Prince Bagenda ashambulia vikali M4C ya CHADEMA

Kada wa chama cha mapinduzi na mwanasiasa mkongwe nchini Prince Bagenda amekishambulia chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kwa operesheni yake ya M4C inayotishia uhai wa CCM.
Katika makala yake ndani ya gazeti la RAI Prince Bagenda amedai M4C ni chama kipya cha siasa ndani ya CDM na kusema hali hiyo ni hatari kubwa kwa ukuaji wa chama hicho na amesema utatokea mvutano mkubwa kati ya wafuasi wa CDM na wafuasi wa itikadi ya M4C.
Bagenda pia amesema kampeni ya M4C wanayoongoza nchi nzima inatangaza sera za shari na chuki.Pia amesema CDM walipata kura nyingi uchaguzi mkuu uliopita kutokana na vita ya makundi ndani ya CCM na kamwe si kutokana na chama hicho kuwa na sera nzuri.Amesema CDM hawana Itikadi inayoeleweka hadi sasa ndiyo maana mpaka sasa wajanja kama yeye wako CCM.

Source:RAI Alhamisi

My Take:
Prince Bagenda alishiriki kusambaratisha chama cha NCCR Mageuzi baada ya kuongoza mgogoro mkubwa huku akikimega chama vipande viwili na yeye akiwa Katibu Mkuu kambi ya Mrema.Baada ya kufanikisha kusambaratisha NCCR,Prince Bagenda alihamia CCM ambapo hadi leo yeye ni kada mwaminifu wa CCM.


Nilikuwa nawaza Amekwenda wapi PRINCE BAGENDA? Kumbe kaanzisha Chama kingine

Ndani ya CCM; kwahiyo yeye ni M4C copy upande wa CCM; CCM wajichunge asiwasambaratishe

kama NCCR Mageuzi... Ana Chuki Kweli...
 
Kwanza kwa nini ajiite Prince? Kuna mwanaJF anajua alilipataje hilo jina lisilomfaa wakuu?
 
Isingekuwa mfumo kumweka mjini Prince Bagenda angekuwa kwao kijijini akiishi na kutafakari maisha ya hukohuko kijijini.

Ndio maana serikali ya CCM imekuwa makini kuhakikisha kwamba watu wa aina ya Prince Bagenda wanakuwepo karibu ili kuvuruga, kukoroga na mwisho kuchanganya wananchi kupitia magazeti yao na yale magazeti saidizi.

Nani amsiemfahamu Prince Bagenda na afadhali Deus Malya umeeleza moja tu ya mapungufu ya huyu jamaa. Ni yeye na wenzie walioorodheshwa na mmoja wetu hapo juu ndio waliotumika pale mwanzo kuvuruga upinzani nchini Tanzania.

Ikiwa mzee wa kiraracha alifundisha majasusi wengi tu pale Mbweni na wengine ambao leo hii wapo CCM kama Mabere Marando, Dr Masumbuko Lamwai, Dr Kabourou na wengine wengi tu ambao wote ni makada wa CCM, je wananchi wa kawaida wasiojua kuchambua mchele na pumba watafanyaje?

Mtu wa aina ya Bagenda leo hii anatumika kusema kwamba CDM na MC4 kuna itikadi tofauti, huu si upotoshaji na uchonganishi wa hali ya juu kabisa?

Halafu kuna mwenzetu mmoja ametaja neno la "mercenary" au mamluki na hili ni kundi ambalo lipo tayari siku zote kuhakikisha watanzania wanakuwa wajinga na hasa wale wa vijijini, na hili ndio eneo ambalo MC4 limelenga.

Halafu anakuwa mjinga zaidi pale anaposema tena kwamba CDM ina itikadi isioeleweka, hivi huyu mzee anatumia akili kweli kujenga hoja?

Pia anasema kwamba CDM inatangaza sera za shari na chuki kitu ambacho sijawahi kukiona kikipikwa na hawa akina Bagenda kwani ni CCM yake mwenyewe inaanda polisi kuzuia mikutano, kuwatuma watu wasioiva kisiasa kama Nape Nnauye kutoa hoja mbovu hadharani na ndio maana CCM wanataka kumtoa ukatibu uenezi kwani hawezi kazi hiyo.

Ingekuwa ni mzee Paul Sozigwa anasema haya ningesema amepitiwa na si Prince Bagenda, lakini si watanzania wa leo watakaokubali madudu haya na MC4 itasafisha nchi nzima.
 
Kada wa chama cha mapinduzi na mwanasiasa mkongwe nchini Prince Bagenda amekishambulia chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kwa operesheni yake ya M4C inayotishia uhai wa CCM.
Katika makala yake ndani ya gazeti la RAI Prince Bagenda amedai M4C ni chama kipya cha siasa ndani ya CDM na kusema hali hiyo ni hatari kubwa kwa ukuaji wa chama hicho na amesema utatokea mvutano mkubwa kati ya wafuasi wa CDM na wafuasi wa itikadi ya M4C.
Bagenda pia amesema kampeni ya M4C wanayoongoza nchi nzima inatangaza sera za shari na chuki.Pia amesema CDM walipata kura nyingi uchaguzi mkuu uliopita kutokana na vita ya makundi ndani ya CCM na kamwe si kutokana na chama hicho kuwa na sera nzuri.Amesema CDM hawana Itikadi inayoeleweka hadi sasa ndiyo maana mpaka sasa wajanja kama yeye wako CCM.

