Pesa Madafu: Hayo mengine sisi hatujui, muhimu uwe na pesa tu!

Doji MD

JF-Expert Member
Dec 27, 2019
1,223
2,414
Habari wakuu, natumaini mapambano ya maisha yanaendelea…

Mimi sio mwandishi mzuri ila nitajihidi nieleweke, bila kupoteza wakati, leo ningependa kushare jambo kuhusu pesa za moto’ (real story)

Jamaa tumuite Hassan’ alichukuliwa na boss mmoja kutoka kijiji nakuletwa mjini kuuza Duka, alifanya kazi kwabidii na miaka ikaenda huku akisave pesa mdogo mdogo…

To cut

Akafanikiwa fungua duka lake kwa mtaji mdogo aliopata na kama unavyojua biashara za uswahilini ikamlazimu atafute waganga kwa nia yake wamsaidie apate wateja wengi na ni jambo ambalo akafanikiwa kwa asilimia kubwa na kuweza kuongeza bidhaa za kutosha dukani lakini hilo halikumfanya atosheke.

Kasafiri mbali zaidi huko mkoani Mbeya kuelekea Songwe kufuata Wataalamu wa jadi na kupewa dawa za biashara na katika Stori za hapa na pale yule Mganga hakuwa nyuma kumdokeza pia kuwa hata pesa za moto anaiweza io kazi na kasaidia wengi kama anahitaji.

Basi bwana Hassan kwasababu hakuwa kwa lengo wakati huo ikabidi akajifakari,

Akaendelea na biashara zake.. asee biashara iliwaka sana wateja kama wote hahaa hakuwa mtu wa kujitegea isitoshe ni mtu katoka bush hukoo hivyo bata ilikuwa kama ugeni na watoto wa mjini..

Siku zikapita basi katika stori moja mbili tatu na rafiki yake kuhusu mambo ya pesa jamaa akaomba connection kwa Hassan kuwa ampeleke kwa huyo mtaalam kwakuwa kauchoka umasikini. Wakapanga siku na kukubaliana kuwa gharama zote atalipa mwenyewe yeye kama msindikizaji tu( jamaa tumuite John).

Siku ikafika, wakaanza safari toka mkoa X kuelekea Mbeya kama ilivyo kawaida kushuka gari kupanda gari na mwisho boda boda mpaka kufika kwa babu(Mganga).

Walipokelewa vizuri baada ya masaa kadhaa wakaingia kwenye Chumba maalumu(kilinge) huku jamaa akieleza Zaidi shida yake.

Ilipofika usiku wakiwa na stori za hapa na pale kibarazani babu akaagiza bia kama nne(bingwa moja) wakiwa katika mzunguko wa watu wanne yani Babu, Hassan, John na yule kijana wa mzee.. wakaanza kukata bia mzee akamimina bingwa kwa John nakumwambia lazima anywe huku Hassan akigoma kuwa safari inamtosha kwakuwa si mpenzi wa vilezi basi ilikua haina budi kwa John kuendelea kupiga bia huku akipigwa na mshangao wa kuwa mbona hakuna pale kwalengo la kunywa lakin ndio hivyo hakuwa na jinsi..

Stori na maelezo mengi yaliendelea toka kwa babu na baada ya kumaliza kunywa muda ulikuwa umeenda hivyo John akaonyeshwa Chumba cha kulala ambacho aliambiwa ni lazima alale na kijana wa yule mzee ambae hakuonekana kutoa hata neno wakati woote, huku Hassan nae akioneshwa chumba kingine alale pekeake….

ITAENDELEA………
 
Tunaemdelea……..

Stori na maelezo mengi yaliendelea toka kwa babu na baada yakumaliza kunywa mda ulikua umeenda hivyo John akaonyeshwa Chumba chakulala ambacho aliambiwa ni lazima alale nakijana wayule mzee ambae hakuonekana kutoa hata neno wakati woote, huku Hassan nae akioneshwa chumba kingine alale pekeake…
Usiku wote huo John akulala zilisikika kelele nyingi sana mpaka ilipofika asubuh sura ya John haikuonekana yenye furaha lakin alijitahid nisielewi kitu..
Kazi yamganga iliendelea akatengenezewa dawa zake ambayo kwamaelezo ya haraka ile dawa unaitia kwenye begi pamoja nashilling elfu tano au kumi unakaa wiki moja huku ukiendelea tumia dawa zingine ,,,hivyo baada ya wiki moja kuisha unachukua ile pesa toka kwenye begi unaenda tumia iishe huku ukiicha pesa nyingine vivyo hivyo kama ni elfu kumi au tano na mwishowe baada ya muda utakutana mzigo wamaana sana wapesa ndani ya begi…..to cut

