Prof. Tibaijuka: Mliopora maeneo jisalimisheni; aanza kwa kasi!

Mimi nina hakika hiyo Wizara Tibaijuka haiwezi kabisaa, hizo ni gear tu za kuingilia ofisini, huyu mama kwa muda mrefu amefanya kazi UN chini ya sera wazi zinazoeleweka. Hapa Bongo mfumo ulishajaa Uozo kiasi kwamba kila mmoja ni fisadi kwa level yake. Atachemsha kabisa mpaka atatia huruma
 
Siyo hayo tu, bado kuna maafisa wake hapo hapo ardhi waliohodhi viwanja kwa ajili ya kuvilangua!!!!!!prof. Tibaijuka analijua hilo!!!!!!!!!!!!!!kwa kweli nakupa pole sana; kazi ni kubwa uliyonayo.......!!!!!!!prof. Nakushauri ufanye survey ya viwanja vyote utagundua kwa kiasi gani maafisa wako wamehodhi viwanja. Kama ulivyotamka huogopi, basi nakuombea mungu akupe ujasiri zaidi, ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi!!!!!!!!!isije ikawa ni nguvu ya soda!!!!!!!!!!!!!!
 
Kama mnakumbuka lilipoteuliwa baraza la mawaziri nilisema Professa Anna Tibaijuka ana kazi kubwa wizara ya ardhi. Uongozaji wa wizara hii si kama kuongoza UN Habitat na hivyo akifanya masikhara anaweza kuumia. Kuna madudu mengi to mentioned the few hayo ila lazima awe bold. Akiyaweza hayo madudu mie nampa kura yangu akigombea urais 2015 maana yuko makini kiutendaji huyu mama. Akiharibu well sina la kusema ila amepewa wizara nzito sana ina madudu mengi mno humo ndani.
 
Akipindisha hili tutamtilia mashaka na yote aliyozungumza kwa waandishi wa habari!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
The legality of the ownership of the land has nothing to do with school fees. If the land was acquired legally then thats fine, angeweza fungua gesti lakini kaweka shule na vyote vina lipa in tanzania gesti zinalipa zaidi probably. So the fact that she decided to build a private school, and since the Ministry of Education has a deficit of schooling facilities, demand exceeds supply.. this is a good thing. You cant just judge the fees without knowing her running costs, she provides employment to Tanzanians and educates our children, even if its those that can afford it, it just means that there are more places in public schools for those who cant afford private education. In the end, more kids go to school. This thread has no merit and these allegations are completely unjustifiable unless it can be shown that the land was acquired contrary to the law of the land. Anything below that pelekeni kwenye stori za baa
 
unayosema kilanga ni kweli but tunaposubili power structure ibadilike kwa katiba kubadilishwa huyu mama afanye kazi yake! Asiiingiliwe na mafisadi!

Ninachokwambia ni kwamba, hawezi kufanya chochote cha maana katika power structure hii, na power structure huwa "haisubiriwi" iondoke, huondolewa, kwa hiyo kama kuna mikakati iwe ni ya kuondoa power structure nzima.

Huyu mama akikuta Rostam kafanya land grab huko mitaa ya kati ataweza kumuadabisha?

Au anatoa political hot air tu?
 
Kwa kuwa ni vizuri viongozi kama yeye wakaongoza kwa kuonyesha mifano ni vyema Prof Anna Tibaijuka akarejesha ardhi ya serikali zaidi ya ekari 100 aliyochukua katika ranchi ya utafiti wa magonjwa ya mifugo iliyoko wilaya ya Kinondoni.

Hebu tuone atakaowabana kurejesha ardhi ni watu wenye makosa gani katika umiliki wa hizo ardhi. Lakin lazima tukubali kuwa njia anayopendekeza kupita ni nzuri japo I doubt it! Vigogo wengi wataguswa na kama akiweza hili basi mengi yatafunuliwa na taifa litafaidika, hata yeye kama anahusika ashugulikiwe kama wengine wote! Haya mama kazi kwako.
 
hapa watakao nyang'anywa ardhi ni sis walalahoi huwezi kumgusa mtu kama RA au EL au hata Kinana
 
Mama Anna T, Mimi nina maswali machache kwako kama sio ushauri,

1). Unaye Mungu wa Kweli ?
2). Unasali wewe?
3). Kama huna Mungu ule ulinzi usionekana, unao?

Mama Anna ukiweza kurekebisha mambo hapa walipokuweka yakanyooka na kila mtu akaona yamenyooka na kukubali basi mimi 2015 sigombei Urais nitakupigia debe wewe wakupe. Lakini anagalizo hayo matatu ya mwanzo sikutishiiii..... take care........mjue Mungu ndio uendeleee na Mipango yako ama sivyo watakuumiza .....:thumb:
 
JAMAN Niwaulize HUYU Prof anasoma JF au Mnajishaua tu?, Bwana future Presdent, acha vitisho kaka, Akiamua anaweza kama nia ipo, akivaa miwani ya mbao atachapa kazi ili mradi apate baraka kutoka kwa mukulu.
 
