Pinda: Dowans hatuirudishi bungeni

Good move mzee Pinda. Kama kisheria tunatakiwa kulipa tuwalipe otherwise deni litakuwa kubwa tutashindwa kulipa matokeo yake tutabakia kugawa rasilimali zetu kama pipi kwa mafisadi.
 
Bunge letu ni la vikaragosi, niliandika article mwaka 2007 kwamba tunaitaji bunge lenye meno. Katiba inasema Bunge ni mshauri wa serikali. sasa kama serikali haitaki kushaurika, then bunge halina kazi.
 
Waandishi wa habari wa Tanzania wamejawa na ulimbukeni kwanini hawajauliza hatma ya wastaafu wa East Africa Community? Kwanini wasingeuliza mbona Valambia hajalipwa na Serikali licha ya mahakama ya rufaa kuamuzru alipwe? Something fishy here anyway nilikuwa napita tu nikasimama kidogo ngoja niendelee na misafara yangu...
 
Waandishi wa habari wa Tanzania wamejawa na ulimbukeni kwanini hawajauliza hatma ya wastaafu wa East Africa Community? Kwanini wasingeuliza mbona Valambia hajalipwa na Serikali licha ya mahakama ya rufaa kuamuzru alipwe? Something fishy here anyway nilikuwa napita tu nikasimama kidogo ngoja niendelee na misafara yangu...

Jibu rahisi sana EAC au Valambhia saga CCM wanafaidika nini? Dowans tunajua kuna Rostam Aziz na wenzie ambao tunajua kinachoendelea nyuma yao ni nini!!!
 
Huu ni ukuku mtupu wa serikali ya JK..... kwani kazi iliyofanywa na Mwanasheria Mkuu na ofisi yake ina mashaka??? kwa nini iundwe timu nyingine tena???.........as always son of the peasant doesnt know what to talk!!!!!
 
“Hatutalipeleka suala hili bungeni….kulipeleka huko itakuwa ni kwenda kujadili siasa na si sheria. Na kwa hili tayari kuna timu ya wabunge wa CCM ambao ni watalaamu wa sheria pamoja na timu itakayoundwa na serikali, timu hizo zitakaa na kupitia kwa makini suala hili ili twende tukatafute ufafanuzi huo wa kisheria,” alisema Pinda.


Inaonekana hawataki kabisa CDM wawe na nafasi kwenye huo mchakato!!Kwani wao hawana wataalam wa sheria wanaoweza kuhusishwa??
 
Good move mzee Pinda. Kama kisheria tunatakiwa kulipa tuwalipe otherwise deni litakuwa kubwa tutashindwa kulipa matokeo yake tutabakia kugawa rasilimali zetu kama pipi kwa mafisadi.

Another CRAP in the house!!!Hizo rasilimali ambazo bado mafisadi hawajagawana ni zipi haswa????
 
Another CRAP in the house!!!Hizo rasilimali ambazo bado mafisadi hawajagawana ni zipi haswa????

Lizzy kwa kukufunua tu,

we have 185 billion we need to pay pia usisahau kuwa there is a 7.5% p.a ,

= $24,168.343.83 plus 7.5% = unapata bei gani? (Kumbuka hiyo ni hadi June 2010).

= $39,935,765.50 plus 7.5% = unapata bei gani (Hadi June 2010).

Sasa jua kwamba tunaelekea June 2011.

Tukiendelea kulumbana tunaingia 2012, 2013 mwishoe tukistuka deni ni kubwa kiasi serikali haitaweza kulipa unadhani serikali yako hata kama ni Dr Slaa atafanya nini?
 
Lizzy kwa kukufunua tu,

we have 185 billion we need to pay pia usisahau kuwa there is a 7.5% p.a ,

= $24,168.343.83 plus 7.5% = unapata bei gani? (Kumbuka hiyo ni hadi June 2010).

= $39,935,765.50 plus 7.5% = unapata bei gani (Hadi June 2010).

Sasa jua kwamba tunaelekea June 2011.

Tukiendelea kulumbana tunaingia 2012, 2013 mwishoe tukistuka deni ni kubwa kiasi serikali haitaweza kulipa unadhani serikali yako hata kama ni Dr Slaa atafanya nini?


Tatizo ni kwamba ccm wanang'ang'ania tulipe sio kwa faida ya nchi kama ulivyoainisha wewe ila kwa faida yao binafsi!Ingekua ni kitu chenye uhalali kusingekua na asilimia kubwa ya watu wanaopinga huo ulipwaji....maana kama mmiliki tu hatajwi unategemea nini???
 
