Sakata la Umeme Nchini: Dr. Rashid Alikuwa Sahihi na kamati ya Bunge Ilikosea

Punguza hamasa mkuu...

Tanesco wanachoweza kufanya ni kushauri...na walifanya hivyo kwa ushahidi wa maneno ya waziri malima....kwamba walishauri nchi iwe na back up ya umeme na ready made solution ilikuwa ni kununua dowans...kilichotokea ni historia...lakini tunachojua kwa hakika ni kuwa dowans ilikataliwa na wizara ilishindwa kuanzisha mchakato wa kutafuta mitambo mipya...na hilo ndio limetufikisha hapa.....je lawama iende kwa tanesco au wizara...jazba itatuongoza kuinyooshea kidole tanesco lakini busara ni wizara kwani mwisho wa siku si tanesco ambayo ingekuwa na ultimate responsibility ya kununua dowans....si tuliona richmond...au ndio tumeshasahau maana lowasa alikuwa kipenzi chetu...mwanamtandao mwenzetu?????

Naona sualahili inabidi litufikishe mahala ambapo kuwe na mgawanyo halisi wa madaraka kati ya serikali na Bunge. Kwa hali ya kawaida, jukumu la kuchukua maamuzi na kuyatekeleza katika kuleta maendeleo ya nchi ni jukumu la serikali. jukumu la Bunge ni kutunga sheria na kuisimamia serikali. Si jukumu la Bunge kuchukua maamuzi ya utendaji wa serikali kama ilivyofanya katika suala hili la Dowans.

Hapa Kamati ya Bunge iliikataza serikali kutekeleza majukumu yake. Kilichotakiwa kufanywa na kamati hiyo ni kutoa ushauri tu na sikuingilia na kukataza. Ingefanya hivyo (kutoa ushauri) serikali ingepima kuendelea na mpango wake au la. Katika hali hiyo, kamati ya Bunge ingekuja kuidhibiti serikali baadaye endapo maamuzi hayo yangeliingiza taifa katika hasara.

Kwa kuwa serikali ilikwisha kubali maamuzi ya kitaalamu ya Tanesco na ikawa tayari kuyatekeleza, na kamati ya Bunge ikatishia in advance kuwa wakitekeleza watawajibishwa, basi ili kuinusuru serikali ya CCM kuangushwa na Bunge wakaamua shingo upande kuachana na wazo hilo ingawa lilikuwa na maslahi kwa taifa.

Katika hali hiyo, kamati ya Bunge haiwezi kukwepa lawama katika hili kwani kama isingeingilia maamuzi ya kitaalmu, hizo mega wati 72 zilizopungua leo lingekuwa si tatizo.
 
Tatizo la watz na serikali yenu, hamfikiri kwa vichwa vyenu, wachache wanaofanya hivyo wanaonekana hawajuwi kitu, hawajasoma au vp. Kama tatizo lilionekana mapema kwa nini busara isingelitumika na mitambo ile ya Dowans ikafanya kazi kunusuru hali. Wakati shirika likijuwa nini kitatokea watz wengi wamebaki kufata kelele za wanasiasa wenye maslahi yao binafsi pembeni, sasa hao wapiga zogo waliotaka mitambo ile isinunuliwe wao wanakaa gizani kama akina "pangupakavu?" au huo waliotaka mitambo ile isinunuliwe kwa visingizio visivyokidhi maslahi ya wananchi kwa tatizo lililotarajiwa kutokea, wapo wapi na huo umeme wao wa "upepo" kuwaokoa watz na giza?
Yupo wapi spika Sitta na wenzake walioona kasoro za kununuliwa mitambo ile bila ya wao kutoa pendekezo la maana la kutatuwa hali ya dharura iliyopo, je wao wanakaa gizani kama akina "fanyakukuche kitanda kinaumiza?"
Watanzania, wakati unakupiteni kutegemea viongozi wabovu wa CCM wakuamulieni kila kitu bila ya ridhaa yenu, mlipaswa hata mufanye kura ya maoni kuamua kama mkubali mitambo ya Dowans isinunuliwe na kuwa tayari kukaa gizani...hata mwaka mzima au masharti ya sheria yalegezwe na mitambo inunuliwe kukidhi hali ya dharura kama ilivyopendekezwa na wataalamu. Badala yake mumewaachia wanasisa "maslahi" kuamua kwa faida ya matumbo yao na hasara kwenu. poleni sana kwa giza.
 
