NMB yapata kufuru ya faida

Rutakyamilwa

JF-Expert Member
Feb 27, 2009
1,872
1,235
Wanajamii, soma habari hii chini. Nimeichukua toka TIJA. WATANZANIA TULISHINDWA NINI KUENDESHA HII BANK, MAKABURU WANAWEZAJE[/I][/B]

QUOTED:
"Nakumbuka miaka michache iliyopita hii bank ikiwa mikononi mwa serikali ilikuwa inaendeshwa kwa hasara mpaka ikauzwa kwa makaburu."


NMB yapata faida ya bilioni 54
Benki ya NMB imepata faida ya shilingi bilioni 54 katika mwaka uliopita baada ya makato ya kodi, ambayo ni ongezeko la asilimia 13.56 kulinganisha na mwaka 2009.

NMB, ambayo ina jumla ya wateja milioni 1.4 hapa nchini, ilipata faida kabla ya makato ya kodi inayofikia shilingi bilioni 78 kwa mwaka 2010.

Hilo ni ongezeko kubwa kulinganisha na mwaka 2009 ambapo benki hiyo ilipata faida kabla ya makato ya kodi ya shilingi bilioni 68 na faida baada ya mapato ya kodi ya shilingi bilioni 47.55.

"NMB imepata mafanikio makubwa kwenye shughuli zake za kibenki na imeendelea kufanya vyema kutokana na mazingira mazuri ya uchumi yaliyopo hapa nchini," Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Mark Wiessing.

Wiessing alisema mahesabu ya mwaka 2010 ya NMB yameonesha kuwa benki hiyo imepata mafanikio makubwa kwenye shughuli zake kuu za kibenki, ikiwemo kufungua matawi mapya na kupata ongezeko la mapato yanayotokana na riba na mengineyo.

"Pamoja na kupunguza riba kwenye soko, faida ya benki kabla ya makato ya kodi iliongezeka mpaka kufikia shilingi bilioni 78 kutokana na mikopo, amana za wateja na ukuaji wa shughuli za kibenki kwa ujumla," alisema.

Alisema mapato ya jumla ya NMB yaliongezeka kwa asilimia 23 mwaka jana kutokana na kuongezeka kwa mapato yanayotokana na yasiyotokana na riba.

"Amana za wateja wetu zimekuwa zikionesha ukuaji mwaka hadi mwaka na kuongezeka kwa asilimia 24 mwaka jana hadi kufikia shilingi trilioni 1.8," alisema.

Alisema jumla ya rasilimali za benki hiyo (total assets) ziliongezeka kwa asilimia 26 mwaka jana hadi kufikia shilingi trilioni 2.1.

"Idadi ya wateja wa benki imeongezeka kufikia jumla ya wateja milioni 1.4 nchi nzima na zaidi ya wateja 400,000 wanatumia huduma za benki zinazotembea (mobile banking channel)," alisema.

Alisema kuwa NMB inatarajia kupata mafanikio makubwa zaidi kwenye kazi zake za kibenki kwa mwaka 2011 kutokana na kuendelea kuboresha huduma zake kwa wateja na kuimarika kwa uchumi wa nchi.

"NMB itaendelea na jitihada zake za kuboresha huduma kwa wateja kwenye kazi zake zote huku ikifanya shughuli zake za kibenki kwa umakini mkubwa," alisema.

CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
 
naona wanakamata hela wabongo wengi wanapenda short cut kwa hiyo hawawezi kusimamia kampuni kifaida ebooo wewe wa wapi?
 
Wapunguze riba ya mikopo yao kwanza walau iwe 1pm maana wanatangaza mafaida makubwa wakati wananchi waliokopa wanahenyeka au kushindwa kurudisha mikopo kutokana na riba kubwa wanazotozwa!halafu huyo meneja bila aibu anasema MAZINGIRA MAZURI YA BIASHARA bila aibu
 
Du namba zinatisha, naona wao NBC baada ya kupata CEO wakibongo (Mafuru) mambo si mazuri, faida imeporomoka si mchezo!!

