MMM,
Kutaka Kikwete asigombee si ni KINYUME cha "UTARATIBU" wetu CCM? Au?
Mkuu,
Sidhani kama kuna mtu ambaye amemilikishwa uongozi wa maisha nchini kwetu,hivyo basi kila mtu anayo haki kabisa kikatiba kugombea nafasi yeyote ile kwenye uchaguzi ili mradi tu awe ametimiza minimum requirements.Huwezi ukanishawishi kuwa hata kama mtu amechemsha kipindi chake cha uongozi,apewe tu 'eti' kwa sababu 'UTARATIBU' ni kuwa lazima vipindi viwili(2) amalize.Tukifuata misingi hii tutaendelea kujenga taifa lisilo na misingi imara.Tukubali kuwa demokrasia ya kweli ni kukubali pia kupingwa.Usipokubali haya basi hautokuwa tofauti sana na dikteta.Kuna nini cha kuogopa mpaka tusikubali wagombea wengine?Kama kweli mtu yupo makini na rekodi yake ni nzuri(kwa kulinganisha mafanikio aliyoyapata kwenye kipindi chake cha kwanza na ahadi alizozitoa)then atadhibitisha kwenye kinyang'anyiro na siyo kukubali tu matokeo kuwa aendelee.
Kuendesha vyama kidikteta sio pia demokrasia.Kwani demokrasia inaanzia ndani na kuonekana nje.Kama ndani ya chama ndio kama haya,unategemea kweli nje mtu ataonekana anahubiri demokrasia?Hapa itakuwa ni kujidanganya na kudanganya wananchi.Kila mtu ana mtizamo wake na he/she is entitled to it.Kila mtu basi yupo responsible kutetea mtizamo wake kwa kutoa maelezo anayoona yana-support huo mtizamo.
Tusijenge tena msingi wa matope tena tukitegemea kuwa kesho utakuwa wa saruji!
Nawasilisha.