Ruhusa kwa Madaktari Kufanya Kazi Binafsi Katika Hospitali za Umma Kutaleta Matabaka

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
610
1,540
Julai 11, 2023, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa ziarani mkoani Simiyu, alitoa ruhusa rasmi kwa madaktari nchini walioajiriwa na Serikali kufanya kazi binafsi kwanye hospitali za umma baada ya muda wao wa kazi kwisha. Waziri Ummy alitoa maelekezo hayo wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu. ACT-Wazalendo kupitia Ofisi ya Wasemaji wa Kisekta tumefanyia tafakuri ya kina maamuzi haya na athari zake kwa lengo la upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wote.

Ufinyu wa mishahara na maslahi kwenye sekta ya afya hasa kwenye vituo vya afya vya Umma husababisha wafanyakazi wachache wa sekta hiyo kulazimika kufanya kazi za ziada kwenye vituo vya afya vya binafsi ili kuweza kujiongezea kipato. Hali hii inaongeza upungufu wa wafanyakazi wa afya kwenye vituo vya afya vya umma, anayeumia ni mwananchi mwenye kipato kidogo.

Muda wa kazi kwa wafanyakazi wa afya hususani madaktari na manesi ni kwa mfumo wa zamu za kazi. Wafanyakazi hawa wanapomaliza zamu zao wanapaswa kupumzika kusubiri zamu nyingine badala ya kuhangaika kujipatia kipato. Uchovu wa wafanyakazi wa afya ni kigezo kikubwa kwenye utoaji wa huduma bila ufanisi na kwa ubaguzi, wenye nacho wakipewa kipaumbele zaidi ya wasionacho; hali inayoongeza matabaka katika upatikanaji wa huduma za Afya.

Baada ya saa za kawaida za kazi kuna wagonjwa wanaoenda kutafuta huduma kwenye vituo vya afya vya umma, kugeuza vituo hivyo kama sehemu ya binafsi ni kumnyima huduma mwananchi asie na fedha za kulipia huduma binafsi. Hii si haki kwani mwananchi analipia huduma hizo kupitia kodi mbalimbali.

Kiini cha huduma mbaya za afya nchini ni mfumo usiofaa uliopo wa kugharamia huduma za afya; mfumo unalaozimisha wananchi walipie huduma kutoka mifukoni mwao. Huu ni mzigo kwa mwananchi hasa aliye kwenye kundi kubwa la wenye kipato kidogo waliojiari katika sekta isiyo rasmi. Aidha, mfumo huu unaikosesha Serikali mapato ya kutosha kuendeleza huduma za afya. Serikali imeacha mzigo wa gharama za huduma ya Afya kwa mwananchi.



Agizo la Waziri wa Afya litakwenda kuharibu kabisa mfumo wa utoaji huduma za Afya kwa Umma. Mfumo mzima wa utoaji wa huduma za afya umegubikwa na changamoto za upungufu wa wataalamu, mazingira duni ya kufanyia kazi, upungufu wa miundombinu na uhaba wa dawa na vifaa tiba. Changamoto hizi zitaweza kutatuliwa kwa urahisi zaidi pindi tukiwa na mfumo bora wa kugharamia huduma za afya na usimamizi wa fedha.

Mapendekezo ya ACT Wazalendo.
Serikali isitishe maramoja utaratibu huu mpya wa wafanyakazi walioajiriwa na Serikali kutoa huduma za afya binafsi kwenye vituo vya afya vya Serikali. Badala yake ije na mbinu za kuboresha huduma za afya na mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa sekta ya afya kwa Umma.

ACT Wazalendo tumependekeza mfumo wa kufungamanisha bima ya afya na mfuko wa hifadhi ya jamii, ambapo kila mwanachama atapata Fao la bima ya Afya. huu ni mfumo wa kugharamia huduma za afya kwa kujiwekea akiba, tofauti na mfumo uliopo wa matumizi pekee. Mfumo tunaoupendekeza unakidhi vigezo vya mfumo unaopendekezwa kimataifa wa kuwezesha kuboresha afya ya jamii sambamba na kupunguza umaskini, kuongeza ajira na kukuza uchumi ili kufikia lengo la Afya kwa wote.

Mfumo wa Kufungamanisha Bima ya Afya na Hifadhi ya jamii utaondoa matabaka katika upatikanaji wa huduma za Afya kwa makundi yote; kundi la wenye Ajira Rasmi, kundi la wasio na ajira Rasmi kama vile wakulima, wavuvi, wafanyabiashara na kundi la wasio na uwezo kabisa kama wazee na wenye ulemavu Makundi yote yatachangia kwenye Skimu ya hifadhi ya jamii kulingana na uwezo wao na watapata huduma kulingana na mahitaji yao bila ubaguzi wala matabaka.

