ifa96
JF-Expert Member
- Jul 25, 2014
- 435
- 222
Nimefaulu moja kutoka kwako mkuu nimeweza kuipinga malaria tangu nianze fuatilia uz wako na hakika nimeweza mpaka sasa Nina miaka 2 malaria naisikiaga tuuMkuu Joni, hayo ni mazingaombwe tuu, au kiini macho!, huyo mtu unayemuona kama anatembea juu ya maji, kwa kule chini amekanyaga kitu ambacho kimefunikwa na maji hivyo nyinyi hamkioni!. Mazingaombwe yanaitwa hypnotism, mfanya mazingaombwe anaitwa hypnotist na kitu kinachofanyika kinaitwa hypnosis, hapa wanatumia nguvu tuu ya ushawishi, iitwayo 'mind suggestibility' kwa kukuzuga kuwa anabadili karatasi kuwa noti, anachinja mtu, etc. Anatumia tricks tuu kuzugia, zipo hadi operations zinaitwa psychic surgery lakini kiukweli hakuna chochote kinachofanyika physically bali ni just playing with peoples mind kama wafanyavyo wahubiri wa miujiza!, unaangalia na kuona unachoona kumbe ni zuga tuu!.
Ila katika zuga hizo, kuna watu wanapona kweli, kinachowafanya wapone ni nguvu za Mungu za uponyaji zilizomo ndani yako ambazo kila binadamu au viumbe hai wanazo, ndio maana hata wanyama kila siku wanaugua na kujitibia wenyewe!.
Huo mchezo wa huko Congo kwa maiti kutembea, inafanywa sana visiwa vya Haiti, Trinidad and Tobago, Babados na america ya kati, kwa kutumia uchawi unaitwa Voodoo, ni kama imani inatwa voodoism, unaweza kuisoma kwenye ile thread ya kwanza kwenye link ya
NB, kwenye hizo links, ukifungua, ili uweze kusoma na kuelewa, ni lazima kwanza uwe na kiwango fulani cha uelewa kwa sababu mambo mengine ni uchawi kabisa, yaani pure magic!, hivyo ushauri wangu ni ujitafakari kwanza kiwango cha uelewa wako kabla hujazama kwenye hizo links, ukifungua na kujiona huelewi, achana nazo!.
Pasco
Na kipindi cha nyuma ilikuwa inanisumbua mno