Nionavyo Udhaifu wa Operesheni Sangara

mchungaji maswali yako na nadharia yako ni tamu sana. Lakini sisi ni nchi ya amani, umoja, mshikamano na utulivu. Kutafuta majibu ya maswali hayo ni sawa na kupandikiza mbegu za chuki na mgawanyiko katika jamii hasa majibu yatakapotolewa kuwa serikali "iko mbioni", "ina nia", "imeanza mchakato" na "ina makusudio" ya kuyashughulikia masuala hayo yote "pindi wafadhili wakipatikana".

Sasa Chadema ikianza kuyapush maswali hayo inaweza kuwafanya waonekane wanataka kuleta mgawanyo na wao wenyewe siyo watu wanaopenda confrontation za kisiasa. Ni kwa sababu hiyo usitarajie kwenye OS kuona wakibeba mabango ya kuwapinga wabunge mbalimbali au CCM au wanachama wao kuandamana hadi kwa mbunge wa CCM kutaka asigombee tena.

Msingi wa OS (niko tayari kusahihishwa) ni hoja za kisomi za kwanini hali ipo jinsi ilivyo. Hoja hizi zinaendana na uanishaji wa hali halisi kwa kutumia takwimu mbalimbali, vielelezo mbalimbali na mifano mbalimbali ambayo inalenga kushawishi akili. Kwa kiasi kikubwa siyo "siasa proper" kama mifano ya karamu za Chai.

Kwa hiyo uelewa wangu wa OS imefanikiwa sana kuwavutia watu kujiunga na Chadema, sijui kwa kiasi gani watu hao watageuka kupigia kura hasa kama CCM itaamua kwenda full throttle kuwabana wapinzani na kuwavutia wananchi.
Kuna haja ya kuweka mikutano kwenye YOUTUBE ili watu wasikie au sisi kama wadau wa JF tunaweza kufanya hivyo maana leo mambo mengi sana Chadema walisema na CCM walifanya hivyo na pia kuna sera nyingi sana ambazo CCM walikuwa wanaiga toka CHADEMA
 
unauona ukiwa ng'mbo kupitia vyombo vya habari............. hutaki hata kukanyaga nchiyako mwenyewe japo ushiriki siku moja..... u radhi kumaliza karne nyingi bila hata ya kupiga kura............ sasa unalilia haki ya kuchukua uraia wa nchi nyingine ili ufaidi memea ya nchi zaidi ya TZ

Badala ya kujibu maswali au kupangua hoja unamshambulia mtu! ad hominem per maximus

hawa unaokosoa, hujawaunga mkono japo kidogo tu, wao wamethubutu.......... wamekenda hadi kule zinakopatikana mbigili, zimewachoma na zinaendelea kuwachoma.......... wewe baada ya kubeba box na kupata senti kidogo, unatafuta mvinyo na kuwasha PC yako unasoam JF na unaanza kupekua wapi pa kukatisha tamaa wapambanaji!!!!!!!!!............... hakika kama seriakli yetu ingekuwa na robo ti ya watu wa aina hii, hali ingekuwa mbaya zaidi ya sasa.......... tungeteamani ufisadi kwani hali ingekuwa mabaya zaiid ya ufisadi............

Kama unaona anayosema hayana ukweli unayapangua tu, kwani lazima watu watoke mbinguni kuja kutuonesha dhambi duniani!?

Dr W. Slaa na chadema, nawashukuru sana kwa huduma yenu hii kwa uuma....... yatasemwa mengi lakini operation hii inatia uhai katika demokrsia ya TZ kila uchao....... japo nami sijawahi kwaunga mkono kwa kusimama mstari wa mbele katika mapambano yenu, lakini walau natambua umuhimu wa mapambano mnayoendesha.......... nawatakia kila la heri..................

sasa kuwatakia kila la heri ndiyo kuwasaidia? Reverend kachokoza maswali ambayo yanawasaidia Chadema kuchanganua na kuchambua mambo na kujiangalia wenyewe. Vinginevyo tutakuwa kama CCM ambapo wanataka kila mtu aimbe sifa zao "CCM nambari wani eeeh!" tusipoimba tutaambiwa "hatuwaungi mkono CCM" na kuwa "tunawakatisha tamaa".
 
Ni kweli kabisa na pia kama Dr .Slaa anamekuja hapa na kuona jinsi gani ambavyo watu makini wanasema kuhusu CHADEMa na sera zao. Hongera CHADEMA
 
Huwa ninajiuliza iwe vipi tukubaliane kuwa tatizo ni uongozi halafu solutions za tatizo hilo ziwe tofauti na uongozi?Kuna mwenye kujuwa ni kwanini?