Basi baada ya yote walifanikiwa rudi salama nakazi ziliendelea ilipita kama miezi mitatu jamaa life lake likaanza kuchange huku hakikata mawasiliano na jamaa yake aliyempeleka(hassan) na miezi kadhaa baada yakupita jamaa akaama kabisa mkoa huku jamaa akiskia kwa wat utu maana hata simu kupokea ilikua shida na akipokea anasema nipo busy ndugu..
Zilisikika taarifa tu kua jamaa kafiwa na mzazi wake nabaada yamazishi karudi mkoa aliohamia bila hata kumpa ripoti yeyote rafiki yake…baada yamwaka namiezi hivi Hassan akapigiwa najamaa akiambia ndugu wewe komaa tu utakufa masikini mwenzako tayari nabiashara yangu nakula nachotaka wakati wowote lakin dah yule kijana wa mzee sio poa aisee we acha tu..
Bwana Hassan alijaribu muuliza lakini jamaa hakutaka aeleze hata kidogo nakumuacha Hassan namaswali mengi.
Hassan aliendelea nabiashara yake ya duka nakufanikiwa kukodai nyumba nzima akiishi namchumba nakula bata kama kawaida maana biashara haikua chini kivile lakini suala la rafiki yake kutoa nakula maisha kufanya biashara kubwa kubwa ikamfanya nae aingiwe natamaa mdogo mdogo..
Jambo la kwanza alilowaza nikutaifisha biashara yake hili aende kwenye kilimo vile vile pesa nyingine atumie kama gharama zausafiri namambo yote yatakayofanyika kwa mtaalam pesa zamoto…
Akawaza kwanza aende kwa mganga wake wakwanza mpakani mwa Moro huko vijijini alipofika akaambiwa aise mimi dawa zangu hazitaki mambo ya damu hivyo usiwe na haraka kama wataka pesa fanya mpango utulie maana usijechanganya maagano hivyo fanya kwanza hivi mbona kamapesa utapata..
Babu akamwambia tu wewe rudi kuna vitu mmi nitaandaa nitafika kukufanyia huko huko nabiashara yako itakua sawa lakini tu nakuomba mjuukuu wangu usifanye au usiweze mambo ya kafara yamtu,,…
Akili ya Hassan ilikua mbali nakuwaza pesa nyingi namaisha ambayo aliyeyoyatamani huku rafiki yake akipeta nakumuongezea ushawishi basi siku zilipita Yule akaja mjini kufanya kazi walioaidiana..
Ilikua usiku wakiwa wawili ndani ya duka lilichimbwa shimo la wastani nakufukiwa kichwa chambuzi huki mganga akinena maneno yake nakumpa dawa ambayo iliyochanganywa nausiri wa bibi kizee kwamaelezo yamganga…kazi ilikua kubwa usiku huo wakiwa wamejifungia ndani ya flem..
Zoezi lilienda vizuri mwishowe bwana Hassan aliona mabariko mazuri yawateja na biqashara ikazidi pamba moto hivyo ikamlazimu pia atomize ahadi yake pia yakwenda shamba lakini mambo si mambo biashara yake ikaanza sua sua baada tu hivyo kukamfanya awasiliane nayule mzee wa Mpakani na Moro kumueleza lakin akaishia kumwambia tu awe mvumilivu kila kitu kitakaa sawa lakini upande wa Hassan harak haraka aliwaza tu ataifishe biashara hili atomize pia lengo lake lakwenda kule alikompeleka rafikiye (John) hili aweze fanikiwa kwa haraka nakutiumiza ndoto zake…
Baada ya siku kupita zogo namkewe likaanza kwasababu zisizoeleweka ikafikia hatua mpaka kutaka kugawana baadhi ya vitu nahilo alikuchelewa kweli wakafanikiwa kugawana huku Hassan akibaki naduka lake huku usafiri na baadhi vitu akichukua mkewe..
Na hilo ndio jambo ambalo lilimpa stress zaid bwana Hassan nakuzidi kuwaza kutaifisha Biasahara yake hili akimbie haraka ka mtaalam wa huko Mbeya kuelekea Songwe..
Kama ilivyoada akafanikiwa kupata mteja na bila kuchelewa akaingia katika usafiri mpaka kwa babu wa Mbeya...baada yakufika tu nakueleza shida yake, yule mzee kama kawaida yake akacheki kwenye lamli kwa haraka akakuta kuna agano ambalo alilifanya kwa Mtaalam mwngine nahakulitizmiza kwa asilimia kubwa lakini akamsihi tu hilo si tatizo hivyo atamfanyia jambo hili atomize lengo lake….
Kama ilivyoada ilipofika usiku akaagiza tena bia kama mwanzo nakumwambia hassan akalale nayule Kijana wa mzee, huo usiku Hassan alitumia nguvu kubwa sana kupata usingizi mpka kulivo kucha, hivyo akapewa nadawa zingine nakurudi mkoa..
Kama ilivyo ada ilitakiwa aandae begi la wastani jeusi huku akiwea kiasi cha elfu kumi maana ilimzam pia hiyo pesa haitumia kwenye matumizi ya pesa iiishe nakula bata…

