Opinion: Shukuru Kawambwa ni waziri mbovu kuliko wote Tanzania

Hawa Ghasia,mmoja kati ya VILAZA wa Mzumbe(IDM) miaka ile.Ndio mazao ya waleee maprof. na maDr.feki.Matunda ya akina KAMALA, hayo.
Hawa ghasia Naye hafai amekaa sana kwenye hiyo wizara na anaboronga tuu Kwanza sijui kasoma nini? Anajifanya Ana hasira sana sio mstaarabu kabisa
 
Makongolo mahanga,naibu waziri pamoja na waziri wake,madudu wakuu
 
mkulo ndo hovyo kabisa

Naaaam...umenena kichefuchefu wa kwanza ni Mustafa Mkulo. lakini tujue vlvl ya kuwa baba ya nkulo ni jkey. sipati picha presida ambaye anataka kuacha legacy ya '' maisha bora" kwa kila mtanzania anateuwa dude kama yule bwana. definetely he had no intention for achievement abinitio. mfano mwingine ni ni wa kumuchagua mwigizaji wa kjiwango cha pwagu na pwaguzi kuongoza chama chake mzee makamba!


jk utakumbukwa kuiumiza nchi yetu. it is already the record mzee...

rip ccm
 
Shukuru Kawambwa sijui analalia bahati gani? Akiwa miundo mbinu aliboronga vibaya na hadi sasa Magufuli anahangaika na madeni. Tanraods ilikuwa tatizo baada ya kushindwa kumuwajibisha mkurugenzi, pia ni chini ya Shukuru Kawambwa ATCL waliingia kwenye huu upatu wa kukodisha ndege mbovu! Sasa yuko elimu ambako mambo viwango vya elimu vinazidi kuporomoka. Sijui alikuwa anafanya nini huyu bwana kabla ya kuingia kwenye siasa lakini kwa hakika hana la maana alilifanya. Ohhhh alikuwa mifugo na uvuvi - zero!

Anapeleka wanaibada wanzake sekondari wakiwa hawajui kusoma na kuandika-Bure kabisa, udini unamsumbua!
 
Kwa mtizamo wangu wafuatao ni feki:
1. Mustafa Mkulo- analalamika kuwa makampuni ya madini yanatuibia wakati yeye ndiye anatakiwa kuzuia na kutoa matamko
2. Sofia Simba- hajui majukumu ya wizara yake, kuna siku kulikuwa na mjadala BBC alizidiwa na wachangiaji wa vijijini
3. William Ngeleja- chini ya uongozi wake ameleta sheria ya tenda za vitalu uliogubikwa na giza na hujama kwa watafiti wasio na God fathers (yeye na Jeykey wanahujumu sekta ya madini kwa kufanya biashara wakiwa wasimamizi wa sekta huska)
4. Ezekiel Maige-huyu anabariki utoroshwaji wa nyara za taifa na pia anaruhusu wageni kuvuna madini kwenye hifadhi zetu bila kufuata taratibu.
5. Shukuru Kawambwa - incompetent na hasitahiri kuwa karibu na baraza la mawaziri (ni miongoni mwa scandal za kikwete katika teuzi za ofisi za umma-nepotism)
6. Jumanne Magembe- profesa wa mitishamba, how he even became minister is beyond me!
7. Makongoro Mahanga - anatuangusha watu wa kanda ya ziwa kwa umbumbu (total disgrace kwa watu wanaokula samaki ambao walistahiri kuwa werevu)
8. List ni ndefu maana baraza limejaa magogo
 
Wakuu miongoni mwa mawaziri wasistahili uteuzi wao ni Shukurukawambwa,tangu wizara ya miundombinu sasa wizara ya elimu ndo inaporomoka kwa kasi. My take mtazamo wangu wakuu nawasilisha

Ni kweli hyu waziri ni kilaza wa kutupwa, huo u-doctor sijui aliupata kwa kukariri na kuwepo chuoni kwa muda mrefuu! Mwenzake ni kilaza Dr David Matayo! Huyu hata simple presantation hawezi ku-flow hadi asome, kzini ndio balaa, hana maamuzi na akiamua jambo utapata kichefux2.

My take: Nchi hii imeharibiwa na hao wanaoitwa wasomi kama ma-doctor, ma-professor! Hebu ona madudu ya hawa:
1. Dr Daudi Balali kule BOT; Mtei na Rutihinda wali-exell
2. Dr Idrisa rashid kule BOT na hatimaye TANESCO; Rubbish
3. Prof. Mahalu Ubalozini Italy; Aibu na wizi mtupu
4. Prof. Kapuya kule wizara ya ulinzi; anakwenda na helcopter nyumbani kwake Kaliua! Lol
5. Prof. Maghembe pale wizara ya elimu; Aibu tupu, angerudisha kitabu kimoja kwa kila mwanafunzi kwa kila darasa.
Kule Kilimo, yeye badala ku-make practice analeta theories na Kilimo kwanza hakua, njaa inazidi.
6. Prof. Mosha kuwe DUSE; Sitaki wala kusimuliwa kwani alitolewa BARU na Lowasa enzi hizo!