Duh.. yaani wewe naweza kukupaka mafuta uwe mrithi wangu.. maana the changes you have gone these few years have been beyond "oustanding" and "impressive".

Hilo swali zuri na la msingi sana. Kama tatizo ni Uongozi kwanini suluhisho lisiwe kwenye uongozi huo huo? Ungekuwa karibu ningekugongea!

keep it up.. napenda watu wanaouliza maswali zaidi ya yale yanayodhaniwa au kutarajiwa.
 
Duh.. yaani wewe naweza kukupaka mafuta uwe mrithi wangu.. maana the changes you have gone these few years have been beyond "oustanding" and "impressive".

Hilo swali zuri na la msingi sana. Kama tatizo ni Uongozi kwanini suluhisho lisiwe kwenye uongozi huo huo? Ungekuwa karibu ningekugongea!

keep it up.. napenda watu wanaouliza maswali zaidi ya yale yanayodhaniwa au kutarajiwa.

Mwanakijiji, rejea kwenye dhana nzima ya "substitute as a lolution" and alternative solution. Ndio maana katika kuondoa mkanganyiko huo Chama cha Dokta Slaa wanakiita ni Chama mbadala.

Ni vigumu kuweka maziwa fresh kwenye dumu lililokuwa na mtindi alafu utegemee maziwa hayo fresh yasiwe mtindi. Unaweza kusema dawa ni kusafisha hilo dumu...lakini kusafisha kunategemea na dhamira ya mwenye dumu. Lakini pia ugumu wa kazi ya kusafisha hilo dumu.
Huwezi kuwa na suluhisho la matatizo ya utawala wa Tanzania eti kwa kisafisha CCM. CCM aisafishiki, dawa ni subsitute....chama mbadala.

Mzitto
 
Mkuu Rev shukrani kwa michango yako mizuri sana ambayo inahamasisha mijadala mizito kuhusu maslahi ya nchi yetu ambayo imetufanya wengi kulipenda jamvi hili. Hongera sana.
 
Nilitarajia Operesheni sangara ingeingia kila Wilaya na Mkoa si kujiuza kuhusu CHADEMA na kupiga vita CCM na kuioanisha na UFISADI, bali ni kuwatikisa Wabunge na Serikali za Wilaya.

Naangalia hii Karamu ya Chai ya Wamarekani wanavyoisakama Serikali na Wawakilishi kwa kuwa mambo kadhaa hayafanyiki kwa manufaa ya Taifa au hao Wanakaramu wa Chai.

Kwangu mimi Operesheni Sangara nilitegemea ingeingia kwenye kila Wilaya ya CCM na kuwauliza wananchi, kwa nini wanaendelea kuiamini CCM na huyo mwakilishi wa CCM?

Ningewauliza tangu wamchague huyo Mbunge wa CCM:

