Rai ya wazi kwa Zitto Kabwe

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kwako Zitto,

Najua kuwa sasa wewe ni mwanachama wa chama kipya kitakachozinduliwa tarehe 29 mwezi huu kiitwacho ACT-Tanzania. Najua pia kuwa umekuwa ukihusishwa na chama hiki tangu kilipopata usajili wa muda na baadaye wa kudumu chini ya Mwenyekiti Kadawi Limbu,ambaye pia alianzisha chama cha ADC. Najua tena kuwa wewe Zitto umekuwa ukikanusha na kukana kuhusika na ACT-Tanzania wakati ukiwa CHADEMA. Ukajiunga mara tu ya kufukuzwa uanachama CHADEMA.

Zitto,

Chokochoko za tuhuma dhidi yako za usaliti zilihusishwa na mkakati na jitihada zako za kuwania Uenyekiti wa CHADEMA. Imeaminishwa hivyo ingawa yawezekana isiwe kweli. Mchoro wako unaochorwa ni mtu mzalendo,mpenda mapambano ya kidemokrasia na unayechukia rushwa na ufisadi. Mchoro wako hauoneshi usakatonge wako. Wewe na wapambe wako mmekuwa mkiufurahia mchoro huu. Yaweza ukawa si mchoro sahihi. Onesha ukweli wa mchoro huo sasa.

Zitto,

Tafadhali usigombee nafasi yoyote ya uongozi ndani ya ACT-Tanzania hapo tarehe 29 Machi, 2015. Jioneshe kuwa wewe si msaka madaraka;hukuwa unahusika na ACT-Tanzania tangu mwanzo na kwamba wewe si mpenda vyeo na msakatonge. Ukigombea chochote au kudai umeombwa kugombea chochote, Tanzania itathibitisha pasi na shaka kuwa wewe ndiye mchoraji bora wa michoro ya kisiasa ikuhusuyo ingawa huchori kitu sahihi.

Ni ushauri na rai tu!


Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Kibaraka wenu K. Limbu hana pa kutokea safari hii.
Zitto ana haki ya kikatiba kugombea nafasi yeyote ndani ya ACT.
 
Kwako Zitto,

Najua kuwa sasa wewe ni mwanachama wa chama kipya kitakachozinduliwa tarehe 29 mwezi huu kiitwacho ACT-Tanzania. Najua pia kuwa umekuwa ukihusishwa na chama hiki tangu kilipopata usajili wa muda na baadaye wa kudumu chini ya Mwenyekiti Kadawi Limbu,ambaye pia alianzisha chama cha ADC. Najua tena kuwa wewe Zitto umekuwa ukikanusha na kukana kuhusika na ACT-Tanzania wakati ukiwa CHADEMA. Ukajiunga mara tu ya kufukuzwa uanachama CHADEMA.

Zitto,

Chokochoko za tuhuma dhidi yako za usaliti zilihusishwa na mkakati na jitihada zako za kuwania Uenyekiti wa CHADEMA. Imeaminishwa hivyo ingawa yawezekana isiwe kweli. Mchoro wako unaochorwa ni mtu mzalendo,mpenda mapambano ya kidemokrasia na unayechukia rushwa na ufisadi. Mchoro wako hauoneshi usakatonge wako. Wewe na wapambe wako mmekuwa mkiufurahia mchoro huu. Yaweza ukawa si mchoro sahihi. Onesha ukweli wa mchoro huo sasa.

Zitto,

Tafadhali usigombee nafasi yoyote ya uongozi ndani ya ACT-Tanzania hapo tarehe 29 Machi, 2015. Jioneshe kuwa wewe si msaka madaraka;hukuwa unahusika na ACT-Tanzania tangu mwanzo na kwamba wewe si mpenda vyeo na msakatonge. Ukigombea chochote au kudai umeombwa kugombea chochote, Tanzania itathibitisha pasi na shaka kuwa wewe ndiye mchoraji bora wa michoro ya kisiasa ikuhusuyo ingawa huchori kitu sahihi.

Ni ushauri na rai tu!


Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

hata prof wake kamsema ni mzigo. hawezi kuwa mwepesi hata siku moja. mwache aendeshwe na hisia zake mwenyewe
 
Hasiiki huyu, alihusishwa act lakini Leo kang'atuka cdm kesho huyooo kwenye chama lake na uenyekiti atagombea
 
@vuta -nkuvute mbona una hangaika sana na mzalendo zitto c mlisha mfukuza unataka Mwenyekit awe kibaraka wenu limbu?

Acha afanye atakavo cz nae anahaki yakufany chochote ndani ya nchi hii
 
Kibaraka wenu K. Limbu hana pa kutokea safari hii.
Zitto ana haki ya kikatiba kugombea nafasi yeyote ndani ya ACT.
MUSSA ALLAN
===>Mh naona umekuwa mpiga debe wa Afande Sele,vp na wewe umehama kwa magamba?au ndio wale wabunge 11 anaosema Zana za Kilimo?
 
Last edited by a moderator:
Hivi jamani, Tanzania hatuna topiki ntingine muhimu zaidi ya hii ya Zitto Kabwe? Hii korasi ishanikinai miye, na tuanzisheni wimbo mwingine. Tuna mambo mengi sana ya kujadili kuhusu taifa hili, hasa mkizingatia huu ni mwaka wa uchaguzi. Kuendelea kumjadili Zitto Kabwe ni kudhihirisha mtazamo wake (au pengine wa mashabiki wake) kuwa yeye alikuwa mtu muhimu na maarufu kuliko Chadema.
 
Kwako Zitto,

Najua kuwa sasa wewe ni mwanachama wa chama kipya kitakachozinduliwa tarehe 29 mwezi huu kiitwacho ACT-Tanzania. Najua pia kuwa umekuwa ukihusishwa na chama hiki tangu kilipopata usajili wa muda na baadaye wa kudumu chini ya Mwenyekiti Kadawi Limbu,ambaye pia alianzisha chama cha ADC. Najua tena kuwa wewe Zitto umekuwa ukikanusha na kukana kuhusika na ACT-Tanzania wakati ukiwa CHADEMA. Ukajiunga mara tu ya kufukuzwa uanachama CHADEMA.

Zitto,

Chokochoko za tuhuma dhidi yako za usaliti zilihusishwa na mkakati na jitihada zako za kuwania Uenyekiti wa CHADEMA. Imeaminishwa hivyo ingawa yawezekana isiwe kweli. Mchoro wako unaochorwa ni mtu mzalendo,mpenda mapambano ya kidemokrasia na unayechukia rushwa na ufisadi. Mchoro wako hauoneshi usakatonge wako. Wewe na wapambe wako mmekuwa mkiufurahia mchoro huu. Yaweza ukawa si mchoro sahihi. Onesha ukweli wa mchoro huo sasa.

Zitto,

Tafadhali usigombee nafasi yoyote ya uongozi ndani ya ACT-Tanzania hapo tarehe 29 Machi, 2015. Jioneshe kuwa wewe si msaka madaraka;hukuwa unahusika na ACT-Tanzania tangu mwanzo na kwamba wewe si mpenda vyeo na msakatonge. Ukigombea chochote au kudai umeombwa kugombea chochote, Tanzania itathibitisha pasi na shaka kuwa wewe ndiye mchoraji bora wa michoro ya kisiasa ikuhusuyo ingawa huchori kitu sahihi.

Ni ushauri na rai tu!


Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

si walisema mtu wa CCM? MARA KAANZISHA CHAMA,

Limbu anashtaki nini?

yaani akiyafanya hayo yote kwa tabia za Mbowe za uzushi unafikiri atakosa la kusema??

give him a break please!!

kwa chuki walizonazo kwa zitto lolote lile watasema tu!
 
Huyu Zitto sidhani kama ataweza kusikiliza rai/oni yako ya yeye kutogombea nafasi yoyote ndani ya chama hicho.
Moja, kama unadhani anaweza kuwa mwanachama wa kawaida tu ndani ya chama kwa nini aliondoka chadema? Kwani ameshindwa kuwa mwnachama wa akawaida tu kule?
Au angeshindwa kuonesha ukomavu halisi wa kisiasa akiwa mwanachama wa kawaida ndani ya chadema?
 
Agombee asigombee anafahamika kuwa ni msaliti, sasa chama ndo hicho, mtoto akililia wembe mpe shoka au jambia
 
Back
Top Bottom