Anyway NMB sasa wanatakiwa wa invest kisawasawa kwenye ICT kwa sababu foleni zao kwenye ATM na banking halls zao si mchezo, zinachefua ni balaa!!!
 
basi ni wakati wa kupunguza interest kwa wakopaji na kupunguza urasimu.
bado wananchi wanapewa mzigo mkubwa sana kabla ya kukopa kwani masharti yanafeva walionacho tu
na wasionacho basi hawana nafasi kabisa.
 
kaka we unaishi wapi mpaka hujui historia ya nmb ilikotokea? mpaka leo hujui nmb ni ya makaburu? serikali ina hisa chache sana pale za kuzugia tu

Hivi kumbe waholanzi wanaitwa makaburu? JF bwana Kila mtu mjuaji.... Nmb inaendeshwa in partnership na Rabo bank ya Netherlands kwa mke wangu mama gaude
 
faida yao inachangiwa pia na mfumo wa serikali wa kulazimisha watumishi wa idara kuweka fedha humo which denies fair competition to other banks na kuwanyima nafasi ya kuchagua watumishi, achilia mbali poor servcies zinazotokana na kubana matumizi wakiangalia bottom line

I am not proud of their profit
 
faida yao inachangiwa pia na mfumo wa serikali wa kulazimisha watumishi wa idara kuweka fedha humo which denies fair competition to other banks na kuwanyima nafasi ya kuchagua watumishi, achilia mbali poor servcies zinazotokana na kubana matumizi wakiangalia bottom line

I am not proud of their profit

Hapo umenena mkuu, na nadhani kunakitu kinaendelea sio bure, kwani wale ambao mishahara yao haipitii NMB unakuta wanachelewa kuingiziwa mishahara yao katika benk nyengine kwa hiyo nikweli NMB inabebwa.
 
Wapunguze riba ya mikopo yao kwanza walau iwe 1pm maana wanatangaza mafaida makubwa wakati wananchi waliokopa wanahenyeka au kushindwa kurudisha mikopo kutokana na riba kubwa wanazotozwa!halafu huyo meneja bila aibu anasema MAZINGIRA MAZURI YA BIASHARA bila aibu

Bongolala , hivi ni riba gani kubwa unayoizungumzia, maanake kwa uelewa wangu mdogo wa kibank, nmb hutoa riba ndogo sana ukilinganisha na crdb na nbc, kwa mfano ukikopa 1mil, kwa six month , utalipa 72,000 kama interest, kwahiyo hii ni interest kubwa kwako?
 
Jamani waturudishie angalau sehemu ya hiyo faida sisi wateja wao.Wapunguze gharama za ATM na pia riba katika mikopo wanayotoa.
 
i wonder.. benki za bongo ni wezi sana. Uta-charge vipi watu kutoa hela kwenye account zao? Banks zinatakiwa ku-charge kama ukitumia ATM za benki nyingine.. na sio kama wanavyofanya sasa. HUu ni wizi!
 
i wonder.. benki za bongo ni wezi sana. Uta-charge vipi watu kutoa hela kwenye account zao? Banks zinatakiwa ku-charge kama ukitumia ATM za benki nyingine.. na sio kama wanavyofanya sasa. HUu ni wizi!

ATM moja inauzwa zaidi ya million 70, watu wawili wanahitajika kwa ajili ya kuhudumia ATM, Mlinzi, karatasi zinazotumia (atm journal roll+ATM receipt), na umeme, jengo(kibanda cha ATM), je BRUTUS haya mabenk yatarudisha vipi hizi gharama walizotumia na wanazotumia kama hawatacharge kila unapotoa fedha kwenye ATM?
 
ATM moja inauzwa zaidi ya million 70, watu wawili wanahitajika kwa ajili ya kuhudumia ATM, Mlinzi, karatasi zinazotumia (atm journal roll+ATM receipt), na umeme, jengo(kibanda cha ATM), je BRUTUS haya mabenk yatarudisha vipi hizi gharama walizotumia na wanazotumia kama hawatacharge kila unapotoa fedha kwenye ATM?
PayGod unataka kuniambia kwa wao kuni-charge mimi napoenda kutoa hela na ATM card yangu that's the only way they can recover their money back?? I don't buy that.
 
ATM moja inauzwa zaidi ya million 70, watu wawili wanahitajika kwa ajili ya kuhudumia ATM, Mlinzi, karatasi zinazotumia (atm journal roll+ATM receipt), na umeme, jengo(kibanda cha ATM), je BRUTUS haya mabenk yatarudisha vipi hizi gharama walizotumia na wanazotumia kama hawatacharge kila unapotoa fedha kwenye ATM?