  1. Maisha yao yameboreshwa kwa kiasi gani katika miaka mitano au kumi ya mbunge huyuhuyu?
  2. Wanafunzi wangapi wa Darasa la Saba wamefaulu na kwenda Shule za Sekondari na kufaulu Kidato cha nne?
  3. Zahanati ngapi zimejengwa?
  4. Vifo vya Watoto na Mama Wajawazito vimepungua kwa kiasi gani?
  5. Je kila nyumba, kijiji, kata na tarafa zina Maji, Umeme na simu?
  6. Je kila familia ina nyumba bora?
  7. Je Wilaya hizi zina shughuli za kiuchumi ambazo zinatoa ajira ukiachia biashara ndogondogo na kilimo?
  8. Je hali za maisha za Wakulima na shughuli za kilimo zimeongezeka kiasi gani?
  9. Je wakulima wana pembejeo, nyenzo, maghala na soko la uhakika kwa mazao yao?
  10. Je kuna waalimu, wauguzi na watendaji wa kutosha wenye uwezo wa kitaaluma na kiufanisi?
  11. Je Wilaya ina miundo mbinu imara, kama barabara za kutosha kuunganisha vijiji, tarafa na kata? mifereji, madaraja na vivuko imara?
  12. Je magonjwa kama Malaria, Kichocho, Utapiamlo, Kipindupindu na magonjwa mengine yanatokea mara ngapi na takwimu zinazokusanywa zinafanyiwa kazi gani kuhakikisha kuwa kuna kampeni imara kupiga vita maradhi?
  13. Je Wazee, Wajane, Wastaafu, Walemavu na Wasiojiweza wanapewa huduma gani na Serikali na maisha yao yana hali gani?
  14. Je Watoto, Wazee na hata watu Wazima wanapata Lishe bora kila siku na kwa uhakika?
  15. Je Kilimo ni cha kisasa na chenye kuwapa Wakulima Uwezo wa kuongeza kipato chao kwa kutumia Ukulima stadi na wa Kisasa bila kutafuta shughuli nyingine kujiongezea kipato?
  16. Je Wilaya hizi zinapiga vita kwa kiasi gani ajira kwa watoto walio chini ya umri wa kuajiriwa?
  17. Je Wilaya zina programu gani za kuwaendeleza watoto na vipaji iwe ni katika masomo, michezo, sanaa na sayansi?
  18. Je Wilaya ina mfumo gani wa kuchochea ubunifu na msukumo wa kueneza Sayansi na mifumo ya kisayansi katika shughuli za uzalishaji mali na nyenzo za uzalishaji mali?
  19. Je Wilaya, Vijiji, Kata, Tarafa na Mitaa zina shughuli za kukuza elimu ya Uraia, Demokrasia na ushirikishi kwa nia ya Kujenga Taifa, bila msuguano wa kiitikadi?
  20. Je Wilaya, Vijiji, Kata, Tarafa na Mitaa zina Viongozi Bora na Siasa Safi na ziko wapi katika kujenga jamii inayojitegemea na yenye ufanisi?
  21. Je Watendaji waliohujumu, kuonea, kuzembea au kufuja mali wamechukuliwa hatua gani katika ngazi za kiuongozi kwatika Mitaa, Kata, Tarafa, Vijiji na Wilaya?
  22. Je Uongozi na Watendaji wa Wilaya wanafuata kanuni na Sheria na ni watiifu kwa Katiba, Sheria na kanuni za kazi na kijamii?
Kama nilivyosema, haya ni maswali ambayo ningetegemea Operesheni Sangara ilipoanza hadi leo hii, ingekuwa inayatumia katika ngazi za Mitaa, Vijiji, Kata na Tarafa kuleta changamoto na kuwaweka Chama Tawala na Watendaji wake kiti moto kwanza ndipo wao wajitangaze kama chama Mbadala na chenye kuweza kuyafanya hayo ambayo Mbunge huyu na Serikali hii ya CCM imeshindwa kuyafanya kwa Miaka 20 iliyopita.
Kama wanafanya hivi sawa na kama hawafanyi I hope wata usoma tena na tena, na kujua waambatanishe vipi hayo mapendekezo na OS. Well said Rev.
 
Dr. Slaa,

Naomba nichukue muda kukuomba radhi kwa kushindwa kukupa shukrani ipaswavyo kwanza.

Umesikia kauli yangu, umekuja na umeijibu kwa kina na kutoa uchambuzi.

Ingekuwa ni yule Mnyiramba Makala, Mgogo Chiligati hata Mgosi Makamba, wangetoa majibu ya upupu na si kujibu hoja.

Shukrani sana kwa kuwa na uwezo wa kujibu hoja na si kuleta dhihaka na maskhara kama kina Lukuvi na Marmo!
 
Monoko Mushi,

Hizi EPA zimeibiwa lini? je Richmond, IPTL, Rada na Ndege koko na upupu mwingine umeanza lini? Kama tutasema ulianza baada ya Azimio la Zanzibar mwaka 1992, hiyo ni miaka 30 tangu tuwe huru na bado tulikuwa na umasikini.

Ufisadi nna kilichohujumiwa katika Ufisadi ni kiwango kidogo sana na si tiba kwa Umasikini wa Tanzania.

Ukisoma ripoti ya CAG, utaona ni jinsi gani pesa zinatumika vibaya na zinaidhinishwa kibajeti, lakini ni mali bila daftari.

Nimekujibu hapo juu, suala ni Uongozi. Kule kwenye mada ya Azimio na Vijiji vya Ujamaa, conclusion yetu wote ni Uongozi.

Ukiwahoji hawa Viongozi kuhusu utendaji na ufanisi, wakashindwa kujibu na kuonyesha matokeo, ndipo utaanza kujenga mtaji imara wa kisiasa ambao utawezesha kupata kura Bungeni ambazo zitalazimisha kutungwa Sheria na hata kubasilisha Katiba.

