Bhbm
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 714
- 208
Asante sana kaka nadhani wewe umemaliza kila kitu.Mungu wangu!! kweli wewe ni mbumbumbu. Mpaka sasa hujajua tofauti ya watu wa aina ya Shibuda na wale wa aina ya Nape Nnauye? Kwa taarifa yako watu kama Nape wameonyesha kabisa kuwa wanatafuta uongozi kwa maslahi yao na sio taifa ndo maana hata baada ya kufanyiwa zengwe ameendelea kuwa mnyenyekevu kwa mafisadi akijua kabisa CHADEMA hamna maslahi. Watu kama Shibuda ni sawa na watenda dhambi waliomrudia mungu baada ya kupata madhara ya dhambi.
Umbumbumbu wako unajionesha zaidi pale unapokuwa hujui hata jinsi unavyoibiwa kodi yako na ccm na hujui hata mgawanyo wa mapato ulivyo ndo maana unataka kuona kama ilemela na nyamagana watapata elimu bure, lakini ungekuwa na ufahamu ungegundua kuwa elimu ni sera ya kitaifa hivyo hata kama uongozi wa jimbo ni mzuri kiasi gani bado utategemea uongozi wa kitaifa.
Nakuomba ndugu yangu zinduka usipende kubaki nyuma kila wakati; yaani tulipokuwa ktk kipindi cha kupigania uhuru aina ya watu kama wewe walikuwa wanatetea wakoloni, ulipokuja mfumo wa chama kimoja nyie mliendelea kuongelea vyama vingi, tuliporudi kwenye mfumo wa vyama vingi nyie mmebaki na mawazo ya chama kimoja, tunaingia kwenye utandawazi nyie bado mmelala usingizi mnafikiri bila ccm hamna Tanzania. MAWAZO MGANDO HAYO!!!