Poleni TISS tena... R.I.P "Dr"

Status
Not open for further replies.
Idara za ujasusi zinaweza kuficha jina halisi la mtu hata likitajwa hapa unaweza kukuta ni la kificho lakini ni kweli msiba wa jasusi mwenye elimu ya PHD na aliyeandika vitabu vingi vya mambo ya ujasusi aliaga dunia mwezi wa kwanza kwa habari ambazo zilizagaa katika mitaa lakini pasipo mtu yoyote kudhibitisha. Nasikia mazishi yake yalijawa na usiri wa hali ya juu sana ili marehemu asitangazwe kama ilivyo kwa wanasiasa, hata hivyo alizikwa kwa heshima kubwa ya kiongozi mwandamizi wa Idara hiyo nyeti ya Taifa. hata viongozi wakuu wa kitaifa waliokwenda kumzika hawakutangangazwa bali ni barabara tu zilikuwa zinasafishwa kuelekea makazi yake na mwisho mazishi yake. Hakuna mwandishi wa habari aliyeruhusiwa kupiga picha kwani picha zote zilikuwa zinapigwa na majasusi wenyewe kwa kumbukumbu zao. Tumesikia Ulinzi ulikuwa mkali kudhibiti habari za kuvuja au kumtambua jasusi mahili aliyeaga dunia baada ya kulitumika taifa kwa weredi wa hali ya juu na kwa kificho kikubwa hadi anakata roho ya kizalendo.

Hivi hao TISS kuna utaratibu gani wa kuzisaidia familia za watumishi wao waliojitolea moyo, mwili na akili kwa taifa hili? au ukishakufa ndio basi tena?
 
Kwa mara nyingine, ninakuja na kutoa rambirambi kwa Idara ya Usalama wa Taifa kwa kumpoteza mmoja wa viongozi wa waandamizi ambao kwa kweli walikulia ndani ya Idara hiyo. Ni pigo kubwa kwa idara hasa kuondokewa na watu wenye weledi na waliojitahidi kufanya kazi yao licha tofauti ambazo zimekolezwa miaka hii michache iliyopita.

Bahati mbaya kutokana na kazi zao watu kama Dr. ni vigumu kuwaona viongozi wa kitaifa wakijitokeza kwenye misiba yao kwani wanalindwa na sheria ya TISS ya 1996. Ni hawa ambao majina yao na sifa za utumishi wao haziandikwi magazetini au hawawezi kuja na kulalamika hadharani jinsi mambo yalivyo magumu kitaifa. Ni hawa ambao huwa wanajikuta wananyong'onyea katika kuta za nyumba zao wasijue wafanye nini. Hawa wasio na watetezi wa wazi.

Na hii ndio sababu siwataji hawa wazee wetu ambao wametumikia taifa katika nafasi mbalimbali na hawakukubali kuwa corrupted kama kundi la baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye idara siku za karibuni na sasa wamegeuka kuwa mabepari uchwara.

Natumaini siku moja idara hii itakuja kufanyiwa maboresho yanayohitajika haraka ili watu kama marehemu wazidi kuvutiwa kulitumikia taifa.

RIP - Amezikwa makaburi ya Kinondoni katikati ya mwezi wa kwanza baada ya kulitumikia taifa kwa muda mrefu na kwa uadilifu.

RIP Dr..

wanaosema umo humo humo wana hoja?
 
Hivi hawa wanasimamia watu wasichakachue mambo mbalimbali kama wala wa CIA au wako kama KGB tu. Poleni Sana kwa Msiba
 
Naambiwa kuwa kuna watu TISS wamebobea kwenye Economic Espionage, hapo kweli naachwa hoi!..wanashindwa vipi kushauri serikali na kuchukua hatua juu ya utoroshaji uliokithiri wa madini nchini ambao unafanywa kupitia baadhi ya viwanja vya ndege!
Ni unazi upi wa kiuchumi na kizalendo walioufanya so far ambao umepelekea nchi kuinuka na tunaweza kujitapa kuwepo kwao?
CURIOUS!