Nitaendeleaa……
 
Habari wakuu, natumaini mapambano ya maisha yanaendelea…

Mimi sio mwandishi mzuri ila nitajihidi nieleweke, bila kupoteza wakati, leo ningependa kushare jambo kuhusu pesa za moto’ (real story)

Jamaa tumuite Hassan’ alichukuliwa na boss mmoja kutoka kijiji nakuletwa mjini kuuza Duka, alifanya kazi kwabidii na miaka ikaenda huku akisave pesa mdogo mdogo…

To cut

Akafanikiwa fungua duka lake kwa mtaji mdogo aliopata na kama unavyojua biashara za uswahilini ikamlazimu atafute waganga kwa nia yake wamsaidie apate wateja wengi na ni jambo ambalo akafanikiwa kwa asilimia kubwa na kuweza kuongeza bidhaa za kutosha dukani lakini hilo halikumfanya atosheke.

Kasafiri mbali zaidi huko mkoani Mbeya kuelekea Songwe kufuata Wataalamu wa jadi na kupewa dawa za biashara na katika Stori za hapa na pale yule Mganga hakuwa nyuma kumdokeza pia kuwa hata pesa za moto anaiweza io kazi na kasaidia wengi kama anahitaji.

Basi bwana Hassan kwasababu hakuwa kwa lengo wakati huo ikabidi akajifakari,

Akaendelea na biashara zake.. asee biashara iliwaka sana wateja kama wote hahaa hakuwa mtu wa kujitegea isitoshe ni mtu katoka bush hukoo hivyo bata ilikuwa kama ugeni na watoto wa mjini..

Siku zikapita basi katika stori moja mbili tatu na rafiki yake kuhusu mambo ya pesa jamaa akaomba connection kwa Hassan kuwa ampeleke kwa huyo mtaalam kwakuwa kauchoka umasikini. Wakapanga siku na kukubaliana kuwa gharama zote atalipa mwenyewe yeye kama msindikizaji tu( jamaa tumuite John).

Siku ikafika, wakaanza safari toka mkoa X kuelekea Mbeya kama ilivyo kawaida kushuka gari kupanda gari na mwisho boda boda mpaka kufika kwa babu(Mganga).

Walipokelewa vizuri baada ya masaa kadhaa wakaingia kwenye Chumba maalumu(kilinge) huku jamaa akieleza Zaidi shida yake.

Ilipofika usiku wakiwa na stori za hapa na pale kibarazani babu akaagiza bia kama nne(bingwa moja) wakiwa katika mzunguko wa watu wanne yani Babu, Hassan, John na yule kijana wa mzee.. wakaanza kukata bia mzee akamimina bingwa kwa John nakumwambia lazima anywe huku Hassan akigoma kuwa safari inamtosha kwakuwa si mpenzi wa vilezi basi ilikua haina budi kwa John kuendelea kupiga bia huku akipigwa na mshangao wa kuwa mbona hakuna pale kwalengo la kunywa lakin ndio hivyo hakuwa na jinsi..

Stori na maelezo mengi yaliendelea toka kwa babu na baada ya kumaliza kunywa muda ulikuwa umeenda hivyo John akaonyeshwa Chumba cha kulala ambacho aliambiwa ni lazima alale na kijana wa yule mzee ambae hakuonekana kutoa hata neno wakati woote, huku Hassan nae akioneshwa chumba kingine alale pekeake….

ITAENDELEA………
Kweli siyo mwandishi mzuri
 
Back
Top Bottom