Rafiki kutambulishwa kwa mke/mume/mchumba? IS IT REASONABLE?

Hatari gani wakati ni urafiki wa kawaida tu? Namleta nyumbani wife anampikia chai, wanapiga stori kama kawaida. Kuna hatari gani hapo?
hatari ni kumtambulisha na si baada ya hapo kaka,je iwapo utatambulisha na baadae baada ya mwenzako kujua mengi kuhusiana na nyinyi akachepuka kimawazo?hatari huanzia hapo
 
Eti Jamani:
Kwa wale wenye mahusiano ya dhati ya kimapenzi. Wenye ndoa zao na wachumba ambao wanatarajia kuingia kwenye ndoa. Au basi ma-boy/girl friends wenye mahusiano ya kingono.

Inawezekana mtu ukawa na rafiki wa jinsia tofauti. Urafiki kwa maana ya urafiki usiohusiana na mambo ya ngono. Mnapiga stori, mnabadilishana mawazo, mnashauriana mambo mengi, mnasaidiana kwa mambo mbalimbali na vitu kama hivyo (Carmel unalielewa hili, japokuwa urafiki wako ulivuka mipaka ukaibua ndoa.)

Je ni sahihi rafiki kama huyu kumtambulisha kwa mumeo/mkeo/mchumba? Yaani Carmel amtambulishe Geoff kwa mume wake kuwa huyu ni rafiki yangu. Au Fidel80 amtambulishe nyamayao kwa mkewe kuwa huyu ni rafiki yangu?

Nina rafiki yangu wa kike nataka nimtambulishe kwa wife, nahofia nisije nikazua msala.

CAN YOU? IS IT REASONABLE?
he he he he !mpwa mimi dada ako akinifanyia hilo ni lazima kuwe na justifications zinazoeleweka!otherwise PATACHIMBIKA
 
FL1 hebu nitajie title ya hii thread tafadhali!

hahahah off-topic zinatokeaga mala moja moja kama wewe huwa hu do powah >>!
ok heading :Rafiki kutambulishwa kwa mke/mume/mchumba? IS IT REASONABLE?

twendelee ....
 
Jamani kwa uzoefu wangu mdogo, hakuna urafiki wa kawaida wa watu wa jinsia 2 wa jinsi hii,hasa kwa wenye ndoa.Ni hatari na hakuna mwanamke au mwanaume yeyote anayeweza kuamini hili.Ni wachache saaaaaaaaaana kama sio sifuri.

ZD wewe si rafiki wa kawaida na geoff, kaizer, fidel?
 
Hahaha! Hapo mkuu umenivunja mbavu. Lakini mimi ni mwaminifu kwa mashemeji. Labda kama angekuwa Fidel. Sasa asipokuambia afu siku ukamkuta na fidel chawote bar wanakunywa mvinyo then akakuintrodyuzi huyu ni rafiki yangu itakuwaje. Si heri angekuambia mapema ujue moja?
ha ha ha Mkuu sijakwambia usimtambulishe...kumtambulisha muhimu nilichosema isiwe mazoea sana!! kwa sababu huna rafiki mmoja tu wa kike wapo wengi ila kwa nn kila siku lazima umtaje taje tu...kitu kidogo oh nanii aliniambia hivi oh jana tulikua zero pub!! hapoa mpwa unatafuta ugomvi!! kama kumtambulisha we mtambulishe tu!! hakuna tatizo!!
 
he he he he !mpwa mimi dada ako akinifanyia hilo ni lazima kuwe na justifications zinazoeleweka!otherwise PATACHIMBIKA

Mpwaaa! Mpwa!!!! Sista hawezi kuwa rafiki wa kawaida wa nguli?
 
ZD wewe si rafiki wa kawaida na geoff, kaizer, fidel?
ha ha ha ha ha!mpwa mimi nina mambo mengi sana moyoni nakwazika kuhusu hii post yako kwakweli!naomba nisiyataje hapa.tuonane ZERO....(ijumaa probably)inshort mimi hili swala patakuwa padogo
 
ndo nakwambia kama hakuna kuaminiana katika mahusiano yenu yote hayo yanaweza kutokea ..
wengine vicheche


hata kama mnaaminiana kivipi lakini mie ctaki anitambulishe wala nimtambulishe......hapo tusameheane, urafiki wenu huko huko sio mpaka home kwangu mana najua na yeye nikimfanyia hilo looo hapatakucha.
 
ha ha ha ha ha!mpwa mimi nina mambo mengi sana moyoni nakwazika kuhusu hii post yako kwakweli!naomba nisiyataje hapa.tuonane ZERO....(ijumaa probably)inshort mimi hili swala patakuwa padogo
Shemji ni tena? mimi ndio nakukwaza? niambie mwendhio!
 
Mpwaaa! Mpwa!!!! Sista hawezi kuwa rafiki wa kawaida wa nguli?
mpwa hapana bana!
itokee leo mimi nachat kwa sms na waifu wako!mwisho wa siku anasema ''SI JAMAA YAKO?''hapana mpwa HAPANA!

imetokea hii nikiwa mwaka wapili asubuhi nilijikuta naamka kitanda kimoja na dem wa rafiki yangu!(after so many taskaaz)

wanawake ni mama zetu lakini naomba wanisamehe tu kwakweli NIME.....
 
ha ha ha ha ha!mpwa mimi nina mambo mengi sana moyoni nakwazika kuhusu hii post yako kwakweli!naomba nisiyataje hapa.tuonane ZERO....(ijumaa probably)inshort mimi hili swala patakuwa padogo

Hahaha! Mpwa umekula SENKSI hapa! LOL
 
Kaka achana na hiyo kitu kabisa wifi ZD lazima atashtuka, alafu eti mmekuja wote kwenye gari unamkaribisha ndani alafu unamwita wife "njoo umsalimie rafiki yangu", NO HAIPANDI.
 
hatari ni kumtambulisha na si baada ya hapo kaka,je iwapo utatambulisha na baadae baada ya mwenzako kujua mengi kuhusiana na nyinyi akachepuka kimawazo?hatari huanzia hapo

Hujanijibu salamu yangu lakini,umenichunia? Nataka nikutambulishe kwa my fiancee.
 
Back
Top Bottom