Shelukindo, Mwakyembe, Sitta wote ni wa kulaumiwa....walichanganya siasa zazo za makambi ndanii ya CCM hata kushindwa kuona maslahi ya taifa na kusababisha taifa kuingia gizani...zitto ametwambia kuwa mgawo wa kwanza ulisababisha uchumi mkubwa(macro economy) uliporomoka kwa kwa nukta moja sawa na billioni250 kutokana na mgawo.....Malima anasema mtu akinunua mitambo ya Dowans, kisha akaiuzia serikali, serikali itanunua...hii maana yake nini?....tumeingiza taifa kwenye giza kwasababu ya cheap politics za akina Mwakyembe pembeni ya Rais mwoga asiye na maamuzi...Gwiji la masuala ya Nishati Benki ya Dunia..mwaka huu .Karhammar alisema katika gazeti moja la nchini Kenya, The east African kwamba...""mjadala wa kununua au kutonunua mitambo ya dowans tanzania umebebwa na siasa zaidi kiasi cha kuweza kujadiliwa kitaalamu""...Tulichopaswa kununua ilikuwa mitambo kwa vigezo vya uwezo na bei, basi. Suala la mitambo hiyo inamilikiwa na kampuni gani lilipaswa kupelekwa mahakamani wakati watanzania wanaendelea kupata umeme...badala ya watu kuendelea kutupigia siasa za porojo za kutafuta umaarufu huku nchi inaingia gizani.....hasara ni kubwa sana ndugu zangu....mimi naomba tuangalie sana mwenendo wa hizi siasa za bongo na makundi yao, nchi inaweza kuunguzwa kwa upumbafu wao....
 
Hii ni lawama ya Serikali na Rashid full stop. Yaani wamekuja bungeni na plan A peke yake na walipoambiwa STOP basi wakazila ili waje waseme "Si tulisema?". Kaulizwa swali na waandishi wa habari, Dr. Mzima kashindwa kajibu.

Kama kununua mitambo mipya mchakato unachukua mwaka mmoja, kwa nini hawakuliomba BUNGE libadili sheria hata kwa muda ama ruhusa ya Special case kununua mitambo moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji na watengenezaji watoe Bima ya mitambo hiyo? Hivi Rais kweli alishindwa kusaidia kutangaza kuwa "inabidi avunje sheria kwa sababu hili swala ni kama vita na ni kwa ajili ya usalama wa Taifa". Ujenzi wa majengo ungelifanywa within 3-4 months na wakati huo, Wahandisi wangelikuwa USA/German kusomea na baadaye kuileta hiyo mitambo mipya. Tungeliazima dege la Mrusi na kwa kipindi cha mwezi mmoja, mitambo ingelikuwa inafanya kazi.

Walipoona Azimio la Arusha linawakera na kuwazibia, walilipiga panga siku moja na wakalizika. Walipotaka pesa BoT kwa ajili ya uchaguzi, walitengeneza EPA na kuchota. Wakaja tena kuzibeba kwa kutumia Deepgreen, Meremeta etc. Walipotaka kuanzisha kampuni ya Richmond, walipindisha kila sheria hadi ikawepo. Hawa watu kama kweli wangelikuwa na NIA ya kuleta mitambo mipya na si kununua mitambo ya Dowans, basi amini usiamini, ingelikuwa sasa hivi inafanya kazi.

Inabidi mwakani tuchague Rais atakayeahidi kumaliza shida ya umeme na maji Tanzania. Kama akishindwa basi mnamuweka pembeni. Akimaliza mnamchagua kwa ngwe ya pili. Akiahidi mambo kibao, mhhhhh. Nawapenda USA ambao waliahidiwa na mgombea kuwa "wakimchagua basi kila chungu jikoni kitakuwa na kuku......... na kweli aliwajaza mikuku..."
 
