Mjanga
JF-Expert Member
- Feb 13, 2011
- 1,238
- 324
Wadau kuna tatizo gani ndani ya hiyo ofisi, hasa sehemu ambako transcripts zinatolewa! Kumekwepo na urasimu usiokuwa na maana sana kwa hawa wahusika: Wako wadada watatu (3), na hawako makini sana kwani wanapochapisha transcripts kuna makosa ya kizembe sana-inaonekana hawafanyi proof reading wao ni kufyatua makaratasi tu, mbaya zaidi: Pale ambapo makosa yao wenyewe wanayageuza kuwa adhabu kwako mteja- maake utaambiwa njoo baada ya wiki tatu, pia wanasahau kuwa kuna watu wanatoka mikoani kwenda kufatilia transcripts-lakini bado utaingizwa kwenye urasimu wa ajabu. Inasikitisha sana mtu unapofatilia transcrip kwa zaidi ya miezi sita bila sababu za msingi!
Wahusika watambue kuwa ofisi hii hapo udsm inachafua sura ya chuo hasa wakati huu tunapohadhimisha miaka 50 toka chuo kianze! Tunaomba wahusika wajirekebishe na kutoa huduma hii kwa wakati!
Kwani usumbufu huu unatukosesha amani ktk maeneo yetu ya kazi-pale mwajiri anapotaka uthibitisho kuwa umegraduate na aone matokeo yako! Mnaboa sana!
Wahusika watambue kuwa ofisi hii hapo udsm inachafua sura ya chuo hasa wakati huu tunapohadhimisha miaka 50 toka chuo kianze! Tunaomba wahusika wajirekebishe na kutoa huduma hii kwa wakati!
Kwani usumbufu huu unatukosesha amani ktk maeneo yetu ya kazi-pale mwajiri anapotaka uthibitisho kuwa umegraduate na aone matokeo yako! Mnaboa sana!