Tume ya Chenge et al ambao ni wezi pamoja na kiranja wao mkuu. Hivi Dowans waliposhindwa kutoa umeme wakati ule walilipa adhabu ambayo ilikubaliwa? Vile vile maagizo ya Bunge kuhusu Richmond yalifuatwa na serikali?

Serikali haiwezi kulirudisha hili swala bungeni kwa sababu wanafahamu nini kitafuata. Ni wajibu wa wabunge wa upimzani kuona swala hili linajadiliwa bungeni ili tukate mzizi wa fitna. Pinda hana uwezo wa kuzuia swala hili kule bungeni.
 
  1. Walitingisha kiberiti kuwa uamuzi umetolewa na ICC eti Dowans walipwe 185 bilioni, tukaguna.
  2. Wakagutuka wakadai kuwa haikuwa 185 bilioni bali 95 bilioni, tukaanza kujiuliza kulikoni ?
  3. Wakati hatujakaa sawa wakasema ni lazima tulipe kwani hamna tena ujanja, tukataharuki.
  4. Wakaanza na vitisho na matusi kwa kudai Ikulu haihusiki na sakata la Dowans, tukaguna tena.
  5. Wakitisha kikao cha walaji (CCM) na kubariki malipo kwa matapeli, tukasema wakilipa hapatatosha.
  6. Wakaitisha kikao cha wabunge kuweka mkakati wa pamoja, Mungu si athumani, wakakwama.
  7. Wakaunda kamati ya wanasheria wao wabunge eti kutafuta muafaka, tukaguna kwa sauti kubwa.
  8. Mwanasheria moja, Mkono, fisadi aliyekubuhu ataka tujadiliane na wezi watupunguzie - iwe bil. 50 ?

Hapana Pinda, ujanja umekuishia kwani umegeuzwa kuwa tambala bovu na chafu la kupigia deki ! Dowans iende bungeni tuwajue kwa majina na sura watakaowatetea hawa wezi tu tuwashughulikie kama maadui wa taifa.
 
Shame on our country

Na Baraka Kimwanga

SERIKALI imesema mjadala kuhusu fidia ya kampuni ya Dowans hautarudishwa bungeni na badala yake itafuata taratibu za kisheria kwa kwenda mahakamani ili mkondo wa sheria uchukue mkondo wake.

Mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara hivi karibuni ililiamuru shirika la uzalishaji na ugavi wa umeme nchini (TANESCO) kuilipa Dowans fidia ya shilingi bilioni 94 baada ya kulitia hatiani kwa kuvunja mkataba baina yake na kampuni hiyo kinyume cha taratibu za kisheria.


Msimamo mpya kuhusu Dowans ulitolewa jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, katika mkutano wake na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika semina ya siku tatu kwa wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), iliyofanyika Blue Peal Hotel, Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam ambapo alisisitiza kwamba suala la fidia ya Dowans halina ujanja kwani ni la kisheria na kwa hiyo ni lazima tulishughulikie kisheria.


“Hatutalipeleka suala hili bungeni….kulipeleka huko itakuwa ni kwenda kujadili siasa na si sheria. Na kwa hili tayari kuna timu ya wabunge wa CCM ambao ni watalaamu wa sheria pamoja na timu itakayoundwa na serikali, timu hizo zitakaa na kupitia kwa makini suala hili ili twende tukatafute ufafanuzi huo wa kisheria,” alisema Pinda.


Alisema mjadala huo wa hukumu ya Dowans umeibua hisia za watu mbalimbali nchini na hata kupelekea baadhi ya viongozi wa serikali kuingilia kati na kutoa misimamo yao hali ambayo haikuleta taswira nzuri kwa taifa.


“Kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake, na hata mawaziri waliopishana kauli ni ugeni wa masuala ya serikali tu, lakini jambo hili ni letu sote kama serikali na hivi sasa tumejiweka sawa ili kuepusha hali kama hii isijirudie tena,” alisema Pinda.


Akisoma maazimio ya semina hiyo Kaimu Katibu wa Kamati ya Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama, alisema kamati yao imeishauri serikali kutafakari kwa makini hukumu hiyo na kutumia njia za kisheria kuangalia uwezekano wa kutolipa fidia hiyo.


“Kuhusu deni la Dowans kwa TANESCO la sh 94 bilioni kamati ya wabunge wa CCM wameitaka serikali kupitia njia za kisheria itazame upya suala hilo kwa nia ya kutafuta uwezekano wa kuwaepushia Watanzania mzigo huu,” alisema Mhagama.


Alisema wabunge wa CCM wametakiwa kutumia kamati ya wabunge kwa ukamilifu kujadili masuala yote na hata kukosoana ndani ya vikao vya kamati kwa uwazi ili kulinda maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.