Pale Ardhi niliwahi kupambana na Fisadi moja alikuwa naibu katibu mkuu? chini ya mama Sijaona, nafikiri alikuwa mtu wa Arusha/Manyara, mwenye kujua jina lake naomba please. Na pia kulikuwa na DMDA wa kutoka Monduli au ni zao la Ufisadi? nilipita wizara ya ardhi kama mteja ndio maana majina yao yana nitoka. nikamkosa Huyo Mama Sijaona ndipo nilipo pewa huyo Mzee.
 
Waziri mpya wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof Anna Tibaijuka jana aliibuka na kuwataka watu wote waliopora ardhi ya serikali na viwanja vya wazi na na kujenga katika maeno ya fukwe wajisalimishe haraka wizarani kwake kabla ya hatua kali za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.

Kwa kuwa ni vizuri viongozi kama yeye wakaongoza kwa kuonyesha mifano ni vyema Prof Anna Tibaijuka akarejesha ardhi ya serikali zaidi ya ekari 100 aliyochukua katika ranchi ya utafiti wa magonjwa ya mifugo iliyoko wilaya ya Kinondoni.

Prof Anna Tibaijuka alitumia ardhi hiyo kwa ajili ya kujenga shule ya sekondari ya wasichana iitwayo Barbro Johansen. Na mara tu alipochaguliwa kuwa Waziri wa Mifugo Mhe John Magufuli aliwahi kutoa wito na kuwataka wote waliomilikishwa ardhi za ranchi za taifa kurejesha ardhi husika kwa maslahi ya sekta ya mifugo.

Kana kwamba hiyo haitoshi, Prof Anna Tibaijuka akaingilia na kuchukua line ya maji iliyokuwa imetengwa kwa ajili ya vijiji vilivyoko jirani na shule yake. Mpaka sasa wakazi wa vijiji hivyo ambao idadi yao inakua kwa kasi sana hawana huduma ya maji ya safi ya bomba.

Najua Prof Anna Tibaijuka anaweza kujitetea kuwa ardhi ilitolewa kwa ajili ya maslahi ya taifa. Lakini kama kweli ardhi hiyo ingekuwa ni kwa maskahi ya taifa na sio binafsi, ada zinazolipwa katika shule yake zingekuwa nafuu kuwawezesha watoto kutoka familia maskini waweze kumudu kuingia shuleni hapo. Raisi Jakaya Kiwete amewahi mara kadhaa kuzitaka shule binafsi kupunguza ada wananzotoza ili kuwawezesha watoto kutoka familia maskini kumudu kusoma katika shule hizo.

Aidha kama mradi huo ungelikuwa ni kwa ajili ya maslahi ya taifa na sio binafsi, wakazi wa vijiji jirani na shule hiyo wangepatiwa huduma ya maji safi ya bomba kutoka shuleni hapo hasa ikizingatiwa kuwa shule hiyo ilichukua line ya maji ya vijiji na hivyo kuwakosesha wanakijiji huduma hiyo.

Naomba kuwasilisha!!!!!!!!!!


Huu ni mkwara mbuzi. Nitaamini kama anamaanisha anachokisema na kama ana ubavu amshughulikie anayejenga hoteli kwenye kiwanja cha serikali njia panda ya kwenda LITI na ofisi ya mkuu wa mkoa Morogoro.
 
Upanga wake utakuwa mzuri kama utakuwa na ncha pande zote. Kuna watu wengi wanaingia kwenye siasa hata kwa kununua wapiga kura ili aweze kulinda vitega uchumi. Endapo atafanikiwa kuwa tight inclg. Mahanga ikithibitika ni kwali basi anaweza kuingia kwenye record ya watakao fikiriw u prest 2015
 
Anna Tibaijuka akiamua kama inavyoonekana ameamua ,ataweza kupambana na hao mafisadi wa ardhi kwani mbona hapo kabla yake Deo Mmari akiwa katibu mkuu aliwanyoosha mafisadi hata kumfunga Baghdadi miaka mingi jela kwa makosa ya kuhujumu viwanja!!
 
wapunguze ada nini? Private schools are expensive everywhere, serikali itoe elimi ya sekondari bure angalau umpaka f4. Kuliko ranch mbovu bora shule atakama ni private, anachangia sekta ya elimu. Na haujatoa maelezo kama hiyo ardhi ilichukuliwa kinyume na sheria au kwa kufwata taratibu za ubinafsishaji. Watu mnakuja tuu na hoja bila kuziweka ipaswavyo...

Mkuu:

Nchi ni lazima iongozwe na sheria. Hapa mama hana tofauti na mtu atayekaenda uwanja wa ndege na kubadilisha bustani za maua kuwa mashamba ya mahindi.
 
Back
Top Bottom