Great Thinker Paka Jimmy
Hiyo idara imeingiliwa na Siasa, nadhani wanasiasa wamekuwa na nguvu mno, sio kweli kuwa jamaa hawaoni, wanaona na wanatoa alert, Alert kizishafika zinaenda kwa wanasiasa ambao ndio wanaoamua, Pale BOT jamaa wamejaa , sasa unataka kuniambia hawakuistukia EPA kuwa ni wizi?, waliistukia na walitoa report lakini utekelezaji ukawa wa kisiasa zaidi (CCM), ni hatari mno kwa wahuni kuingia mpaka reserve bank na kuchota pesa
 
nyie mmesahau yule jamaa wa TAKUKURU alivyojitetea?........kama na Ara tu ze Oo angepewa chansi ya kujitetea naye angesema ripoti tunapeleka ila ........
 
kama ni kufungwa jf ingekuwa imefunga zamani sana..........tena sana tu........hii kitu inaisaidia sana serikali yenu kujua mambo kibao.....na humu ndani wapo wengi tu ila kwa kuwa maadili hakuna siku hizi wanaanza kuvujisha siri......ndio maana hata mwanakijiji ametoa thread yake hii na kuficha jina lakini kwa kuwa humu ndani wako wengi tena level ya repoter wamediriki kutaja jina la marehem Heri Lupembe (Dr).

na kwakupitia jf tanzania hapatakuja kutokea vurugu kama za huko tunisia au masri.......sababu kubwa ni hii jf inavujisha sana habar na kuipa mwanya serikali kwa kujipanga kujibu mapigo............ ( MARK THIS POST)

kuna ndugu mmoja FMES siku hizi anapita humu kupunga mkono na kuonyesha kuwa bado yuko hai lakini hachangii mada kama zamani .....sababu alijianika siku moja huko na kutoa ID yake ya jf jama mmoja akaja akamwaga data za FMES , mwisho wa siku fems alipaki na kusepa. huko TISS tuna maanadili na miiko lakini kwa kuwa siku hizi wengi wanaokwenda malindi ni ndugu wa karibu na wakubwa na hawana maadili ndio maana kila kitu kinavuja........... halafu mwanakijiji hii iwe mara ya mwisho kuja na habari thread kama hizi unatukosea heshima..... kwa kuwa tumekula kiapo cha cha kufanya kazi bila kujulikana wacha tufe na habari zetu zisijulikane .........miiko hii hata wewe unayo na unaijua maana na wewe ni wa huku.......... mambo mengine kaaga kimya tu
 
...I'm speechless na hayo mambo ya TISS na siri.......! siri nyingi zisizo na manufaa yoyote kwa taifa! hao TISS wanaonekana kwanza sio wazalendo, maufisadi yote tunayosikia leo yamefanyika ikiwa hao wazee wapo huko ndani, wanafanya nini? wapo kwaajili ya usalama wa nani, Taifa au Ikulu? Taifa linaibiwa, taifa lidhulumiwa mali zake, Taifa linafanywa gofu.....wao kimyaaaaa!

Siku hizi tena hivyo vi-TISS kazi yao ni kututishatisha huku kwenye vipombe na vipisto vyao.....! wameacha majukumu yao makuu, wanajifanya miungu watu hawa......! lao ni moja katika kuifanyia ufisadi nchi hii! System yote ya TISS inahitaji overhaul ya nguvu......!

Sorry nikisikia TISS huwa napata kichefuchefu ...... But R.I.P DR. TISS!

No more comment!
 
