kibokomchapaji
Senior Member
- Aug 18, 2017
- 165
- 307
Na, _Nodius Rwegoshora, Bukoba_
Pamoja na kubanwa na majukumu ya shamba, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu kwenye mitandao ili kufahamu dunia inakwendaje kwa sasa.
Nimepezuri na kukutana na habari ya ndugu yangu ambaye wakati anagombea Ubunge kipindi kilichopita, atakumbuka mambo tuliyofanya na kusikia.
Kwa hali ninavyoona, mwenzangu ANSBERT NGURUMO wakati anaandika makala yake yenye kichwa cha habari “Bukobayavamiwa: Bashiru aangukia pua kwa Meya ChifuKarumuna” hakuwaza zaidi ya habari alizopewa na wanaompa umbea wa hapa nyumbani.
Kueleza kuwa Serikali na CCM wanaratibu njama za kumlaghai Meya wa Manispaa ya Bukoba mjini Chifu KARUMUNA ili ajiunge na Chama Cha Mapinduzi *si kweli*. Nakumbuka mengi sana ndani ya CHADEMA yanayofanya watu waondoke. Hata mimi, nasubiri tu wakati ufike ili niweze kuondoka.
Taarifa za kuaminika kutoka katika vyanzo vyangu vya ndani ya CHADEMA bado kuna wimbi la viongozi wanaosubiri muda usogee ili waondoke. Huwezi amini, wapo Wabunge na Madiwani ukiacha wanachama wa kawaida.
Vyama vya upinzani Tanzania vinakwama kwa kuwa ndani yao havijaweka misingi imara ya kiuongozi. Malumbano na uchu wa madaraka yanachangia kutoa mwanya wa watu kuona wamepotea.
Ni wangapi wameondoka CHADEMA na wameeleza sababu za wao kuondoka! Hili nalo linahitaji mtu kufanya utafiti? Ni wangapi wamekosoa uongozi wa CHADEMA ngazi ya Taifa na Mikoa! Sasa hivi hawajui kuwa hata Tundu Lissu na Freeman Mbowe wamegombana kwasababu ya madaraka na urais! Hivi mnajua kuwa CHADEMA wanaogopa kumpendekeza Lissu urais kwa sababu ana makesi mahakamani?
Msingi wa wanachama wa CHADEMA kuondoka ni Chama kukosa nidhamu, weledi na mwelekeo wa kitaifa bali maslahi binafsi ya watu wachache.
Hebu tujikumbushe waliotoka walisema nini: _”Napenda niwaambie wanachadema kinachoendelea ndaniya chama chetu (CHADEMA) ni mapambano kati yawaumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhilifu, mapambanokati ya wanaopenda siasa safi dhidi ya wanaotukuza siasaza maji taka”_– Zitto Kabwe, 2013
Wakati huo Zitto alimtekenya Mbowe kwenye madaraka. Akaishia kufukuzwa!
