Freeman Mbowe Mwenyekiti wa CDM amempongeza raisi JK kwa ujenzi wa miundo Mbinu hasa ya barabara hii inaonyesha ukomavu wa kisiasa kwani angeweza kumtolea vijembe na kejeli lakini nadhani hii pongezi haiondoi ukweli kuwa kuna pengo kubwa sana kati ya kilichofanyika na kilichotakiwa kufanyika hasa ukizingatia rasilimali tulizonazo
Nawasilisha
Uzalendo mbele itikadi nyuma=maendeleo kwa Watanzania wote.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Hai Mhe Novatus Makunga katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo
Akihutubia
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaidiwa kuzindua jiwe la msingi na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na kupewa shukurani na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Miundombinu Mhe John Pombe Magufuli Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe L:eonidas Gama na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe wakikata utepe mojawapo ya magreda katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Miundombinu Mhe John Pombe Magufuli Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Leonidas Gama na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Kilimanjaro baada ya uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo
Imekuwa ni kawaida kwa WanaCDM wakiongozwa na Katibu wao Mkuu kutoa matamko yasiyo na tija hasa katika swala la maendeleo ya Taifa letu, matamko ambayo mengi yamejaa kejeli na uhuni unaopaswa kupuuziwa kuliko upuuzi wenyewe.
Katika kudhihirisha kuwa hawajui wayanenayo leo Mwenyekiti wa CDM Taifa amesikika akitoa tamko ambalo kimsingi litakuwa kama funzo kwa Katibu wake Mkuu na baadhi ya WanaCDM.
Mbowe kasema yeye amezunguka sana hapa Nchini kwa anga na barabara na amejionea maendeleo ambayo Serikali ya CCM imefikia na kwa hilo anampongeza Rais pamoja na Serikali yake. Hapa Mbowe hakutaka kumumunya maneno hata kidogo.
Hili ni fundisho kwa Slaa na wenzie ambao wamezoea kutamka kuwa miaka 50 CCM haijafanya kitu. Lakini nimekuja kugundua kuwa Samaki akianza kuzeeka huanzia kwenye Ubongo.
Mh. Freeman hongera sana kwa hayo uliyoyaona na kuyasema na tunaamini kuwa utaendelea kuwaeleza na hao wengine na wataelewa tu taratibu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.