josiah2008
Member
- May 22, 2010
- 51
- 23
Mgombea ubunge katika jimbo la Kilombero kwa tiketi ya CHADEMA Regia Mtema atapata ushindi mkubwa dhidi ya mgombea wa CCM Abdul Mteketa. Regia Mtema ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja kushawishi na kuwa na majibu ya matatizo ya muda mrefu ya wananchi wa jimbo la kilombero.
Mgombea wa CCM hana uwezo wa kujieleza kabisa hali iliyolazimu makada wa chama kuja kujaribu kukinusuru.Sofia Simba,Kingunge,Getrude Lwakatare pamoja na mjumbe wa halmashauri kuu CCM wote hawakuweza kubadili upepo wa mabadiliko.Hata JK alipokuja alishindwa kumnadi na kuishia kumwagia sifa mgombea udiwani wa kata ya Ifakara.
Regia Mtema amemalizia kampeni zake kwenye kata ya Lumemo mkutano ambao umevunja rekodi kwa idadi ya watu waliohudhuria.Kila mtu hapa anataka mabadiliko kitu ambacho huwezi kuamini kwani jimbo hili CCM walikuwa wamejichimbia mizizi sana.Walidiriki kusema hata ukiweka koti kwa tiketi ya CCM litashinda.
Kwa hali ilivyo Regia Mtema atapata kura za CHADEMA ,CUF na CCM kwani katika wagombea wote yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kuleta maendeleo hapa Kilombero na anakubalika.
Tumeshajiandaa vizuri majina yetu tumeshayaona asubuhi na mapema tunakwenda kutoa hukuma kwa kosa la kututawala kwa miaka 50 tukiwa kwenye nyumba za Tembe.
KILOMBERO4CHANGE
Mgombea wa CCM hana uwezo wa kujieleza kabisa hali iliyolazimu makada wa chama kuja kujaribu kukinusuru.Sofia Simba,Kingunge,Getrude Lwakatare pamoja na mjumbe wa halmashauri kuu CCM wote hawakuweza kubadili upepo wa mabadiliko.Hata JK alipokuja alishindwa kumnadi na kuishia kumwagia sifa mgombea udiwani wa kata ya Ifakara.
Regia Mtema amemalizia kampeni zake kwenye kata ya Lumemo mkutano ambao umevunja rekodi kwa idadi ya watu waliohudhuria.Kila mtu hapa anataka mabadiliko kitu ambacho huwezi kuamini kwani jimbo hili CCM walikuwa wamejichimbia mizizi sana.Walidiriki kusema hata ukiweka koti kwa tiketi ya CCM litashinda.
Kwa hali ilivyo Regia Mtema atapata kura za CHADEMA ,CUF na CCM kwani katika wagombea wote yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kuleta maendeleo hapa Kilombero na anakubalika.
Tumeshajiandaa vizuri majina yetu tumeshayaona asubuhi na mapema tunakwenda kutoa hukuma kwa kosa la kututawala kwa miaka 50 tukiwa kwenye nyumba za Tembe.
KILOMBERO4CHANGE