Hitimisho
ACT Wazalendo inaamini katika kuzingatia haki na usawa kwa wote katika kupata huduma za Afya ili kufikia lengo la Afya kwa Wote na kusisitiza umuhimu wa wafanyakazi wa afya kufanya kazi katika mazingira wezeshi, kupata mshahara wa kutosha, na mapumziko ya kutosha kabla ya kubadilisha zamu za kazi, ili kuwewawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi. Haya yatafanikiwa kwa kuwepo na mfumo bora wa kugharamia huduma za afya.

Mfumo tunaoupendekeza ACT Wazalendo ni wa kuunganisha Hifadhi ya Jamii na Bima ya Afya. Mfumo huu utamwezesha kila Mtanzania kuwa na Bima ya Afya itakayompa uhakika wa matibabu, afya bora na kumuinua kiuchumi. Halikadhalika mfumo huu utawezesha kuboresha mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa afya.

Imetolewa na;
Dr Elizabeth Sanga
Twitter: @DrBSanga
Waziri Kivuli wa Afya - ACT Wazalendo.
Julai 15, 2023
 
Julai 11, 2023, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa ziarani mkoani Simiyu, alitoa ruhusa rasmi kwa madaktari nchini walioajiriwa na Serikali kufanya kazi binafsi kwanye hospitali za umma baada ya muda wao wa kazi kwisha. Waziri Ummy alitoa maelekezo hayo wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu. ACT-Wazalendo kupitia Ofisi ya Wasemaji wa Kisekta tumefanyia tafakuri ya kina maamuzi haya na athari zake kwa lengo la upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wote.

Ufinyu wa mishahara na maslahi kwenye sekta ya afya hasa kwenye vituo vya afya vya Umma husababisha wafanyakazi wachache wa sekta hiyo kulazimika kufanya kazi za ziada kwenye vituo vya afya vya binafsi ili kuweza kujiongezea kipato. Hali hii inaongeza upungufu wa wafanyakazi wa afya kwenye vituo vya afya vya umma, anayeumia ni mwananchi mwenye kipato kidogo.

Muda wa kazi kwa wafanyakazi wa afya hususani madaktari na manesi ni kwa mfumo wa zamu za kazi. Wafanyakazi hawa wanapomaliza zamu zao wanapaswa kupumzika kusubiri zamu nyingine badala ya kuhangaika kujipatia kipato. Uchovu wa wafanyakazi wa afya ni kigezo kikubwa kwenye utoaji wa huduma bila ufanisi na kwa ubaguzi, wenye nacho wakipewa kipaumbele zaidi ya wasionacho; hali inayoongeza matabaka katika upatikanaji wa huduma za Afya.

Baada ya saa za kawaida za kazi kuna wagonjwa wanaoenda kutafuta huduma kwenye vituo vya afya vya umma, kugeuza vituo hivyo kama sehemu ya binafsi ni kumnyima huduma mwananchi asie na fedha za kulipia huduma binafsi. Hii si haki kwani mwananchi analipia huduma hizo kupitia kodi mbalimbali.

Kiini cha huduma mbaya za afya nchini ni mfumo usiofaa uliopo wa kugharamia huduma za afya; mfumo unalaozimisha wananchi walipie huduma kutoka mifukoni mwao. Huu ni mzigo kwa mwananchi hasa aliye kwenye kundi kubwa la wenye kipato kidogo waliojiari katika sekta isiyo rasmi. Aidha, mfumo huu unaikosesha Serikali mapato ya kutosha kuendeleza huduma za afya. Serikali imeacha mzigo wa gharama za huduma ya Afya kwa mwananchi.



Agizo la Waziri wa Afya litakwenda kuharibu kabisa mfumo wa utoaji huduma za Afya kwa Umma. Mfumo mzima wa utoaji wa huduma za afya umegubikwa na changamoto za upungufu wa wataalamu, mazingira duni ya kufanyia kazi, upungufu wa miundombinu na uhaba wa dawa na vifaa tiba. Changamoto hizi zitaweza kutatuliwa kwa urahisi zaidi pindi tukiwa na mfumo bora wa kugharamia huduma za afya na usimamizi wa fedha.

Mapendekezo ya ACT Wazalendo.
Serikali isitishe maramoja utaratibu huu mpya wa wafanyakazi walioajiriwa na Serikali kutoa huduma za afya binafsi kwenye vituo vya afya vya Serikali. Badala yake ije na mbinu za kuboresha huduma za afya na mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa sekta ya afya kwa Umma.

ACT Wazalendo tumependekeza mfumo wa kufungamanisha bima ya afya na mfuko wa hifadhi ya jamii, ambapo kila mwanachama atapata Fao la bima ya Afya. huu ni mfumo wa kugharamia huduma za afya kwa kujiwekea akiba, tofauti na mfumo uliopo wa matumizi pekee. Mfumo tunaoupendekeza unakidhi vigezo vya mfumo unaopendekezwa kimataifa wa kuwezesha kuboresha afya ya jamii sambamba na kupunguza umaskini, kuongeza ajira na kukuza uchumi ili kufikia lengo la Afya kwa wote.