Extract 5

"(Shellukindo) aliishauri serikali kupitia Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2004, kuona namna ya kuondoa urasimu uliopo ili usiathiri manunuzi ya mitambo miwili itakayozalisha umeme wa jumla ya megawati 160, katika miji ya Dar es Salaam na Mwanza.

Hivi Shelukindo anaona udhaifu wa sheria ya manunuzi leo? miaka yote yopo serikalini alikuwa hajaliona hilo? nashangaa kwasababu moja ya sababu ambayo yeye na mwakyembe wameirejea mara kadhaa ni kwamba walipinga kununuliwa mitambo ya dowans kwasababu ni kinyume cha sheria ya manunuzi ya 2004....tunapaswa kujua kwamba uchumi ni ajenda ya kwanza kabla ya sheria, siasa,nk.....akina shelukindo wangekuwa na dhamira njema wasingethubutu sheria dhaifu na siasa zao chovu kusababisha mgawo wa umeme....Idrissa hana kosa....ana mikakati....anajua kushauri...ni mtaalamu....ahukumiwe kwa makosa yake....lakini katika hili hana kosa, wanaopaswa kuwajibika kisiasa ni hawa akina Mwakyembe
 
TANESCO inaongozwa na kamati ya Bunge iliyojaa kina John Komba then tunategemea matatizo ya umeme yaishe...hamko serious nyie!
 
""Hii ni lawama ya Serikali na Rashid full stop. Yaani wamekuja bungeni na plan A peke yake na walipoambiwa STOP basi wakazila ili waje waseme "Si tulisema?". Kaulizwa swali na waandishi wa habari, Dr. Mzima kashindwa kajibu""-SKONGE

Mimi siamini kama Idrissa ana kosa. wenye kosa ni Kamati ya Shellukindo na serikali....wabunge ni washauri wa serikali...hawana mamlaka ya kufanya mamuzi...wabunge walifanya mamuzi ya kisiasa, serikali ilipaswa kuyapuuza na kufanya maamuzi ya kitaalamu...Idrissa alikuja na pendekezo...likakataliwa...waliokataa hawakutoa pendekezo mbadala...na ukumbuke baada ya Idrisa kutoa pendekezo, serikali ilipitisha, kamati ya shellukindo ndio ikakataa..sasa Idrissa hakuajiriwa na kamati ya shellukindo, aliajiriwa na serikali...aliona serikali imeyumba kipumbavu, akamua kukaa na kusubiri kuona serikali itamwambia afanye nini....haikumwambia...kamati ya shellukindo...haikumwambia...siasa za kisasa sio kupinga tu...ni kupendekeza mbadala zaidi
 
Kwanini hao waandishi wa habari hawakwenda muuliza Mh . Mwakyembe aliyesema hatutaki ile mitambo hata nchi ikiingia kwenye giza? Kwa sasa Mh. huyu anahoja gani au kuna mipya inakuja? Nchi inataendelea vipi DS kila kona...Kama hukuimarisha umeme maendeleo ni ndoto.

Ataleta umeme wa upepo...sijuhi utaliweza janga hili
 
Junius,
Mkuu wangu usimsome Kasheshe kufikia maamuzi pasipo wewe kufikiria kwa kichwa chako undani wa tatizo hili la Umeme.
Kwanza kabisa hapa nanukuu maneno ya Malima alivyosema.
Hata hivyo, baada ya shellukindo kusema kwamba sakata la Dowans limekwisha zikwa, Naibu waziri wa Nishati na Madini, Adama Malima aliyekuwepo katika mkutano huo aliongeza kuwa, serikali haina mpango tena wa kununua mitambo hiyo ya kufufua umeme ya Dowans, lakini endapo mtu binafsi atainunua na kuiuzia Tanesco umeme kwa sheria ya sasa itakubali.

