Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Nilitarajia Operesheni sangara ingeingia kila Wilaya na Mkoa si kujiuza kuhusu CHADEMA na kupiga vita CCM na kuioanisha na UFISADI, bali ni kuwatikisa Wabunge na Serikali za Wilaya.
Naangalia hii Karamu ya Chai ya Wamarekani wanavyoisakama Serikali na Wawakilishi kwa kuwa mambo kadhaa hayafanyiki kwa manufaa ya Taifa au hao Wanakaramu wa Chai.
Kwangu mimi Operesheni Sangara nilitegemea ingeingia kwenye kila Wilaya ya CCM na kuwauliza wananchi, kwa nini wanaendelea kuiamini CCM na huyo mwakilishi wa CCM?
Ningewauliza tangu wamchague huyo Mbunge wa CCM:
Ndio maana nilitahamaki sana niliposikia kuwa Vyama vingi vya Upinzani havikushiriki kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hasa CHADEMA ambayo ilikuwa na uwakilishi mdogo kwa kuwa wao wameekeza macho na akili zao kwenye Ubunge na Urais kupitia Uchaguzi Mkuu wa 2010!
Kampeni hii ya kuhoji Wabunge na Serikali si kitu cha kunyemelea majira ya Uchaguzi Mkuu pekee, ni suala la kila siku kujikumbusha na kukosoa ili Watanzania waweze kuanza kuwa na upeo wa kufikira nje ya ahadi za Wanasiasa na Serikali ambazo hazitimizwi au zinanufaisha wachache!
Ni maswali ya kwenda kuwabana kila Mbunge na Mkuu wa Wilaya ambaye ni wa CCM, bila kujali yeye ni Mpiganaji au ukaribu wake kwa Rais au bila kujali eti yeye ni kigogo au kizito wa chama.
Bila kuanza kampeni hii kuhoji na kuonyesha udhaifu na mapungufu ya CCM na si kuzungumzia EPA, Richmond na mambo ya magazeti, itakuwa ni vigumu kujiuza kama chama kinachojua kinachofanya na chenye uwezo wa kurekebisha kasoro zilizofanywa na CCM na Serikali yake.
Hivyo kama CHADEMA na Operesheni Sangara inakosa nguvu na ladha ya kuhoji haya, je tutegemee vipi kuwa watauzika na kuwa watakuwa Chama makini wakipewa dhamana ya kuongoza nchi?
Naangalia hii Karamu ya Chai ya Wamarekani wanavyoisakama Serikali na Wawakilishi kwa kuwa mambo kadhaa hayafanyiki kwa manufaa ya Taifa au hao Wanakaramu wa Chai.
Kwangu mimi Operesheni Sangara nilitegemea ingeingia kwenye kila Wilaya ya CCM na kuwauliza wananchi, kwa nini wanaendelea kuiamini CCM na huyo mwakilishi wa CCM?
Ningewauliza tangu wamchague huyo Mbunge wa CCM:
- Maisha yao yameboreshwa kwa kiasi gani katika miaka mitano au kumi ya mbunge huyuhuyu?
- Wanafunzi wangapi wa Darasa la Saba wamefaulu na kwenda Shule za Sekondari na kufaulu Kidato cha nne?
- Zahanati ngapi zimejengwa?
- Vifo vya Watoto na Mama Wajawazito vimepungua kwa kiasi gani?
- Je kila nyumba, kijiji, kata na tarafa zina Maji, Umeme na simu?
- Je kila familia ina nyumba bora?
- Je Wilaya hizi zina shughuli za kiuchumi ambazo zinatoa ajira ukiachia biashara ndogondogo na kilimo?
- Je hali za maisha za Wakulima na shughuli za kilimo zimeongezeka kiasi gani?
- Je wakulima wana pembejeo, nyenzo, maghala na soko la uhakika kwa mazao yao?
- Je kuna waalimu, wauguzi na watendaji wa kutosha wenye uwezo wa kitaaluma na kiufanisi?