Focus yetu ya kuleta maendeleo tumeiwekeza kwenye kulilia tulihujumiwa na Richmond. tumeunda kmati, tumechunguza, lakini hakuna hatua za kisheria au kinidhamu zimechukuliwa. Sawa na suala la EPA, Mzee Balali katutoka, hakuna ambye yuko tayari kumkaba koo aliyekuwa Waziri wa Fedha hata Rais kujua iweje kulikuwa na uzembe na kukosekana kwa ufuatiliaji makini ambao usingetuletea EPA?

Leo hii tunajiuliza, pamoja na kelele zote kuhusu Ufisadi, sijui EPA na upuuzi mwingine, Watu wamejichoeta Bilioni 300 kutoka mabenki ya Tanzania, je hatukujifunza kujenga mfumo bora wa kifedha baada ya EPA?

Jibu lake ni moja, hatuna Uongozi Imara, hatuna Uongozi Makini na hivyo kushinda Umasikini wa Tanzania si vita vya UFISDI pekee, bali ni kuwa na Uongozi Fanisi na Imara unaojua kuchapa kazi na unaowajibika na kuwepo na chombo chenye uwezo wa kuwajibisha!

Mzee wangu Reverand Kishoka nimekuapata,hata hivyo nina kijiswali;Je utawaambia wananchi tatizo la hao viongozi tusiowataka warudi madarakani ni yapi?

Yes ni kweli utawaambia kuwa hatuna uongozi imara na makini,sasa ni kipi haswa kinachopelekea viongozi hao kutokuwa imara na makini kama si ufisadi?
Hakuna wanachokifanya ambacho hakihusishi maslahi binafsi,that by itself constitutes ufisadi!

Ni lazima tu identify matatizo yaliyoko mbele yetu and what led to them....Najua umezungumzia hapo nyuma na kutolea mifano ya chaguzi mbali mbali walizoshindwa chadema licha ya kuwaeleza wananchi kuhusiana na ufisadi wa Richomd nk,hata hivyo sidhani kama hilo ndilo tatizo ama sababu kwamba hawakuchaguliwa,yani kuwajulisha kuhusu ufisadi,tuendelee kuwaelimisha wananchi kuhusiana na ubovu wa viongozi "Ufisadi" Halafu kama wameeelewa,then tuangalie sasa ni kwanini bado wanaendelea kuwachagua mafisadi hao....Kama ilivyoonekana huko Busanda nk!

Kama ulipitia ile thread yangu yenye kuuliza ni wapi tumekwama,utaona nilitolea mfano wa kauli ya Dr Slaa kuhusiana na mapokeo ya rushwa kwa wananchi kutoka kwa mafisadi hao nyakati za uchaguzi,there binafsi i believe is one of the critical problems pengine wananchi hawajui kuwa rushwa pia ni ufisadi?

Je na sisi hapa JF kama tusipo udefine ufisadi ipasavyo mwananchi wa kawaida itakuwaje?Ufisadi certainly si EPA na Richomnd pekee,hiyo ni mifano tu,Ufisadi ndiyo sytle yetu ya uongozi hilo wana JF tulielewe,muda ni mfupi uliobaki,tulitakiwa kwa sasa tuwe tumesha identify sababu na wapi tumekwama na kwa wakati huu, ilitakiwa tuwe tuna angalia ni kwa namna gani wananchi nao wataelimishwa kuwa hata rushwa ni ufisadi na wala si ishara ya upendo,Unaweza kuona tatizo hata la ku identify kuwa ni wapi tumekwama linatukabili hata sisi wana JF!

Cha muhimu hapa kwa wananchi ni uelewa kuwa hata ubaya una dalili za wema,nilishatoa mfano huko nyuma kwamba tunaweza kuwa in a wrong direction lakini dalili za njiani zitakawa kama ni right directions, hata shetani alimcorrupt mwanadamu kwa kujifanya anampenda na kupelekea mwana wa Adam kulimung'unyua tunda la mti wa kati wa bustani ya Eden!

Ni lazima tuwe na pahala pa kushikilia wakati wa madai yetu ya uhuru mpya!In times of crisis kama tuliyoko,ni lazima tuwe na yale tunayoyashikilia na kuamini kuwa ndio nguzo ya kutunasua! Ukikwama baharini na kama hutaki uzame,ni lazima uwe na mambo kadhaa ya kutilia maanani,kwa mfano ni lazima ufloat,na kama hujui kuogelea,ni lazima uhold on on something that floats....Pia huwezi kutapa tapa na kutaka kushikilia kila kitu! Utazama!