Mfumo wa Kufungamanisha Bima ya Afya na Hifadhi ya jamii utaondoa matabaka katika upatikanaji wa huduma za Afya kwa makundi yote; kundi la wenye Ajira Rasmi, kundi la wasio na ajira Rasmi kama vile wakulima, wavuvi, wafanyabiashara na kundi la wasio na uwezo kabisa kama wazee na wenye ulemavu Makundi yote yatachangia kwenye Skimu ya hifadhi ya jamii kulingana na uwezo wao na watapata huduma kulingana na mahitaji yao bila ubaguzi wala matabaka.

Hitimisho
ACT Wazalendo inaamini katika kuzingatia haki na usawa kwa wote katika kupata huduma za Afya ili kufikia lengo la Afya kwa Wote na kusisitiza umuhimu wa wafanyakazi wa afya kufanya kazi katika mazingira wezeshi, kupata mshahara wa kutosha, na mapumziko ya kutosha kabla ya kubadilisha zamu za kazi, ili kuwewawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi. Haya yatafanikiwa kwa kuwepo na mfumo bora wa kugharamia huduma za afya.

Mfumo tunaoupendekeza ACT Wazalendo ni wa kuunganisha Hifadhi ya Jamii na Bima ya Afya. Mfumo huu utamwezesha kila Mtanzania kuwa na Bima ya Afya itakayompa uhakika wa matibabu, afya bora na kumuinua kiuchumi. Halikadhalika mfumo huu utawezesha kuboresha mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa afya.

Imetolewa na;
Dr Elizabeth Sanga
Twitter: @DrBSanga
Waziri Kivuli wa Afya - ACT Wazalendo.
Julai 15, 2023
Tamko la kipumbavu.


Unaanza na stori za MaDaktari bingwa kufanya kazi kwenye hospital binafsi au kutumia vituo vya umma kufanya kazi binafsi.


Halafu unamalizia na gharama za matibabu kwa wananchi, na kupendekeza Mfumo wa Bima ya Afya kufungamanisha na mfumo wa hifadhi ya Jamii.

Kwahiyo ukifungamanisha bima na hifadhi ndio utaboresha Maslahi ya MaDaktari bingwa ili waache kufanya kazi kwenye kliniki binafsi????

Unachanganya vitu viwili kwa pamoja kipuuzi
 
Shida ni yule mwanamke mropokaji alivyoiongea na namna alivyotoa kibali as if ni swala jepesi kweli.

Natoa ruksa kuanzia sasa, what a stupid woman atakwenda kuuwa watu.

Hao wanaofanya hivyo kama Muhimbili na kwengine duniani ni University hospitals ndio wana haya mambo ya intramural practice (lengo hasa ni walimu wasipoteze practice skills), sisi waafrica tushageuza na kuona fursa ya kibiashara kwa kila mtu.

Pamoja na hayo misingi ya intramural practice inasimamiwa na taasisi husika, obvious kutakuwa na services costing za huduma za afya daktari analipia gharama za upande wa taasisi.

Ni mambo ambayo yapo well planned, regulated and supervised na taasisi husika. Ni kama vile services za hospitali za kawaida tu sema ukienda kumuona Dr muda huo ni more pay kwa utashi wako.

Shida ni namna alivyo ropoka na kutoa ruksa as if ni mambo yanayofanyika kirahisi wakati yapo well planned na hospitali inaamua aina ya huduma zinazoweza tolewa na mfumo ambao umepangwa vizuri and supervised.

Lenyewe natoa ruksa kuanzia leo, without the supervision mechanism in place, aina ya huduma hospitali inayoruhusu; just a stupid woman lililojiropokea tu.
 
acheni wapumue wanateseka sana, wanasheria nk mbona hamuwasemi. Acha wafaid matunda ya kazi zao walizosoma kwa tabu. Mnawaendesha sana..
 
Nadhani point zimekuwa diluted na maelezo mengi hivyo wengine kuona umeandika upupu lakini kuna points muhimu chache...

Hospital ni pamoja na facilities; na madaktari wanalipwa kulingana na muda wanaofanya hapo....

Sasa kama muda wao umekwisha wanahitaji kupumzika (sitaki kuongelea issue ya kama mteja anapata uangalizi tosha kwa mtu aliyechoka / overtime) ila nitaongelea facilities....

