Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,150
Kama kuna mtu anayepata shida sasa na hili sakata la TANESCO ni HR,
Habari zilizotufikia kuna vituko vitupu watu wana vyeti vya copy na walipobanwa wapeleke original kila mtu anamuomba Mungu kama ni mapenzi yako basi kikombe hiki kinipite.
Sasa basi pengine si suala la kucheka hili ni tatizo la kudumu kama mabalozi wetu tunavyowahalalisha huko UN na kwingineko.
Pamoja na kwamba hawana vyeti, wengi wao unakuta wana uzoefu wa miaka 10 nk. Na hapa ndipo vichwa vinawaka moto hata mabosi wanajiuliza wamekaaje kwenye vyeo hivi bila ya kuhalalishwa shule zao tangu mwanzoni.
Naamini matatizo haya ni wakati muafaka wa kuwapa nafasi watu waliosoma na kuachana na watoto wa momba, shangazi na wengineo.
Kaimu Mkurugenzi mtumishi wa Mungu Mramba najua uko na wakati mgumu lakini kutokana na maombi yako na jinsi unavyomjua Mungu naamini utapita kwenye vita hivi vizito.
Ni wakati sasa wa kukutana na majaribu kama ulikuwa ukiyasikia utaanza kuyaona live, wapo wanaokimbilia Bagamoyo na Tanga wanajua wanafuata nini.
Lakini kama uliyenae ni mkuu kuliko hao wanaokimbizana nao, tunaomba suala la vyeti liendeelee kila sehemu kwenye sekta za serikali kuwapa nafasi wanaostahili.
Kuna uchafu mwingi sana wa vyeti huko serikalini, wengi wao hata original ni vya kufoji.
Raha ya milele ampe ee ex director na mwanga wa milele apumzike kwa amani na hela zetu za tanesco milli 800 loh!!
Habari zilizotufikia kuna vituko vitupu watu wana vyeti vya copy na walipobanwa wapeleke original kila mtu anamuomba Mungu kama ni mapenzi yako basi kikombe hiki kinipite.
Sasa basi pengine si suala la kucheka hili ni tatizo la kudumu kama mabalozi wetu tunavyowahalalisha huko UN na kwingineko.
Pamoja na kwamba hawana vyeti, wengi wao unakuta wana uzoefu wa miaka 10 nk. Na hapa ndipo vichwa vinawaka moto hata mabosi wanajiuliza wamekaaje kwenye vyeo hivi bila ya kuhalalishwa shule zao tangu mwanzoni.
Naamini matatizo haya ni wakati muafaka wa kuwapa nafasi watu waliosoma na kuachana na watoto wa momba, shangazi na wengineo.
Kaimu Mkurugenzi mtumishi wa Mungu Mramba najua uko na wakati mgumu lakini kutokana na maombi yako na jinsi unavyomjua Mungu naamini utapita kwenye vita hivi vizito.
Ni wakati sasa wa kukutana na majaribu kama ulikuwa ukiyasikia utaanza kuyaona live, wapo wanaokimbilia Bagamoyo na Tanga wanajua wanafuata nini.
Lakini kama uliyenae ni mkuu kuliko hao wanaokimbizana nao, tunaomba suala la vyeti liendeelee kila sehemu kwenye sekta za serikali kuwapa nafasi wanaostahili.
Kuna uchafu mwingi sana wa vyeti huko serikalini, wengi wao hata original ni vya kufoji.
Raha ya milele ampe ee ex director na mwanga wa milele apumzike kwa amani na hela zetu za tanesco milli 800 loh!!