Nilishasema hapo awali kuwa kuna dalili ambazo tunapewa na Mungu lakini tuna zi ignore kwasababu tuna zi missidentify!

Kimsingi ili kuondoka tulipokwama ni lazima tuhold on something that we know it will help us achieving our goal,that is to get out of the current mess! This time kuwaelimisha wananchi nini haswa maana ya ufisadi na consequences zake,na kabla ya kuwaelimisha wananchi,sisi wenyewe kwanza tuelimishane,halafu kama tukikubaliana kuwa ni wapi tumekwama na and therefore what we should do,then ni lazima tuwe na one voice for sure kwamba this is what we think it will get us through!

Tukipotezana hapo haitajalisha busara na hekima walizonazo wengi wetu humu,tutabaki pale pale and the time tunarealise,its a whole new ball game!
 
Watanzania tunapenda majibu rahisi na ya mkato sana.

Umasikini wa Tanzania si ufisadi, japo ni kweli ufisadi unachangia lakini asilimia yake ni neglegible. Na hata hivyo basically, kila mtanzania ni fisadi na ndiyo maana mnaolia kubadili chama kwa nia ya kukombati ufisadi naweza kusema hesabu zenu ni butu.

Mtanishambulia, nakusema wale sio sisi hiyo ni kweli kama utarusha juu DICE mara kumi, lakini ukiirusha DICE hiyohiyo mara milioni ni hakika uta converge palepale kama, wao na hao si wengine, ni wakenya kumwondosha MOI na KANU yake ufisadi kule umeongezeka, wameuana hata kumeingia virtual serikali (MUNGIKI).

Nikirudi hapa tena, Kipindi cha Nyerere haukuwepo ufisadi na kama ulikuwepo basi kwa asilimia ambazo ni ndogo sana,lakini nakumbuka enzi hizo umasikini kwa watanzania ulikuwa sugu, nakumbuka sana ile mifuko ya kaki mzee alipokuwa ananunua sukari kilo moja kwa miezi na sababuni za magwaji na hasa zile shati za juliana bila kusahau ile kitu pima kwa mwaga na kiatu fulani ile kuwa na sole ndefu sana.Kifupi hapa nasema hakukuwa na ufisadi lakini umasikini ulikuwa umeshamili.

Ukiangalia trends za wapinzani wetu, mie naamini hawana malengo tofauti na waliopo madarakani yani kupata upenyo na huo upenyo kuutumia inavyowezekana ili wapate kufisadi kwa bidii ile ile.

Hawana njia wala hawajui kwa nini sie ni masikini ,wanatumia njia ambazo ni availlable lakini zisizo-solve tatizo kwa vile mawindo yao ni yale yale. kama Mamba atowapo tabasamu akiona mawindo yanafanikiwa.

Bahati mbaya ama nzuri karibu wote walio ktk politiks ktk vyama vyote wamepata kuwepo ktk awamu zote.Sasa unapata kuwashangaa kama wanapokuja na suluhisho rahisi kabisa kwamba umasikini wetu ni ufisadi na mikataba mibovu.
 
Kama tunaongea kuhusu ideal operation, labda Sangara haipo huko. Lakini pragmatically, naamini Sangara ina impact katika jamii ya watanzania.

Hayo mambo wanayoyafanya yanahitaji rasilimali, ambazo kwa chama kisicho na dola, nadhani inahitaji kujitolea zaidi. Tuwapongeze na kuwaunga mkono katika hilo.
 
Watanzania tunapenda majibu rahisi na ya mkato sana.

Umasikini wa Tanzania si ufisadi, japo ni kweli ufisadi unachangia lakini asilimia yake ni neglegible. Na hata hivyo basically, kila mtanzania ni fisadi na ndiyo maana mnaolia kubadili chama kwa nia ya kukombati ufisadi naweza kusema hesabu zenu ni butu.

Mtanishambulia, nakusema wale sio sisi hiyo ni kweli kama utarusha juu DICE mara kumi, lakini ukiirusha DICE hiyohiyo mara milioni ni hakika uta converge palepale kama, wao na hao si wengine, ni wakenya kumwondosha MOI na KANU yake ufisadi kule umeongezeka, wameuana hata kumeingia virtual serikali (MUNGIKI).

