Mchumi wa kati
Member
- Jun 21, 2021
- 34
- 29
Wanabodi,
Nashawishika kuamini kwamba kwa shughuli za kisiasa wanazozifanya CHADEMA kwa sasa katika jimbo la Segerea zinazotokana na mtaji mkubwa wa kisiasa ulichonacho chama hicho jimboni hapo.
Tumeshuhudia vuguvugu la kudai katiba mpya likianzishwa pale, na sasa ufunguzi wa ofisi ya chama huku kukiwa na mikakati mingi ya kusukuma agenda za kudai katiba mpya kutokea jimbo hilo.
Hii ni wazi kuwa chama hicho kinaungwa mkono na kinaamini kwamba kina wafuasi wa kutosha kuunga mkono juhudi hizo vinginevyo shughuli hizo zisingeelekezwa jimboni hapo.
Kwa upande mwingine, nauona udhaifu mkubwa wa CCM katika jimbo la Segerea ambao unabakia kuangalia tu michakato ya kujenga chama ikifanyikia kwenye uwanja wao.
Itoshe tu kusema CCM jimbo la Segera imelala usingizi wa pono tokea kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa karibu yote 2019 na uchaguzi wa ubunge mwaka 2020.
CCM haifanyi harakati zozote iwe za kisiasa au za maendeleo zaidi ya yale mambo ya lazima na yaliyoanza siku za nyuma kama ujenzi wa machinjio ya kisasa na barabara kuelekea machinjioni ambazo ni agenda zilizoanza kabla ya 2020.
Zaidi ya hapo miradi mingine ya kuliteka jimbo kama ujenzi wa barabara ya barakuda-maji chumvi, urudishaji wa maeneo yaliyoporwa kama soko la Liwiti, urasimishaji wa makazi yaliyoendelezwa n.k vikiwa havishughulikiwi kabisa.
Nikiri tu kwamba hata madiwani waliochaguliwa baadhi ya maeneo ya jimbo kama Liwiti hawafahamiki kwa wananchi, na hata mbunge Bonna Kamoli akiwa anaishi kama mbunge aliyeridhika huku akiwakimbia wananchi wake.
Ikumbukwe CHADEMA hawajawahi kushinda nafasi ya ubunge katika jimbo hilo ila walishinda kata zaidi ya asilimia 90%. Je, CHADEMA wana mtaji katika ngazi za chini ambayo inasababisha CCM kujikuta wakiwa watazamaji wa yanayofanyika?
Siku zote mambo ya harakati yakifanikiwa historia huandikwa, ni aibu kwa historia kuandikwa katika jimbo la Segerea. CCM amkeni.
Nashawishika kuamini kwamba kwa shughuli za kisiasa wanazozifanya CHADEMA kwa sasa katika jimbo la Segerea zinazotokana na mtaji mkubwa wa kisiasa ulichonacho chama hicho jimboni hapo.
Tumeshuhudia vuguvugu la kudai katiba mpya likianzishwa pale, na sasa ufunguzi wa ofisi ya chama huku kukiwa na mikakati mingi ya kusukuma agenda za kudai katiba mpya kutokea jimbo hilo.
Hii ni wazi kuwa chama hicho kinaungwa mkono na kinaamini kwamba kina wafuasi wa kutosha kuunga mkono juhudi hizo vinginevyo shughuli hizo zisingeelekezwa jimboni hapo.
Kwa upande mwingine, nauona udhaifu mkubwa wa CCM katika jimbo la Segerea ambao unabakia kuangalia tu michakato ya kujenga chama ikifanyikia kwenye uwanja wao.
Itoshe tu kusema CCM jimbo la Segera imelala usingizi wa pono tokea kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa karibu yote 2019 na uchaguzi wa ubunge mwaka 2020.
CCM haifanyi harakati zozote iwe za kisiasa au za maendeleo zaidi ya yale mambo ya lazima na yaliyoanza siku za nyuma kama ujenzi wa machinjio ya kisasa na barabara kuelekea machinjioni ambazo ni agenda zilizoanza kabla ya 2020.
Zaidi ya hapo miradi mingine ya kuliteka jimbo kama ujenzi wa barabara ya barakuda-maji chumvi, urudishaji wa maeneo yaliyoporwa kama soko la Liwiti, urasimishaji wa makazi yaliyoendelezwa n.k vikiwa havishughulikiwi kabisa.
Nikiri tu kwamba hata madiwani waliochaguliwa baadhi ya maeneo ya jimbo kama Liwiti hawafahamiki kwa wananchi, na hata mbunge Bonna Kamoli akiwa anaishi kama mbunge aliyeridhika huku akiwakimbia wananchi wake.
Ikumbukwe CHADEMA hawajawahi kushinda nafasi ya ubunge katika jimbo hilo ila walishinda kata zaidi ya asilimia 90%. Je, CHADEMA wana mtaji katika ngazi za chini ambayo inasababisha CCM kujikuta wakiwa watazamaji wa yanayofanyika?
Siku zote mambo ya harakati yakifanikiwa historia huandikwa, ni aibu kwa historia kuandikwa katika jimbo la Segerea. CCM amkeni.