Nyufa kubwa na mfumo mbaya wa maji taka vya hatarisha udom

Haraka haraka yetu ndo inatuponza.Mchina anakupatia kitu kulingana na pesa unayompa.Kamwe jengo lenye gorofa haliwezi kuwa imara kwa kujengwa na kukamilika ndani ya miezi 3.
 
HAPA naona kuna issue mbili :
  1. Ubora wa Majengo na mfumo ya Maji taka ya UDOM
  2. Uhusiano wa nafasi ya NAPE na chuo
Michango ya hili la kwanza nameipenda- ukweli kama kawaida hatuko makini kuhakikisha ubora wa kazi yunazofanyiwa mnakumbuka hata stadium tulilizwa.

Kuhusu hili la pili mimi sijaelewa justification ya NAPE kwenda kukagua na kutoa maagizo imekaaje?

Je yatosha kusema- ujenzi wa UDOM ulikuwa agizo la Mkiti wa CCM ambayo Nape ni katibu muenezi wake?

Taasisi za hivyo ziko nagapi na kama hii ndiyo job description yake basi tumekwisha
 
acha propaganda hiki sio chuo cha chama nape yupo waziri husika uwe muwazi kuwa ulikuwa unaka kukagua mwenendo wa kisiasa hapa chuoni sio majengo.NI KWELI MAJENGO HAYA YAWEZA KUWA NA UMRI MREFU WALAU 10 YEARS.2kiombee
 
Hivi hiki chuo kimejengwa kwa pesa za ccm. Mbona Nape anafuatilia vitu ambavyo havimhusu. Yeye angeenda kufungua tawi la chama na kutafuta wanachama sio kutuzuga eti anakagua majengo for what then what next, yaani ccm inatapatapa.
 
kwan kuweka picha chumbani ni kufanya siasa chuoni?????? umemuona Nape Tshirt aliyovaa???? nani kati ya aliyebandika picha chumbani na aliyevaa tshirt ya chama ndo mpiga siasa chuoni hapo?????
 
Faculty of social sciences and Humanities ya chuo kikuu cha Dodoma, ina nyufa kubwa sana zinazohatarisha maisha ya wanafunzi wa chuo hicho. Pia mifumo ya majitaka ni mibovu kiasi cha kusababisha harufu mbaya kwenye ma bweni na kuna muda hata maji hayapandi kwenye vyoo na baadhi ya vyoo vimefungwa kiasi cha kuwafanya wanafunzi wahamie facult nyingine kwa ajili ya kupata huduma hiyo muhimu.

Hayo yote yameshuhudiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM ndugu Nape baada ya msafara wake uliokuwa umetoka kwa Mkuu wa Chuo Pro. Kikula kusimamishwa na wanafunzi na kumwambia aende akaone hali halisi na kumuomba aongee na Rais ili serikali itatue hili haraka iwezekanavyo.

Nape alijionea mwenyewe na kuwa ahidi vijana wa UDOM kuwa suala hili atalishughulikia kwani lengo la CCM ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata elimu katika mazingira mazuri na pia alisisitiza mifumo hiyo mibovu ya maji taka ni hatari kwa magonjwa ya milipuko kama kipindupindu.

Vijana wa UDOM wamekuwa na imani sana na huyo kiongozi kijana anayekuja kwa kasi katika kuisimamia serikali kutekeleza wajibu wake.


Hivi Udom kinamilikiwa na wanamagamba!
 
Hivi hiki chuo kimejengwa kwa pesa za ccm. Mbona Nape anafuatilia vitu ambavyo havimhusu. Yeye angeenda kufungua tawi la chama na kutafuta wanachama sio kutuzuga eti anakagua majengo for what then what next, yaani ccm inatapatapa.

Some people are nuts. Hao magamba tangu lini yakawa wataalamu wa majengo. Mtu kama huyu anafikiri kivipi jamani?

Fine , waje basi na data ni jinsi gani huo ujenzi ulivyochakachuliwa hadi majengo yanaanza kuporomoka. Ufisadi mtupu. Magamba walijisifia eti ni chuo bora kumbe ndio haya , yumkini chaitwa chuo cha kata . Ubabaishaji wa hali ya juu.
 
