Rais wa Malawi Awananga Waandishi wa Habari wa Tanzania

Ukweli unauma!! Ni kweli vyombo vyetu vya habari havina wabunifu wa kujadili hoja, nilitegemea waandishi wetu wangekuwa wanatoa somo zaidi katika inshu nyingi kuelimisha jamii badala yake karibia waandishi wote wanaegemea kwenye kuripoti habari kutoka kwa wanasiasa zaidi. Vyombo vya habari vijifunze namna ya kujenga hoja zikakubalika kwenye jamii badala ya kukimbilia/kutegemea wanasiasa na watu wengine waropoke ndiyo wapate habari za kuandika.

Mkuu uko sahihi kabisa, waandishi wetu wanasubiri habari ya kuambiwa na mtu tu. Hawawezi kufanya uchambuzi, mimi kwa sasa huwa sinunui magazeti kwa kuwa kinachoandikwa ni ushabiki zaidi bila utafiti.
 
Pamoja na kwamba tuna matatizo ya uandishi na waandishi wa habari bt kwa hili wanapewa lawama zicizo zao.. Vyombo vya habari vichache makini viliripoti vizuri.. Baadhi ya magazeti yalitoa tahariri ya kuomba diplomasia ifanye kazi.. Wote tuliwacikia Membe & co walipokuwa wanaongea tough words (and I agree wit them).. Linapokuja suala la mipaka lazima tuwe wakali.. Kumbukeni Malawi walianza kabisa na shughuli za utafutaji mafuta kuonyesha kwamba walikuwa na ill intentions.. Ninaamini maneno makali yamesaidia kuwarudishia akili za kufikiri..

Sent from Kandahar..
 
Mwandishi hawezi sifiwa kwa kila aandikacho au akifaniacho utafiti.
Ni nani aliyetuelewesha kuwa kuna Ndege zinatafiti mafuta na Gesi ndani ya maji ya Ziwa Malawi?
Ni nani aliyetuambia kuwa ni makampuni ya Uingereza ndiyo yaliyopewa Kandarasi hiyo ya kutafuta mafuta na gesi?
JAMANI bado waandishi nawasifia kwa kutushtua kuwa hata ramani zetu ziko vibaya mpaka Ujumbe wa Tanzania ulipofika kwenye Kikao na kuonyesha vithibitisho vya mipaka hiyo kuwa vimekaliwa mpaka leo.
Kwa hiyo huyo Mama J Banda asiwachokoze watammwaga hadharani
 
huyu mama mbona kila siku anatoa matamko yasiyoeleweka si akae kimya Dipromasia ichukue mkondo wake.!
 
President Joyce Banda Sunday commended journalists in the country for their professional reporting on the wrangle between Malawi and Tanzania over Lake Malawi.


The President made the commendation in Lilongwe the during press conference soon after her arrival from Mozambique saying if journalists in the country reported in the same way their counterparts in Tanzania were doing, the two countries could have been involved in a war.


“Thank you so much for articulating this story with sober minds,” President Banda said amidst applause from party supporters.

Source: Nyasa Times


My Take: Waandishi wa habari wa Tanzania wanaandika yale yanayosemwa na wanasiasa kuhusu suala la mpaka.


So; She took a HIGH ROAD in a Sense she even criticize JM Kikwete, Sababu Kikwete kajipendekeza kwa huyu Mama kumuita

Dada na kusema hakuna VITA huyu Mama akamwambia pale pale ZIWA lote ni letu; Kikwete akachekelea chekelea tu; Yaani

He's not a Presidential at all hata Mwanamke anamvimbia, Sasa Kikwete anapingana na Wanaume wenye Ubavu bungeni kwake

Huyu Mama anawakandia wooote, na sasa anawashangilia Waandishi wa MALAWI na kumbuka Waziri wao wa Nje alivyokuwa

akisema Maneno Makali na waliyaandika...

UAMSHO wenyewe wanamtoa JASHO rais wetu sababu wanampa hongera haingilii Masuala ya Zanzibar; Sasa Wameingia Bara

Na kuwaambia Masheikh wa Bara kukataa SENSA... Yeye anakimbilia KUPANDA NDEGE... NYERERE alisema kweli HUYU KIJANA

HAFAI URAISI... WAKENYA WANASEMA TUNABABAISHWA NA UZURI na KUVAA VIZURI... TUNAENDA kwenye MOTO...
 
Kimsingi pale ikulu tumefeli.

Anyway, tunaendelea kujipanga kwa ajili ya kuweka kichwa chenye tija zaidi...
Ishu ya kuwa na waandishi wa habari majuha, sio ya kushtua sana... ka mnavyojua, tuna watu majuha zaidi na kwenye sehemu nyeti kiasi kwamba huamini kuwa kesho yake bado nchi ni yetu!

Ukweli ni kwamba waandishi wachache walioandika ishu hii kwa staili ya kumwonya mama B, wamefanya sahihi sana, hii ni ishu ya kuizungumzia kwenye levo ya jino kwa jino, tukiichukulia hii ishu kama ambavyo tumefanya kwa kina lowasa, vijisenti, n.k, sasa hivi utasikia wacongo nao wanadai ziwa tanganyika lao, haitaishia hapo, mlima kilimanjaro utaenda kwa washkaji hapo, n.k.

Hii sio ishu ya kuporana ardhi kule kwa wachaga!

