Ahaa haaa mgosi watafuta habari za ukweli za CUF ndani JF? ni sawa kusema bahari ya Hindi imepita imepita Mashewa!
Chama
Gongo la mboto DSM
Nadhani kuna kampeni maalum inayofanywa kisanii kujaribu kupunguza nguvu za CDM. Jumamosi nikiwa maeneo ya Ubungo niliona mabasi mengi yakiwa yamejaa watu huku yakiwa yamefungwa bendera za CUF. Nilipodadisi nikaambiwa wanakwenda kwenye mkutano wa hadhara Arusha. Nilishangaa sana kwa sababu sio kawaida wafuasi wa chama kusafirishwa kutoka mkoa mmoja hadi mwingine eti kuhudhuria mkutano wa hadhara. Hapa kuna jambo! Kingine kilichonishangaza ni kauli ya kiongozi wa UPDP aitwaye DOVUTWA alipoitisha mkutano wa waandishi wa habari na kumlaani Dk Slaa aliyeiponda CCM kwa kuwakumbatia mafisadi kwenye uchaguzi wao wa NEC. NIONAVYO mimi, baada ya CCM kuelekea kushindwa kuzima nguvu ya CDM (hata baada ya kutumia polisi kuua), sasa wanajaribu kuvitumia vyama dhaifu vya upinzani (ambavyo ni matawi yao) kujaribu kupambana na PEOPLE'S POWER. Wataweza?
Ukiangalia kichwa cha habari hapo juu utagundua kuwa unachoenda kukipata si cha kweli na kimejaa uongo ndani yake. Heading hiyo iko kwenye gazeti la sauti huru.
Sauti huru nila kada wa ccm lakini hapa linatumika kujenga uongo wa mchana kweupe! Labda mlioko Arusha mumsaidie muandishi kumuambia ukweli.
Hilo gazeti ni noma. CUF
wenyewe kwenye risala yao kwa Sultan walisema wamepata wanachama 100 na
hao wanachama 3000 waliwapatia wapi? make kwenye mkutano sijaona mtu
akirudisha kadi
jamani mkutano wenyewe ukitoa watu walioletwa na mabasi kutoka Dar na Morogoro hawakuzidi 100 Na hata ukijumlisha waliotoka Dar na Moro na watu wa Arusha kwa pamoja hawakuzidi 700 sasa hao 3000 wanatoka wapi? au waliimanisha watatu kama ni watatu ni kweli na majina nawafahamu..