa miaka miwili na aliyetoka direct na kwenda masters utampa wa miaka miwili kazi c wa masters,kwa nini watu wanasoma masters?mi nadhani ina umuhmu ukishakaa kazini kidogo,

Kwa uzoefu wangu kusoma masters kuna umuhimu hasa kwa jinsi tech. invyobadilika kwa kasi. Undergrad unapata sanasana basics za kuweza kufanya kazi kwahiyo na ukiwa field utakuwa unajiongezea ujuzi zaidi kutokana na challenge ambazo utakuwa unazipata ukiwa huko. Lakini ukisoma masters kuna utakuja kugundua undergrad mlikuwa mnagusagusa tu. kwahiyo inategemeana hasa upo wapi. Lakini cha msingi huwezi ukasoma daraja/nyumba etc kwenye makaratasi lazima ili kuelewa na kuwa mwepesi hasa kwa hawa walimu uwe na uwezoefu wa jinsi kazi zinavyofanyika huko site.

Waandisi nao wajue "Good judgement comes from experience, but experience comes from bad judgement" kwa tujifunze kila siku tunapokuwa site.
 
Back
Top Bottom