Kwanza rada yenyewe imepona? Tusije tukawatafuta kwa darubini wakianza...
 
wamalawi wasipoangalia huyu mama atawapoteza ni kama mtu anayetafuta umaarufu/sifa kwa njia yoyote. Wote humu tuliona habari za mgogoro kupitia media za malawi na jinsi walivyoweka ushabiki wa kuingia vitani. Leo hii anataka kugeuza yale magazeti ya malawi yaliandikwa na watanzania. Angalie umakini wake sasa..
Siku zingine unatoa hoja tofauti na jezi yako. Huyu mama ni puppet wa makaburu na anweza kutumiwa kuleta machafuko barani. Kuna taarifa moja alisema kwamba atailanda ardhi ya nchi yake kwa maisha yake kwenye sherehe ya jadi.
 
Ukweli unauma!! Ni kweli vyombo vyetu vya habari havina wabunifu wa kujadili hoja, nilitegemea waandishi wetu wangekuwa wanatoa somo zaidi katika inshu nyingi kuelimisha jamii badala yake karibia waandishi wote wanaegemea kwenye kuripoti habari kutoka kwa wanasiasa zaidi. Vyombo vya habari vijifunze namna ya kujenga hoja zikakubalika kwenye jamii badala ya kukimbilia/kutegemea wanasiasa na watu wengine waropoke ndiyo wapate habari za kuandika.
Huu ndo ukweli, waandishi wa hapa kwetu wanapaswa kuwa weledi sio kuchochea na kuongeza chuki.
 
Huyu ni rais wa pili kutamka ubovu waandishi wa Tanzania. Wa Kwanza alikuwa ni Rais Benjamin ambaye November 24, 2001 alitamka kwamba waandishi wa Tanzania wanatakiwa kuacha uvivu wa kutafiti.

Iliwauma hadi leo wanaikumbuka baadhi ya waandishi.

Mbona wanaoandika habari za kutafiti wanawafungia?
 
Kauli John Mnyika kuwa Rais wetu ni DHAIFU itatimia muda si mrefu,pia huyu Mama anawakingia kifua Nyasa Times ambao wanaandika vitu hovyo heri waandishi wetu mara mia.
 
Nakumbuka kuna gazeti liliweka picha za ndege za kijeshi, vifaru, mizinga huku likisema majeshi yaelekea mpakani mwa tz na malawi lazima waogope,huku EL akipiga biti zito.
 
Bila shaka tabia ya kukimbilia mahakamani kwenye kila mgogoro wa serikali na wananchi Banda akadhani na hili jamaa ataenda mahakamani. Pamoja na kuwa vita ni mbaya, kwenye hili ni muhimu watanzania tukawa wamoja. Siamini kama opposition parties wanaangalia tu madaraka bali wanauchungu na nchi yao pia. Utani anaouleta mkuu wa kaya kwa kutugawa kwa mtazamo wa itikadi za kisiasa kwenye mgogoro huu ni vema tukaukataa kwa sasa......

Nilikua nakufuatilia na comment yako, mwanzoni umeenda vizuri ila umekuja kuharisha mwishoni halafu ukakalia.

Hhapo mkuu wa nchi anatugawa vipi, wakati chochoko zilizopo hapa ni za wananchi wenyewe ambao wanaitikikadi za kibinafsi kuhusu dini zao?

Kila mmoja anataka dhehebu lake lipate keki ya taifa kwa wingi kuliko mwingine, na hata yule mwengine anapodai haki zake anabezwa, sasa hapo tatizo la mkuu wa kaya lipo wapi? cha msingi tujirekebishe ndo upendo na umoja wa kweli utakuwepo, vingiveyo tutachekeana kwenye meni tu.
 
Ni ukweli kabisa huyo mama kafunguka, bongo msiba mkubwa ni waandishi habari na wanajitengenezea mazingira wasikosolewe.
 
Kauli John Mnyika kuwa Rais wetu ni DHAIFU itatimia muda si mrefu,pia huyu Mama anawakingia kifua Nyasa Times ambao wanaandika vitu hovyo heri waandishi wetu mara mia.
Unajua wakati mwingine watu wanafikira za afadhali hata nguruwe, Rais ametumia hekima kutozungumzia suala la malawi hadi alipokutana na mwenzie ndo unaona mambo yametulia na yanaenda kidiplomasia zaid kuliko mwanzo walivoropoka watu bila kuwa na mamlaka sahihi, sasa hapo udhaifu wa rais uko wapi? try to be fair, fikiri kwa kutumia kichwa na sio tumbo.
 
Kwa tabasamu la mkulu wa magogoni yule mama nilijua atalegea tu ahahhahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, BANDA wa Malawi.
 
Nilikua nakufuatilia na comment yako, mwanzoni umeenda vizuri ila umekuja kuharisha mwishoni halafu ukakalia.

Hhapo mkuu wa nchi anatugawa vipi, wakati chochoko zilizopo hapa ni za wananchi wenyewe ambao wanaitikikadi za kibinafsi kuhusu dini zao?

Kila mmoja anataka dhehebu lake lipate keki ya taifa kwa wingi kuliko mwingine, na hata yule mwengine anapodai haki zake anabezwa, sasa hapo tatizo la mkuu wa kaya lipo wapi? cha msingi tujirekebishe ndo upendo na umoja wa kweli utakuwepo, vingiveyo tutachekeana kwenye meni tu.


Umemiss basis ya argument yangu. Statement ya Mkuu wa kaya kuwa opposition wametoa matamko yasiyo rasmi kuhusu uvamizi wa malawi kinaashiria kuwa anaataka tuamini kuwa kwenye hili pia tunatofautiana kiitikadi wakati sio sahihi. Uko sahihi kuona kuwa maoni ya wenzio ni uharo
 
Back
Top Bottom