Hata hivyo Mhagama alisema semina hiyo imewapa uhuru kamili wabunge hao kuikosoa serikali na kutoa mawazo yao kuhusu masuala yote yenye maslahi kwa taifa ili mradi watumie lugha ya ufasaha.


“Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete, imetupa uhuru wa kuikosoa serikali na vyombo vyake ili mradi tu lugha ya ufasaha itumike katika kutoa maoni,” alisema Mhagama.


Alisema wabunge hao wameunda kamati ndogo ya kufanya marekebisho ya kanuni za wabunge wa kamati wa CCM na kuwa na wajumbe kumi ambao wataongoza timu hiyo.


Aliwataja wajumbe wa kamati ya marekebisho ya kanuni za CCM kuwa ni Jenista Mhagama, Dk. Maua Daftari, Pindi Chana, Bernadeta Mushashu, Christopher Ole Sendeka na Andrew Chenge.


Wengine ni Dk. Harison Mwakyembe, Gosbert Blandes, Mshadhi Maalim na George Simbachawene.


Kuhusu migomo ya vyuo vikuu

Pinda alisema serikali imepitia kwa makini na kuunda kamati na kugundua matatizo ya mawasiliano baina ya utawala, wafanyakazi na wanafunzi waliopo masomoni hali inayopelekea kutokea migomo ya mara kwa mara.

Alisema njia ambazo serikali imeshauri ni kuhakikisha kunakuwa na ujenzi wa miundombinu ya uhakika katika vyuo vyote vya umma pamoja na kuwa na utaratibu wa kufanya ukaguzi wa mahesabu kupitia ofisi ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali.


Mgao wa Umeme

Alisema kwa mujibu wa Waziri wa Nishati na Madini imebainika hivi sasa Tanzania inakabiliwa na uchavu na uduni wa miuondombinu katika vyanzo vya umeme nchini.

Alisema kukosekana kwa maji ya uhakika kumepelekea kutokea mgao wa mara kwa mara nchini hali ambayo inarudisha nyuma maendeleo ya taifa na watu wake.


“Utafiti unaonyesha kuwa matumizi ya umeme nchini yameongezeka kuliko uwezo wetu lakini serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na tatizo hili ili limalizike kabisa,” alisema Pinda.


Source: Tanzania Daima
 
Tatizo ni kwamba ccm wanang'ang'ania tulipe sio kwa faida ya nchi kama ulivyoainisha wewe ila kwa faida yao binafsi!Ingekua ni kitu chenye uhalali kusingekua na asilimia kubwa ya watu wanaopinga huo ulipwaji....maana kama mmiliki tu hatajwi unategemea nini???
Nakubaliana na wewe, ila tatizo Lizzy kama umetafakari vizuri hii sarakasi mafisadi wamejipanga na kuibana serikali kisheria sasa sijui hata tukipinga sijui kitu gani tutafaidika nacho!
 
Nakubaliana na wewe, ila tatizo Lizzy kama umetafakari vizuri hii sarakasi mafisadi wamejipanga na kuibana serikali kisheria sasa sijui hata tukipinga sijui kitu gani tutafaidika nacho!

Yani wewe Mdondoaji ni mdhaifu sana....kwahiyo kama wamejipanga na sisi hatuwezi kujipanga????
Acha kua mwepesi wa kukubali kushindwa kiasi hicho!!
Refer post ya Mag3 ....kama tungekubali tangu mwanazo kulipa Bil 185 tungekua tumejisaidia au tumewasaidia?Think about it!!!
 
Yani wewe Mdondoaji ni mdhaifu sana....kwahiyo kama wamejipanga na sisi hatuwezi kujipanga????
Acha kua mwepesi wa kukubali kushindwa kiasi hicho!!
Refer post ya Mag3 ....kama tungekubali tangu mwanazo kulipa Bil 185 tungekua tumejisaidia au tumewasaidia?Think about it!!!

Sawa Lizzy,
Hata hivyo kama mtu niliyepitia sheria kidogo napendelea kulifahamu na kulisupport jambo ambalo kisheria we can build a case to defend it. Sasa kama jambo naliona kabisa tunaelekea kushindwa tukawa tunalazimisha tu kwakuwa wengi wanaliunga mkono I stand away from the crowd!!!
 