Nikirudi hapa tena, Kipindi cha Nyerere haukuwepo ufisadi na kama ulikuwepo basi kwa asilimia ambazo ni ndogo sana,lakini nakumbuka enzi hizo umasikini kwa watanzania ulikuwa sugu, nakumbuka sana ile mifuko ya kaki mzee alipokuwa ananunua sukari kilo moja kwa miezi na sababuni za magwaji na hasa zile shati za juliana bila kusahau ile kitu pima kwa mwaga na kiatu fulani ile kuwa na sole ndefu sana.Kifupi hapa nasema hakukuwa na ufisadi lakini umasikini ulikuwa umeshamili.

Ukiangalia trends za wapinzani wetu, mie naamini hawana malengo tofauti na waliopo madarakani yani kupata upenyo na huo upenyo kuutumia inavyowezekana ili wapate kufisadi kwa bidii ile ile.

Hawana njia wala hawajui kwa nini sie ni masikini ,wanatumia njia ambazo ni availlable lakini zisizo-solve tatizo kwa vile mawindo yao ni yale yale. kama Mamba atowapo tabasamu akiona mawindo yanafanikiwa.

Bahati mbaya ama nzuri karibu wote walio ktk politiks ktk vyama vyote wamepata kuwepo ktk awamu zote.Sasa unapata kuwashangaa kama wanapokuja na suluhisho rahisi kabisa kwamba umasikini wetu ni ufisadi na mikataba mibovu.
Hapa Murawasu hujatoa solution. Sasa kama upinzani nao hawana suluhu ni heri tuendelee na CCM ambayo inazidi kutufisidi? Si afadhali at least waenguliwe waone kuwa kumbe wanaweza kupoteza madaraka na upinzani ukiboronga tuwaondoe?

Ni kweli enzi za Nyerere tulikuwa maskini. Lakini maskini wa enzi hizo alipata matibabu, alisomesha wanae bure na aliweza kumudu milo miwili kwa siku. Leo ni bahati kama maskini anamudu mlo mmoja.
 
Rev. Amani iwe na kwako pia !

Nchi hii ni yetu sote ndio maana Dr.Slaa amesema CHADEMA ipo tayari kupokea ushauri au kukosolewa kwa nia ya kuisadia.

Nakubaliana na Dr kwamba yapo mafanikio kiasi na huu ni mchakato ambao unapaswa kuendelea na kuungwa mkono hata kama tija itonekana baada ya muda mrefu tatizo ni mapokeo. Kama watu wote wangekua wanatekelza mahubiri ya makanisani na misikitini watu wasingetenda dhambi lakini pengine ndio maumbile yetu hivyo basi kushindwa kwa CHADEMA katika chaguzi mbalimbali si kwa sababu CHADEMA haijasema au kuuliza hayo. Rev. ameyaainisha ni kwa sababu uamuzi ni utashi wa mtu mwenyewe.

Wahenga walisema ukipenda chongo utaita kengeza! Watu wanaichagua CCM huku wakijua fika kama huna fedha ya kuchangia matibabu basi na ufe. Unafanya vipi katika hali kama hii ndo maana CHADEMA inajikita na ufisadi na kuwaeleza wananchi kama fedha hizo zingepelekwa kununua dawa mtoto wako wako asingekufa jana kwa maradhi yanayotibika.

Nadhani wafanyacho CHADEMA sasa na operation sangara ni sahihi ni uamsho tu wasikate tamaa kama wasemavyo mpaka kieleweke na kitaeleweka tu muda utaamua
 
Duh.. yaani wewe naweza kukupaka mafuta uwe mrithi wangu.. maana the changes you have gone these few years have been beyond "oustanding" and "impressive".

Hilo swali zuri na la msingi sana. Kama tatizo ni Uongozi kwanini suluhisho lisiwe kwenye uongozi huo huo? Ungekuwa karibu ningekugongea!

keep it up.. napenda watu wanaouliza maswali zaidi ya yale yanayodhaniwa au kutarajiwa.

Mkuu MKJJ,you're shoes are too big for me!

Hata hivyo nashukuru kwa maneno yenye kutia moyo,tuko pamoja mkuu....The way i look at it ni kwamba i have concluded that it is definetly too legit to quit,and we pray you dont quit and none of the patriots quits!

Nasema tuko pamoja kwasababu hata makaa ya moto yasipokuwa pamoja,basi huzimika!

God willing,we will be Victorious!
 
Nilitarajia Operesheni sangara ingeingia kila Wilaya na Mkoa si kujiuza kuhusu CHADEMA na kupiga vita CCM na kuioanisha na UFISADI, bali ni kuwatikisa Wabunge na Serikali za Wilaya.

