Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
FILM: KITISHO
MTUNZI: Richard MWAMBE
1
Mbowe club saa 1:23 usiku
RADI kali ilipasua anga na kufanya mchoro wa kutisha, mwanga wake ulilipoteza giza kwa sekunde kadhaa, kila kilichojificha kilionekana wazi.
Hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa nje muda huo. Ni mvua kubwa na ngurumo za kutisha zilitawala kila kona, ilikuwa ni hali ya kuogofya sana. Mifereji na mito ya dhalura ilianzishwa na maji ya mvua hiyo.
Kama ilivyo ada katika jiji la Dar es salaam, barabara zote zilikuwa zimejaa maji, kama ukiwa dereva mgeni basi hutoweza kujua ni wapi barabara ilipo. Sehemu kubwa ya mji hasa katikati ya jiji gari nyingi ziliegeshwa kando ya barabara kusubiri mvua iishe lakini haikuwa hivyo kwani mvua ilikazana zaidi ya saa nne.
Wakati hayo yote yakiendelea, ndani ya ukumbi mkubwa wa starehe unaojulikana kama ‘Mbowe Club’ watu hawakuwa wakijua kama nje kuna mvua, disco liliendelea kwa nguvu zote, watu walicheza, wakanywa na kuburudika. Katika kaunta kubwa ya ukumbi huo kulikuwapo walevi kadhaa ambao tayari walikwishabadilisha lugha ya mawasiliano kutoka Kiswahili na kuwa Kiingereza.
Gina binti Komba Zingazinga alikuwa ni miongozi mwa watu wachache waliokuiwa wamesaliwa na akili zao na utashi pia, alikuwa akinywa kinywaji chake taratibu huku jamaa mmoja akijitahidi kumzengea zengea lakini asifanikiwe. Kila wakati alionekana kuitazama saa yake aliyoivaa mkononi na aliposhusha mkono aliinua ule uliokamata ile bilauri yenye kiuno iliyojaa mvinyo kutoka Dodoma. Baada ya kupiga funda moja kasha la pili aliiteremsha taratibu na kuiweka juu ya mbao mwororo iliyoifunika na kuipendezesha kaunta ya ukumbi huo. Macho yake yalikuwa yakizunguka huku na kule yakitazama au kutafuta kitu ambacho hata yenyewe hayakukijua.
Upande wa pili wa ukumbi huo, kwenye sakafu iliyojengwa juu kidogo na ili uifikie itakulazimu kuzikwea ngazi kadhaa, kulikuwako watu watatu, wawili wanaume na mmoja mwanamke. Mwanaume mmoja alikuwa na tambo kubwa lililojaa kimazoezi, enzi za utoto wetu tungeweza kumwita Pawa, lakini enzi hizi wanamwita Baunsa, yote hayo ni mabadiliko ya nyakati. Watu wale watatu walikuwa wakiongea jambo Fulani na meza yao ilikuwa imechakazwa kwa pombe kalikali na sahani za nyama zilizokuwa zikipishana, vyote hivyo vilimiminwa katika matumbo hayo matatu. Ilikuwa ni vigumu kusikia nini wanachokiongea kutokana na muziki mkubwa uliokuwa ukipigwa ndani humo. Kati ya kaunta alipokuwapo Gina na ule upande kulitenganishwa na kundi la vijana waliokuwa wacheza muziki huo kwa mitindo mbalimbali. Gina alihakikisha hapotezi macho yake upande ule kwani mwili wake ulikuwa ukisisimka mara kwa mara na hiyo kwake ilikuwa ni ishara ya hatari.
Dakika chache baadae alimuona Yule mwanamke akiinuka na kutoka katika vile viti, akitembea kwa mwendo wa ki-levi levi. Akamtazama na kujua mara moja kuwa alikuwa anaelekea chooni, Gina akajikuta akishuka kutoka kwenye kiti kirefu alichokuwa amekalia, akaigugumia pombe yake yote kinywani mwake, kasha akavuta hatua fupifupi akikumbana na walevi na wacheza muziki akaelekea kule alikokwenda Yule mwanamke.
Halafu nitamwuliza nini? Akajiuliza pa si na kupata jibu. Lakini aliendelea kuvuta hatua kuelekea kule chooni, akapinda kona ya kwanza na kuingia kwenye milango Fulani iliyokuwa ikielekea huko atakako, mbele kidogo alimuona Yule mwanamke akiingia katika moja milango ya vyoo vile. Gina; mkono wa kulia ukiwa nyuma ya suruali yake ndani kidogo ya jaketi lake, sikwambii alishika kitu gani, aliuendea ule mlango, mara ghafla akaanza kuhisi kitu kikimfinya mkononi mwake, ilikuwa ni saa kubwa ya mkononi, saa yenye uwezo wa kupokea nukushi, kupiga picha za mjongeo na mnato, yenye uwezo wa kurekodi sauti na pia unaweza kuitumia kama simu. Akainua mkono na kubofya kitufe Fulani kasha akasubiri kidogo. Wakati akisubiri kijimkanda hicho chembamba kikitoka kwenye saa yake, Yule mwanamake bado alikuwa chooni.
Mama yuko mahututi Shamba, Tena Saan Aisee! Uikuwa ni ujumbe uliosomeaka hivyo katika kile kijimkanda. Akakikata na kukitia mfukoni mwake kisha akaanza safari ya kutoka ndani ya Klabu ile, akili yake ilikwisha sahau juu ya Yule mwanamke, akapita mlangoni na kukumbana kikumbo na Yule mwanaume mwenye tambo kubwa, akielekea kule choo cha wanawake, Gina akasukumwa pembeni; na Yule bwana akapita.
Nje ya Klabu hiyo ndipo alipokutana na mvua ya kutisha, akapachua kikofia katika ukosi wa jaketi lake na kukivaa kisha akaliendea gari lake, mita kadhaa kabla hajalifikia akapiga breki na kuacha kinywa wazi, hakuamini anachokiona. Vioo vyote vya gari yake vilikuwa vimevunjwa, tairi hazina upepo na ndani kulijaa maji ya mvua. Wameiba? Akajiuliza, kisha kwa mwendo wa tahadhari akasogea kwenye lile gari, juu ya kiti cha dereva kulikuwa na bahasha ngumu ya khaki, akatazama huku na kule, alipojihakikishia usalama akaingiza mkono kwa minajiri ya kuichukua ile bahasha ijapokuwa ilionekana kulowana.
Daraja la sarenda saa 1:55 usiku.
BMW nyeusi iliyokuwa iking’azwa kwa mwanga wa radi, ilshuka katika barabar hiyo ya Kenyata kwa kasi sana ikitokea maeneo ya Masaki. Ilipofika katika makutano ya barabar hiyo na ile ya Ally Hassan Mwinyi mkabala na Ubalozi wa Ufaransa iliingia barabara kubwa bila kungalia usalama huku ikirusha maji juu kutokana na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha usiku huo.
Madam S alikuwa katulia kwenye usukani akiiongoza gari hiyo ya Mwingereza kwa umahiri mkubwa. Akakunja ushoto na kukanyaga mafuta kueleka mjini. Ilikuwa ni tabu kuona mbele kutokana na wingi wa mvua, barabara imejaa maji, umeme umekatika, ilikuwa ni shida juu ya shida. Madam S hakujali alilikanyaga daraja la Salenda na kuendelea mbele, lakini kabla hajalimaliza, hamad, kulikuwa a mwili wa mwanadamu uliolala barabarani huku mikono yake ikiwa imefungwa nyuma. Akaiyumbisha gari kuukwepa mwili huo, gari ikasota na kukosa muelekeo, akarudisha usukani kulia kuukwepa mwamba wa daraja, akaknyaga krachi na kuachia mafuta kasha akatoa gia ya tano na kushusha ya nne, kutahamaki gari yake ilikuwa ikihamia barabara ya pili, akakanyaga breki lakini ikashindwa kusimama, akaknyaga tena breki bado gari ilikuwa ikiendelea, ikapanda tuta lakutenga barabara, ikajipigia na kutua barabara ya pili, akili ikamrudia, akavuta breki ya mkono na ile BMW ikaserereka na kujizungusha.