- Je Wilaya ina miundo mbinu imara, kama barabara za kutosha kuunganisha vijiji, tarafa na kata? mifereji, madaraja na vivuko imara?
- Je magonjwa kama Malaria, Kichocho, Utapiamlo, Kipindupindu na magonjwa mengine yanatokea mara ngapi na takwimu zinazokusanywa zinafanyiwa kazi gani kuhakikisha kuwa kuna kampeni imara kupiga vita maradhi?
- Je Wazee, Wajane, Wastaafu, Walemavu na Wasiojiweza wanapewa huduma gani na Serikali na maisha yao yana hali gani?
- Je Watoto, Wazee na hata watu Wazima wanapata Lishe bora kila siku na kwa uhakika?
- Je Kilimo ni cha kisasa na chenye kuwapa Wakulima Uwezo wa kuongeza kipato chao kwa kutumia Ukulima stadi na wa Kisasa bila kutafuta shughuli nyingine kujiongezea kipato?
- Je Wilaya hizi zinapiga vita kwa kiasi gani ajira kwa watoto walio chini ya umri wa kuajiriwa?
- Je Wilaya zina programu gani za kuwaendeleza watoto na vipaji iwe ni katika masomo, michezo, sanaa na sayansi?
- Je Wilaya ina mfumo gani wa kuchochea ubunifu na msukumo wa kueneza Sayansi na mifumo ya kisayansi katika shughuli za uzalishaji mali na nyenzo za uzalishaji mali?
- Je Wilaya, Vijiji, Kata, Tarafa na Mitaa zina shughuli za kukuza elimu ya Uraia, Demokrasia na ushirikishi kwa nia ya Kujenga Taifa, bila msuguano wa kiitikadi?
- Je Wilaya, Vijiji, Kata, Tarafa na Mitaa zina Viongozi Bora na Siasa Safi na ziko wapi katika kujenga jamii inayojitegemea na yenye ufanisi?
- Je Watendaji waliohujumu, kuonea, kuzembea au kufuja mali wamechukuliwa hatua gani katika ngazi za kiuongozi kwatika Mitaa, Kata, Tarafa, Vijiji na Wilaya?
- Je Uongozi na Watendaji wa Wilaya wanafuata kanuni na Sheria na ni watiifu kwa Katiba, Sheria na kanuni za kazi na kijamii?
Ndio maana nilitahamaki sana niliposikia kuwa Vyama vingi vya Upinzani havikushiriki kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hasa CHADEMA ambayo ilikuwa na uwakilishi mdogo kwa kuwa wao wameekeza macho na akili zao kwenye Ubunge na Urais kupitia Uchaguzi Mkuu wa 2010!
Kampeni hii ya kuhoji Wabunge na Serikali si kitu cha kunyemelea majira ya Uchaguzi Mkuu pekee, ni suala la kila siku kujikumbusha na kukosoa ili Watanzania waweze kuanza kuwa na upeo wa kufikira nje ya ahadi za Wanasiasa na Serikali ambazo hazitimizwi au zinanufaisha wachache!
Ni maswali ya kwenda kuwabana kila Mbunge na Mkuu wa Wilaya ambaye ni wa CCM, bila kujali yeye ni Mpiganaji au ukaribu wake kwa Rais au bila kujali eti yeye ni kigogo au kizito wa chama.
Bila kuanza kampeni hii kuhoji na kuonyesha udhaifu na mapungufu ya CCM na si kuzungumzia EPA, Richmond na mambo ya magazeti, itakuwa ni vigumu kujiuza kama chama kinachojua kinachofanya na chenye uwezo wa kurekebisha kasoro zilizofanywa na CCM na Serikali yake.
Hivyo kama CHADEMA na Operesheni Sangara inakosa nguvu na ladha ya kuhoji haya, je tutegemee vipi kuwa watauzika na kuwa watakuwa Chama makini wakipewa dhamana ya kuongoza nchi?