Haikuishia hapo, soma hii
_”Ugomvi wangu na Mbowe sasa hivi, ni kwasababu kunauchaguzi wa Chama, mimi nilisema kwamba huyu mtuameongoza chama miaka 20 ni umri wa mtu mzima, nachama kinaitwa chama cha Demokrasia na maendeleolakini demokrasia mimi sioni, hakuna uchaguzi ila kunakupachika pachika”_– Mwita Waitara, 2018
Akaendelea kueleza, _”Tulikuwa na Mbunge CHACHA WANGWE alikuwaMakamu Mwenyekiti wa CHADEMA, aliposema kwambaanataka agombee nafasi ya Mwenyekiti Chama Taifa, akaambiwa atashughulikiwa na aliambiwa na Mbowe mwenyewe, tunapozungumza Chacha hayupo”_ - Mwita Waitara, 2018
Katika ngazi za juu zaidi tunaona pia watu ambao wangekuwa msaada kwa CHADEMA wanaondoka na kusema mazito kuhusu hali ilivyo sasa ndani ya Chama. Soma hii _”Nilikwenda kujenga upinzani, ila kwa nilichokikuta huko, kazi kubwa ni kupambana na polisi na usalama wa Taifa hawana ajenda nyingine, hakuna upinzani dhahiri ni upinzania maslahi”_ -Frederick Sumaye, 2020
Na hivi karibuni tunasikia tena _”Wananchi wa Ndanda walinipa heshima ya kuwa mbunge wao, leo ninatukanwa na Vibaraka wa Mbowe kuwa mimi ni dogo, nadhani imefika hatua ya wananchi wa Ndanda na Mtwara kwa ujumla kukataa kabisa uhuni na ubaguzi wa Chadema na kutokaa na kadi zao kwenye nyumba zetu”_ - Cecil Mwambe, 2020
Ansbert, hata haya huyasikii! Hivi kweli mtu ananunuliwa kwa hali hii au anaamua kujiondoa kwa manufaa ya walio wengi!!? Soma maneno haya _”Sioni utayari wa CHADEMA kuwaletea wananchi Maendeleo, nikilinganisha na CCM, wala sioni nia hiyo ndani yao ....CHADEMA imekosa uelewano ndani na hata nje ya chama”_ -Anthony Komu, 2020.
Hayo nayo ni kununuliwa!!
Naomba nisema; Vyama vya upinzani vina jukumu la msingi la kuikosoa Serikali kwa staha ili itimize wajibu wake kwa wananchi. Suala la watu kuhama vyama ni hiari na huwezi kuwazuia pale mnapoharibu mambo au nafsi zao zinapofika ukomo wa uvumilivu.
Navishauri vyama hivyo kutumia nafasi hiyo kukosoa na kushauri masuala yenye tija kwa wananchi na kwa Taifa badala ya kujikita kuupotosha umma.
Hapa tusitafute mchawi! Watu wanahama wenyewe na hakuna masuala ya kununuana.
*Wakora waitu!!!!!!!*
Pamoja na kubanwa na majukumu ya shamba, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu kwenye mitandao ili kufahamu dunia inakwendaje kwa sasa.
Nimepezuri na kukutana na habari ya ndugu yangu ambaye wakati anagombea Ubunge kipindi kilichopita, atakumbuka mambo tuliyofanya na kusikia.
Kwa hali ninavyoona, mwenzangu ANSBERT NGURUMO wakati anaandika makala yake yenye kichwa cha habari “Bukobayavamiwa: Bashiru aangukia pua kwa Meya ChifuKarumuna” hakuwaza zaidi ya habari alizopewa na wanaompa umbea wa hapa nyumbani.
Kueleza kuwa Serikali na CCM wanaratibu njama za kumlaghai Meya wa Manispaa ya Bukoba mjini Chifu KARUMUNA ili ajiunge na Chama Cha Mapinduzi *si kweli*. Nakumbuka mengi sana ndani ya CHADEMA yanayofanya watu waondoke. Hata mimi, nasubiri tu wakati ufike ili niweze kuondoka.
Taarifa za kuaminika kutoka katika vyanzo vyangu vya ndani ya CHADEMA bado kuna wimbi la viongozi wanaosubiri muda usogee ili waondoke. Huwezi amini, wapo Wabunge na Madiwani ukiacha wanachama wa kawaida.
Vyama vya upinzani Tanzania vinakwama kwa kuwa ndani yao havijaweka misingi imara ya kiuongozi. Malumbano na uchu wa madaraka yanachangia kutoa mwanya wa watu kuona wamepotea.
Ni wangapi wameondoka CHADEMA na wameeleza sababu za wao kuondoka! Hili nalo linahitaji mtu kufanya utafiti? Ni wangapi wamekosoa uongozi wa CHADEMA ngazi ya Taifa na Mikoa! Sasa hivi hawajui kuwa hata Tundu Lissu na Freeman Mbowe wamegombana kwasababu ya madaraka na urais! Hivi mnajua kuwa CHADEMA wanaogopa kumpendekeza Lissu urais kwa sababu ana makesi mahakamani?