Kishindo kikubwa kikasikika, BMW iligongana na Land Rover Defender, ikaangushwa pembeni. Madam S akajikuta kwenye pori la mikoko chini ya daraja la Salenda, akafyatua mkanda, akapiga kioo cha mbele kwa kukikanyaga kwa mguu, akatoka, akajipapasa na kukuta bastola zake zipo salama.
Damu zilizikuwa zikitiririka semu ya paji la uso juu kidogo ya jicho la kulia, wakati akijitahidi kusimama, radi kali ilipiga na kufanya mwanga mkubwa uliong’aza vichaka vyote, Madam S akaona mbele yake kama kivuli cha mtu aliyesimama nyuma yake. Akajua ni mawenge ya ajali tu, akageuka nyuma na mara ghafla akakutana na pigo la kitu kizito kilichotua katikati ya paji la uso, akayumba vibaya lakini mikono yake tayari ilikuwa imekwishachomoa bastola zake, kabla hajafyatua akafunikwa na gza nene lililomfanya ashindwe kuona chchote, akaanguka kama mzigo na bastola zikimtoka mikononi mwake.
Ofisi ya usalama wa taifa saa 2:00 usiku.
MAAFISA wa Idara ya Usalama wa Taifa walikuwa wakiendelea na shughuli zao kama kawaida usiku huo. Katika moja ya ofisi za jengo hilo, vijana wawili na msichana mmoja walikuwa bize kutazama luninga nyingi zilizowazunguka zinazoonesha maeneo mbalimbali muhimu ya Jiji la Dar es salaam. Kupitia luninga hizo waliweza kuona moja kwa moja kile kinachotokea kwenye maeneo hayo kama Uwanja wa ndege, Bandarini, Stesheni ya Treni, Uwanja wa Sabasaba, Makao makuu ya Rais na maeneo mengine mengi ambayo yamepewa umuhimu wa pekee kwa sababu hii au ile.
Avant, msichana mbichi wa miaka takribani thelathini hivi alikuwa katingwa kuangalia tukio la ajali iliyotokea daraja la Salenda, bado alikuwa anapata shida kujua hasa nini kinaendelea kutokana na ile picha kufichwa na mvua ilikua ikinyesha eneo hilo lakini kila ilipokuwa radi ikipiga ndipo alipoweza kuona kitu, baada ya dakika kadhaa alipuuza na kuendelea kutazama maeneo mengine.
Mubah akajikohoza kidogo na kumgutusha Avanti kutoka pale alipokuwa akitazama.
“Si ukapime, au Mama yako anajua?” Avanti akamtania Mubah.
“Unanianza we mrembo, mi nasubiri time hapa niingie viwanja!” Mubah akajibu, huku akitoka kwenye kiti chake na kukiendea kile alichoketi Avant, akasimama nyuma yake, machoye akiwa kayakaza kwenye ile luninga.
“Shiit! Avant, nini hicho?” akauliza huku akisogea jirani zaidi.
“Ajali, imetokea kama dakika kumi hivi,” Avant akajibu.
“Kwa nini usipige simu polisi wawahi kama kuna chochote cha kuokoa?” Mubah akahoji.
“Sasa Mubah, Salenda pale kituo kipo jirani wataenda tu,” akaeleza huku akimtazama Mubah usoni.
“Yaani wewe! Kitendo cha kuitega kamera pale hatukufanya kwa makosa, lile ni eneo nyeti sana, kama ni ajali lazima polisi wafike mapema ili kuondoa kilichopo, pale vipngozi asilimia 99 wanapita, ikiwa hujuma utalaumiwa wewe kwani ndio eneo lako la kutazama leo!” Mubah akalalamika huku akiliendea kabati dogo lililo hapo jirani.
Avant akainua simu na kubofya tarakimu Fulani Fulani kasha akatoa taarifa hiyo kituo cha polisi cha Salenda. Haikupita dakika tano tayari kupitia luninga yake aliweza kuona gari na nyendo za polisi eneo hilo bila kujali mvua iliyopo. Avant aliendelea kutazama huku akigonga gonga karamu yake.
§§§§§
Gina alivuta hatua na kuingia katika lango kuu la Ofisi Nyeti, Shamba, akabofya namba zake za siri, kasha akaweka kiganja chake juu ya kioo Fulani kilichopo mlangoni na baada ya hapo akafanya kama anachungulia, kijimwanga chekunfu kikapita kati ya macho yake na kitasa cha ule mlango kikafyatuka, akaufungua na kuingia ndani. Moja kwa moja akaingia chumba Fulani na kuvua jaketi alilovaa, akabadilisha nguo na kurudi katika hali ya ukavu, akatoka na kutembea mwendo mfupi kabla hajagonga mlango Fulani kwa mtindo wa pekee na mlango ule ukafunguliwa.
“Karibu Gina!” Dkt Jasmine akamkaribisha na nukta chache baadae akampatia kikombe cha kahawa.
“Hawajafika?” Gina akauliza.
“Hapana, we ndiye wa kwanza, leo sijui kuna nini, labda kwa sababu ya mvua,” Dkt. Jasmin akaeleza.
Gina akashusha pumzi ndefu, mazungumzo mengine yakaendelea huku wakiwasubiri wengine, kila mara walikuwa wakitazama saa zao, hakuna simu wa taarifa yoyote iliyokuwa ikifika katika nyumba hiyo, Gina na Jasmine wakaanza kupata wasiwasi. Jasmine akainua uso na kuitazama saa kubwa ya ukutani, ikamwonesha kuwa ni saa 3:15 usiku.
“Hapana Gina, hii sio kawaida, tuanze kuwatafuta mmoja baada ya mwingine,” Dkt. Jasmin akamweleza Gina, kasha wote wawili wakaenda kwenye chumba maalumu cha mawasiliano, ndani ya chumba hicho ambamo ndiyo ofisi ya kudumu ya Chiba wa Chiba kulijawa na makompyuta na luninga nyingi huku na kule, simu za upepo, za kawaida na zile za satellite zilikuwepo. Kila kitu kilikuwa kinafanya kazi kwani haikuruhusiwa kuzima chochote labda tu kama kuna matengenezo, kila mmoja akaketi katika kiti chake na kuanza kucheza na simu zao za siri zilizounganishwa moja kwa moja.
Hakuna simu ya mkononi iliyokuwa ikipatikana si ya Madam S wala ya nani, walipigwa na butwaa na kubwa simu za nyumbani zote zilikuwa zikiita bila kukoma hazikupokelewa. Gina akamgeukia Dkt. Jasmine.
“Oya Shost, hapa ni mguu kwa mguu nyumba moja baada ya nyingine tukapate kujua kilichojiri,” Gina akamwambia Jasmine kasha wote wakaingia vyumbani na walipotoka walikuwa katika mavazi ya kazi, kila moja alibeba silaha anazoamini zingemfaa usiku huo kwani hawakujua hatari itakayowakabili. Wakiwa katika harakati hizo ndipo Gina alipokumbuka ile bahasha.
“Nisubiri Jasmine!” akarudi kwenye kile chumba akaichukua ile bahasha, bado ilikuwa imelowa akaichana taratibu na kuitoa karatasi ya ndani kwa uangalifu.
“Nini Gina?” Jasmine akauliza.
“Hii bahasha niliiokota kwenye ari yangu lakini sikuwahi kuifungua ndani,” akamjibu.
