Pinda: Serikali kuunda jopo kuchunguza madai ya katiba mpya

Ndugu zangu naomba niwapongeze wapenda mabadiliko bila kuisahau CDM na viongozi wake kwa kuwaelimisha waTZ kuhusu katiba mpya kwani waTZ wote sasa wanaelewa hata chanzo cha umasikini wao unatokana na Katiba iliyoko sasa kwani inampa rais na serikali madaraka makubwa makubwa mno ambayo kwa miaka 49 sasa yamekuwa yakitumiwa vibaya sana ndio maana nhi hii na rasilimali zote ni masikini na watu wake ni masikini ile hali viongozi wakiwa matajiri wa kutupwa.

Pili nawapongeza wanaJF kwa kuzidi kuongeza kasi katika kudai haki, na katiba mpya ya nchi naomba mijadala hii iendelee hadi tutakapowashinda mafisadi nchi hii maana kama alivyosema mtoto wa mkulima mafisadi wana hela nyingi sana na wana nguvu sana kama ambavyo wamekuwa wakiwarubuni viongozi machachari nchi wakitaka kupanga safu ya viongozi watakao watetea hadi kwenye vyama vya siasa kama tuliyona siku za hivi karibuni.


Tatu naomba kumpongeza kamanda mbowe akisaidiwa na Dr. Slaa kwa misimamo yake kwani amekuwa mwiba kwa Mafisadi na ndio waTZ tunataka mtu wa namna hiyo, mapambano daima hadi kieleke wananchi wapo pamoja nanyi. watu wamechoka kimsingi na wako tayari kwa mabadiliko kwa gharama yeyote.


Kwa kweli mwaka huu nafikiri mafisadi wametumia mbinu zote hadi zimekwama kwa chadema, tuendellee na moyo huo na kama vipi watu wako tayari kugharamikia Democrasia.


Peoples Power.
 
/Mimi sijamsikia huyu mtoto wa mkulima,kuna mwenye detailed news?
naomba iwekwe hadharani tuione kabla ya kutoa maoni.
 
Sorry but to be honest, ni kwamba sijawahi ona waziri ambaye ni serious kwene baraza la brazaman, only Makufuli ya pombe... ukiangalia kwa undani hata PM nae hajaongea jambo lolote la maana ni yale yale ya kumwambia mtoto "acha kulia nitakununulia pipi kesho ee mtoto mzuri"
 
Watanzania tunasikitisha kweli, hasa hao chadema eti wanapongezana. Mhhhhhhhhhhh
Pamoja ccm kuwakubali kuwa ni mafisadi lakini pia sisiti kuwakubali kwa mbinu na namna ya kutawanya mijadala, unaona kabisa ni watu wenye uwezo wa kiakili tatizo wakiwa wamewekeza kwenye mchapuko hasi. Sasa Chadema tafuteni issue ingine ya kutokea hii imezimwa rasimi .
 
Futa kila kitu njooni na rim tu tuanze upppppppyyyyyyyyyyaaaaaaaaaaa kabisa katiba yetu ni mbaya dunia nzima mbaya mbaya mbayaaaaa saaaaaaana kabisa tunaanza ukurasa upya kabisa
 
wazo binafsi:
1. Huyu waziri kombani (ni taka nyingine iliyowekwa na kikwete). Ajiuzulu tu.
2. Katiba ni ya wananchi na siyo blablaz za wabunge (vihiyo) wa ccm wakapige makofi kwa wananchi ili kuongeza viraka, wananchi wahusishwe kwa vikao vya wadau wanaoweza kuleta mabadiliko.
3. Tume ya kuunda katiba ihusishe wadau kuto chama kikuu cha upinzania (isipokuwa zito kabwe kwa unafiki aliouonesha).
4. Uundwaji wa katiba hii uwe chini ya waziri mkuu na siyo wizara hii inayoongozwa na huyu mama (kihiyo wa kusoma nyakati).
5. ............
 
Katiba si ilani ya CCM au mwongozo wa rais. Ni sheria mama ya taifa zima. Pinda ana dhana potofu kwamba rais ndio aliye na uamuzi wa mwisho juu ya mabadiliko tunayoyataka. Rais hana kauli ya mwisho kwa masuala ya katiba ila wananchi. Tunanataka katiba mpya na si huruma ya rais! Pinda na rais washauriane au la hayo ni yao... wasome alama za nyakati. Katiba mpya ni lazima na delaying tactics au janja nyingine hazikubaliki! Tume ngapi Nyalali, Kisanga, Warioba etc zimeundwa zote zikionyesha umuhimu wa marekebisho ya sheria? Hawakufanya sasa tumechoka tutawalazimisha Katiba mpya na tume huru ni lazima!
 
Futa kila kitu njooni na rim tu tuanze upppppppyyyyyyyyyyaaaaaaaaaaa kabisa katiba yetu ni mbaya dunia nzima mbaya mbaya mbayaaaaa saaaaaaana kabisa tunaanza ukurasa upya kabisa

TANZANIA HAISTAHILI VIRAKA ZAIDI

TANZANIA, safari hii vijana wako tume jiandaa vilivyo KUNUNULIA SUTI TENA ILE YA KUJIPIMIA MWENYEWE!!!!