Sasa kama facilities ni mali ya mpaka wale ambao hawana uwezo wa kumuona mtatibu private je ni haki huyu mtabibu kutumia facilities za hawa watu wasioweza kulipa ili kuhudumia hawa wanaolipa ?; Je hii haitaleta Msongamano ambao tayari upo kwa kukosa facilites

Na je wale wanaolipa pesa yao ili wapate Premium Service watapata ile Premium Service kwa kusongamana na wale wa huduma za jumla jumla ?

In Short agizo lile sidhani kama lina ufanisi zaidi ya kuwa tamko la Kisiasa...
 
Nadhani point zimekuwa diluted na maelezo mengi hivyo wengine kuona umeandika upupu lakini kuna points muhimu chache...

Hospital ni pamoja na facilities; na madaktari wanalipwa kulingana na muda wanaofanya hapo....

Sasa kama muda wao umekwisha wanahitaji kupumzika (sitaki kuongelea issue ya kama mteja anapata uangalizi tosha kwa mtu aliyechoka / overtime) ila nitaongelea facilities....

Sasa kama facilities ni mali ya mpaka wale ambao hawana uwezo wa kumuona mtatibu private je ni haki huyu mtabibu kutumia facilities za hawa watu wasioweza kulipa ili kuhudumia hawa wanaolipa ?; Je hii haitaleta Msongamano ambao tayari upo kwa kukosa facilites

Na je wale wanaolipa pesa yao ili wapate Premium Service watapata ile Premium Service kwa kusongamana na wale wa huduma za jumla jumla ?

In Short agizo lile sidhani kama lina ufanisi zaidi ya kuwa tamko la Kisiasa...
Shida ni namna alivyoilezea yeye mara ya kwanza.

Patient safety, quality ya huduma inayotolewa, medical procedures na kila muongozo wa afya unabaki under the hospital supervision.

Kinachofanyika ‘after hours’ services cost zote za hospitali mgonjwa atakazo tumia anatozwa independently + higher charges za kumuona Dr muda huo.

Ni kwamba ukienda muda wa kawaida ukitaka kumuona Dr fulani you have to wait on the queue, lakini ukienda ‘after hours’ at premium charge unaweza kumuona kirahisi and that’s what all it is.

Sio kwamba daktari ‘after hours’ anakuwa na clinic yake anaendesha mwenyewe kama alivyosema mara ya kwanza. More like overtime ambayo Dr anaamua malipo yake + service costs za huduma mgonjwa atakazopewa.

Overall it’s not a good idea to normalise na kuna mambo kadhaa ya ku control conflict of interest.

Chimbuko lake ni university hospitals kuwapa fursa Md.Dr wanaofundisha full kuendelea ku practice medicine part time.

Ni mfumo ambao wizara ilitakiwa ku-regulate before rolling out nationwide. Wanaotaka kuanza kufanya hivyo management ikajifunze Muhimbili au taasisi zingine zenye mfumo huo tayari.

Lakini yeye katoa kauli ya hatari sana as if ni jambo ambalo hospitali yeyote zisizo na experience na huo mfumo na wenyewe wanaweza lianzisha ata kesho tu, so reckless.
 
Shida ni namna alivyoilezea yeye mara ya kwanza.

Patient safety, quality ya huduma inayotolewa, medical procedures na kila muongozo wa afya unabaki under the hospital supervision.
Even when this chap is operating / working in his own private venture ? Does he / she pay for the facilities ?
Kinachofanyika ‘after hours’ services cost zote za hospitali mgonjwa atakazo tumia anatozwa independently + higher charges za kumuona Dr muda huo.
Indeed; but how does the hospital benefit for its premises to be used ?
Ni kwamba ukienda muda wa kawaida ukitaka kumuona Dr fulani you have to wait on the queue, lakini ukienda ‘after hours’ at premium charge unaweza kumuona kirahisi and that’s what all it is.
But the Hospital operates for 24 Hours au Hospitali kuna muda wa kuugua na kumuona daktari kwamba ikiwa jioni basi wewe muda wako umekwisha (if that is the case wagonjwa ambao wanalipia Bima na matozo yote wanakuwa short changed na kama wahudumu hawatoshi its about time waongezwe...
Sio kwamba daktari ‘after hours’ anakuwa na clinic yake anaendesha mwenyewe kama alivyosema mara ya kwanza. More like overtime ambayo Dr anaamua malipo yake + service costs za huduma mgonjwa atakazopewa.
At Hospital Premises ? katika mapato yake anawalipa rent Hospitali ?; Na kwanini tuweke After hours kwa hospital na sio kwa mtu - Kwamba Hospital ni 24 Hours.... Kama kumbe kuna wateja after official hours kwanini Hospital isiwahudumie hao wateja ? Kama issue hakuna manpower mbona vyuo vinatema watu kila mwaka ?!!!
 
acheni wapumue wanateseka sana, wanasheria nk mbona hamuwasemi. Acha wafaid matunda ya kazi zao walizosoma kwa tabu. Mnawaendesha sana..
Kwamba wanasheria wanatumia kale kaofisi kuona wateja wao binafsi baada ya muda wa kazi ? Kaofisi ambako kanakuwa shared na wengine ili waweze kupata huduma hio hio
 
Even when this chap is operating / working in his own private venture ? Does he / she pay for the facilities ?