Gina alibaki kakodoa macho baada ya kukutana na kichwa cha habari kikubwa kilichosomeka ‘KITISHO!’ kisha chini yake kuliandikwa sentensi moja tu
Mwisho wa zama zenu umefika, mtaongea na Mzee Ngurumo.
Maneno hayo yalizigonga kwa nguvu nyoyo za wadada hawa, wakabaki wakitazamana, wkageuza macho yao wakaitazama tena ile karatasi.
“Gina!” Jasmine akaita.
“Jasmine!” naye akaitikia na wote wakatoka na kuingia kwenye gari ya Jasmine na kuondoka eneo hilo.
§§§§§§
Kerege – bagamoyo saa 4:07 usiku
TOYOTA Hilux Double Cabins, iliingia taratibu getini na kuegeshwa karibu na bustani ya maua iliyotengenezwa ndani ya ngome kubwa iliyobeba jengo la kifahari kuliko fahari yenyewe. Walinzi kadhaa walionekana kwenye kona zake, hawakushughulika kabisa na gari hiyo bali kila mmoja alishika lindo lake.
Dereva akashuka na watu wengine kama watatu hivi wakashuka, wakazunguka nyuma na kufungua funiko kubwa la alluminium lililotengenezwa ili kufunika mzigo uliopo ndani yake.
“Washushe hao, kisha wapeleke Kuzimu,” mmoja wa wale vijana aliyekuwa ameketi mbele akawaagiza wenzake kasha yeye akazikwea ngazi kulielekea jengo hilo lililoendezeshwa kwa taa zenye marembo mbalimbali.
Sauti za viatu vyenye kisigino kigumu zilisikika zikitembea lakini aliyevaa hakuonekana, Bwana Mpaya alibaki kusimama na kutazama kule sauti ile ilikokuwa ikitokea na asione mtu zaidi ya giza lililomlaki isipokuwa aliposimama yeye mwanga ulikuwapo na kufaya nuru ya kupendeza. Kasha ukimya ukatawala na sauti nzito ikalipenya lile giza.
“Ndio Bwana Mpaya, karibu sana, natumaini umekamilisha nililokutuma, sivyo?” alikuwa ni Pancho Panchilio aliyeyafikia masikio ya Mpaya aliyekuwa amesimama katikati ya sebule pana lakini asimwone anayeongea naye, isipokuwa sauti tu.
“Ndiyo Boss, tumewaleta lakini hali zao ni mbaya sana,” akaeleza.
“Vizuri sana, nani na nani mmempata?” akauliza tena.
“Tumempata Boss wao na Mtaalamu wao wa kompyuta,” akajibu.
“Ha! Ha! Ha! Ha! Ha!” akacheka cheko la pesa.
“Ok, wape vijana posho yao kama nilivyokwambia kisha unitafutie kichwa cha Kamanda Amata, huyu hasa ndiye mwiba kwangu, nataka apotee kwenye uso wa nchi ili binadamu tule vizuri, kuna pesa ndefu sana nimeiandaa mkilikamilisha hili,” Pancho akiwa mafichoni mwake akakohoa kidogo wakati Mpaya alikuwa akitoka, “Sikia Mpaya, hakikisha ukimuua Kamanda Amata, mkate kichwa, kisha kiwiliwili mkichome moto na kichwa mniletee, mbwa wangu hawajala nyama siku nyingi sana, maana Yule ni shetani anaweza kujiunganisha tena halafu akaangusha balaa, kwa heri!”
Alipomaliza kusema hayo na taa ndani ya jengo lile zikazimika.
2
KAMANDA Amata akaitazama gari yake aia ya Subaru Forester jinsi ilivyochakazwa kwa risasi, akashusha pumzi ndefu.
Wadude hawa wangeniua! Akajisemea moyoni huku akijaribu kuiwasha nayo ikawaka, akairudisha barabarani na kushika njia ya kwenda mjini, alijipapasa mifukoni hakuiona simu yake, wala saa yake mkononi haikuwepo. Any way! Akajipa moyo. Huku akiendelea kuutafuta mji wa Dar es salaam, saa ya ndani katika gari yake ilimwonesha kuwa ni saa tano za usiku.
Gina sijui kama atanielewa, maana tulikubaliana saa moja na robo, labda nitamkuta! Akaendelea kuongea na nafsi yake, huku akiiacha Gongo la Mboto na kuitafuta Uwanja wa Ndege. Katikati ya safari yake akafungua redio ndani ya gari na kusikiliza kinachoendelea. Ilikuwa ni kituo kimoja cha redio binafsi kikirusha habari hiyo ya dharula iliyoyanasa masikio ya Amata usiku huo.
…Mwili wa Mheshimiwa huyo umekutwa sakafuni bila uhai na kitu kama matundu ya risasi yakionekana kifuani mwake. Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wake ili kuwakama waliohusika na mauaji hayo…
Amata akakanyaga breki kali na kuitoa gari barabarani kwani taarifa hiyo haikujitosheleza kwake, akaegesha gari pembeni na kutazama huku na kule hakuona mtu kupita eneo hilo, pembeni yake kulikuwa na bar iliyokuwa ikiendelea kuburudisha watu kwa vinywaji na vilaji, akashuka na kuiendea, alipofika tu akakutana na mwanadada mrembo aliyevalia nguo nyeupe juu na sketi nyeusi chini.
“Karibu kaka, karibu kiti,” Yule dada akamkaribisha Amata huku akifuta meza iliyokuwa hapo. Ijapokua haikuwa nia ya Kamanda kuketi, akajikuta amefanya hivyo, “Pole!” neon hilo likaupasua moyo wa Amata akamtazama Yule dada Mhudumu wa bar.
“Pole ya nini?” akauliza
“Una damu kichwani,” akamwambia.
“Shiit!” akang’aka na kujigusa, kweli akahisi maumivu na kitu kama jeraha.
“Asante sana!” akamjibu, “Unaweza kunisaidia simu yako?” akamwuliza.
“Haina salio lakini, halafu ni kisimu cha tochi,” akajibu kwa aibu.
“Naomba hivyo hivyo.”
Yule mwanadada akachomoa simu yake akampatia Amata. Ilikuwa ni simu iliyochakaa, iliyoonekana kupita katika mikono mingi ya watu mpaka kuifikia mikono hii ya huyu Mhudumu wa baa. Ilifungwa kwa mipira ya manati, betri lake lilishikiliwa na kipande cha mpira wa manati. Hakujali, aliitazama vyema kasha akaanza kubofya hapa na pale.
“Haina vocha hiyo!” Yule Mhudumu akaeleza tena.
“Usijali, kaniletee Bia baridi sana bila glass tafadhali,” Kamanda akamwagiza Yule dada lakini alilotaka yeye haikuwa bia ila zile dakika mbili za kubaki peke yake. Vidole vyake vikaanza kutomasa tarakimu Fulani Fulani na alipomaliza, akapumzika, wakati huo bia yake ilikuwa imefika, akaigusa, akamwonesha Yule Mhudumu alama ya dole gumba, kisha akabaki na hamsini zake.
Meseji iliyofuata katika simu hiyo ilikuwa ni kutoka katika kampuni moja ya simu nchini, Kamanda Amata alikuwa amechukua muda wa hewani kwa namna yao ya siri na sasa simu ile Kimeo ilipata uhai.
Akaanza kupiga namba za maswahiba wake wa kazi, Chiba; simu haikuita kabisa, Madam S vivyo hivyo, akaduwaa wa sekunde kadhaa, haikuwa kawaida kwa watu hao kuwakosa kwenye simu, akili ya Kamanda ikiruka chogo chemba. Mbele yake kulikuwa na luninga kubwa iliyokuwa ikionesha matukio mbalimbali ya Kitaifa na lile lililomvutia ni ajali ya Salenda, alisahau kupiga simu na kutazama tukio lile. Kamanda Amata alikaza jicho kutazama picha hizo lakini hakuzitilia maanani kwani wakati wa mvua ajali kama hizo ni za kawaida sana.