Naangalia hii Karamu ya Chai ya Wamarekani wanavyoisakama Serikali na Wawakilishi kwa kuwa mambo kadhaa hayafanyiki kwa manufaa ya Taifa au hao Wanakaramu wa Chai.

Kwangu mimi Operesheni Sangara nilitegemea ingeingia kwenye kila Wilaya ya CCM na kuwauliza wananchi, kwa nini wanaendelea kuiamini CCM na huyo mwakilishi wa CCM?

Ningewauliza tangu wamchague huyo Mbunge wa CCM:

  1. Maisha yao yameboreshwa kwa kiasi gani katika miaka mitano au kumi ya mbunge huyuhuyu?
  2. Wanafunzi wangapi wa Darasa la Saba wamefaulu na kwenda Shule za Sekondari na kufaulu Kidato cha nne?
  3. Zahanati ngapi zimejengwa?
  4. Vifo vya Watoto na Mama Wajawazito vimepungua kwa kiasi gani?
  5. Je kila nyumba, kijiji, kata na tarafa zina Maji, Umeme na simu?
  6. Je kila familia ina nyumba bora?
  7. Je Wilaya hizi zina shughuli za kiuchumi ambazo zinatoa ajira ukiachia biashara ndogondogo na kilimo?
  8. Je hali za maisha za Wakulima na shughuli za kilimo zimeongezeka kiasi gani?
  9. Je wakulima wana pembejeo, nyenzo, maghala na soko la uhakika kwa mazao yao?
  10. Je kuna waalimu, wauguzi na watendaji wa kutosha wenye uwezo wa kitaaluma na kiufanisi?
  11. Je Wilaya ina miundo mbinu imara, kama barabara za kutosha kuunganisha vijiji, tarafa na kata? mifereji, madaraja na vivuko imara?
  12. Je magonjwa kama Malaria, Kichocho, Utapiamlo, Kipindupindu na magonjwa mengine yanatokea mara ngapi na takwimu zinazokusanywa zinafanyiwa kazi gani kuhakikisha kuwa kuna kampeni imara kupiga vita maradhi?
  13. Je Wazee, Wajane, Wastaafu, Walemavu na Wasiojiweza wanapewa huduma gani na Serikali na maisha yao yana hali gani?
  14. Je Watoto, Wazee na hata watu Wazima wanapata Lishe bora kila siku na kwa uhakika?
  15. Je Kilimo ni cha kisasa na chenye kuwapa Wakulima Uwezo wa kuongeza kipato chao kwa kutumia Ukulima stadi na wa Kisasa bila kutafuta shughuli nyingine kujiongezea kipato?
  16. Je Wilaya hizi zinapiga vita kwa kiasi gani ajira kwa watoto walio chini ya umri wa kuajiriwa?
  17. Je Wilaya zina programu gani za kuwaendeleza watoto na vipaji iwe ni katika masomo, michezo, sanaa na sayansi?
  18. Je Wilaya ina mfumo gani wa kuchochea ubunifu na msukumo wa kueneza Sayansi na mifumo ya kisayansi katika shughuli za uzalishaji mali na nyenzo za uzalishaji mali?
  19. Je Wilaya, Vijiji, Kata, Tarafa na Mitaa zina shughuli za kukuza elimu ya Uraia, Demokrasia na ushirikishi kwa nia ya Kujenga Taifa, bila msuguano wa kiitikadi?
  20. Je Wilaya, Vijiji, Kata, Tarafa na Mitaa zina Viongozi Bora na Siasa Safi na ziko wapi katika kujenga jamii inayojitegemea na yenye ufanisi?
  21. Je Watendaji waliohujumu, kuonea, kuzembea au kufuja mali wamechukuliwa hatua gani katika ngazi za kiuongozi kwatika Mitaa, Kata, Tarafa, Vijiji na Wilaya?
  22. Je Uongozi na Watendaji wa Wilaya wanafuata kanuni na Sheria na ni watiifu kwa Katiba, Sheria na kanuni za kazi na kijamii?
Kama nilivyosema, haya ni maswali ambayo ningetegemea Operesheni Sangara ilipoanza hadi leo hii, ingekuwa inayatumia katika ngazi za Mitaa, Vijiji, Kata na Tarafa kuleta changamoto na kuwaweka Chama Tawala na Watendaji wake kiti moto kwanza ndipo wao wajitangaze kama chama Mbadala na chenye kuweza kuyafanya hayo ambayo Mbunge huyu na Serikali hii ya CCM imeshindwa kuyafanya kwa Miaka 20 iliyopita.