Nimekasirika, sitaki hata kuendelea, endelezeni wanajamiiforums
 
Shukuru Kawambwa sijui analalia bahati gani? Akiwa miundo mbinu aliboronga vibaya na hadi sasa Magufuli anahangaika na madeni. Tanraods ilikuwa tatizo baada ya kushindwa kumuwajibisha mkurugenzi, pia ni chini ya Shukuru Kawambwa ATCL waliingia kwenye huu upatu wa kukodisha ndege mbovu! Sasa yuko elimu ambako mambo viwango vya elimu vinazidi kuporomoka. Sijui alikuwa anafanya nini huyu bwana kabla ya kuingia kwenye siasa lakini kwa hakika hana la maana alilifanya. Ohhhh alikuwa mifugo na uvuvi - zero!


tatiza la watanzania wengi ni wepesi wa kusahau eti mtu anakuja humu ansema shukura ana bahati, HIVI WEWE HUJUI KUWA ANATEULIWA KWA SIFA MBILI MOJA WAKWETU, NDUGU ILI KIPATO KIONGEZEKE?

HUYU NA HAWA GHASIA WAKIRUDISHWA MWISHO WAO 2015
 
shukuru kawambwa
wiliam ngeleja
adam malima
mustapha mkulo
sophia simba
shamsi vuai nahodha


hawa ni ZERO ongezeni na wengine
 
Hata lukuvi aliteuliwa kama zawadi,kweli wanageuza nchi shamba la bibi,Mungu atulinde uchaguzi ujao(2015)nchi iwe chini ya wazalendo wa kweli,wote wanaojilimbikizia(mawaziri) mali watafilisiwa na kufungwa iwe fundisho kwa wengine
 
mtoa mada angesema ktk mawaziri nani anafaa kiasi maana baraza lote bovu! Wenye unafuu hawazi 5
1)Magufuli
2)naibu wa elimu anamfunika waziri wake
3)Mr six
4)....
5)....
 
Mbona kimya wakuu au mnamkubali

Tuko kimya kwa sababu tunafahamu kuwa hawezi kuachwa kutokana na mahusiano yao ya kidugu. Hata ungekuwa wewe ungeweza kumtupa mtoto wa dada yako hata akiwa bogus?
 
Kawambwa navosikia ana uhusiano na Kikwete kwa hiyo tunasema kilichofanyika hapo ni NEPOTISM na sio uwezo basi si ajabu kuona hafanyi vizuri
 
hayo ndio matokeo ya kuteuana kwa kujuana hawa ghasia shemeji,kawambwa tumetoka naye sehemu moja kifupi ambaye hafai ni yule aliyewateua haiwezekani waboronge kote na bado aliyewatteua anazidi kuwapa dhamana katiba mpya idhibiti hii hali kama tukiiacha hata vyama vingine vitafanya uozo huo huo tumeona kwenye uteuzi wa viti maalumu hakuna chama kitakacho mjali mtanzania kama tutakuwa na katiba mbovu
 
kuanzia rais mpaka mawaziri wake wote hawafai katika CCM labda magufuli kidogoo ana msimamo wa kiutendaji sema anazidiwa na uongozi mbovu.
 
Tatizo kubwa la baadhi mawaziri (si wote) wa ni kwamba wanaamini wao pekee ndio wemye uwezo mkubwa kufanya lolote, kufaidi kila kitu kadiri watakavyo na kuwaburuza watanzania watakavyo.
matokeo yake wamekuwa jeuri, kiburi na wanakosa unyenyekevu kwa watanzania.
Wengi ni wanafiki wanosema wasichokiamini.
Kwa mfano mdogo ni kutoka wizara ya elimu. Mfano Waziri Kawambwa angeweza kukataa mpango wa NECTA kuanzisha utaratibu wa maswali ya kuchagua katika somo la hisabati darasa la saba. sijui kama anajua impact yake kwa maendeleo ya elimu.hili linataka uchambuzi zaidi lakini kwa kweli walimu hawridhiki na hili.
Kuna mparaganyiko wa upangaji wa walimu katika mashule. mfano katika baadhi ya shule za msingi kuna walimu wenye masters na bachelor's degrees wala hawatambuliwi wala kutumiwa ipasavo huku shule za sekondari hazina walimu wa kutosha.
Mpangilio wa kupeana vyeo una dalili za kujuana. Kama mtu hana bosi anayemjua wizarani atabaki palepale alipo.
fikra kubwa ni kuwa mtu anapewa madaraka kwa sababu atanufaika yeye zaidi na sio wizara na elimu kwa ujumlandio maana kuna upendeleo.
Walimu wakuu na wakuu wa shule kila siku ni kusumbuliwa kuandika taarifa zile zile na vikao lukuki ambavyo havina hata tija. Pamoja na maendeleo ya teknohama utuzaji wa kumbukumu ni wa makaratasi ndiyo maana kila siku walimu wakuu huishia kupeleka makaratasi wilayani badala ya kukaa shuleni kusimamia taaluma
kwa ujumla kuna haja ya kufanya mabadiliko ndani ya wizara. Sijui kama Kawambwa na waliomtangulia wamelijua hilo. yako mapungufu mengi muda nafasi havitoshi kuyaeleza kwa sasa.
 
Back
Top Bottom