Anagiza kama nani?, anamuagiza nani?. Anayepaswa kuulizwa kwa nini majengo ni sub std ni JK mwenyewe kwani anajua undani wa ujenzi huu+uchakachuaji wake- so nape namuagiza mwenyekiti wake achukue hatua haraka?!. Tutaona mengi mwaka huu.
Who is Nape?
 
Hivi hiki chuo kimejengwa kwa pesa za ccm. Mbona Nape anafuatilia vitu ambavyo havimhusu. Yeye angeenda kufungua tawi la chama na kutafuta wanachama sio kutuzuga eti anakagua majengo for what then what next, yaani ccm inatapatapa.
wana ccm nape anatuangushe he pretends to know everything sasa itabidi uandikiwe kazi za kufunya
 
Kuna madaraja; madarasa; dispensari na mabweni ya shule mbalimbali hapa nchini yamejengwa chini ya viwango! Sijasikia Nape wala CCMlist mwingine (wa ngazi za juu) akisema yakakaguliwe! Ina maana ukaguzi wa nyufa hadi MAJEMNGO YAWE YALIJENGWA KWA AMRI YA MWENYEKITI WA CCM???Common CCM; chuo kimejengwa na hela zetu walipa kodi! Mie wala sina hata kadi ya chama chochote labda ile isiyo rasmi ya wanywa KONYAGI!!!! Tufanye mambo kwa utaratibu na kitaalamu; siyo KISIASA NA KUTAFUTA CHEAP POPULARITY!! MUNGU ISAIDIE TANZANIA kwani sasa inaanza kuonekana inapelekwa kwenye gonjwa baya!
 
Nape angetembelea madarasa na Dispensary ya Social Sciences asingeamini kabisa. Kule kuna kubomoka siyo nyufa peke yake. Kuvuja ndiyo usiseme. Big up Nape!! Huo ni ufisadi uliofanywa na Mlacha pamoja na Weja
 
Hivi hii tabia ya kukata umeme usiku hapa UDOM Tanesco wameikuta wapi? na nani kawatuma? hivi hawajui kama usiku watu wanajisomea kujiandaa na test pamoja na UE? na hawajui katika haya maghorofa ya UDOM kama kuna giza kuna maovu mengi yanatendeka? mbona walipewa mda wa mgawo kuwa ni jumamosi na jumapili mchana wamesahau?
 
Vyombo vya habari jana vimetuonyesha katibu uenezi na itikadi wa chama cha mapinduzi (CCM) ndugu Nape Nnauye akiwa katika ziara ya kikazi pale University of Dodoma (UDOM).

Mambo aliyoyafanya ni pamoja na kukagua majengo na miundombinu ya Chuo lakini pia alitoa maagizo kwa uongozi wa chuo kurekebisha matatizo madogo madogo aliyoyabaini katika miundombinu. Pamoja na hilo alikutana na wanachuo wanachama wa CCM wa mwaka wa tatu wa sayansi ya jamii (nadhani ni graduates to be). Sina uhakika kama ukumbi waliotumia upo chuoni au ni nje ya chuo maana haukutajwa jina katika vyombo vya habari. Ninachojiuliza ni mipaka ya sheria ya siasa katika vyuo vyetu ikoje? au inaviongelea vyama vya upinzani tu?

Lakini kikubwa zaidi ni mamlaka ya katibu wa chama cha siasa kupewa mapokezi na utawala UDOM hali kadhalika kutoa maagizo kwa uongozi wa UDOM kama kwamba hatuna Mawaziri wanaohusika na vyuo vikuu..!! Hii inatoa picha ipi kiutendaji? ina maana ile semina elekezi bado haikuainisha inter-communication katika baraza la mawaziri na nje hadi kwa viongozi wa chama? Nini mahusiano kati ya udom na ccm?

Je, kweli tutegemee wahitimu mahili kutoka katika chuo hiki kinachoonyesha mahusiano na vyama vya siasa? hakina uwezo wa kupata mahusiano na vyuo vingine duniani?

Nadhani viongozi waandamizi wa CCM walioko humu wanisaidie kupata ufafanuzi wa ile ziara ili nitoe wasi wasi wangu wa kiutendaji na umahili wa UDOM.
 
Mkuu Eng inapofika swala la mipaka ya chama kwenye taasisi za elimu CCM inakuwa sio chama cha siasa kwani kuna double standards za kudifine chama cha siasa. Na hii ndio Tanzania zaidi ya ujiavyo.
 
Back
Top Bottom