Hapo ujuu katika maandishi menkundu inaonyesha wazi kwamba serikali yetu imeshapania kuuza mitambo hiyo kwa Tanesco. Wanaposema endapo mtu binafsi akinunua mitambo hiyo anaweza kuiuzia Tanesco Umemem ina maana gani?.. Dowans ni shrika binafsi ikiwa na maana kuna mtu binafsi aliyeinunua hiyo mitambo toka Richmond na wote hawa walitakiwa kuiuzia Tanesco Umeme..Sasa kilichoshindikana ni kipi toka mwanzo! - kwa sababu ya Ufisadi... na pili Dowans ingechukua tender kinyumwe cha sheria pasipo kutangazwa tender huru kwa wawekezaji..Leo tunapitisha sheria ya kununua mitambo hiyo hiyo chini ya maamuzi ambayo ni pinzani na sheria yetu ya manunuzi...Licha ya yote hayo tumeona shirika kama Songos wakiuponda mtambo huo kuwa ni mtumba, haifai ni chavu...leo nchi nzima tunashindwa ktk maamuzi na shirika moja dogo ambalo tumeliajiri sisi wenyewe!

Mkuu hakuna asiyejua kwamba mitambo hiyo ni mali ya MTANDAO, hii ndio fact! hao kina Lowassa na Rostam kwa hiyo jina la mtu binafsi yoyote linaweza kuwekwa kama mnunuzi na tukarudi ktk makosa yale yaliyofanyika toka mwanzo..Rostam akinunua mtambo huo wa Dowans hawezi kuandika jina lake ila atazua jina jingine la kampuni. Je, mmeshasahau kwamba ni serikali hiyo hiyo hadi leo imekataa katakata kututajia nani mwenye kumiliki shirika hilo tena walidiriki hata kusema HAWAJUI mwenye kumiliki shirika hilo, iweje leo tukanunue mitambo toka shirika ambalo viongozi wetu hawafahamu mwenyewe..Hii inaingia akilini kweli?

Pili, nakumbuka vizuri kuwa kamati ya madini na Nishati kwa maneno yake Zitto mwenyewe alisema malengo ya Tanesco kununua mitambo ile ni kuiwezesha Tanesco kuwa na mitambo yake yeynyewe badala ya kukodisha jambo ambalo limetugharimu sana kwa kipiundi kifupi toka mashirika binafsi, leo hii tunarudi ktk janga lile lile. Hivi kweli mtu unaweza pindisha sheria tukanunua mali ya wizi kwa sababu mwizi ni binadamu sio mali iliyoibiwa!

Mkuu wangu ikiwa mitambo hii ina mashaka ya Ufisadi na wahusika wake ni Rostam na Lowassa basi seriikali wala shirika haliwezi kununua mitambo hiyo hadi janga la Richmond limepatiwa ufumbuzi. Mitambo ya Dowans ni ushahidi wa kesi ya Richmond ambayo kisheria inatakiwa kuwa confiscated na mashtaka kufunguliwa mahakamani lakini tunapouza ushahidi huu ni mbinu mojawapo ya kupoteza ushahidi.

Tatu,
tatizo la Umeme kwa maelezo ya Shelukindo ni tatizo ambalo LIPO toka Kikwete anaingia madarakani yalikuwepo na ktk kiwango hicho hicho.. Tuliambiwa maelezo yote alozungumza Shelukindo, hakuna jipya na wanachi tulivaa vibwebwe pamoja na ahadi ya mvua za kisayansi na kufua umeme wa makaa ya mawe, kuboresha mabwawa yetu na mengine mengi ambayo rais mwenyewe aliwaahidi wananchi kabla hata hajakaa Ikulu..Loe hii ni miaka MINNE hakuna jipya!