“Kaka hadi bia imepoa!” Yule Mhudumu alipita tena kwenye ile mea aliyokaa Amata.
“Oh, sorry,” akamjibu kasha akainua chupa na kujijiminia mafunda kadhaa, alipoishusha ilikuwa nusu tu.
Akaitazama tena ile simu akabofya tarakimu nyingine, akaweka sikioni, simu ikaita na kuita haikupokelewa kama ilivyokuwa kwa simu za nyumbani za Chiba na Madam S, akashusha pumzi. Nini kinaendelea? Akajiuliza. Akarudia kuipiga namba ya mwisho, akaweka simu sikioni, baada ya dakika moja ile simu ikakwapuliwa na sauti nyororo ya kike ikasikika tofauti na alivyotegemea.
“…Polisi Kituo cha Kati, nikusaidie nini?” ile sauti ikauliza.
“Mwenye Ofisi, Inspekta Simbeye yupo?” Kamanda akauliza.
“…Inspekta leo alitoka kama mida ya saa tisa alasiri, hajarudi bado…” Yule mwanadada akajibu.
“Alisema kuwa atarudi au aliacha maagizo yoyote?” Kamanda akauliza.
“…alisema tu kuwa angerudi kabla ya saa kumi na ni kawaida yake kutoka saa tisa na kurudi saa kumi kila siku, lakini leo mpaka sasa hajarudi…” sauti ile iliendelea kueleza.
“We umeingia kazini saa ngapi?” akamwuliza.
“…nimeingia saa nane nitatoka saa nne usiku… samahani lakini naogea na nani?” Yule mwanadada alipouliza hivyo simu ikakatika.
Ndipo Kamanda alipojikuta hayuko peke yake mezani, mbele yake kulikuwa na mwanamke mmoja aliyevaa vazi refu jeusi, hijab na kujificha uso wote isipokuwa macho. Kamanda Amata akamtazama mtu huyo kwa tuo, akainua chupa yake na kupiga funda la mwisho, alipoishusha ilikuwa haina kitu ndani.
“Kwa nini unapenda kudhalilisha dini ya watu? Unaingia baa na vazi kama hilo?” Kamanda akaanza uchokozi, lakini Yule mtu hakujibu kitu, alikuwa akimwangalia tu. Jinni au! Akajiwazia, kabaridi ka haja kakapita kutoka utosini mpaka unyayoni.
§§§§§§
GINA aliegesha gari mita mia mbili hivi kutoka katika lango la kuingilia nyumba ya Madam S kule Masaki, akateremka na Jasmine akafanya vivyo hivyo, kisha wote wawili wakarudi taratibu wakiachina nafasi ya mita kadhaa katikati.
Lango la mbele lilikuwa limefungwa, Gina alitazama huku na huko hakuona hata dalili ya binadamu kupita myaa ule, isipokuwa manyunyu tu ya mvua yalikuwa yakimnyurunyuta mwilini mwake. Akajipapasa katika kiuno cha suruali yake na kufatua kijipini chenye ncha mbili zilizojikunja kwa mtindo wa pekee, kishapo akachukua kipini kingne kutoka kwenye kibanio cha nywele zake, akatanguliza kile chenye ncha mbili katika tundu la funguo ya lango hilo, akachukua kile cha tatu na kukitumbukiza kati, akafanya manuva kidogo tu, kitasa kutoka Uingereza kikafyatuka na kuuruhusu lango lile kuwa wazi.
Skunde mbili zikapita, ya tatu na ya nne bila Gina kuingia ndani ya wigo ule mkubwa, akatazama tena usalama, bado barabara ilikuwa tupu, hakumuona Jasmine, moja kwa moja akajua kuwa kwa vyovyote keshajiweka katika kona maalum ya kumlinda swahiba wake. Akaingia ndani ya wigo huku bastola yake aina ya Winchester ikiwa mkononi. Akatembea kwa hadhari kubwa huku na huko akitazama hakuona mtu. Hatua tatu kuelekea mlango wa nyumba hiyo, ndipo alipoona kitu kilichomshtua sana, akasimama mapigo ya moyo yakimwendea kasi kifuai mwake.
Mbele yake kulikuwa na mwili wa Binadamu uliolala chali ukiitupa mikono yake huku na huko, hakuwa na uhai. Gina akajiweka tayari kwani aliona huo unaweza kuwa mtego kwake, akatazama jumba la Madam S, taa za ndani zilikuwa zikiwaka kwa mwanga wa kupendeza, ina akajikuta anaishiwa nguvu, akainua mkono wake na kuizungusha saa yake kwa namna ya pekee kasha akaisogeza karibu na kinywa chake.
“…Jasmine …” akaita, hakupata jibu, akazidi kuingiwa na wasiwasi. Dina akatulia pembeni ya ule mwili, akahisi kama kuna mtu anayekuja nyuma yake, akakamata bastola yake barabara, liwalo na liwe, akageuka ghafla tayari kwa shambulizi, hakuna mtu.
Shiit! Akajisemea. Akauruka ule mwili na kuufikia mlango wa nyumba ile kubwa, akatoa gloves mfukoni na kuivaa, kisha akashika kitasa kwa mkono wa kushoto uliokuwa na gloves akaingia ndani ya sebule pana, iliyomlaki bila hiana. Kila kitu kilikuwa katika utulivu wa hali ya juu sana, hakukuonekana kama kulikuwa na purukushani yoyote ndani ya nyumba hiyo, akajivuta kuelekea chumba cha Madam S, akaufikia mlango na kuujaribu, ulikuwa umefungwa. Akatumia hila ileile na kuufungua. Hata chumbani kulikuwa tulivu kabisa, hakukuwa na ishara yoyote iliyoonesha kama kulikuwa na pambano la kufa na kupona.
Akaenda pembeni mwa kitanda upande wa kichwani, akachuchumaa na kubonya vijinamba Fulani vya kificho ambavyo kwa mtu wa kawaida huwezi kuvigungua mpaka mmiliki akuoneshe. Droo moja ikafunguka na ndani yake ikajifunua kompyuta kubwa ika simama mbele yake, Gina akatikisa kichwa juu chini, kwani alijua kama hiyo kompyuta haipo mahala pake basi hali ya Taifa iko hatarini. Alikumbuka maneno ya Madam S siku alipomkaribisha nyumbani kwake kwa mara ya kwanza.
….heri mimi nife lakini hii kompyuta ibaki. Nikifa au nikipotea kabla hamjatangaza kifo change hakikisheni mnang’oa kompyuta hii na kuikimbiza Shamba kisha mtangaze matanga. Siri yote ya Taifa hili ipo hapa, mipango yote mibaya na mizuri ipo humu, watu wote wabaya na wazuri wapo humu…
Gina alijikuta analia machozi peke yake, nifanyeje, niondoke nayo? Akajiuliza, nitaifikisha Shamba salama? Akajiuliza bila majibu. Gina alijikuta kachanganyikiwa, hajui la kufanya, aichukue au aiache, kichwani mwake alielewa kuichukua kompyuta hiyo ina maana kuwa Madam S kafa au katoweka, na je kama kuna wanaotaka na wameshindwa kuipata hatoweza kuwa kawarahisishia kazi?
Ulikuwa ni mgongano mkubwa wa mawazo kati ya roho, moyo na ubongo wake, akaamua kuiacha. Akabofya tena zile tarakimu na ile kompyuta ikajirudisha ndani taratibu na kujigia mahala pake. Gina akashusha pumzi ndefu, akaitazama bastola yake na kunyayuka taratibu, akaufuata mlango na kutoka akiufunga nyuma yake.
ITAENDELEA.