Wakoloni wote wa Kiarabu na kizungu walitutawala kwa kutumia Katiba na sheria.
Wlitunyanyasa kwa kutumia katiba na sheria.
Walituibia na kutupokonya kila kitu kwa kutumia katiba nasheria.
Walitufanya watwana na kutuweka pamoja na kundi la hayawani kwa kutumia katiba na sheria.
Walituziba macho na masikio na kutufunga midomo midomo yetu kwa kutumia katiba na sheria.
Walitufanya tuamini unyonge,umasikini, mardhi na hali yetu duni ni majaliwa yetu kwa kutumia katiba na sheria.
Walitufanya tuamini kwamba kila wasemalo ni kweli kwa kutumia katiba na sheria.
Walitutetemesha kwa katiba na sheria.

Kwa kutamani matunda waliyofaidi wakoloni kwa kutunyonya bila Huruma Viongozi wa CCM wanatumia katiba kuwanyonya kwanza wanachama wanyonge na ndondocha wa CCM wanao unga mkono uwepo wa CCM huku CCM ikiendelea kuwatia katika umasikini.
Pili wanawanyonya Watanzania wote kwa kuwalazimisha kuamini kwamba hawana namna nyingine kuweka mambo yao sawa bali kutii bila maswali hoja za CCM, na zaidi kuamini kwamba kitokacho midomoni mwao ni wakfu.

Leo hii CCM nao wanatuingiza tena katika makucha ya kugandamizwa kiuchumi kisiasa na kiutamaduni kwa kutumia katiba na sheria ya nchi.
Wanaruhusu wageni kurudi tena nchini na kutuibia tena kwa kutumia hial zile zile za Kikarlpeters ( Waziri anapewa shanga za kiunoni na kuvaa yeye na mke wake kisha nasign mkataba wa kuliingizia taifa mabilioni) kwa kutumia katiba,sheria, PORISI na RISASI.

Tuliwafukuza wakoloni weupe kwa kupiga mayowe tukabwetekaa, tukatoa mwanya kwa wakoloni weusi ambao wananyonya hadi kukata ziwa na chuchu zake.
Tunapambana na wakoloni Weuse wa Mashati ya kijani wanaolindwa na Kikosi cha Uslama wa Taifa na RiMwema na maPolisi wote na Viongozi wa ngazi za juu wa JWTZ wasiojali Captain kala nini.
Wako tayari kuweka watu jela na hata kuua ili kukata kiu yao ya Kinyonyaji.

Ukoloni ni ukoloni tu ufanywe na mtu mweupe au mweusi.
CCM ni Genge la Wakoloni weusi.


Sisi waTanzania ni kwa uwing na ujumla wetu ni WAFAAKIRI.

Ukweli ni huu kama tulivyo vaa khanga na kofia za kijani na kufakamia masinia ya wali na kuwapigia kura ili wapate rungu la kutubonda, ni hivyohivyo itabidi tusimame kidete kuwaondoa hata kama gharama yake ni uhai wetu.
 
Ha ha Tanzania is a special case. Raisi anaweza aka jitokeza na kusema tofauti na waziri mkuu. Kisha tutaambiwa haya yalikua maoni binafsi ya Mizengo Pinda na si tamko rasmi kutoka kwa waziri mkuu. Mh au wana tingisha kiberiti tena???
 
Pinda is not the pinda anymore ameishapinda tayari, hakuna cha mtoto wa mkulima anymore wameishamvisha joho la ufisadi, mafisadi wameishateka akili yake hawezi fikiria wala kusema chochote against them he has already lost credibility.

Halafu hii serikali inanishangaza sana kila mtu anaongea la kwake halafu rais yuko kimya ndio maana siku moja jamaa mmoja aliuuliza hivi rais wa nchi hii ni nani?
 
And as far as i know haya siyo maamuzi ya serikali kama pinda anavyosema bali ni maamuzi ya cc ya ccm halafu anakuja kusema serikali wakati ishu hata bungeni haijafika what a crap huyu jamaa akili zake wameishazichezea
 
Ha ha Tanzania is a special case. Raisi anaweza aka jitokeza na kusema tofauti na waziri mkuu. Kisha tutaambiwa haya yalikua maoni binafsi ya Mizengo Pinda na si tamko rasmi kutoka kwa waziri mkuu. Mh au wana tingisha kiberiti tena???

He he he thats what i was talking about Pinda atakuja na la kwake, Mwanasheria mkuu naye atasema la kwake yaani ni mvurugani at the end of the day all i can see here is a kind of game being played kuwapumbaza watu, chukulia mfano ishu ya katiba kila mtu alikuwa anaongea la kwake kuanzia Tambwe Hizza, Makamba, Mwanasheria Mkuu, Celina Kombani halafu at the end of the day Rais naye anakuja na statement tofauti kabisa kama sio kucheza na akili za watu maana yake ni nini???
 
Back
Top Bottom