Na sote tunaelewa kwamba Tender ya Richmond, Watsila na mashirika mengine zilikubaliwa kama ni tatizo lka dharura ambalo lilitakiwa haraka iwezekanavyo kwa wakati ule...Ilichukua mwaka mzima kwa Richmond kufikisha mitambo yao na haraka sana tuligundua Ubabaishaji wao na tukawasimamisha.. Toka Richmond wasimamishwe ni miaka MITATU mingine imepita wakati Tanesco na serikali wakijua kwamba hizo MW 100 ni muhimu sana iweje walishindwa muda wote huo kufidia hjizo Mw 100, ila wakazanie kununua mitambo hiyo tu kwa miaka yote mitatu?.. Hivi kweli tulishindwa kuagiza mitambo mingine au hata kuwapa hiyo Tender Watsila au shirika jingine ambalo linawauzia umeme Tanesco kwa uhalali isipokuwa Dowans pekee!..

Mkuu it's been FOUR Yrs toka tuna matatizo ya umeme kwa jiji la Dar pekee na miaka zaidi ya 20 kwa mikoa ambayo imetajwa kuwa na shida ya umeme wa dharura. Ni miaka 40 kwa nchi nzima tukiondoa wakati wa mkoloni iweje leo somo kubwa la ununuzi wa mitambo ya Dowans tena Mw100 iwe makosa makubwa ya serikali ambayo imehsindwa kuanzisha vyanzo vipya vya umeme toka mwalimu Nyerere atoke madarakani.

Hadi leo hii tunategemea vyanzo vya mwalimu Nyerere ambaye alivijenga ktk wakati mgumu sana, wakati ambao serikali iligharamia kila matumizi ya huduma za wizara na taasisi zake, leo tunashindwa kabisa kujenga vyanzo vipya wakati serikali inavuta kodi pasipo matumizi makubwa lakini wepesi kuzungumzia Dowans ambayo inaingia kinyume cha sheria.
 
[QUOTE=Mbala-mwezi;612730]""Hii ni lawama ya Serikali na Rashid full stop. Yaani wamekuja bungeni na plan A peke yake na walipoambiwa STOP basi wakazila ili waje waseme "Si tulisema?". Kaulizwa swali na waandishi wa habari, Dr. Mzima kashindwa kajibu""-SKONGE

Mimi siamini kama Idrissa ana kosa. wenye kosa ni Kamati ya Shellukindo na serikali....wabunge ni washauri wa serikali...hawana mamlaka ya kufanya mamuzi...wabunge walifanya mamuzi ya kisiasa, serikali ilipaswa kuyapuuza na kufanya maamuzi ya kitaalamu...Idrissa alikuja na pendekezo...likakataliwa...waliokataa hawakutoa pendekezo mbadala...na ukumbuke baada ya Idrisa kutoa pendekezo, serikali ilipitisha, kamati ya shellukindo ndio ikakataa..sasa Idrissa hakuajiriwa na kamati ya shellukindo, aliajiriwa na serikali...aliona serikali imeyumba kipumbavu, akamua kukaa na kusubiri kuona serikali itamwambia afanye nini....haikumwambia...kamati ya shellukindo...haikumwambia...siasa za kisasa sio kupinga tu...ni kupendekeza mbadala zaidi[/QUOTE]

nasikia kwa kina Dr Rashidi na Kwa Sherukindo umeme full...Hakuna cha mgao wala nini.Ndo maana hawakuchukua hatua za kutafuta altenative nyingine....

Zito yeye yuko gizani,pamoja na kuwaunga mkono akina rashidi....
 
Extract 3

"Pamoja na kukiri kwamba, kikao chao kilibaini kuwa, tatizo la umeme litaendelea kulisumbua taifa kwa kipindi kirefu zaidi, Shellukindo alisema suala la kuitaka serikali kununua mitambo ya Dowans halikuwa sehemu za ajenda walizozijadili.

Hata hivyo, baada ya shellukindo kusema kwamba sakata la Dowans limekwisha zikwa, Naibu waziri wa Nishati na Madini, Adama Malima aliyekuwepo katika mkutano huo aliongeza kuwa, serikali haina mpango tena wa kununua mitambo hiyo ya kufufua umeme ya Dowans, lakini endapo mtu binafsi atainunua na kuiuzia Tanesco umeme kwa sheria ya sasa itakubali.