Indeed; but how does the hospital benefit for its premises to be used ?

But the Hospital operates for 24 Hours au Hospitali kuna muda wa kuugua na kumuona daktari kwamba ikiwa jioni basi wewe muda wako umekwisha (if that is the case wagonjwa ambao wanalipia Bima na matozo yote wanakuwa short changed na kama wahudumu hawatoshi its about time waongezwe...

At Hospital Premises ? katika mapato yake anawalipa rent Hospitali ?; Na kwanini tuweke After hours kwa hospital na sio kwa mtu - Kwamba Hospital ni 24 Hours.... Kama kumbe kuna wateja after official hours kwanini Hospital isiwahudumie hao wateja ? Kama issue hakuna manpower mbona vyuo vinatema watu kila mwaka ?!!!
Ni kama kufanya overtime tu, sasa badala ya hospital kukupangia mshahara wa overtime unajiamualia mwenyewe ila kwa wagonjwa ambao wapo tayari kukulipa hiyo extra.

Mengine yote yale yale ya hospitali, kwenye bill ya mgonjwa inajumlisha muda wa Dr (anachukua yeye) + hospital other services costs (wanachukua hospitali).

Na utaratibu wote unasimamiwa na hospitali sio kwamba daktari anajiendeshea tu. Halafu ni kwa baadhi ya huduma tu sio kila huduma na hospitali ndio inaamua ni huduma gani.

Shida ni alivyoileta na namna alivyotoa ruksa ndio wengi wetu tukashtuka. Halafu sio busara kila hospitali kuanza huo mfumo bila ya management kwenda kujifunza muhimbili kwanza.

Logic ni kwamba walau ichukue mwaka ndio iwe rolled nationwide if it is necessary. Maana lazima wajifunze kwa wengine wenye hiyo mifumo, kwa sababu ni national policy wizara iweke regulations na lazima hospitali zitengeneze kanuni za huo mfumo na usimamizi wake wa ndani, kuweka pilot schemes kupima ufanisi kama hakuna athari kwa huduma za hospitali.

Ni hivi yule dada pale wanalazimisha tu government policies aren’t announced carelessly kama alivyofanya na kuweza kuharibu huduma za afya pamoja na kuhatarisha maisha ya watu.
 
Ni kama kufanya overtime tu, sasa badala ya hospital kukupangia mshahara wa overtime unajiamualia mwenyewe ila kwa wagonjwa ambao wapo tayari kukulipa hiyo extra.

Mengine yote yale yale ya hospitali, kwenye bill ya mgonjwa analipia muda wa Dr + hospital other services costs (huduma zingine za hospitali atakazopewa).

Na utaratibu wote unasimamiwa na hospitali sio kwamba daktari anajiendeshea tu. Halafu ni kwa baadhi ya huduma tu sio kila huduma na hospitali ndio inaamua ni huduma gani.

Shida ni alivyoileta na namna alivyotoa ruksa ndio wengi wetu tukashtuka. Halafu sio busara kila hospitali kuanza huo mfumo bila ya management kwenda kujifunza muhimbili kwanza.

Logic ni kwamba walau ichukue mwaka ndio iwe rolled nationwide if it is necessary. Maana lazima wajifunze kwa wengine wenye hiyo mifumo, kwa sababu ni national policy wizara iweke regulations na lazima hospitali zitengeneze kanuni za huo mfumo na usimamizi wake wa ndani, kuweka pilot schemes.

Ni hivi yule dada pale wanalazimisha tu government policies aren’t announced carelessly kama alivyofanya na kuweza kuharibu huduma za afya na kuhatarisha maisha ya watu.
Okay ni kama nimekupata kidogo.., sijafanya research je bottleneck katika huduma bado ni experts i.e. Madaktari au na hizo facilities bado zina tatizo / hazitoshi (yaani Madaktari wanaweza kutaka kuona watu kumbe vyumba / facilities hazitoshi....

Mbili hivi muda wa clinic huwa ni day time (yaani saa 12 na sio 24 hours) Je hatuwezi tukaongeza ukawa hata mpaka saa 6 usiku (ningesema 24 hours ila huenda wagonjwa kufika usiku wa manane huenda ikawa shida kurudi kwao)

Tatu unaonaje haya mambo mengine ya diagnosis yasifanywe hata na nurse kwa msaada wa Diagnosis softwares nadhani hapo tungepunguza muda wa madaktari kutumia muda wao kwa vitu basic / procedural issues....

