Borakufa
JF-Expert Member
- May 26, 2011
- 1,503
- 390
- Thread starter
- #81
Umefanya Utangulizi Mzuri sana, lakini bado hauja unganisha kichwa cha habari na habari yenyewe. Nina Maana ni jinsi gani hao uliowataja wanahusika na malalamiko yako.
Radio imani siku hizi kila siku lazima waje na mada ambayo majadiriano yake ni ya kisiasa! na mbaya zaidi siasa za kukilinda chama kimoja na kukishambulia chama kingine (huo ni mtazamo wangu) Mie nilitegemea kama wangeamua kuingia katika siasa basi wangekuwa balanced wangemnusuru anayedhurumu na anayedhurumiwa hiyo ndiyo dini ya ALLAH inavyotaka.
Sasa wao Radio iman kuungana na Shura ya maimamu,Basuta na baadaye Bakwata (habari ya Mkuu wa wilaya ya igunga) Kutengeneza mada za kisiasa zitakazopelea uma huu wa kiislam kuwachukia wakristo wakati wengine ni ndugu zetu tunaishi nao nyumba kwa nyumba, maofisini, mashuleni n.k si busara kabisa!
Huwezi kuuondoa munkari kwa munkari mwingine! Ni kweli waislam tuliaachwa nyuma pengine kwa maksudi au kwa bahati mbaya la muhimu hapa si kutengeneza mazingira ya chuki na baadae inaweza kuzuka vita bali nikutafuta njia sahhi nasi tufikie au tuvuke walikofikia wakristo.
Haitatokea hata siku moja eti nchi hii ikawa ya waislam tu! Aliondoka Mtume (SWA) akawacha makafiri na kiama kitasimama bado wanaompinga ALLAH wapo ndiyo maana kuna pepo na moto.