Katika hilo, Malima alisema kwa sheria ya sasa, Tanesco ina uwezo wa kununua umeme kutoka katika makampuni na taasisi binafsi ili iweze kukidhi mahitaji yake ya kuhakikisha kuwa nishati hiyo inakuwepo wakati wote nchini""


mmhmmh....hapa pazuri kujadili....
 
Hii ni lawama ya Serikali na Rashid full stop. Yaani wamekuja bungeni na plan A peke yake na walipoambiwa STOP basi wakazila ili waje waseme "Si tulisema?". Kaulizwa swali na waandishi wa habari, Dr. Mzima kashindwa kajibu.

Kama kununua mitambo mipya mchakato unachukua mwaka mmoja, kwa nini hawakuliomba BUNGE libadili sheria hata kwa muda ama ruhusa ya Special case kununua mitambo moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji na watengenezaji watoe Bima ya mitambo hiyo? Hivi Rais kweli alishindwa kusaidia kutangaza kuwa "inabidi avunje sheria kwa sababu hili swala ni kama vita na ni kwa ajili ya usalama wa Taifa". Ujenzi wa majengo ungelifanywa within 3-4 months na wakati huo, Wahandisi wangelikuwa USA/German kusomea na baadaye kuileta hiyo mitambo mipya. Tungeliazima dege la Mrusi na kwa kipindi cha mwezi mmoja, mitambo ingelikuwa inafanya kazi.

Walipoona Azimio la Arusha linawakera na kuwazibia, walilipiga panga siku moja na wakalizika. Walipotaka pesa BoT kwa ajili ya uchaguzi, walitengeneza EPA na kuchota. Wakaja tena kuzibeba kwa kutumia Deepgreen, Meremeta etc. Walipotaka kuanzisha kampuni ya Richmond, walipindisha kila sheria hadi ikawepo. Hawa watu kama kweli wangelikuwa na NIA ya kuleta mitambo mipya na si kununua mitambo ya Dowans, basi amini usiamini, ingelikuwa sasa hivi inafanya kazi.

Inabidi mwakani tuchague Rais atakayeahidi kumaliza shida ya umeme na maji Tanzania. Kama akishindwa basi mnamuweka pembeni. Akimaliza mnamchagua kwa ngwe ya pili. Akiahidi mambo kibao, mhhhhh. Nawapenda USA ambao waliahidiwa na mgombea kuwa "wakimchagua basi kila chungu jikoni kitakuwa na kuku......... na kweli aliwajaza mikuku..."

Mimi nililofarijika katika hili ni kuwa, kwa kauli yake mwenyewe, Shellukindo kakiri kuwa safari hii amekubali maelezo ya WATAALAMU kama walivyoyatowa katika mkutano. Naamini kuwa safari hii serikali hata wangetoa ushauri wa kununua mitambo ya Dowans angekubaliana nao maana janga lote sasa limemungukia yeye, hamuoni Mwakyembe wala Sitta, kila kitu inabidi yeye ajibu.

Na pia kwa jinsi ninavyomfahamu Mzee huyu (Shellukindo) hana matatizo, inaonyesha yeye maskini alikuwa akiendeshwa na wale vijana mpaka wakaandika ripoti ya Richmond kwa kuwatumia ma Partner wao walioko Marekani wakati yeye hana habari.

Mimi serikali siilamumu sana maana ukiona jinsi kundi la vijana hawa lilivyopania kuiangusha Bungeni naona ni bora walivyowaridhisha kuliko nchi kuingia katika gharama nyingine ya kuitisha uchaguzi mkuu mapema with risk ya CCM kupoteza serikali.

Serikali na Tanesco inalaumika vipi wakati muda wa mchakato wa miezi 12 bado haujaisha kufuatana na sheria na kanuni zilizopo? Pia unataka wazipinde ili wawape Wabunge Sugu nafasi ya kuwaletea matatizo zaidi?
 
Haiingii akilini kabisa eti matatizo na mgawo wa umeme ni kwa sababu tulikataa kununua mitambo ya Dowans,kwani nani aliwazuia au kwanini hawakununua mitambo mipya kutoka kampuni zinazoeleweka,sioni hata haja ya discussion kwenye hii issue zaidi ya kuwatimua viongozi wote wa TANESCO na Waziri wa Nishati Ngereja!
 
