Prof.Mshigeni: Namibia wanamuenzi, Tanzania haimtambui!!

Inafika kipindi tuache kuilamu sana serikali na tuangalie jamii zetu. Kuna watanzania wengi hapa USA ni mameneja wa Subways, Mac Donald na mambo mengine.

Ukipima ufanisi wao unaona wanafanya kazi nzuri sana. Lakini kwa nafasi hizohizo wakipewa nafasi Tanzania watavurunda na kuboronga.


Huyu Professor ameweza kufanya vizuri nje ya nchi kwa sababu katika nchi za watu, wanataka waone kazi yako na ukishindwa wanampa mtu mwingine, Hivyo kuna check and balance ya kuona kazi yao imefanyika.

Lakini huyuhuyu professor angefanya kazi bongo basi angetaka pesa anazopewa kufanyia research ajengee nyumba kwao, awe na vimada watatu na ampe kazi ya maabara ndugu yake alifeli kidato cha nne.

Kwa maoni yangu, watanzania na waafrika wengi wakifanya kazi nje ya nchi zao wanajaribu kuwa responsible lakini wakiwa kwenye nchi zao porojo nyingi.

Tamati


Kwa ninavyomfahamu mimi Prof. Mshigheni ni mtu asiye na tamaa, yeye kani ni kazi tu. Na anapenda sana maendeleo na kusaidia watu. Akipewa nafasi atafanya makubwa mengi.
 
Mnaonaje Prof Mshigeni arudi bongo agombee Ubunge then awe waziri wa Kilimo
 
Masatu said:
Mnaonaje Prof Mshigeni arudi bongo agombee Ubunge then awe waziri wa Kilimo

Masatu,

..akagombee ubunge wapi?

..Mshigeni atakuwa anatoka maeneo wanakotokea hawa:prof.Maghembe,Dr.David Matayo, ua Anne Malecela.

..nani kati ya hao yuko tayari kuutema Ubunge?

..au, labda kwasababu ya kuwa msomi wa pale mlimani anaweza kugombea jimbo la Ubungo. huko nako tayari tuna kijana wetu John Mnyika, na Mzee Keenja.

NB:

..TURUDI TU KWENYE MADA KUU. JE, TANZANIA TUMEUTUMIA VIZURI UTAALAMU WA Dr.MSHIGENI?
 
Masatu,

..akagombee ubunge wapi?

..Mshigeni atakuwa anatoka maeneo wanakotokea hawa:prof.Maghembe,Dr.David Matayo, ua Anne Malecela.

..nani kati ya hao yuko tayari kuutema Ubunge?

..au, labda kwasababu ya kuwa msomi wa pale mlimani anaweza kugombea jimbo la Ubungo. huko nako tayari tuna kijana wetu John Mnyika, na Mzee Keenja.

NB:

..TURUDI TU KWENYE MADA KUU. JE, TANZANIA TUMEUTUMIA VIZURI UTAALAMU WA Dr.MSHIGENI?

Haya ndiyo ninayopinga mimi. Watu mahiri katika fani zao tunataka tukawashindilie kwenye siasa (wakatukanwe na kukashifiwa, na wakishaujua mchezo waanze nao kutukana na kukashifu!) Huko kwenye fani zao tunataka tumwache nani? Kwa nini kila mtu asifanye kile ambacho anakimudu zaidi kuliko vingine. Matumizi mazuri ya rasilmali ni kwenye maximal utilization of potential.
 
Mnaonaje Prof Mshigeni arudi bongo agombee Ubunge then awe waziri wa Kilimo

Sawa mkuu,laiti tungekuwa na uwezo wa kikatiba wa kuchagua na Mawaziri vileX2.kwasababu ukishakuwa na Vilaza huko juu,basi matokeo yake unakuta Wahandisi wanapangiwa wizara za Kilimo au Uvuvi na mali asili,madaktari-ulinzi....taabu tupu.
 
SO WHAT?
MLITAKA TUMPIGIE VIGELEGELE?SI NI VC WA HURBERT KARIUKI?
ACHENI USeNG. NYIE.
 
siku tanzania tukianzisha tuzo za kazi walizofanya wenzetu wasomi humu nchini basi matunda yataojekana,wanasiasa wanathamini sana wafanyabiashara na ndio sababu sayansi huku kwetu shida tupu,kipato kidogo,kazi ngumu,full frastration. motivation especially to scientist is very very important.
 
SIMPLE: Kama alichagua kuwatumikia Namibia kwa nini ategemee kusifiwa Tanzania...je ni mzalendo wa kweli?
 
Back
Top Bottom