Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,644
- 19,614
- Thread starter
- #861
Mkuu engine ya gari yangu Nissan winroad ilikua inagonga na kutoa sauti kama machine ya kusaga ya diesel. Nimenunua engine engine , sasa hii ingine mpya imefungwa leo lakini kwenye test haina nguvu kabisaa . ukikanyaga mafuta ndo kabisaa inapiteza nguvu. Pia inapoteza nguvu kwenye mlima na kuspeed up kwenye mteremko . tatizo litakua nini chief
Tukichukulia kuwa kila kitu kimefungwa vizuri, na wala hakuna bomba la hewa amabalo halikufungwa sawasawa, yaani hakuna leakage ya hewa, inawezekana kuwa injini uliyonunua imeshakula sana piston rings. Hebu waambie wafanye compression test; inatakiwa compression iwe kama 40-45 PSI yaani kati ya 28kPa mpaka 31kPa hivi. Kama compress ni chini ya hapo, basi piston rings zimekwisha utatakiwa kuweka nyingine.
Tatizo jingine ambao sielewe linaweza kuwa limejitokezaje ni pale fuel pump haipeleki mafuta ya kutosha; yaani ule mrija wa mafuta haukufungwa vizuri kwa hiyo kuna mafuta yanavuja, ila hilo unaweza kusikia harufu ya mafuta na kuna matoen ya mafuta yanadondoka chini, inawa mengi yanaveporate kabla ya kufika chini.