Tutajadili sana hapa JF, lakini source ya matatizo yote haya ni ufisadi, kundi la mafisadi wamemweka Idrisa hapa Tanesco ili kulinda na kutetea ufisadi wao naye kwa kutokuwa na uzalendo na kulewa hela chafu alichokuwa anafikiria ni deal lake la Dowans tu. Baada ya kupigwa chini ndio anashangashangaa tu hapo Tanesco na hakuna la maana alilofanya.
 
Kitakachofuata ni mkubwa fulani au mdosi kununua hiyo mitambo kwa bei poa, na kuzalisha umeme atakao uuza kwa tanesco na kuchota mara mbili ya bei ya mitambo yenyewe na bado next yr atatuuzia tena tu...Goli la kisigino hilo wazee....pamoja na kuwa nchi itapigika kwa mgao, bado hela ile ile itawatoka walipa kodi kwa kulipia capacity charge na bei atakayo taka atakaye nunua hiyo mitambo.....mnakataa kununua mitambo chakavu waka uwezo wa mipya hamna. wa TZ wangapi wana vaa mitumba, wanatembelea used car, mlo wa shida unadhani hawapenda nunua vipya?...bilioni ngapi zinapotea kwa nchi kukosa umeme?
 
Kusema kweli nilkkuwa mshabiki sana wa Zitto na Shelukindo lakini sasa navua manyanga na nadhani hata siasa na vyama inabidi nichukue breaktime!
 
Mimi siamini kama Idrissa ana kosa. wenye kosa ni Kamati ya Shellukindo na serikali....wabunge ni washauri wa serikali...hawana mamlaka ya kufanya mamuzi...wabunge walifanya mamuzi ya kisiasa, serikali ilipaswa kuyapuuza na kufanya maamuzi ya kitaalamu...Idrissa alikuja na pendekezo...likakataliwa...waliokataa hawakutoa pendekezo mbadala...na ukumbuke baada ya Idrisa kutoa pendekezo, serikali ilipitisha, kamati ya shellukindo ndio ikakataa..sasa Idrissa hakuajiriwa na kamati ya shellukindo, aliajiriwa na serikali...aliona serikali imeyumba kipumbavu, akamua kukaa na kusubiri kuona serikali itamwambia afanye nini....haikumwambia...kamati ya shellukindo...haikumwambia...siasa za kisasa sio kupinga tu...ni kupendekeza mbadala zaidi

Ana makosa mengi tu.

Kwanza unaanzia pesa alizozipata kwenye manunuzi ya RADA.

Sasa tuje kwenye hili la umeme: Siku moja nikibadili chanel, nikapita MTV na kukuta Rusell Simons akimtukana kijana aliyedesign nguo na kuzipa mpangilio mbaya. Sijui yalianzia wapi ila niliona Rusell akimtukana, na baadaye akazirukia hizo nguo zilizokuwa chini na kuzikanyagakanyaga na baada ya kurusha matusi kadhaa, akaTEMEA mate na kuondoka.

Amini usiamini kama Kikwete angelikuwa ni Putin, basi Rashid angelipewa maneno yake LIVE mbele za watu na kutukanwa. Kinachofuata ni kuwa au UKIMBIE kazi au uje na kitu kinachoeleweka. Baada ya Rashid kukataliwa kununua mitambo mibovu na mchakato wa kununua mitambo mipya ni mrefu, je alikuja na plan yoyote ya KUWALAZIMISHA wabunge wabadili sheria au hata kuomba kibali MAALUMU kwa BUNGE na RAIS ili kununua mitambo "moja kwa moja" kwa watengenezaji? Hivi Tanesco si waliambiwa na akina Lukindo wanunue mitambo mipya? Sasa walikuwa wanatangaza tena tender ya nini? Wangelipeleka Wahandisi USA/German na kwenda kuchukua offer za makampuni na wakaja nazo. Au hata Mabalozi wangelienda na kuchukua offer na kuzituma Tz. Kwa kipindi kifupi, Wahandisi wa Tanesco, serikali, Bunge na washauri wa Rais wangelikutana na kuchagua wapi inunuliwe. Wanaita Waandishi wa habari wa Upinzani na kusema "inabidi tufanye hivi ili kuokoa nchi kwenye giza". Amini usiamini, wangelishangiliwa kama mashujaa.