Ingawa point yako nimeipata kwa mbali na kama ndivyo basi ni shida ya wanasiasa kuongelea issues mwisho wa siku wanaharibu ili tu wapate political mileage
 
Shida ni yule mwanamke mropokaji alivyoiongea na namna alivyotoa kibali as if ni swala jepesi kweli.

Natoa ruksa kuanzia sasa, what a stupid woman atakwenda kuuwa watu.

Hao wanaofanya hivyo kama Muhimbili na kwengine duniani ni University hospitals ndio wana haya mambo ya intramural practice (lengo hasa ni walimu wasipoteze practice skills), sisi waafrica tushageuza na kuona fursa ya kibiashara kwa kila mtu.

Pamoja na hayo misingi ya intramural practice inasimamiwa na taasisi husika, obvious kutakuwa na services costing za huduma za afya daktari analipia gharama za upande wa taasisi.

Ni mambo ambayo yapo well planned, regulated and supervised na taasisi husika. Ni kama vile services za hospitali za kawaida tu sema ukienda kumuona Dr muda huo ni more pay kwa utashi wako.

Shida ni namna alivyo ropoka na kutoa ruksa as if ni mambo yanayofanyika kirahisi wakati yapo well planned na hospitali inaamua aina ya huduma zinazoweza tolewa na mfumo ambao umepangwa vizuri and supervised.

Lenyewe natoa ruksa kuanzia leo, without the supervision mechanism in place, aina ya huduma hospitali inayoruhusu; just a stupid woman lililojiropokea tu.
Huyo Waziri wenu ana kimdomo Kama chuchunge.


Anachojua ni kubweka bweka na kumsifia Samia kwenye Media akijua ndio uchapakazi
 
Okay ni kama nimekupata kidogo.., sijafanya research je bottleneck katika huduma bado ni experts i.e. Madaktari au na hizo facilities bado zina tatizo / hazitoshi (yaani Madaktari wanaweza kutaka kuona watu kumbe vyumba / facilities hazitoshi....

Mbili hivi muda wa clinic huwa ni day time (yaani saa 12 na sio 24 hours) Je hatuwezi tukaongeza ukawa hata mpaka saa 6 usiku (ningesema 24 hours ila huenda wagonjwa kufika usiku wa manane huenda ikawa shida kurudi kwao)

Tatu unaonaje haya mambo mengine ya diagnosis yasifanywe hata na nurse kwa msaada wa Diagnosis softwares nadhani hapo tungepunguza muda wa madaktari kutumia muda wao kwa vitu basic / procedural issues....

Ingawa point yako nimeipata kwa mbali na kama ndivyo basi ni shida ya wanasiasa kuongelea issues mwisho wa siku wanaharibu ili tu wapate political mileage
Shida ni huyo dada kupewa wizara technical yeye anaelezea mambo kirahisi sana na kuropoka natoa ruksa kuanzia leo.

Wakati wanaofanya hivyo kuna mechanism in place on how it works and hospital management still holds the role of supervision.

Nadhani badala ya kuwapa watu overtime hours ili kupunguza bottle neck ya watu wanaotaka kukutana na consultants. Wamechagua huo mfumo wa intramural wale wenye pesa wakitaka kuruka queue wanaweza kuwaona madaktari on their free time with extra costs.

Kwa sasa ni taasisi chache zinazo fanya hivyo, if you are gonna role out nationwide wizara inatakiwa kuweka policy rasmi na kutunga kanuni or else kutakuwa na variations kwenye hiyo mifumo na inaweza kuwa hatari.

Basically if you ask me hiyo wizara inahitaji technocrat to sort the mess zilizopo afya.
 
Huyo Waziri wenu ana kimdomo Kama chuchunge.


Anachojua ni kubweka bweka na kumsifia Samia kwenye Media akijua ndio uchapakazi
Ndio shida yake na anadhani wanaompinga wana personal issues nae. Bila ya kuelewa hiyo wizara ni technical na sio sehemu ya kujiropokea tu.

Afya ni sector pekee duniani ambayo ni highly regulated practice wise, with a pyramid organisation structure kutoka wizarani watu awajifanyii tu mambo at service level bila ya miongozo ya wizara au sheria za nchi.
 
Ndio shida yake na anadhani wanaompinga wana personal issues nae. Bila ya kuelewa hiyo wizara ni technical na sio sehemu ya kujiropokea tu.

Afya ni sector pekee duniani ambayo ni highly regulated practice wise with a pyramid organisation structure kutoka wizarani watu awajifanyii tu mambo at service level bila ya miongozo.
Kama ni mfuatiliaji utagundua kuwa:

Kwasasa serikali inajitoa kwenye kila kitu, ibaki na URATIBU na UDHIBITI tu.

Watawala hawataki kabisa stress za kufikiria, kila mmoja anataka abaki KULA BATA tu na kuzurula.