SEHEMU YA PILI
SEHAMU YA TATU
SEHEMU YA NNE
SEHEMU YA TANO
MTUNZI: Richard MWAMBE
1
Mbowe club saa 1:23 usiku
RADI kali ilipasua anga na kufanya mchoro wa kutisha, mwanga wake ulilipoteza giza kwa sekunde kadhaa, kila kilichojificha kilionekana wazi.
Hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa nje muda huo. Ni mvua kubwa na ngurumo za kutisha zilitawala kila kona, ilikuwa ni hali ya kuogofya sana. Mifereji na mito ya dhalura ilianzishwa na maji ya mvua hiyo.
Kama ilivyo ada katika jiji la Dar es salaam, barabara zote zilikuwa zimejaa maji, kama ukiwa dereva mgeni basi hutoweza kujua ni wapi barabara ilipo. Sehemu kubwa ya mji hasa katikati ya jiji gari nyingi ziliegeshwa kando ya barabara kusubiri mvua iishe lakini haikuwa hivyo kwani mvua ilikazana zaidi ya saa nne.
Wakati hayo yote yakiendelea, ndani ya ukumbi mkubwa wa starehe unaojulikana kama ‘Mbowe Club’ watu hawakuwa wakijua kama nje kuna mvua, disco liliendelea kwa nguvu zote, watu walicheza, wakanywa na kuburudika. Katika kaunta kubwa ya ukumbi huo kulikuwapo walevi kadhaa ambao tayari walikwishabadilisha lugha ya mawasiliano kutoka Kiswahili na kuwa Kiingereza.
Gina binti Komba Zingazinga alikuwa ni miongozi mwa watu wachache waliokuiwa wamesaliwa na akili zao na utashi pia, alikuwa akinywa kinywaji chake taratibu huku jamaa mmoja akijitahidi kumzengea zengea lakini asifanikiwe. Kila wakati alionekana kuitazama saa yake aliyoivaa mkononi na aliposhusha mkono aliinua ule uliokamata ile bilauri yenye kiuno iliyojaa mvinyo kutoka Dodoma. Baada ya kupiga funda moja kasha la pili aliiteremsha taratibu na kuiweka juu ya mbao mwororo iliyoifunika na kuipendezesha kaunta ya ukumbi huo. Macho yake yalikuwa yakizunguka huku na kule yakitazama au kutafuta kitu ambacho hata yenyewe hayakukijua.
Upande wa pili wa ukumbi huo, kwenye sakafu iliyojengwa juu kidogo na ili uifikie itakulazimu kuzikwea ngazi kadhaa, kulikuwako watu watatu, wawili wanaume na mmoja mwanamke. Mwanaume mmoja alikuwa na tambo kubwa lililojaa kimazoezi, enzi za utoto wetu tungeweza kumwita Pawa, lakini enzi hizi wanamwita Baunsa, yote hayo ni mabadiliko ya nyakati. Watu wale watatu walikuwa wakiongea jambo Fulani na meza yao ilikuwa imechakazwa kwa pombe kalikali na sahani za nyama zilizokuwa zikipishana, vyote hivyo vilimiminwa katika matumbo hayo matatu. Ilikuwa ni vigumu kusikia nini wanachokiongea kutokana na muziki mkubwa uliokuwa ukipigwa ndani humo. Kati ya kaunta alipokuwapo Gina na ule upande kulitenganishwa na kundi la vijana waliokuwa wacheza muziki huo kwa mitindo mbalimbali. Gina alihakikisha hapotezi macho yake upande ule kwani mwili wake ulikuwa ukisisimka mara kwa mara na hiyo kwake ilikuwa ni ishara ya hatari.
Dakika chache baadae alimuona Yule mwanamke akiinuka na kutoka katika vile viti, akitembea kwa mwendo wa ki-levi levi. Akamtazama na kujua mara moja kuwa alikuwa anaelekea chooni, Gina akajikuta akishuka kutoka kwenye kiti kirefu alichokuwa amekalia, akaigugumia pombe yake yote kinywani mwake, kasha akavuta hatua fupifupi akikumbana na walevi na wacheza muziki akaelekea kule alikokwenda Yule mwanamke.
Halafu nitamwuliza nini? Akajiuliza pa si na kupata jibu. Lakini aliendelea kuvuta hatua kuelekea kule chooni, akapinda kona ya kwanza na kuingia kwenye milango Fulani iliyokuwa ikielekea huko atakako, mbele kidogo alimuona Yule mwanamke akiingia katika moja milango ya vyoo vile. Gina; mkono wa kulia ukiwa nyuma ya suruali yake ndani kidogo ya jaketi lake, sikwambii alishika kitu gani, aliuendea ule mlango, mara ghafla akaanza kuhisi kitu kikimfinya mkononi mwake, ilikuwa ni saa kubwa ya mkononi, saa yenye uwezo wa kupokea nukushi, kupiga picha za mjongeo na mnato, yenye uwezo wa kurekodi sauti na pia unaweza kuitumia kama simu. Akainua mkono na kubofya kitufe Fulani kasha akasubiri kidogo. Wakati akisubiri kijimkanda hicho chembamba kikitoka kwenye saa yake, Yule mwanamake bado alikuwa chooni.
Mama yuko mahututi Shamba, Tena Saan Aisee! Uikuwa ni ujumbe uliosomeaka hivyo katika kile kijimkanda. Akakikata na kukitia mfukoni mwake kisha akaanza safari ya kutoka ndani ya Klabu ile, akili yake ilikwisha sahau juu ya Yule mwanamke, akapita mlangoni na kukumbana kikumbo na Yule mwanaume mwenye tambo kubwa, akielekea kule choo cha wanawake, Gina akasukumwa pembeni; na Yule bwana akapita.
Nje ya Klabu hiyo ndipo alipokutana na mvua ya kutisha, akapachua kikofia katika ukosi wa jaketi lake na kukivaa kisha akaliendea gari lake, mita kadhaa kabla hajalifikia akapiga breki na kuacha kinywa wazi, hakuamini anachokiona. Vioo vyote vya gari yake vilikuwa vimevunjwa, tairi hazina upepo na ndani kulijaa maji ya mvua. Wameiba? Akajiuliza, kisha kwa mwendo wa tahadhari akasogea kwenye lile gari, juu ya kiti cha dereva kulikuwa na bahasha ngumu ya khaki, akatazama huku na kule, alipojihakikishia usalama akaingiza mkono kwa minajiri ya kuichukua ile bahasha ijapokuwa ilionekana kulowana.
Daraja la sarenda saa 1:55 usiku.
BMW nyeusi iliyokuwa iking’azwa kwa mwanga wa radi, ilshuka katika barabar hiyo ya Kenyata kwa kasi sana ikitokea maeneo ya Masaki. Ilipofika katika makutano ya barabar hiyo na ile ya Ally Hassan Mwinyi mkabala na Ubalozi wa Ufaransa iliingia barabara kubwa bila kungalia usalama huku ikirusha maji juu kutokana na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha usiku huo.
Madam S alikuwa katulia kwenye usukani akiiongoza gari hiyo ya Mwingereza kwa umahiri mkubwa. Akakunja ushoto na kukanyaga mafuta kueleka mjini. Ilikuwa ni tabu kuona mbele kutokana na wingi wa mvua, barabara imejaa maji, umeme umekatika, ilikuwa ni shida juu ya shida. Madam S hakujali alilikanyaga daraja la Salenda na kuendelea mbele, lakini kabla hajalimaliza, hamad, kulikuwa a mwili wa mwanadamu uliolala barabarani huku mikono yake ikiwa imefungwa nyuma. Akaiyumbisha gari kuukwepa mwili huo, gari ikasota na kukosa muelekeo, akarudisha usukani kulia kuukwepa mwamba wa daraja, akaknyaga krachi na kuachia mafuta kasha akatoa gia ya tano na kushusha ya nne, kutahamaki gari yake ilikuwa ikihamia barabara ya pili, akakanyaga breki lakini ikashindwa kusimama, akaknyaga tena breki bado gari ilikuwa ikiendelea, ikapanda tuta lakutenga barabara, ikajipigia na kutua barabara ya pili, akili ikamrudia, akavuta breki ya mkono na ile BMW ikaserereka na kujizungusha.