Rashid na U-dr wake alipokataliwa Dowans, akaona "niliwaambia, sasa ngoja muone cha mtema kuni....." Ingelikuwa nchi za wakorofi, si tu kuwa anafukuzwa kazi ila anahukumiwa kama Mhujumu uchumi.
 
Yupo wapi Dr Mwakyembe alie sema ikibidi nchi iwe kizani lakini no to Dowans, haya sasa yametimia.

Tunazunguka mbuyu tu hapa siasa zimeingilia utaalamu matokeo yake ndio haya sasa. Walio likoroga akina Sitta, DrMwakyembe, Shulukindo, Eng Manyanya etc wamekaa pembeni kama hawapo.

Tutake tusitake ya wataalamu waachiwe wataalamu. Anaeumia sasa ni Mtanzania wa kawaida.

Akina Zitto waliyaona haya tukawaita majina sijui fisadi kijana nk. Leo watu tunakosa uthubutu walau wa kusema samahani tulisokea na wenzetu walikuwa sahihi. Na kwa mjadala unavyokwenda hapa nakumbuka maneno ya FMES " Viongozi wetu ni reflection ya sisi wenyewe" ndio maana bado tunadai "mkosaji" ni Idris na Tanesco yake! hivi hili nalo ni Calculus pia!
 
Sikonge,
Tusimlaumu Rashid Idirsa pekee yake..kumbuka hata Kikwetenmwenyewe aliulizwa swala hili akatoa AHADI kwamba mitambo ya Dowans haitanunuliwa tena na akasema kuna mipango inafanyika hivyo tatizo la umeme halitakuwepo..Nakumbuka vizuri maneno hyaya ya JK mwenye akiwahakikishia wananchi baada ya bunge kukataa kununua mitambo ya Dowans...sasa kilichoshindikana ni kitu gani! - Maelezo ya Shelukindo na Malima hayakuelezea hata kidogo sababu zilizoshindikana kutoweza pata mitambo mingine kwa karibu miaka mitatu iliyopita! Hivyo bila shaka wananchi tunahitaji maelezo ya kina KULIKONI?
 
Yupo wapi Dr Mwakyembe alie sema ikibidi nchi iwe kizani lakini no to Dowans, haya sasa yametimia.

Tunazunguka mbuyu tu hapa siasa zimeingilia utaalamu matokeo yake ndio haya sasa. Walio likoroga akina Sitta, DrMwakyembe, Shulukindo, Eng Manyanya etc wamekaa pembeni kama hawapo.

Tutake tusitake ya wataalamu waachiwe wataalamu. Anaeumia sasa ni Mtanzania wa kawaida.

Akina Zitto waliyaona haya tukawaita majina sijui fisadi kijana nk. Leo watu tunakosa uthubutu walau wa kusema samahani tulisokea na wenzetu walikuwa sahihi. Na kwa mjadala unavyokwenda hapa nakumbuka maneno ya FMES " Viongozi wetu ni reflection ya sisi wenyewe" ndio maana bado tunadai "mkosaji" ni Idris na Tanesco yake! hivi hili nalo ni Calculus pia!
No mkuu wangu,Viongozi ni reflection yetu kwa sababu viongozi wanataka kununua mitambo ya Dowans by all means necessary na wewe na wengine wengi wenu mnataka pia kununua mitambo chakavu kwa sababu zisizokuwa na maana kabisa!..MNAFANANA kimawazo!

Hivi kweli tukinunua mitambo ya Dowans tatizo litakwisha?.. HAPANA! mbona nawe unafikiri kama viongozi wetu mkuu wangu!..
 
Back
Top Bottom