Maxence Melo
JF Founder
- Feb 10, 2006
- 4,230
- 13,415
Mkuu,thank you for stating this, jf inameanza kua huru hadi sasa watu wameanza ku-advocate violence na ku-post vitu vya ajabu. Nahisi amani yangu inachezewa sana na power ya cyber.
Baada ya mods kunifahamisha juu ya uvumi huu ilibidi niingie kuweza kufafanua juu yake. Kuna watu wanafurahia ku-advocate violence lakini nishauri kuwa ziangalieni posts vema; zilizokaa ki-shari tufahamisheni tuzipitie na kufanya verification.
Mkuu, si kama hakukataa.Si kweli, ina maana hakukataa bali alipokea?
Kwa mujibu wa Regia, hakuna hata mtu alom-approach na wala hakujakuwepo na kitu kama hicho.
Tetesi zikiingia JF, husambaa via sms na mpaka huko Kilombero zimefika. Wapiga kura wake wamechukizwa, wanaweza kumtoa roho bure! Yeye anachosema ni kuwa anaenda mahakamani kupinga matokeo, sasa anayeenda mahakamani anatumia hela hizo hizo za kuhongwa? Ili iweje?