Sasa hivi, serikali imejitoa kabisa kwenye kugharamia matibabu ya watu.

Gharama za Uendeshaji wa sekta ya Afya zinategemea.

- NHIF ( inayokaribia kufa)

- User fees ( wanaolipa cash)

- iCHF ( vibima vya mchongo,vijijini)

- Busket funds ( Pesa ya wafadhili)


Kwenye makusanyo hayo,ndio MaDaktari wanatakiwa kulipa:

  • Watu wa usafi
  • Walinzi
  • Maji
  • Umeme
  • Extra duty
  • Kuajiri vibarua wa kujitolea
  • Kununua dawa na vifaa tiba

Na Kwasababu, kazi za serikali hazilipi na mazingira ya kazi ni magumu, wanaona Intramural ndio suluhisho la kufanya specialist wafanye kazi serikalini.

Yaani Sasa hivi serikali Ina visystem vidogo vidogo viiiiingi ambavyo haviingiliani, na kila kitaasisi kinahamasisha kukusanya mapato ili kitumie kwenye shughuli zake za Uendeshaji.


Kwasababu serikali kuu haina muda huo, na ndio maana changamoto ngazi ya chini haziishi na Rais anakuwa na fungu la pesa kibao hazina kazi mpaka anaamua kuhonga Wanasiasa, machawa na kununua magoli.

Maana changamoto za afya, barabara, shule, vituo vya afya ni hiari yake kuboresha au kuacha.
 
Kama ni mfuatiliaji utagundua kuwa:

Kwasasa serikali inajitoa kwenye kila kitu, ibaki na URATIBU na UDHIBITI tu.

Watawala hawataki kabisa stress za kufikiria, kila mmoja anataka abaki KULA BATA tu na kuzurula.

Sasa hivi, serikali imejitoa kabisa kwenye kugharamia matibabu ya watu.

Gharama za Uendeshaji wa sekta ya Afya zinategemea.

- NHIF ( inayokaribia kufa)

- User fees ( wanaolipa cash)

- iCHF ( vibima vya mchongo,vijijini)

- Busket funds ( Pesa ya wafadhili)


Kwenye makusanyo hayo,ndio MaDaktari wanatakiwa kulipa:

  • Watu wa usafi
  • Walinzi
  • Maji
  • Umeme
  • Extra duty
  • Kuajiri vibarua wa kujitolea
  • Kununua dawa na vifaa tiba

Na Kwasababu, kazi za serikali hazilipi na mazingira ya kazi ni magumu, wanaona Intramural ndio suluhisho la kufanya specialist wafanye kazi serikalini.

Yaani Sasa hivi serikali Ina visystem vidogo vidogo viiiiingi ambavyo haviingiliani, na kila kitaasisi kinahamasisha kukusanya mapato ili kitumie kwenye shughuli zake za Uendeshaji.


Kwasababu serikali kuu haina muda huo, na ndio maana changamoto ngazi ya chini haziishi na Rais anakuwa na fungu la pesa kibao hazina kazi mpaka anaamua kuhonga Wanasiasa, machawa na kununua magoli.

Maana changamoto za afya, barabara, shule, vituo vya afya ni hiari yake kuboresha au kuacha.
Kuna ukweli fulani hapo
 
Julai 11, 2023, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa ziarani mkoani Simiyu, alitoa ruhusa rasmi kwa madaktari nchini walioajiriwa na Serikali kufanya kazi binafsi kwanye hospitali za umma baada ya muda wao wa kazi kwisha. Waziri Ummy alitoa maelekezo hayo wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu. ACT-Wazalendo kupitia Ofisi ya Wasemaji wa Kisekta tumefanyia tafakuri ya kina maamuzi haya na athari zake kwa lengo la upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wote.

Ufinyu wa mishahara na maslahi kwenye sekta ya afya hasa kwenye vituo vya afya vya Umma husababisha wafanyakazi wachache wa sekta hiyo kulazimika kufanya kazi za ziada kwenye vituo vya afya vya binafsi ili kuweza kujiongezea kipato. Hali hii inaongeza upungufu wa wafanyakazi wa afya kwenye vituo vya afya vya umma, anayeumia ni mwananchi mwenye kipato kidogo.

Muda wa kazi kwa wafanyakazi wa afya hususani madaktari na manesi ni kwa mfumo wa zamu za kazi. Wafanyakazi hawa wanapomaliza zamu zao wanapaswa kupumzika kusubiri zamu nyingine badala ya kuhangaika kujipatia kipato. Uchovu wa wafanyakazi wa afya ni kigezo kikubwa kwenye utoaji wa huduma bila ufanisi na kwa ubaguzi, wenye nacho wakipewa kipaumbele zaidi ya wasionacho; hali inayoongeza matabaka katika upatikanaji wa huduma za Afya.

