Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kwa mara nyingine, ninakuja na kutoa rambirambi kwa Idara ya Usalama wa Taifa kwa kumpoteza mmoja wa viongozi wa waandamizi ambao kwa kweli walikulia ndani ya Idara hiyo. Ni pigo kubwa kwa idara hasa kuondokewa na watu wenye weledi na waliojitahidi kufanya kazi yao licha tofauti ambazo zimekolezwa miaka hii michache iliyopita.
Bahati mbaya kutokana na kazi zao watu kama Dr. ni vigumu kuwaona viongozi wa kitaifa wakijitokeza kwenye misiba yao kwani wanalindwa na sheria ya TISS ya 1996. Ni hawa ambao majina yao na sifa za utumishi wao haziandikwi magazetini au hawawezi kuja na kulalamika hadharani jinsi mambo yalivyo magumu kitaifa. Ni hawa ambao huwa wanajikuta wananyong'onyea katika kuta za nyumba zao wasijue wafanye nini. Hawa wasio na watetezi wa wazi.
Na hii ndio sababu siwataji hawa wazee wetu ambao wametumikia taifa katika nafasi mbalimbali na hawakukubali kuwa corrupted kama kundi la baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye idara siku za karibuni na sasa wamegeuka kuwa mabepari uchwara.
Natumaini siku moja idara hii itakuja kufanyiwa maboresho yanayohitajika haraka ili watu kama marehemu wazidi kuvutiwa kulitumikia taifa.
RIP - Amezikwa makaburi ya Kinondoni katikati ya mwezi wa kwanza baada ya kulitumikia taifa kwa muda mrefu na kwa uadilifu.
RIP Dr..
Bahati mbaya kutokana na kazi zao watu kama Dr. ni vigumu kuwaona viongozi wa kitaifa wakijitokeza kwenye misiba yao kwani wanalindwa na sheria ya TISS ya 1996. Ni hawa ambao majina yao na sifa za utumishi wao haziandikwi magazetini au hawawezi kuja na kulalamika hadharani jinsi mambo yalivyo magumu kitaifa. Ni hawa ambao huwa wanajikuta wananyong'onyea katika kuta za nyumba zao wasijue wafanye nini. Hawa wasio na watetezi wa wazi.
Na hii ndio sababu siwataji hawa wazee wetu ambao wametumikia taifa katika nafasi mbalimbali na hawakukubali kuwa corrupted kama kundi la baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye idara siku za karibuni na sasa wamegeuka kuwa mabepari uchwara.
Natumaini siku moja idara hii itakuja kufanyiwa maboresho yanayohitajika haraka ili watu kama marehemu wazidi kuvutiwa kulitumikia taifa.
RIP - Amezikwa makaburi ya Kinondoni katikati ya mwezi wa kwanza baada ya kulitumikia taifa kwa muda mrefu na kwa uadilifu.
RIP Dr..