Safari ya Andrew Chenge kuwania Uspika wa JMT

Wow nice pic!God bless you A chenge!MUNGU AKUKOMFORT KATIKA HIKI KIPINDI KIGUMU!
YOTE YANA MWISHO!IKOSHILA DUHU HAYA NI MAPITO TU KATIKA HII DUNIA!
Grazie!
Hollo

We actually dont need people like this warudisha maendeleo nyuma.
 
we stand by our bunge and speaker
nadhani spika huyu ni kiboko kwa jinsi anavyojua kucheza karata zake. kwanza kile kitendo cha kuruhusu ripoti ya mwakyembe kusomwa bungeni ni dalili kuwa hauymbishwi kama alivyokuwa msekwa......

chenge nadhani anaujuha fulani hata ukimwangalia ktk face yake anaonekana si mtu wa kurelay on...
 
Huu ni mwaka wa shetani kwa Chenge,atake asitake lazima aanguke tu,sasa kutafuta mtu wa kuanguka naye ni suala la mfa maji.

Hivi spika alimtuma kufanya ufisadi?
 
wanaomtetea chenge nisawa na wale waisifuyo mvua kwa kuwa imewanyea, bei zao ni ndogo mno!kwa kuwa wamevalishwa miwani za mbao ili wasione kinachoendelea, wanapishana na mama zao wakijifungua barabarani kwa kuwa hakuna hospitali, wanapishana na vibaka barabarani hata wakati mwingine kunyanganywa kamera zao, lakini hawaelewi kuwa vibaka hawa ni kundi lililozulumiwa kwa kukosa ajira kwa ajili ya ufisadi wa chenge na wenzao, wamevaa miwani za mbao na kuziba maskiko yao kwa pamba! msipoteze muda wenu kwa fedhuli hawa
 
Mhe.Chenge amedai kwamba Spika amemchafulia jina Nationally and Internationally.
He says he is going to push for a Parliamentary Disciplinary Committee to oversee this issue.
His Lawyers are going to act promptly.
Kivumbi hichooo!

Tuwaache waparurane wenyewe kwa wenyewe labda chama chao cha mafisadi kitasambaratika na hivyo kuleta mabadiliko makubwa katika anga za kisiasa Tanzania.
 
yetu macho na masikio . kwetu sisi ndio movie ilinaanza.wacha wachafuane mwisho wa siku ukweli utajulikana tu , who is responsible !!!
 
Tuwaache waparurane wenyewe kwa wenyewe labda chama chao cha mafisadi kitasambaratika na hivyo kuleta mabadiliko makubwa katika anga za kisiasa Tanzania.


Sawa Bubu. Ila inabidi kuweka chombezo kidogo kidogo ili kuparurana kwao kunoge zaidi. Tukiwaacha sana wataweka mikakati ya kula pamoja ndani wakati sisi tunasubiri nje kuwa hao ndani wanaparuana.
 
Wakuu,
Chenge ni fisadi lakini kwa hili la UCHAWI mimi nashindwa kumuhukumu kwani inahitaji uwe na imani ya KISHIRIKINA ili uweze kufanya hivo. Nashindwa ku-imagine hata hawa police wamedhamilia kufanya kitu gani cha maana baada ya uchunguzi wa ile sample ya vumbi lililopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa serikali!

Karibu kila Mtanzania anafahamu kwamba kuna tukio limejitokeza bungeni ambalo linahusishwa na imani za KISHIRIKINA. Kwa kifupi ni kwamba wabunge na baadhi ya watanzania wameamini kweli kwamba mzee wa vijisenti alikusudia ama kuwadhuru wabaya wake bungeni, au kujisafisha madhambi yake kwa njia ya KISHIRIKINA.

Ninachofahamu ni kwamba, Maabara ya Mkemia Mkuu haina vipimo vya UCHAWI kwa maana ya UCHAWI. Kitu pekee inachoweza kufanya ni kujua kama hilo vumbi ni KEMIKALI au la, na si vinginevo.

Pamoja na kwamba KEMIKALI inaweza ikatumika kwenye tendo la UCHAWI lakini pia nafahamu fika kwamba UCHAWI ni NGUVU ambayo ni MATOKEO au ni ZAO linaloweza kutokea baada ya kuchanganya KEMIKALI na IMANI ya KISHIRIKINA. IMANI YA KISHIRIKINA iliyokomaa ni kiungo muhimu sana hapa, vinginevo utaambulia kupata KEMIKALI tu na si UCHAWI.

Sisemi kwamba kilichotokea bungeni si uchawi, la hasha. Point na swali langu hapa ni kwamba, kama uchunguzi wa Maabara ya Mkemia Mkuu utabaini kweli kwamba lile VUMBI ni KEMIKALI, je, polisi watawezaje kusema waziwazi kwamba TUKIO LA MZEE WA VIJISENT LILIKUWA NI USHIRIKINA??!!

Ikumbukwe kwamba serikali yetu ya ccm kwa muda mrefu sasa imekuwa ikidai kwamba HAIAMINI USHIRIKINA! Pamoja na kutokuamini huko, ni ukweli uliowazi kwamba tumekuwa tukisikia au kushuhudia matukio mbalimbali yanayodhihilisha kwamba viongozi wetu wa SERIKALI WANAAMINI USHIRIKINA tena kwa kiwango cha juu. Mfano mzuri ni hili tukio ililotokea bungeni ambapo tumeshuhudia wengi wao wakiogopa hata kuingia kwenye ukumbi wao wa bunge kwa KUHOFIA USHIRIKINA WA MZEE WA VIJISENT!

Binafisi naishauli serikali na bunge kutunga sheria itakayosimamia kisheria IMANI YA USHIRIKINA ili wahusika wa ushirikina kama mzee wa vijisenti na wengine wote wanaowaua VIKONGWE huko Shinyanga na Mara waweze kushugulikiwa kisheria na HAKI itendeke. Vinginevo imani ya uchawi itazidi kushamiri na wachawi watazidi kutesa kwa kukumbatiwa na serikali ya ccm inayodai kutoutambua ushirikina.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
UCHAWI UCHAWI UCHAWI...
anyway tutakufa na wengine watazaliwa hakuna atakayeishi milele
 
KUHUSU UCHAWI, hata sisi hapa tunaamini hakuna uchawi, lakini tuanchosisitiza ni kuwa chenge yeye ndo muumini wa uchawi, ingawa uchawi haupo lakini chenge amepotoshwa na waganga wake wa bagamoyo. siku moja nikiwa nasoma katika mojawapo ya chuo kikuu cha nchi yetu, tulikuwa na mgomo. akaja waziri mmoja kutusilikiza tukampa sharti asije na principal wetu naye akakubali akamwambia principal usije. wakati mkutano ndo uko nusu na waziri huo, mara tukamwona principal ameingia mwenyewe. ndo tukaulizana kulikoni? ndipo mmojo wetu kwa utani aksema, principal alikuwa bagamoyo na mganga wake amemdanganya kuwa ukiingia kwenye ule mkutano hakuna atakaye kuona. chenge naye alidanganywa na sangoma ukienda kuweka hii dawa pale kwa spika na hawa na hawa wote watakuwa bubu tena utaendelea kupeta, hakuna atakaye uliza habari ya visenti wala richmond. tunamlaumu chenge mhitimu wa harvard kwa kujitumbukiza kwenye imani zinazoendelea kuwaua maalbino na wazee wetu hasa huko lake zone. lakini tunafarijika kuwa AMEUMBULIWA NA SANGOMA WAKE HUYO
 
Jamani ndugu zangu hili BUNGE LA CCM iliyogawanyika hivyo litayatetea vipi maslahi ya wananchi?
Ni wazi kuna makundi humo CCM ambayo yamepelkea conflict of interests kwenye maamuzi yao humo bungeni kiasi cha kuwa kama shule ya sekondari inayojiandaa kwa mgomo na wala si mahali pa takatifu ambapo mustakabali wa nchi huamuliwa kwa mawazo yao na vitendo vyao.
Waturudishie watu nyumbani bana...This is too much wanaweza wakauana..Niliwaambia huko nyuma wawakamate...Lakini sasa wameshawapa muda na kibri cha kujitetea hata ndani ya bunge letu tukufu.
 
anayechafuliwa jina ni aliyemsafi na si mchafu kama Chenge
bado ni mtuhumiwa tu ,mpaka ithibitike si umeona akina Lowasa sasa eti wamikuwa wasafi baadaya kusafishwa na Chama chao Chama Cha Matopasi.
 
BUNGE NDIO LAST OPTION...Ujumbe wangu kwa wale wabunge wa CCM wasiomuunga mkono Mama Anna Kilango ni huu...Mwelekeo wao ni mbaya kwani mwisho wake kwao waweza kuwa si mzuri.
 
wanaomtetea chenge nisawa na wale waisifuyo mvua kwa kuwa imewanyea, bei zao ni ndogo mno!kwa kuwa wamevalishwa miwani za mbao ili wasione kinachoendelea, wanapishana na mama zao wakijifungua barabarani kwa kuwa hakuna hospitali, wanapishana na vibaka barabarani hata wakati mwingine kunyanganywa kamera zao, lakini hawaelewi kuwa vibaka hawa ni kundi lililozulumiwa kwa kukosa ajira kwa ajili ya ufisadi wa chenge na wenzao, wamevaa miwani za mbao na kuziba maskiko yao kwa pamba! msipoteze muda wenu kwa fedhuli hawa

Mkuu! Haya yote yana uhusiano gani na tuhuma za ulozi? Sidhani kama kuna mtu anayemtetea kuhusu suala la vijisenti. Tunachosema wengine ni kuwa hili la ulozi limekaa vibaya. Sasa kwa kusema hivyo unatutuhumu na hayo mengine? Wapi na wapi, Mkuu!
 
siyo mambo yote yanayosemwa ni uchawi yanahusiana na mashetani au visivyoelezeka kisayansi. Kuna mambo yanayofanywa na wachawi lakini msingi wake uko katika sayansi.
 
Wacha wakabane , lakini Spika kuna kitu kafanya ama kasema kuhusiana na Chenge ama ndiyo bifu za kuachia mjadala wa Richmonduli ?
 
Wacha wakabane , lakini Spika kuna kitu kafanya ama kasema kuhusiana na Chenge ama ndiyo bifu za kuachia mjadala wa Richmonduli ?

Chenge hakufurahishwa na kauli ya Sitta kuwa watawashughulikia mafisadi huko bungeni.
Na ndio maana Chenge akatumia VITISHO ili bunge lisiyajadili madhambi yoyote ya mafisadi.
Thats my take for now...Tunasubiri kuona kama watakamatana.
 
Chenge hakufurahishwa na kauli ya Sitta kuwa watawashughulikia mafisadi huko bungeni.
Na ndio maana Chenge akatumia VITISHO ili bunge lisiyajadili madhambi yoyote ya mafisadi.
Thats my take for now...Tunasubiri kuona kama watakamatana.

Hawawezi kumpata Mhe. Sitta, ebo kumtisha ili mafisadi wasishughulikiwe! wamechemsha. Mambo yanayotokea Tanzania sasa ni mkono wa Mungu si wa mwanadamu. Ndiyo maana wajanja wamesoma nyakati na kuunga mkono vita dhidi ya ufisadi.

Lakini inashangaza, kuna wabunge wanaona hakuna ufisadi tanzania, akina Serukamba, siamini!!
 
Back
Top Bottom