Source:RAI Alhamisi

My Take:
Prince Bagenda alishiriki kusambaratisha chama cha NCCR Mageuzi baada ya kuongoza mgogoro mkubwa huku akikimega chama vipande viwili na yeye akiwa Katibu Mkuu kambi ya Mrema.Baada ya kufanikisha kusambaratisha NCCR,Prince Bagenda alihamia CCM ambapo hadi leo yeye ni kada mwaminifu wa CCM.

anayosema yanaweza kuwa maneno ya kutafakari maana hata saa mbovu inakuwa sahii walau maramoja kwa siku. lakini yeye binafsi hana ujanja wowote kwa kuunga mkono udharimu wala hana usafi wa kusema hayo. lamsingi tuimarishe misingi na falisafe ya M4C tutafanikiwa tu.
 
Watanzania wenzangu hasa wale wananchi wa Muleba Kaskazini, tumsamehe bure bila hela ndugu yetu Prince.Bagenda kumbe muda wote huo aliuza nguvu ya Wtz waliopoteza muda wao mwingi wakimuunga mkono katika chaguzi mbalimbali akiwa mpinzani wa chama cha Mapinduzi CCM, amesahau ya kwamba wahaya kwa maelfu walipoteza muda wao mwingi sana Kumsaport katika chaguzi zile ingawa hata kesi zake mahakamani hakushinda. kitendo cha kuwageuka na kukiunga mkono chama pinzani kwake Utastaaaaaaaaaaajabu sana kulisikia hilo angalu angelipa fadhila ya wahaya wenzake waliokuwa wanaacha shuguli zao na kumuunga mkono kisiasa waswahili walisema ukistaajabu ya Mussa uyaona ya Filauni. inanikumbusha maneno matakaatifu yasemayo ninanukuu, Sio wote walitajao jina la Mungu watauona Ufalme wa Mbingu.kumbe Prince Bagenda ulikuwa kiini macho kwa walala hoi wa Tz ungetumia busara zaidi kuwasaidia wale woote waliokuunga mkono wakidhani ungewakomboa kumbe mgogoro wa NCCR uliwasaidia sana waliokwishapata matumaini ya Bagenda kuwa mkombozi wao mwenyezi mungu akawaonyesha njia kama Mussa alivyo waongoza wana wa Israel kutoka nchi ya Misri.
 
Naona yeye kajadili issue, badala ya kujadili hoja mnamjadili mtu, hii nyie ni wazima kweli. Watu makini hujadili issues si mtu, nitawaambia hadi lini, ndio maana mnaonekana dhaifu humu ndani, hata huyoo aliyesafiri naye kama kasoma lakini hakuelewa. Mungu saidia kizazi hiki
 
Huyu Bagenda na akina Salva ni jamii moja. Njaa iliwafanya wakane weledi wao. Sisi tuliowafahamu hakika twawaita "marehemu"
 
kuna siku tulikuwa UDSM kwenye kongamano la KATIBA watu walimzomea huyu jamaa na macho yake utazani kinyonga nilimwonea huruma manake alitoka povu then watu wakamzomea sana
 
Nilikuwa nawaza Amekwenda wapi PRINCE BAGENDA? Kumbe kaanzisha Chama kingine

Ndani ya CCM; kwahiyo yeye ni M4C copy upande wa CCM; CCM wajichunge asiwasambaratishe

kama NCCR Mageuzi... Ana Chuki Kweli...

Na njaa pia anayo.
 
Naona yeye kajadili issue, badala ya kujadili hoja mnamjadili mtu, hii nyie ni wazima kweli. Watu makini hujadili issues si mtu, nitawaambia hadi lini, ndio maana mnaonekana dhaifu humu ndani, hata huyoo aliyesafiri naye kama kasoma lakini hakuelewa. Mungu saidia kizazi hiki

Sasa wewe ndie unaharibu.

Hoja huangaliwa na ikionekana ina kasoro si anaangaliwa anaeleta hio hoja ama vipi?.

Prince Bagenda ameleta hoja mbovu na haileweki si inabidi kumwangalia mtu mwenyewe au wewe umeonaje hoja yake?

Ikiwa unaungana nae basi usijibu swali langu bali chambua hoja yake, na kama unaona hoja yake ina mapungufu basi wewe ongezea mapungufu hayo.
 
Mnafiki huyo!

Kama M4C itaivuruga CDM, yeye kinamuuma nini maana hilo sio ndio lengo na dua yake na ccm? Therefore the opposite is the truth, M4C ya CDM inaua ccm ya Bagenda!
 
Alipokuja kugombea ubunge Muleba Kusini aliuzwa swali moja "Twambie unalala wapi?" ............

Hakuna mwanasiasa njaa na mchumia tumbo kama Bagenda, nikikumbuka tulivyomtesekea huyu bwana huwa sitaki hata kumuona. Mpuuzi yule
 
kuna siku tulikuwa UDSM kwenye kongamano la KATIBA watu walimzomea huyu jamaa na macho yake utazani kinyonga nilimwonea huruma manake alitoka povu then watu wakamzomea sana

Yap nakumbuka siku hiyo nilikuwepo.Alizomewa mpaka akachanganyikiwa akapotea kiti alichokuwa amekaa wakati anarudi kwenye seat yake.
 
Prince Bagenda is a delinquent politico. Thank you for your misguided,misconstrued,deviant, hemorrhaging analysis, Mr. Bagenda. Who reads RAI anyway. All things considered CCM is going through painful labour, and something beautiful will be born out of this.. that is Government of Chedema in 2015!
 
nashkuru katambua M4C ni tishio...... kma anategemea harakati za kinyonga hko alipokimbilia ndo kunamfaa haswaaaaaaaaaa.....!
 
Hakuna wa kuzuia moto wa M4C, ishu ni kuwafanya wananchi kuwa aware na maisha yao na wajali nchi na maslai yao,,,hii kitu itawasumbua balaaa..........
 
Back
Top Bottom