Rose Kamili amemsafisha Dr. Wilbrod Slaa. Hongera Rose Kamili na wenzako mliofanikisha hilo

kelele zoteeee ni kuona upepo wa kiasa unawaendea vibaya na dk is likely to be so wanaamua kumchafua, nyie mchafueni ila mjue ssm hatuipi, hatuitakin na tumeichoka!
 
jana niliandika katika ule uzi mwingine ifahamike kuwa makanisa,wakuu wa wilaya na misikiti ni agents wa serikali kufungisha ndoa. Ni lazima waaply serikalini ili wapate kibali cha kufungisha ndoa pamoja na kununua vyeti vya ndoa. mfano sisi waluteri ukifunga ndoa hupewa cheti kingine cha ziada cha ndoa kinachotolewa na kanisa ambacho pamoja na mambo mengine huandikwa maneno "alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe".

Mkuu,

Sisi wakatoliki cha muhimu ni ndoa kama sakramenti iliyoanza kutolewa miaka 2012. Hiki cheti cha ndoa cha kiserikali na kama ni Serikali ya Tanganyika basi kilianza miaka 50 tu iliyopita na hivyo nafasi yake ni ndogo sana kanisani.

Tuna utaratibu wetu na vyeti vyetu kwa sakarament kadhaa kama vile Ubatizo, Kipaimara, ndoa na upadri. Na tunapoviweka ni kwa ajili ya mambo yetu ya kidini ambayo hatujawahi kutaka yawe ya kiserikali au yaingizwe kwenye katiba.

Hivyo, walioleta hicho cheti cha serikali ni serikali yenyewe na sisi Tanzania ikiacha tutaendelea na utaratibu wetu wa miaka 2012 sasa na wala hatutaathirika au kuwafuata Serikali.
 
Bado naona kuna mambo mengi yanaweza kuchafua zaidi kutokana na hii stori yako. Sitaki kuongea sana, ila inavyoonekana maaskofu an mapadri basi wana mengi yaliyojificha tofauti na waumini wao wengi wanavyowachukulia. Na hili si kwa kanisa katoliki tu bali dini zote.
 
Bado naona kuna mambo mengi yanaweza kuchafua zaidi kutokana na hii stori yako. Sitaki kuongea sana, ila inavyoonekana maaskofu an mapadri basi wana mengi yaliyojificha tofauti na waumini wao wengi wanavyowachukulia. Na hili si kwa kanisa katoliki tu bali dini zote.

Inaelekea umejikita kusoma magazeti ya hapa nchini. Ungekuwa umejikita international news hizi habari zimeshakuwa kawaida tangu hata hujazaliwa.
 
Mkuu naanza kukubaliana na nyinyi. Unajua wakati wa John Paul II kuomba petition uliaweza kutumia hata miaka minane kupata.

Na kuanzia mwaka 1980 hadi 1985, John Paul II alizuia kabisa haya mambo ya laicization.
at early 90's aliomba petition reason ikiwa ni family(Rose na watoto) ,ambayo alijibiwa mwanzoni mwa miaka ya 2000.....sasa if this is the case Slaa alipaswa kulimaliza hili kwa heshima zake na siyo kienyeji ,kwasababu hata majibu ya petition yalimtambua Rose na watoto wake na siyo josephine.
 
Sasa unataka kutuambia nini? inahusiana nini na shida za Watanzania? Ina uhusiano gani na mfumuko wa bei uliofikia 19%? Je hiyo habari inasaidia nini kuondoa mikataba mibovu nchini? Hebu nieleze vizuri mkuu
 
Rose Kamili kachanganyikiwa, amemshindwa Mary Nagu sasa anarukia waume za watu, atulize makalio chini, kama anataka mabwana aende chama cha kijani , wako bwelele wameungua nyuso kwa ARV

mbona unatoa viroja badala ya hoja,wewe mke wa Dr. Slaa Nini.?
 
Probelm ni kwamba kitabu kitakatifu hakijatoa ruksa ya DIVORCE and there is nobody to change that.

Wewe unamini Kitabu Kipi kama kitakatifu kwako? Ni ndoa Gani isiyovunjika katika hicho kitabu kitakatifu unachozungumzia?

 
jana niliandika katika ule uzi mwingine ifahamike kuwa makanisa,wakuu wa wilaya na misikiti ni agents wa serikali kufungisha ndoa. Ni lazima waaply serikalini ili wapate kibali cha kufungisha ndoa pamoja na kununua vyeti vya ndoa. mfano sisi waluteri ukifunga ndoa hupewa cheti kingine cha ziada cha ndoa kinachotolewa na kanisa ambacho pamoja na mambo mengine huandikwa maneno "alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe".

Ndoa katika Kanisa Katoliki:

1. Haiwezi kutenguliwa:
a. Kama imefungwa kwa uhuru kamili na wahusika na imefuata utaratibu unaofahamika na kukubalika na Kanisa Katoliki.
b. Kama wanandoa hawana uhusiano wowote wa damu au uhusiano unaotokana na ndoa ya awali (kama ipo) na mmoja wa wanandoa si mtoto aliyelelewa na yeye kama mzazi wake (adoption).
c. Hakuna ndoa nyingine halali kabla au wakati ndoa inafungwa mmoja wa wanandoa hakuwa anafungwa na sakramenti ya daraja au nadhiri za utawa.
d. Mmojawapo siyo ******* (impotent).
e. Ndoa iliyofungwa imekamilika (consumation)
f. Kama mmoja wa wanandoa hakudanganya (mfano kama angesema ukweli ndoa isingefungwa)

2. Hakuna ndoa halali na inaweza kutenguliwa kama kinyume cha moja au yote hayo ni kweli.
 
Mimi sina nia mbaya na huyu mzee ila kwa umri ule kweli haipendezi kukimbizana na wanawake.Kama anataka heshima yake isishuke afanye mambo mengine aachane na pilika pilika na wanawake
 
Mkuu,

Sisi wakatoliki cha muhimu ni ndoa kama sakramenti iliyoanza kutolewa miaka 2012. Hiki cheti cha ndoa cha kiserikali na kama ni Serikali ya Tanganyika basi kilianza miaka 50 tu iliyopita na hivyo nafasi yake ni ndogo sana kanisani.

Tuna utaratibu wetu na vyeti vyetu kwa sakarament kadhaa kama vile Ubatizo, Kipaimara, ndoa na upadri. Na tunapoviweka ni kwa ajili ya mambo yetu ya kidini ambayo hatujawahi kutaka yawe ya kiserikali au yaingizwe kwenye katiba.

Hivyo, walioleta hicho cheti cha serikali ni serikali yenyewe na sisi Tanzania ikiacha tutaendelea na utaratibu wetu wa miaka 2012 sasa na wala hatutaathirika au kuwafuata Serikali.

well said na ndicho waislam wanalilia ile mahakama ya kadhi
 
Kwani Rose Kamili aliwahi kuolewa na Dr Slaa au walizaa watoto tu ?.
 
at early 90's aliomba petition reason ikiwa ni family(Rose na watoto) ,ambayo alijibiwa mwanzoni mwa miaka ya 2000.....sasa if this is the case Slaa alipaswa kulimaliza hili kwa heshima zake na siyo kienyeji ,kwasababu hata majibu ya petition yalimtambua Rose na watoto wake na siyo josephine.

Mzee,

Umeanza vizuri sijui kimetokea nini hadi ukamaliza hivyo kwenye red. Kwanza hapo inafurahisha kwamba umetujulisha kwamba Petition ya Dr. Slaa kwenda Vatican kujiondoa upadrini ilianza 1990. Kama unasema kweli basi Rozi Kamili anaidanganya mahakama kuwa Slaa alianza mara moja kushughuulikia hii petition wakati kumbe alianza miaka mitatu baadaye.

Tuje kwenye suala la petition kumtamua Rose Kamili. Nakujibu hili nikijua najibizana na mkatoliki aliye na undani kabisa na masuala haya maana si rahisi kujua petition ya Slaa kama haumo kwenye mfumo wa Kanisani. Suala la kujua petition maana yake Vatican inajua kwamba Padri Slaa amezaa na Rose Kamili na inawajua watoto wa Rose Kamili.

asakuta,

Unajua wengi hamjijui kuwa mnampa sifa Dr. Slaa kuwa alikuwa muaminifu kuwataja Rose Kamili na watoto wake wawili hadi Vatican ikawajua kwenye petition. Hebu sema wewe mwenyewe ni maaskofu wangapi duniani hapa na mapadri wana watoto lakini wanawatunza kinyemela wengine tunajua na wengine hatujui.

Petition hiyo ilimpa urahisi Padri Slaa kuachana na celibacy vows kwani haikuwa na maana Vatican kumng'ang'ania aendelee kuwa altareni huku kukiwa na obligation za kutunza familia na kuna uwezekano wangemkatalia basi Slaa mwenyewe angeweza kuiweka scandal hiyo hadharani ili aondoke kama alidhamiria.

Hiyo ndiyo issue ya petition. Uzito mwingine wa petition ni kwamba Vatican na Kanisa kwa ujumla wataishia kujua kwamba Wilbrod Slaa ana mwanamke na amezaa watoto.

Wewe ni mkatoliki na unajua petition kuwa, kamwe haigeuki kuwa cheti cha kanisa cha ndoa. Wanaweza wakaishia kusema huyo anafanya uasherati kwa sababu hajafunga ndoa kanisani.

Hivyo, Dr. Slaa hana wajibu unaosema wa kulimaliza suala hili kwa heshima wakati kila mmoja wetu tulikuwa tumetulia na habari za bunge ghafla huyu mama Rose Kamili ndiye akaliibua kwa kulipeleka mahakamani.

Ukweli ambao wewe unaujua kwamba ndoa kwa sisi wakatoliki ni Sakramenti na wala hatujihangaishi kujua wengine ikiwemo serikali inaijua vipi.

Dr. Slaa hajapata Sakrament ya ndoa (Matrimony) na hivyo mwanamke atakayekuja naye altareni siku ile ya July 21, 2012 ndiye dunia na Vatican watatambua kwamba huyo ndiye mwanandoa wake na si hizi porojo za wajinga zinazoendelea mtaani.

Wakumbushe wasiojua uthabiti wa Kanisa Katoliki kuhusu Mfalme Henry VIII wa England alivyozuiwa na Kanisa kuoa mke mwingine hadi akaamua kuanzisha kanisa lake la Anglican na likawa Kanisa rasmi la Uingereza akaachana na Kanisa Katoliki.
 
Mimi sina nia mbaya na huyu mzee ila kwa umri ule kweli haipendezi kukimbizana na wanawake.Kama anataka heshima yake isishuke afanye mambo mengine aachane na pilika pilika na wanawake

Rais Nelson Mandela wa South Africa akiwa na umiri wa miaka 78 aliachana na Winnie Mandela na mwaka uliofuata akamuoa mke wa rafiki yake Samora Machel.
 
Back
Top Bottom