Kishindo kikubwa kikasikika, BMW iligongana na Land Rover Defender, ikaangushwa pembeni. Madam S akajikuta kwenye pori la mikoko chini ya daraja la Salenda, akafyatua mkanda, akapiga kioo cha mbele kwa kukikanyaga kwa mguu, akatoka, akajipapasa na kukuta bastola zake zipo salama.
Damu zilizikuwa zikitiririka semu ya paji la uso juu kidogo ya jicho la kulia, wakati akijitahidi kusimama, radi kali ilipiga na kufanya mwanga mkubwa uliong’aza vichaka vyote, Madam S akaona mbele yake kama kivuli cha mtu aliyesimama nyuma yake. Akajua ni mawenge ya ajali tu, akageuka nyuma na mara ghafla akakutana na pigo la kitu kizito kilichotua katikati ya paji la uso, akayumba vibaya lakini mikono yake tayari ilikuwa imekwishachomoa bastola zake, kabla hajafyatua akafunikwa na gza nene lililomfanya ashindwe kuona chchote, akaanguka kama mzigo na bastola zikimtoka mikononi mwake.
Ofisi ya usalama wa taifa saa 2:00 usiku.
MAAFISA wa Idara ya Usalama wa Taifa walikuwa wakiendelea na shughuli zao kama kawaida usiku huo. Katika moja ya ofisi za jengo hilo, vijana wawili na msichana mmoja walikuwa bize kutazama luninga nyingi zilizowazunguka zinazoonesha maeneo mbalimbali muhimu ya Jiji la Dar es salaam. Kupitia luninga hizo waliweza kuona moja kwa moja kile kinachotokea kwenye maeneo hayo kama Uwanja wa ndege, Bandarini, Stesheni ya Treni, Uwanja wa Sabasaba, Makao makuu ya Rais na maeneo mengine mengi ambayo yamepewa umuhimu wa pekee kwa sababu hii au ile.
Avant, msichana mbichi wa miaka takribani thelathini hivi alikuwa katingwa kuangalia tukio la ajali iliyotokea daraja la Salenda, bado alikuwa anapata shida kujua hasa nini kinaendelea kutokana na ile picha kufichwa na mvua ilikua ikinyesha eneo hilo lakini kila ilipokuwa radi ikipiga ndipo alipoweza kuona kitu, baada ya dakika kadhaa alipuuza na kuendelea kutazama maeneo mengine.
Mubah akajikohoza kidogo na kumgutusha Avanti kutoka pale alipokuwa akitazama.
“Si ukapime, au Mama yako anajua?” Avanti akamtania Mubah.
“Unanianza we mrembo, mi nasubiri time hapa niingie viwanja!” Mubah akajibu, huku akitoka kwenye kiti chake na kukiendea kile alichoketi Avant, akasimama nyuma yake, machoye akiwa kayakaza kwenye ile luninga.
“Shiit! Avant, nini hicho?” akauliza huku akisogea jirani zaidi.
“Ajali, imetokea kama dakika kumi hivi,” Avant akajibu.
“Kwa nini usipige simu polisi wawahi kama kuna chochote cha kuokoa?” Mubah akahoji.
“Sasa Mubah, Salenda pale kituo kipo jirani wataenda tu,” akaeleza huku akimtazama Mubah usoni.
“Yaani wewe! Kitendo cha kuitega kamera pale hatukufanya kwa makosa, lile ni eneo nyeti sana, kama ni ajali lazima polisi wafike mapema ili kuondoa kilichopo, pale vipngozi asilimia 99 wanapita, ikiwa hujuma utalaumiwa wewe kwani ndio eneo lako la kutazama leo!” Mubah akalalamika huku akiliendea kabati dogo lililo hapo jirani.
Avant akainua simu na kubofya tarakimu Fulani Fulani kasha akatoa taarifa hiyo kituo cha polisi cha Salenda. Haikupita dakika tano tayari kupitia luninga yake aliweza kuona gari na nyendo za polisi eneo hilo bila kujali mvua iliyopo. Avant aliendelea kutazama huku akigonga gonga karamu yake.
§§§§§
Gina alivuta hatua na kuingia katika lango kuu la Ofisi Nyeti, Shamba, akabofya namba zake za siri, kasha akaweka kiganja chake juu ya kioo Fulani kilichopo mlangoni na baada ya hapo akafanya kama anachungulia, kijimwanga chekunfu kikapita kati ya macho yake na kitasa cha ule mlango kikafyatuka, akaufungua na kuingia ndani. Moja kwa moja akaingia chumba Fulani na kuvua jaketi alilovaa, akabadilisha nguo na kurudi katika hali ya ukavu, akatoka na kutembea mwendo mfupi kabla hajagonga mlango Fulani kwa mtindo wa pekee na mlango ule ukafunguliwa.
“Karibu Gina!” Dkt Jasmine akamkaribisha na nukta chache baadae akampatia kikombe cha kahawa.
“Hawajafika?” Gina akauliza.
“Hapana, we ndiye wa kwanza, leo sijui kuna nini, labda kwa sababu ya mvua,” Dkt. Jasmin akaeleza.
Gina akashusha pumzi ndefu, mazungumzo mengine yakaendelea huku wakiwasubiri wengine, kila mara walikuwa wakitazama saa zao, hakuna simu wa taarifa yoyote iliyokuwa ikifika katika nyumba hiyo, Gina na Jasmine wakaanza kupata wasiwasi. Jasmine akainua uso na kuitazama saa kubwa ya ukutani, ikamwonesha kuwa ni saa 3:15 usiku.
“Hapana Gina, hii sio kawaida, tuanze kuwatafuta mmoja baada ya mwingine,” Dkt. Jasmin akamweleza Gina, kasha wote wawili wakaenda kwenye chumba maalumu cha mawasiliano, ndani ya chumba hicho ambamo ndiyo ofisi ya kudumu ya Chiba wa Chiba kulijawa na makompyuta na luninga nyingi huku na kule, simu za upepo, za kawaida na zile za satellite zilikuwepo. Kila kitu kilikuwa kinafanya kazi kwani haikuruhusiwa kuzima chochote labda tu kama kuna matengenezo, kila mmoja akaketi katika kiti chake na kuanza kucheza na simu zao za siri zilizounganishwa moja kwa moja.
Hakuna simu ya mkononi iliyokuwa ikipatikana si ya Madam S wala ya nani, walipigwa na butwaa na kubwa simu za nyumbani zote zilikuwa zikiita bila kukoma hazikupokelewa. Gina akamgeukia Dkt. Jasmine.
“Oya Shost, hapa ni mguu kwa mguu nyumba moja baada ya nyingine tukapate kujua kilichojiri,” Gina akamwambia Jasmine kasha wote wakaingia vyumbani na walipotoka walikuwa katika mavazi ya kazi, kila moja alibeba silaha anazoamini zingemfaa usiku huo kwani hawakujua hatari itakayowakabili. Wakiwa katika harakati hizo ndipo Gina alipokumbuka ile bahasha.
“Nisubiri Jasmine!” akarudi kwenye kile chumba akaichukua ile bahasha, bado ilikuwa imelowa akaichana taratibu na kuitoa karatasi ya ndani kwa uangalifu.
“Nini Gina?” Jasmine akauliza.
“Hii bahasha niliiokota kwenye ari yangu lakini sikuwahi kuifungua ndani,” akamjibu.