Baada ya saa za kawaida za kazi kuna wagonjwa wanaoenda kutafuta huduma kwenye vituo vya afya vya umma, kugeuza vituo hivyo kama sehemu ya binafsi ni kumnyima huduma mwananchi asie na fedha za kulipia huduma binafsi. Hii si haki kwani mwananchi analipia huduma hizo kupitia kodi mbalimbali.

Kiini cha huduma mbaya za afya nchini ni mfumo usiofaa uliopo wa kugharamia huduma za afya; mfumo unalaozimisha wananchi walipie huduma kutoka mifukoni mwao. Huu ni mzigo kwa mwananchi hasa aliye kwenye kundi kubwa la wenye kipato kidogo waliojiari katika sekta isiyo rasmi. Aidha, mfumo huu unaikosesha Serikali mapato ya kutosha kuendeleza huduma za afya. Serikali imeacha mzigo wa gharama za huduma ya Afya kwa mwananchi.



Agizo la Waziri wa Afya litakwenda kuharibu kabisa mfumo wa utoaji huduma za Afya kwa Umma. Mfumo mzima wa utoaji wa huduma za afya umegubikwa na changamoto za upungufu wa wataalamu, mazingira duni ya kufanyia kazi, upungufu wa miundombinu na uhaba wa dawa na vifaa tiba. Changamoto hizi zitaweza kutatuliwa kwa urahisi zaidi pindi tukiwa na mfumo bora wa kugharamia huduma za afya na usimamizi wa fedha.

Mapendekezo ya ACT Wazalendo.
Serikali isitishe maramoja utaratibu huu mpya wa wafanyakazi walioajiriwa na Serikali kutoa huduma za afya binafsi kwenye vituo vya afya vya Serikali. Badala yake ije na mbinu za kuboresha huduma za afya na mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa sekta ya afya kwa Umma.

ACT Wazalendo tumependekeza mfumo wa kufungamanisha bima ya afya na mfuko wa hifadhi ya jamii, ambapo kila mwanachama atapata Fao la bima ya Afya. huu ni mfumo wa kugharamia huduma za afya kwa kujiwekea akiba, tofauti na mfumo uliopo wa matumizi pekee. Mfumo tunaoupendekeza unakidhi vigezo vya mfumo unaopendekezwa kimataifa wa kuwezesha kuboresha afya ya jamii sambamba na kupunguza umaskini, kuongeza ajira na kukuza uchumi ili kufikia lengo la Afya kwa wote.

Mfumo wa Kufungamanisha Bima ya Afya na Hifadhi ya jamii utaondoa matabaka katika upatikanaji wa huduma za Afya kwa makundi yote; kundi la wenye Ajira Rasmi, kundi la wasio na ajira Rasmi kama vile wakulima, wavuvi, wafanyabiashara na kundi la wasio na uwezo kabisa kama wazee na wenye ulemavu Makundi yote yatachangia kwenye Skimu ya hifadhi ya jamii kulingana na uwezo wao na watapata huduma kulingana na mahitaji yao bila ubaguzi wala matabaka.

Hitimisho
ACT Wazalendo inaamini katika kuzingatia haki na usawa kwa wote katika kupata huduma za Afya ili kufikia lengo la Afya kwa Wote na kusisitiza umuhimu wa wafanyakazi wa afya kufanya kazi katika mazingira wezeshi, kupata mshahara wa kutosha, na mapumziko ya kutosha kabla ya kubadilisha zamu za kazi, ili kuwewawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi. Haya yatafanikiwa kwa kuwepo na mfumo bora wa kugharamia huduma za afya.

Mfumo tunaoupendekeza ACT Wazalendo ni wa kuunganisha Hifadhi ya Jamii na Bima ya Afya. Mfumo huu utamwezesha kila Mtanzania kuwa na Bima ya Afya itakayompa uhakika wa matibabu, afya bora na kumuinua kiuchumi. Halikadhalika mfumo huu utawezesha kuboresha mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa afya.

Imetolewa na;
Dr Elizabeth Sanga
Twitter: @DrBSanga
Waziri Kivuli wa Afya - ACT Wazalendo.
Julai 15, 2023
Point ya muhimu sana hii. Jirani yetu alisubiri sana kabla ya kupata nafasi ya kumuona daktari bingwa. Kumbe alikuwa na saratani. Alipomwona daktari tatizo likawa limeshakuwa kubwa matibabu yake makubwa na gharama zaidi , akafariki.

Alishauriwa alipie kumwona daktari bingwa haraka lakini hakuwa na fedha na familia haijiwezi

Hiki alichotangaza waziri kinaweza kusababisha watu wasio na matatizo makubwa wamuone bingwa kabla ya wale wenye matatizo makubwa waliotakiwa kupewa appointment mapema
 
Back
Top Bottom