Kamwe HAKUNA TUTAKAYEMRUHUSU KUKUVALISHA MITUMBA ZAIDI, VIRAKA ZAIDI NA MIGUNIA ZAIDI wakati wao wanakula wanashaza kuponda mali zako ovyo ovyo kana kwamba mwenye mali hayupo.

Tabasamu basi Mpendwa Mama Tanzania!! Nguo yako safari hii MPYAAAA YAKUJIPIMISHA tutakavyo vijana wako kwa raha zetu mamaaa!!!! Ole wao wale waliozoea kukutupia tambara na viraka wakajitokeza tena wakidhani ya kwamba wewe kawaida yako miaka yote mtu WA DHIKI TU.

Kama hivyo vivyo ndivyo mama, sasa kwa nini ulituzaa, ukatulea kwa shida kubwa, UMEBAKWA MARA KADHAA na MAFISADI mbele ya macho yetu bila kujali sisi watoto wako tutajisikiaje.

Jamani, SWALA LA MUDA GANI NI MUAFAKA ZAIDI WA KUMNUNULIA KIPENZI MAMA YETU TANZANIA nguo mpya katu hatuchaguliwi na mtu yeyeyote!!!

Na hata CCM kuwataka CHADEMA wakakutane faragha kujadili kama mama yetu apate nguo mpya au laa ni makosa na matusi makubwa kwetu wakaki sisi wananchi wenye Mama yao tupo!!!
 
Mkuu,

Wakati wa kupongezana bado, ni mapema sana. Asante kwa ufafanuzi.

Hakuna haja ya kusubiri kupongezana hadi pale katiba mpya inapokabidhiwa rasmi kwa Watanzania. Kwa mara ya kwanza katika kudai katiba mpya kuna makada mbali mbali wa CCM ambao wameunga mkono madai ya katiba mpya ambako huko miaka ya nyuma haijawahi kutokea.

Makada hao wakiwemo Mkapa, Mawaziri wakuu wa zamani Warioba na Sumaye (nasikia na SAS naye anaunga mkono katiba mpya labda waandishi wakimdodosa anaweza kutoa tamko rasmi la kuunga mkono katiba mpya) Hashim Mbita, na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Tendwa. Hili pamoja na kuwa ni fanikio dogo sana lakini inabidi kulifurahia labda ni dalili ambazo zinaweza kufungua. Ndiyo maana hata wazazi hufurahia sana hatua ndogo ndogo katika maisha ya mtoto kama vile kukaa chini, kutambaa, kuanza kusimama n.k. pamoja na kuwa Wazazi wanafahamu mtoto yule bado ana safari ndefu sana katika maisha yake lakini hufurahia mafanikio madogo madogo katika maisha ya mtoto wao.

Hivyo kwa maoni yangu sioni ubaya wa kupongeza haya mafanikio japo ni madogo na safari bado ni ndefu sana.

Weekend njema
 
Katiba mpya naiona ileeeeeeeee....ila yenye matakwa ya watawala,mchakato utaburuzwa na maoni ya watanzania yatachakachuliwa,jopo la wataalam litaongozwa na wataalam wasio wazalendo kama kabudi wa udsm na benson bana..hawa jamaa ni wasanii,ishu ni kuingia msituni tu no option!..
 
Akizungumzia suala hili Mizengo Pinda amesema haja ipo ila bado haijaamua kama mabadiliko yanayoitajika ni makubwa au madogo

Ndiyo tatizo la nchi yetu, mambo yanafanywa kwa maslahi ya kikundi kidogo cha wananchi kwa manufaa binafsi. Hata jopo la wataalam watakaoteuliwa kuipitia katiba na kuona kama kuna umuhimu wa mabadiliko litawekwa kwa maslahi ya wachache. Watanzania tufike mahali tuseme imetosha. Huu siyo muda wa kujadili kama kuna umuhimu wa katiba mpya bali ni wakati wa kuitupa jalalani katiba iliyopo na kuunda mpya inayoendana na mazingira ya sasa.
 
JK ndiye aliyetakiwa kuongea haya. Lakini amegundua nii too late na hivyo hataki kuliongelea kwa sasa sababu ataonekana amekubalianana pressure za wataka mabadiliko wakiogozwa na CDM.

Hapa PM katumwa kuficha aibu ya bosi Mkuu wa nchi

Wanatakiwa wacheze beats za muziki ulioko hewani. wakizdi kuchelewa CCM watashangaa.
 
katiba ijumuishe maoni ya watanzania wote si ccm tu plse ccm nawaonya juu la hilo mmetunyima haki yetu muda mrefu sanaaaaaaaaa.

Umeamini vipi kua Pinda asemacho ni kweli kua KATIBA itabadilishwa na kuwa Kombani alisema uongo. Jua tu kua Kombani na Pinda wote ni viongozi wa juu katika serikali ya CCM. Utaaminije ukweili wa wasemacho mawaziri wa CCM kua Katiba itabadilishwa kama hamna iliyetengua usemi wa Kombani.