Gina alibaki kakodoa macho baada ya kukutana na kichwa cha habari kikubwa kilichosomeka ‘KITISHO!’ kisha chini yake kuliandikwa sentensi moja tu
Mwisho wa zama zenu umefika, mtaongea na Mzee Ngurumo.
Maneno hayo yalizigonga kwa nguvu nyoyo za wadada hawa, wakabaki wakitazamana, wkageuza macho yao wakaitazama tena ile karatasi.
“Gina!” Jasmine akaita.
“Jasmine!” naye akaitikia na wote wakatoka na kuingia kwenye gari ya Jasmine na kuondoka eneo hilo.
§§§§§§
Kerege – bagamoyo saa 4:07 usiku
TOYOTA Hilux Double Cabins, iliingia taratibu getini na kuegeshwa karibu na bustani ya maua iliyotengenezwa ndani ya ngome kubwa iliyobeba jengo la kifahari kuliko fahari yenyewe. Walinzi kadhaa walionekana kwenye kona zake, hawakushughulika kabisa na gari hiyo bali kila mmoja alishika lindo lake.
Dereva akashuka na watu wengine kama watatu hivi wakashuka, wakazunguka nyuma na kufungua funiko kubwa la alluminium lililotengenezwa ili kufunika mzigo uliopo ndani yake.
“Washushe hao, kisha wapeleke Kuzimu,” mmoja wa wale vijana aliyekuwa ameketi mbele akawaagiza wenzake kasha yeye akazikwea ngazi kulielekea jengo hilo lililoendezeshwa kwa taa zenye marembo mbalimbali.
Sauti za viatu vyenye kisigino kigumu zilisikika zikitembea lakini aliyevaa hakuonekana, Bwana Mpaya alibaki kusimama na kutazama kule sauti ile ilikokuwa ikitokea na asione mtu zaidi ya giza lililomlaki isipokuwa aliposimama yeye mwanga ulikuwapo na kufaya nuru ya kupendeza. Kasha ukimya ukatawala na sauti nzito ikalipenya lile giza.
“Ndio Bwana Mpaya, karibu sana, natumaini umekamilisha nililokutuma, sivyo?” alikuwa ni Pancho Panchilio aliyeyafikia masikio ya Mpaya aliyekuwa amesimama katikati ya sebule pana lakini asimwone anayeongea naye, isipokuwa sauti tu.
“Ndiyo Boss, tumewaleta lakini hali zao ni mbaya sana,” akaeleza.
“Vizuri sana, nani na nani mmempata?” akauliza tena.
“Tumempata Boss wao na Mtaalamu wao wa kompyuta,” akajibu.
“Ha! Ha! Ha! Ha! Ha!” akacheka cheko la pesa.
“Ok, wape vijana posho yao kama nilivyokwambia kisha unitafutie kichwa cha Kamanda Amata, huyu hasa ndiye mwiba kwangu, nataka apotee kwenye uso wa nchi ili binadamu tule vizuri, kuna pesa ndefu sana nimeiandaa mkilikamilisha hili,” Pancho akiwa mafichoni mwake akakohoa kidogo wakati Mpaya alikuwa akitoka, “Sikia Mpaya, hakikisha ukimuua Kamanda Amata, mkate kichwa, kisha kiwiliwili mkichome moto na kichwa mniletee, mbwa wangu hawajala nyama siku nyingi sana, maana Yule ni shetani anaweza kujiunganisha tena halafu akaangusha balaa, kwa heri!”
Alipomaliza kusema hayo na taa ndani ya jengo lile zikazimika.
2
KAMANDA Amata akaitazama gari yake aia ya Subaru Forester jinsi ilivyochakazwa kwa risasi, akashusha pumzi ndefu.
Wadude hawa wangeniua! Akajisemea moyoni huku akijaribu kuiwasha nayo ikawaka, akairudisha barabarani na kushika njia ya kwenda mjini, alijipapasa mifukoni hakuiona simu yake, wala saa yake mkononi haikuwepo. Any way! Akajipa moyo. Huku akiendelea kuutafuta mji wa Dar es salaam, saa ya ndani katika gari yake ilimwonesha kuwa ni saa tano za usiku.
Gina sijui kama atanielewa, maana tulikubaliana saa moja na robo, labda nitamkuta! Akaendelea kuongea na nafsi yake, huku akiiacha Gongo la Mboto na kuitafuta Uwanja wa Ndege. Katikati ya safari yake akafungua redio ndani ya gari na kusikiliza kinachoendelea. Ilikuwa ni kituo kimoja cha redio binafsi kikirusha habari hiyo ya dharula iliyoyanasa masikio ya Amata usiku huo.
…Mwili wa Mheshimiwa huyo umekutwa sakafuni bila uhai na kitu kama matundu ya risasi yakionekana kifuani mwake. Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wake ili kuwakama waliohusika na mauaji hayo…
Amata akakanyaga breki kali na kuitoa gari barabarani kwani taarifa hiyo haikujitosheleza kwake, akaegesha gari pembeni na kutazama huku na kule hakuona mtu kupita eneo hilo, pembeni yake kulikuwa na bar iliyokuwa ikiendelea kuburudisha watu kwa vinywaji na vilaji, akashuka na kuiendea, alipofika tu akakutana na mwanadada mrembo aliyevalia nguo nyeupe juu na sketi nyeusi chini.
“Karibu kaka, karibu kiti,” Yule dada akamkaribisha Amata huku akifuta meza iliyokuwa hapo. Ijapokua haikuwa nia ya Kamanda kuketi, akajikuta amefanya hivyo, “Pole!” neon hilo likaupasua moyo wa Amata akamtazama Yule dada Mhudumu wa bar.
“Pole ya nini?” akauliza
“Una damu kichwani,” akamwambia.
“Shiit!” akang’aka na kujigusa, kweli akahisi maumivu na kitu kama jeraha.
“Asante sana!” akamjibu, “Unaweza kunisaidia simu yako?” akamwuliza.
“Haina salio lakini, halafu ni kisimu cha tochi,” akajibu kwa aibu.
“Naomba hivyo hivyo.”
Yule mwanadada akachomoa simu yake akampatia Amata. Ilikuwa ni simu iliyochakaa, iliyoonekana kupita katika mikono mingi ya watu mpaka kuifikia mikono hii ya huyu Mhudumu wa baa. Ilifungwa kwa mipira ya manati, betri lake lilishikiliwa na kipande cha mpira wa manati. Hakujali, aliitazama vyema kasha akaanza kubofya hapa na pale.
“Haina vocha hiyo!” Yule Mhudumu akaeleza tena.
“Usijali, kaniletee Bia baridi sana bila glass tafadhali,” Kamanda akamwagiza Yule dada lakini alilotaka yeye haikuwa bia ila zile dakika mbili za kubaki peke yake. Vidole vyake vikaanza kutomasa tarakimu Fulani Fulani na alipomaliza, akapumzika, wakati huo bia yake ilikuwa imefika, akaigusa, akamwonesha Yule Mhudumu alama ya dole gumba, kisha akabaki na hamsini zake.
Meseji iliyofuata katika simu hiyo ilikuwa ni kutoka katika kampuni moja ya simu nchini, Kamanda Amata alikuwa amechukua muda wa hewani kwa namna yao ya siri na sasa simu ile Kimeo ilipata uhai.
Akaanza kupiga namba za maswahiba wake wa kazi, Chiba; simu haikuita kabisa, Madam S vivyo hivyo, akaduwaa wa sekunde kadhaa, haikuwa kawaida kwa watu hao kuwakosa kwenye simu, akili ya Kamanda ikiruka chogo chemba. Mbele yake kulikuwa na luninga kubwa iliyokuwa ikionesha matukio mbalimbali ya Kitaifa na lile lililomvutia ni ajali ya Salenda, alisahau kupiga simu na kutazama tukio lile. Kamanda Amata alikaza jicho kutazama picha hizo lakini hakuzitilia maanani kwani wakati wa mvua ajali kama hizo ni za kawaida sana.