Hizo ni investiments zao. By the way.. ATM..Automated Teller Machines zinatakiwa zifanye kazi kama jina lake lilivyo.. AUTOMATED! Hazihitaji wahudumu .. maybe walinzi. Banks need to update their programs! Modern ATM inajiendesha yenyewe na iko FAST!
Hizi habari za kuchaji mtu kuchukua hela toka kwenye Account yake.. ni wizi. Ni hapa kwetu tu.. neither America nor Europe utakutana na upuuzi wa aina hii.
Inabidi Banks zi-come up with new investiments ideas.. and not stealing from poor people!
nchi yetu ni masikini.. kuna opportunities nyingi zana za investiments..so waache uvivu wa kufikiri. Inabidi wawe creative!
huu ndio ubepari tuliokuwa tunauogopa. Kunyonya jasho la masikini bila hata aibu!
Kuna faida gani ya masikini kuweka hela benki ikiwa anachajiwa shs 500 au 1000 kutoa hela zake kwenye benki hiyo hiyo? Utamlaumu akiamua kutengeneza Safe Deposit box chumbani kwake akazichimbia?
 
Lakini kama ndiyo hivyo wanashindwaje kuboresha huduma za ATM pamoja na kuongeza mashine nyingi zaidi matawini hususani mikoani? Utakuta benki yote ina ATM moja tu kulikoni?

Wanajamii, soma habari hii chini. Nimeichukua toka TIJA. WATANZANIA TULISHINDWA NINI KUENDESHA HII BANK, MAKABURU WANAWEZAJE[/I][/B]

QUOTED:
"Nakumbuka miaka michache iliyopita hii bank ikiwa mikononi mwa serikali ilikuwa inaendeshwa kwa hasara mpaka ikauzwa kwa makaburu."


NMB yapata faida ya bilioni 54
Benki ya NMB imepata faida ya shilingi bilioni 54 katika mwaka uliopita baada ya makato ya kodi, ambayo ni ongezeko la asilimia 13.56 kulinganisha na mwaka 2009.

NMB, ambayo ina jumla ya wateja milioni 1.4 hapa nchini, ilipata faida kabla ya makato ya kodi inayofikia shilingi bilioni 78 kwa mwaka 2010.

Hilo ni ongezeko kubwa kulinganisha na mwaka 2009 ambapo benki hiyo ilipata faida kabla ya makato ya kodi ya shilingi bilioni 68 na faida baada ya mapato ya kodi ya shilingi bilioni 47.55.

"NMB imepata mafanikio makubwa kwenye shughuli zake za kibenki na imeendelea kufanya vyema kutokana na mazingira mazuri ya uchumi yaliyopo hapa nchini," Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Mark Wiessing.

Wiessing alisema mahesabu ya mwaka 2010 ya NMB yameonesha kuwa benki hiyo imepata mafanikio makubwa kwenye shughuli zake kuu za kibenki, ikiwemo kufungua matawi mapya na kupata ongezeko la mapato yanayotokana na riba na mengineyo.

"Pamoja na kupunguza riba kwenye soko, faida ya benki kabla ya makato ya kodi iliongezeka mpaka kufikia shilingi bilioni 78 kutokana na mikopo, amana za wateja na ukuaji wa shughuli za kibenki kwa ujumla," alisema.

Alisema mapato ya jumla ya NMB yaliongezeka kwa asilimia 23 mwaka jana kutokana na kuongezeka kwa mapato yanayotokana na yasiyotokana na riba.

"Amana za wateja wetu zimekuwa zikionesha ukuaji mwaka hadi mwaka na kuongezeka kwa asilimia 24 mwaka jana hadi kufikia shilingi trilioni 1.8," alisema.

Alisema jumla ya rasilimali za benki hiyo (total assets) ziliongezeka kwa asilimia 26 mwaka jana hadi kufikia shilingi trilioni 2.1.

"Idadi ya wateja wa benki imeongezeka kufikia jumla ya wateja milioni 1.4 nchi nzima na zaidi ya wateja 400,000 wanatumia huduma za benki zinazotembea (mobile banking channel)," alisema.

Alisema kuwa NMB inatarajia kupata mafanikio makubwa zaidi kwenye kazi zake za kibenki kwa mwaka 2011 kutokana na kuendelea kuboresha huduma zake kwa wateja na kuimarika kwa uchumi wa nchi.

"NMB itaendelea na jitihada zake za kuboresha huduma kwa wateja kwenye kazi zake zote huku ikifanya shughuli zake za kibenki kwa umakini mkubwa," alisema.

CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
 
faida yao inachangiwa pia na mfumo wa serikali wa kulazimisha watumishi wa idara kuweka fedha humo which denies fair competition to other banks na kuwanyima nafasi ya kuchagua watumishi, achilia mbali poor servcies zinazotokana na kubana matumizi wakiangalia bottom line

I am not proud of their profit


watu huwa mnaakili kumbe ila linapokuja suala la chama cha nyumbani ndio mnajitoa akili
 
Back
Top Bottom