CCM bado wala hawana mpango wa kubadili katiba kwa maslahi ya wote. Kila kiongozi wa CCM katika ngazi yake ataendelea kuropoka tu yale atayoona kupooza walalahoi ili kuvuta muda mpaka 2015.
 
Katika mazungumzo ya PM sikuona nia ya dhati ya serikali kuhusu katiba mpya, ni kama vile serikali inataka kutuliza huu upepo unaovuma kwa kasi.......ni kama kutaka kusema ''si tumesema tunalishughulikia sasa mnalalamika nini''. Kuna machache ambayo sikuyaelewa:


  • PM ni sehemu ya serikali, atasemaje atamshauri rais, mimi nadhani msimamo aliokuja kuusema ni wa serikali yote sasa atmshauri rais yeye kama nani, mtu, mbunge au......?
  • Vinginevyo asema alikuwa anakanusha tamko la Kombani ambaye yuko chini ya ofisi yake, hivyo wao kama ofisi ya waziri mkuu watamshauri Rais akubali mawazo ya katiba mpya (haina mantiki kabisa)
Viongozi wawe wanaongea mambo ambayo yanasaidia kuweka wazi misimamo ya serikali. Mimi nafikiri PM angesema mambo mawili: Moja serikali kama inaafiki kuandikwa katiba upya au inataka kuweka viraka, mbili ni lini serikali itaanzisha huo mchakato.............. basi
 
Baada ya kilio cha muda mrefu cha madai ya Katiba, hatimae hii leo serikali ya Tanzania imekiri kuwa ipo haja ya kuifanyia mabadiliko Katiba ya sasa ili iweze kukidhi mahitaji na mabadiliko ya sasa.


Akiongea na wahariri wa vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda amesema serikali itaunda jopo la wataalam kupitia mapendekezo ya awali na ya sasa yaliyotolewa kuhusiana na mabadiliko ya Katiba.


Hata hivyo Mh. Pinda amesema serikali bado haina jibu iwapo yafanyike mabadiliko makubwa ama mabadiliko madogo kutokana na mapendekezo yaliyokwishatolewa, au suala hilo lipelekwe bungeni ama lirudishwe kwa wananchi kwa maamuzi.


Source-Mimi

Katiba mpya ni wazo zuri tena ambalo limepitwa na wakati.Lakini kwanini swala hilo liibuliwe sasa wakati ambapo wananchi wanalia huku wakilalamika kwamba wamedanganywa katika uchaguzi uliopita?My take is this: ingawa swala hili ni la msingi lakini limeibuliwa sasa so as to divert attention from the election issue.Kwangu mimi swala la kuendelea kuongelea udanganyifu uliofanyika katika uchaguzi uliopita na hata possibly kuiomba jumuiya ya kimataifa kuichukulia serikali ya Kikwete hatua muafaka ni muhimu sana.Kwahiyo ni vema mjadala kuhusu fraud iliyofanyika wakati wa uchaguzi ukaendelezwa sambamba na wa katiba mpya.
 
Ndugu zangu naomba niwapongeze wapenda mabadiliko bila kuisahau CDM na viongozi wake kwa kuwaelimisha waTZ kuhusu katiba mpya kwani waTZ wote sasa wanaelewa hata chanzo cha umasikini wao unatokana na Katiba iliyoko sasa kwani inampa rais na serikali madaraka makubwa makubwa mno ambayo kwa miaka 49 sasa yamekuwa yakitumiwa vibaya sana ndio maana nhi hii na rasilimali zote ni masikini na watu wake ni masikini ile hali viongozi wakiwa matajiri wa kutupwa.

Pili nawapongeza wanaJF kwa kuzidi kuongeza kasi katika kudai haki, na katiba mpya ya nchi naomba mijadala hii iendelee hadi tutakapowashinda mafisadi nchi hii maana kama alivyosema mtoto wa mkulima mafisadi wana hela nyingi sana na wana nguvu sana kama ambavyo wamekuwa wakiwarubuni viongozi machachari nchi wakitaka kupanga safu ya viongozi watakao watetea hadi kwenye vyama vya siasa kama tuliyona siku za hivi karibuni.

Tatu naomba kumpongeza kamanda mbowe akisaidiwa na Dr. Slaa kwa misimamo yake kwani amekuwa mwiba kwa Mafisadi na ndio waTZ tunataka mtu wa namna hiyo, mapambano daima hadi kieleke wananchi wapo pamoja nanyi. watu wamechoka kimsingi na wako tayari kwa mabadiliko kwa gharama yeyote.

Kwa kweli mwaka huu nafikiri mafisadi wametumia mbinu zote hadi zimekwama kwa chadema, tuendellee na moyo huo na kama vipi watu wako tayari kugharamikia Democrasia.

Peoples Power.

Natabiri Jopo la wataalamu:

1. Yusufu Makamba
2. Rizuani Kikwete
3. Shelukamba
4. Mudhihili Mudhihili
5. Kingunge Ngombalemwilu
6. Jaji Makame wa NEC
7. Kiravi wa NEC


Note: Serikali isije ikatuchezea !!!!!, tunataka watu makini sio usanii maana ndio zenu.
 
Back
Top Bottom