“Kaka hadi bia imepoa!” Yule Mhudumu alipita tena kwenye ile mea aliyokaa Amata.
“Oh, sorry,” akamjibu kasha akainua chupa na kujijiminia mafunda kadhaa, alipoishusha ilikuwa nusu tu.
Akaitazama tena ile simu akabofya tarakimu nyingine, akaweka sikioni, simu ikaita na kuita haikupokelewa kama ilivyokuwa kwa simu za nyumbani za Chiba na Madam S, akashusha pumzi. Nini kinaendelea? Akajiuliza. Akarudia kuipiga namba ya mwisho, akaweka simu sikioni, baada ya dakika moja ile simu ikakwapuliwa na sauti nyororo ya kike ikasikika tofauti na alivyotegemea.
“…Polisi Kituo cha Kati, nikusaidie nini?” ile sauti ikauliza.
“Mwenye Ofisi, Inspekta Simbeye yupo?” Kamanda akauliza.
“…Inspekta leo alitoka kama mida ya saa tisa alasiri, hajarudi bado…” Yule mwanadada akajibu.
“Alisema kuwa atarudi au aliacha maagizo yoyote?” Kamanda akauliza.
“…alisema tu kuwa angerudi kabla ya saa kumi na ni kawaida yake kutoka saa tisa na kurudi saa kumi kila siku, lakini leo mpaka sasa hajarudi…” sauti ile iliendelea kueleza.
“We umeingia kazini saa ngapi?” akamwuliza.
“…nimeingia saa nane nitatoka saa nne usiku… samahani lakini naogea na nani?” Yule mwanadada alipouliza hivyo simu ikakatika.
Ndipo Kamanda alipojikuta hayuko peke yake mezani, mbele yake kulikuwa na mwanamke mmoja aliyevaa vazi refu jeusi, hijab na kujificha uso wote isipokuwa macho. Kamanda Amata akamtazama mtu huyo kwa tuo, akainua chupa yake na kupiga funda la mwisho, alipoishusha ilikuwa haina kitu ndani.
“Kwa nini unapenda kudhalilisha dini ya watu? Unaingia baa na vazi kama hilo?” Kamanda akaanza uchokozi, lakini Yule mtu hakujibu kitu, alikuwa akimwangalia tu. Jinni au! Akajiwazia, kabaridi ka haja kakapita kutoka utosini mpaka unyayoni.
§§§§§§
GINA aliegesha gari mita mia mbili hivi kutoka katika lango la kuingilia nyumba ya Madam S kule Masaki, akateremka na Jasmine akafanya vivyo hivyo, kisha wote wawili wakarudi taratibu wakiachina nafasi ya mita kadhaa katikati.
Lango la mbele lilikuwa limefungwa, Gina alitazama huku na huko hakuona hata dalili ya binadamu kupita myaa ule, isipokuwa manyunyu tu ya mvua yalikuwa yakimnyurunyuta mwilini mwake. Akajipapasa katika kiuno cha suruali yake na kufatua kijipini chenye ncha mbili zilizojikunja kwa mtindo wa pekee, kishapo akachukua kipini kingne kutoka kwenye kibanio cha nywele zake, akatanguliza kile chenye ncha mbili katika tundu la funguo ya lango hilo, akachukua kile cha tatu na kukitumbukiza kati, akafanya manuva kidogo tu, kitasa kutoka Uingereza kikafyatuka na kuuruhusu lango lile kuwa wazi.
Skunde mbili zikapita, ya tatu na ya nne bila Gina kuingia ndani ya wigo ule mkubwa, akatazama tena usalama, bado barabara ilikuwa tupu, hakumuona Jasmine, moja kwa moja akajua kuwa kwa vyovyote keshajiweka katika kona maalum ya kumlinda swahiba wake. Akaingia ndani ya wigo huku bastola yake aina ya Winchester ikiwa mkononi. Akatembea kwa hadhari kubwa huku na huko akitazama hakuona mtu. Hatua tatu kuelekea mlango wa nyumba hiyo, ndipo alipoona kitu kilichomshtua sana, akasimama mapigo ya moyo yakimwendea kasi kifuai mwake.
Mbele yake kulikuwa na mwili wa Binadamu uliolala chali ukiitupa mikono yake huku na huko, hakuwa na uhai. Gina akajiweka tayari kwani aliona huo unaweza kuwa mtego kwake, akatazama jumba la Madam S, taa za ndani zilikuwa zikiwaka kwa mwanga wa kupendeza, ina akajikuta anaishiwa nguvu, akainua mkono wake na kuizungusha saa yake kwa namna ya pekee kasha akaisogeza karibu na kinywa chake.
“…Jasmine …” akaita, hakupata jibu, akazidi kuingiwa na wasiwasi. Dina akatulia pembeni ya ule mwili, akahisi kama kuna mtu anayekuja nyuma yake, akakamata bastola yake barabara, liwalo na liwe, akageuka ghafla tayari kwa shambulizi, hakuna mtu.
Shiit! Akajisemea. Akauruka ule mwili na kuufikia mlango wa nyumba ile kubwa, akatoa gloves mfukoni na kuivaa, kisha akashika kitasa kwa mkono wa kushoto uliokuwa na gloves akaingia ndani ya sebule pana, iliyomlaki bila hiana. Kila kitu kilikuwa katika utulivu wa hali ya juu sana, hakukuonekana kama kulikuwa na purukushani yoyote ndani ya nyumba hiyo, akajivuta kuelekea chumba cha Madam S, akaufikia mlango na kuujaribu, ulikuwa umefungwa. Akatumia hila ileile na kuufungua. Hata chumbani kulikuwa tulivu kabisa, hakukuwa na ishara yoyote iliyoonesha kama kulikuwa na pambano la kufa na kupona.
Akaenda pembeni mwa kitanda upande wa kichwani, akachuchumaa na kubonya vijinamba Fulani vya kificho ambavyo kwa mtu wa kawaida huwezi kuvigungua mpaka mmiliki akuoneshe. Droo moja ikafunguka na ndani yake ikajifunua kompyuta kubwa ika simama mbele yake, Gina akatikisa kichwa juu chini, kwani alijua kama hiyo kompyuta haipo mahala pake basi hali ya Taifa iko hatarini. Alikumbuka maneno ya Madam S siku alipomkaribisha nyumbani kwake kwa mara ya kwanza.
….heri mimi nife lakini hii kompyuta ibaki. Nikifa au nikipotea kabla hamjatangaza kifo change hakikisheni mnang’oa kompyuta hii na kuikimbiza Shamba kisha mtangaze matanga. Siri yote ya Taifa hili ipo hapa, mipango yote mibaya na mizuri ipo humu, watu wote wabaya na wazuri wapo humu…
Gina alijikuta analia machozi peke yake, nifanyeje, niondoke nayo? Akajiuliza, nitaifikisha Shamba salama? Akajiuliza bila majibu. Gina alijikuta kachanganyikiwa, hajui la kufanya, aichukue au aiache, kichwani mwake alielewa kuichukua kompyuta hiyo ina maana kuwa Madam S kafa au katoweka, na je kama kuna wanaotaka na wameshindwa kuipata hatoweza kuwa kawarahisishia kazi?
Ulikuwa ni mgongano mkubwa wa mawazo kati ya roho, moyo na ubongo wake, akaamua kuiacha. Akabofya tena zile tarakimu na ile kompyuta ikajirudisha ndani taratibu na kujigia mahala pake. Gina akashusha pumzi ndefu, akaitazama bastola yake na kunyayuka taratibu, akaufuata mlango na kutoka akiufunga nyuma yake.
ITAENDELEA.
SEHEMU YA PILI
SEHAMU YA TATU
SEHEMU YA NNE
SEHEMU YA TANO