Msingi wa wanachama wa CHADEMA kuondoka ni Chama kukosa nidhamu, weledi na mwelekeo wa kitaifa bali maslahi binafsi ya watu wachache.
Hebu tujikumbushe waliotoka walisema nini: _”Napenda niwaambie wanachadema kinachoendelea ndaniya chama chetu (CHADEMA) ni mapambano kati yawaumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhilifu, mapambanokati ya wanaopenda siasa safi dhidi ya wanaotukuza siasaza maji taka”_– Zitto Kabwe, 2013
Wakati huo Zitto alimtekenya Mbowe kwenye madaraka. Akaishia kufukuzwa!
Haikuishia hapo, soma hii
_”Ugomvi wangu na Mbowe sasa hivi, ni kwasababu kunauchaguzi wa Chama, mimi nilisema kwamba huyu mtuameongoza chama miaka 20 ni umri wa mtu mzima, nachama kinaitwa chama cha Demokrasia na maendeleolakini demokrasia mimi sioni, hakuna uchaguzi ila kunakupachika pachika”_– Mwita Waitara, 2018
Akaendelea kueleza, _”Tulikuwa na Mbunge CHACHA WANGWE alikuwaMakamu Mwenyekiti wa CHADEMA, aliposema kwambaanataka agombee nafasi ya Mwenyekiti Chama Taifa, akaambiwa atashughulikiwa na aliambiwa na Mbowe mwenyewe, tunapozungumza Chacha hayupo”_ - Mwita Waitara, 2018
Katika ngazi za juu zaidi tunaona pia watu ambao wangekuwa msaada kwa CHADEMA wanaondoka na kusema mazito kuhusu hali ilivyo sasa ndani ya Chama. Soma hii _”Nilikwenda kujenga upinzani, ila kwa nilichokikuta huko, kazi kubwa ni kupambana na polisi na usalama wa Taifa hawana ajenda nyingine, hakuna upinzani dhahiri ni upinzania maslahi”_ -Frederick Sumaye, 2020
Na hivi karibuni tunasikia tena _”Wananchi wa Ndanda walinipa heshima ya kuwa mbunge wao, leo ninatukanwa na Vibaraka wa Mbowe kuwa mimi ni dogo, nadhani imefika hatua ya wananchi wa Ndanda na Mtwara kwa ujumla kukataa kabisa uhuni na ubaguzi wa Chadema na kutokaa na kadi zao kwenye nyumba zetu”_ - Cecil Mwambe, 2020
Ansbert, hata haya huyasikii! Hivi kweli mtu ananunuliwa kwa hali hii au anaamua kujiondoa kwa manufaa ya walio wengi!!? Soma maneno haya _”Sioni utayari wa CHADEMA kuwaletea wananchi Maendeleo, nikilinganisha na CCM, wala sioni nia hiyo ndani yao ....CHADEMA imekosa uelewano ndani na hata nje ya chama”_ -Anthony Komu, 2020.
Hayo nayo ni kununuliwa!!
Naomba nisema; Vyama vya upinzani vina jukumu la msingi la kuikosoa Serikali kwa staha ili itimize wajibu wake kwa wananchi. Suala la watu kuhama vyama ni hiari na huwezi kuwazuia pale mnapoharibu mambo au nafsi zao zinapofika ukomo wa uvumilivu.
Navishauri vyama hivyo kutumia nafasi hiyo kukosoa na kushauri masuala yenye tija kwa wananchi na kwa Taifa badala ya kujikita kuupotosha umma.
Hapa tusitafute mchawi! Watu wanahama wenyewe na hakuna masuala ya kununuana.
*Wakora waitu!!!!!!!*