unayosema kilanga ni kweli but tunaposubili power structure ibadilike kwa katiba kubadilishwa huyu mama afanye kazi yake! Asiiingiliwe na mafisadi!
Kwa kuwa ni vizuri viongozi kama yeye wakaongoza kwa kuonyesha mifano ni vyema Prof Anna Tibaijuka akarejesha ardhi ya serikali zaidi ya ekari 100 aliyochukua katika ranchi ya utafiti wa magonjwa ya mifugo iliyoko wilaya ya Kinondoni.
Waziri mpya wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof Anna Tibaijuka jana aliibuka na kuwataka watu wote waliopora ardhi ya serikali na viwanja vya wazi na na kujenga katika maeno ya fukwe wajisalimishe haraka wizarani kwake kabla ya hatua kali za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.
Kwa kuwa ni vizuri viongozi kama yeye wakaongoza kwa kuonyesha mifano ni vyema Prof Anna Tibaijuka akarejesha ardhi ya serikali zaidi ya ekari 100 aliyochukua katika ranchi ya utafiti wa magonjwa ya mifugo iliyoko wilaya ya Kinondoni.
Prof Anna Tibaijuka alitumia ardhi hiyo kwa ajili ya kujenga shule ya sekondari ya wasichana iitwayo Barbro Johansen. Na mara tu alipochaguliwa kuwa Waziri wa Mifugo Mhe John Magufuli aliwahi kutoa wito na kuwataka wote waliomilikishwa ardhi za ranchi za taifa kurejesha ardhi husika kwa maslahi ya sekta ya mifugo.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Prof Anna Tibaijuka akaingilia na kuchukua line ya maji iliyokuwa imetengwa kwa ajili ya vijiji vilivyoko jirani na shule yake. Mpaka sasa wakazi wa vijiji hivyo ambao idadi yao inakua kwa kasi sana hawana huduma ya maji ya safi ya bomba.
Najua Prof Anna Tibaijuka anaweza kujitetea kuwa ardhi ilitolewa kwa ajili ya maslahi ya taifa. Lakini kama kweli ardhi hiyo ingekuwa ni kwa maskahi ya taifa na sio binafsi, ada zinazolipwa katika shule yake zingekuwa nafuu kuwawezesha watoto kutoka familia maskini waweze kumudu kuingia shuleni hapo. Raisi Jakaya Kiwete amewahi mara kadhaa kuzitaka shule binafsi kupunguza ada wananzotoza ili kuwawezesha watoto kutoka familia maskini kumudu kusoma katika shule hizo.
Aidha kama mradi huo ungelikuwa ni kwa ajili ya maslahi ya taifa na sio binafsi, wakazi wa vijiji jirani na shule hiyo wangepatiwa huduma ya maji safi ya bomba kutoka shuleni hapo hasa ikizingatiwa kuwa shule hiyo ilichukua line ya maji ya vijiji na hivyo kuwakosesha wanakijiji huduma hiyo.
Naomba kuwasilisha!!!!!!!!!!
http://http://annatibaijuka.org/?lang=en
Tafadhali naomba umtumie huo ujumbe kwenye hiyo site yake hapo juu,utakuwa umesaidia Tanzania kama Taifa.
wapunguze ada nini? Private schools are expensive everywhere, serikali itoe elimi ya sekondari bure angalau umpaka f4. Kuliko ranch mbovu bora shule atakama ni private, anachangia sekta ya elimu. Na haujatoa maelezo kama hiyo ardhi ilichukuliwa kinyume na sheria au kwa kufwata taratibu za ubinafsishaji. Watu mnakuja tuu na hoja bila kuziweka ipaswavyo...