Kwani CIA wanafanya kazi kama TISS. Tutafute policy zao na kuona kama kuna uelekeo. Aibu Jamani. Nilikua Nchi Fulani, ukikutwa na madini bullet, wanasema hizo ni nyara za serikali. Ile nchi iko Africa na inaendelea kwa kasi sana. TISS yao ina meno kwa manufaa ya umma.
 
kama ni kufungwa jf ingekuwa imefunga zamani sana..........tena sana tu........hii kitu inaisaidia sana serikali yenu kujua mambo kibao.....na humu ndani wapo wengi tu ila kwa kuwa maadili hakuna siku hizi wanaanza kuvujisha siri......ndio maana hata mwanakijiji ametoa thread yake hii na kuficha jina lakini kwa kuwa humu ndani wako wengi tena level ya repoter wamediriki kutaja jina la marehem Heri Lupembe (Dr).

na kwakupitia jf tanzania hapatakuja kutokea vurugu kama za huko tunisia au masri.......sababu kubwa ni hii jf inavujisha sana habar na kuipa mwanya serikali kwa kujipanga kujibu mapigo............ ( MARK THIS POST)

kuna ndugu mmoja FMES siku hizi anapita humu kupunga mkono na kuonyesha kuwa bado yuko hai lakini hachangii mada kama zamani .....sababu alijianika siku moja huko na kutoa ID yake ya jf jama mmoja akaja akamwaga data za FMES , mwisho wa siku fems alipaki na kusepa. huko TISS tuna maanadili na miiko lakini kwa kuwa siku hizi wengi wanaokwenda malindi ni ndugu wa karibu na wakubwa na hawana maadili ndio maana kila kitu kinavuja........... halafu mwanakijiji hii iwe mara ya mwisho kuja na habari thread kama hizi unatukosea heshima..... kwa kuwa tumekula kiapo cha cha kufanya kazi bila kujulikana wacha tufe na habari zetu zisijulikane .........miiko hii hata wewe unayo na unaijua maana na wewe ni wa huku.......... mambo mengine kaaga kimya tu

Kama tu ni kweli, makubwa basi!
 
Kwa mara nyingine, ninakuja na kutoa rambirambi kwa Idara ya Usalama wa Taifa kwa kumpoteza mmoja wa viongozi wa waandamizi ambao kwa kweli walikulia ndani ya Idara hiyo. Ni pigo kubwa kwa idara hasa kuondokewa na watu wenye weledi na waliojitahidi kufanya kazi yao licha tofauti ambazo zimekolezwa miaka hii michache iliyopita.

Bahati mbaya kutokana na kazi zao watu kama Dr. ni vigumu kuwaona viongozi wa kitaifa wakijitokeza kwenye misiba yao kwani wanalindwa na sheria ya TISS ya 1996. Ni hawa ambao majina yao na sifa za utumishi wao haziandikwi magazetini au hawawezi kuja na kulalamika hadharani jinsi mambo yalivyo magumu kitaifa. Ni hawa ambao huwa wanajikuta wananyong'onyea katika kuta za nyumba zao wasijue wafanye nini. Hawa wasio na watetezi wa wazi.

Na hii ndio sababu siwataji hawa wazee wetu ambao wametumikia taifa katika nafasi mbalimbali na hawakukubali kuwa corrupted kama kundi la baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye idara siku za karibuni na sasa wamegeuka kuwa mabepari uchwara.

Natumaini siku moja idara hii itakuja kufanyiwa maboresho yanayohitajika haraka ili watu kama marehemu wazidi kuvutiwa kulitumikia taifa.

RIP - Amezikwa makaburi ya Kinondoni katikati ya mwezi wa kwanza baada ya kulitumikia taifa kwa muda mrefu na kwa uadilifu.

RIP Dr..

Mwanakijiji usingeileta hii habari hapa JF kwani haina tija.Hata kama alifanya utumishi uliotukuka lakini kama sheria haziruhusu watu wa TISS kuwa exposed basi ni heri habari zao pia zikiendelea kufichwa hata wanapofariki kama wenyewe wanavyoapa kuwa wasijulikane mpaka kufa.
Anyway RIP Marehemu
 
Kumekucha MM unawafanya watu wanakosa usingizi maana wanashindwa kuelewa. Safi sana wachanganye tu mpaka wachanganyikiwe waokote vindude teh teh teh
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom