Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
- Thread starter
- #41
Monoko Mushi,
Umeulizia kuhusu ni vipi tunaweza kuwaambia wananchi kuwa viongozi walioko ndio tatizo.
Hatuna ushahidi wa Viongozi kuwa mafisadi, lakini tuna Ushahidi wa wao kuwa wazembe na matunda ya uzembe wao.
HIvyo ni rahisi kuwafikia Wananchi katika vita vya Ufisadi kwa kwanza kuonyesha Uzembe wa Viongozi hawa na kisha wakishaondolewa na kuaibishwa, ndipo nguvu mpya iingie na kutumia sheria zilizopo au kuongeza sheria nyingine kubainisha Ufisadi wa Viongozi hawa.na kuwafunga.
Kwenda kuwahoji viongozi na wabunge wa CCM kuhusiana na walichofanya na kupima ufanisi waa na uwezo wa kiutendaji kuleta maendeleo na kupiga vita Ujnga, Umasikini na Maradhi ndio njia pekee ya kuwaangusha na kuwaondoa kwenye nafasi za kushikilia na kuiongoza Serikali yetu.
Ushahidi wa kuwaonyesha Watanzania kuwa shida na tabu katika maisha yao na kukwama kwao kupiga hatua kuondokana na umasikini upo tena mwingi sana.
Nenda kijijini Maswa umuulize Msukuma kwa nini bado anakwenda mtoni au bwawani kuteka maji na amekuwa akiahidiwa maji safi kwa miaka 30 iliyopita? Ukimuonyesha Msukuma huyu udhaifu wa kiuongozi na kukosekana mwamko wa kiongozi huyu kumletea Msukuma maendeleo na ukamuonyesha ni jinsi gani wewe utayaleta maendeleo haya, basi ni wazi kwa kiasi fulani Msukuma atakuelewa maana umeoanisha hali yake halisi na kumwonyesha ni jinsi gani Mbunge wake amekuwa akitoa ahadi hewa.
Naomba usichukulie kuwa natangazia umma kuwa hakuna haja ya kupiga vita ufisadi. La hasha, bali ni ukweli dhahiri kuwa Vita vya Ufisadi havitafanikiwa kama hakutakuwa na mabadiliko ya Uongozi na kuanza kutumika kwa Sheria au kuboresha sheria dhaifu. Aidha wananchi wengi hawaelewi chochote kuhusu EPA au Richmond kwa kuwa hata bila hujuma hizo mbili, wao bado wamekuwa wakitaabika.
Sasa ukitaka wafikia Wananchi, basi waonyeshe kile ambacho wanakiona kwa macho yao kila siku.
Ni kweli fedha za EPA zingesaidia kuleta maendeleo fulani, lakini je tatizo ni fedha?
Leo ukiwaambia Wananchi kuwa bajeti na fungu la bajeti iliyopaswa kuleta Hospitali au kujenga barabara, Uongozi wa Wilaya umezitumia visivyo, ni rahisi kwa wao kuelewa kuliko kuanza kuwaelezea kuhusu EPA.
Kwanza tukianza kuwaambia Wananchi kuhusu EPA na kusema pesa zimeibiwa, ni rahisi wao kutupuuzia maana kila siku kauli wanazozisikia kutoka kwa Viongozi ni kuwa Tanzania haina pesa na wameshawishika vizuri kuamini kuwa hakuna fedha.
Ndio maana unakuta wanashangilia pale mtu anapokuja na kudai ati ana Wafadhili au marafiki ulaya ambao watatuletea misaada. Hii ni kutokana na wao kuamini Tanzania haina uwezo na Serikali yao bado inajaribu kujikwamua tangu tamko la Mwalimu Nyerere baada ya vita vya kagera aliposema tujifunge mkanda!
Umeulizia kuhusu ni vipi tunaweza kuwaambia wananchi kuwa viongozi walioko ndio tatizo.
Hatuna ushahidi wa Viongozi kuwa mafisadi, lakini tuna Ushahidi wa wao kuwa wazembe na matunda ya uzembe wao.
HIvyo ni rahisi kuwafikia Wananchi katika vita vya Ufisadi kwa kwanza kuonyesha Uzembe wa Viongozi hawa na kisha wakishaondolewa na kuaibishwa, ndipo nguvu mpya iingie na kutumia sheria zilizopo au kuongeza sheria nyingine kubainisha Ufisadi wa Viongozi hawa.na kuwafunga.
Kwenda kuwahoji viongozi na wabunge wa CCM kuhusiana na walichofanya na kupima ufanisi waa na uwezo wa kiutendaji kuleta maendeleo na kupiga vita Ujnga, Umasikini na Maradhi ndio njia pekee ya kuwaangusha na kuwaondoa kwenye nafasi za kushikilia na kuiongoza Serikali yetu.
Ushahidi wa kuwaonyesha Watanzania kuwa shida na tabu katika maisha yao na kukwama kwao kupiga hatua kuondokana na umasikini upo tena mwingi sana.
Nenda kijijini Maswa umuulize Msukuma kwa nini bado anakwenda mtoni au bwawani kuteka maji na amekuwa akiahidiwa maji safi kwa miaka 30 iliyopita? Ukimuonyesha Msukuma huyu udhaifu wa kiuongozi na kukosekana mwamko wa kiongozi huyu kumletea Msukuma maendeleo na ukamuonyesha ni jinsi gani wewe utayaleta maendeleo haya, basi ni wazi kwa kiasi fulani Msukuma atakuelewa maana umeoanisha hali yake halisi na kumwonyesha ni jinsi gani Mbunge wake amekuwa akitoa ahadi hewa.
Naomba usichukulie kuwa natangazia umma kuwa hakuna haja ya kupiga vita ufisadi. La hasha, bali ni ukweli dhahiri kuwa Vita vya Ufisadi havitafanikiwa kama hakutakuwa na mabadiliko ya Uongozi na kuanza kutumika kwa Sheria au kuboresha sheria dhaifu. Aidha wananchi wengi hawaelewi chochote kuhusu EPA au Richmond kwa kuwa hata bila hujuma hizo mbili, wao bado wamekuwa wakitaabika.
Sasa ukitaka wafikia Wananchi, basi waonyeshe kile ambacho wanakiona kwa macho yao kila siku.
Ni kweli fedha za EPA zingesaidia kuleta maendeleo fulani, lakini je tatizo ni fedha?
Leo ukiwaambia Wananchi kuwa bajeti na fungu la bajeti iliyopaswa kuleta Hospitali au kujenga barabara, Uongozi wa Wilaya umezitumia visivyo, ni rahisi kwa wao kuelewa kuliko kuanza kuwaelezea kuhusu EPA.
Kwanza tukianza kuwaambia Wananchi kuhusu EPA na kusema pesa zimeibiwa, ni rahisi wao kutupuuzia maana kila siku kauli wanazozisikia kutoka kwa Viongozi ni kuwa Tanzania haina pesa na wameshawishika vizuri kuamini kuwa hakuna fedha.
Ndio maana unakuta wanashangilia pale mtu anapokuja na kudai ati ana Wafadhili au marafiki ulaya ambao watatuletea misaada. Hii ni kutokana na wao kuamini Tanzania haina uwezo na Serikali yao bado inajaribu kujikwamua tangu tamko la Mwalimu Nyerere baada ya vita vya kagera aliposema tujifunge mkanda!