Ndio maana nilitahamaki sana niliposikia kuwa Vyama vingi vya Upinzani havikushiriki kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hasa CHADEMA ambayo ilikuwa na uwakilishi mdogo kwa kuwa wao wameekeza macho na akili zao kwenye Ubunge na Urais kupitia Uchaguzi Mkuu wa 2010!

Kampeni hii ya kuhoji Wabunge na Serikali si kitu cha kunyemelea majira ya Uchaguzi Mkuu pekee, ni suala la kila siku kujikumbusha na kukosoa ili Watanzania waweze kuanza kuwa na upeo wa kufikira nje ya ahadi za Wanasiasa na Serikali ambazo hazitimizwi au zinanufaisha wachache!

Ni maswali ya kwenda kuwabana kila Mbunge na Mkuu wa Wilaya ambaye ni wa CCM, bila kujali yeye ni Mpiganaji au ukaribu wake kwa Rais au bila kujali eti yeye ni kigogo au kizito wa chama.

Bila kuanza kampeni hii kuhoji na kuonyesha udhaifu na mapungufu ya CCM na si kuzungumzia EPA, Richmond na mambo ya magazeti, itakuwa ni vigumu kujiuza kama chama kinachojua kinachofanya na chenye uwezo wa kurekebisha kasoro zilizofanywa na CCM na Serikali yake.

Hivyo kama CHADEMA na Operesheni Sangara inakosa nguvu na ladha ya kuhoji haya, je tutegemee vipi kuwa watauzika na kuwa watakuwa Chama makini wakipewa dhamana ya kuongoza nchi?
Rev. Kishoka,

Unajua ni rahisi sana kushauri au kusema lakini muda wote matatizo ni katika kutenda. Unapotenda ndio unagundua ugumu wa jambo maana factors kibao ambazo hukuziweka wakati unapendekeza, zinaanza kujitokeza.

Pamoja na ushauri mzuri sana uliotoa, mimi naamini hayo yote CHADEMA wanafanya ila yanaingia na kutoka masikioni mwa Watanzania. Tatizo ni kwamba hata wakijua ubovu wa CCM lakini je nani atawaokoa? Hilo ndilo tatizo kubwa. Hawaoni kama viongozi wa CHADEMA wana tofauto yoyote na CCM.

CHADEMA na vyama vingine wangefaidika zaidi kama wangelikuwa na watu kule chini ambao wanashirikiana na wananchi kwenye matatizo mbalimbali. Hao watu wa CHADEMA ndio waonyeshe kwa matendo kwamba wao wako tofauti na CCM na wala sio kwa maneno majukwaani.

Nakubaliana na wewe kwamba kosa kubwa walilofanya CHADEMA ni kupuuzia uchaguzi wa serikali za mitaa na kuwaacha CCM wanyakua karibu viti vyote. Hao waliochaguliwa kwenye serikali za mitaa ndio wataandaa uchaguzi wa mwaka 2010 na kama kuna kuiba au kuendesha kampeni ya nyumba kwa nyumba basi hao ndio wenyewe. Bahati mbaya CHADEMA haina hao watu na wataendelea kutegemea elimu ya kutolewa na watu ambao wanapita mara moja kwa mwezi.

Tatizo kubwa huenda ni resources ambazo zinatakiwa nyingi kweli kuelemisha wananchi kwa kule chini na pia kuzuia viongozi wenu wasiporwe na mwewe.

Kufanya mabadiliko kule chini sio kazi rahisi kama ambavyo mtu unaweza kuona ukipita.
 
Moniko Mushi,

Wabunge in BUTU, hata leo CHADEMA wakija madarakani, Wabunge wataendela kuwa BUTU bila kubadilisha mfumo wa Serikali yetu.

Wengi wenu mnaweza kuchukulia uchochezi wangu wa kuhoji haya mafanikio kwa ufupi sana bila kuangalia kuwa matokeo yake yanaweza kuwa yapi.

Kwanza tukiangalia kauli na matendo ya Wabunge wengi, utaona kuwa kila mmoja anategemea kutafuta wafadhili au kikundi cha watu binafsi kuleta maendeleo na si kuishinikiza Serikali Kuu. Hili ni tatizo, na linapaswa kutatuliwa haraka sana na njia pekee ni kuanza kuwafundisha wananchi kupima matokeo na si ahadi. aidha kuna ulazima wa Wananchi kuanza kujua kodi zao zinatumika vipi na si kushangilia mbunge kuwanunulia Ambulance au kujenga kisima cha maji na kuwaletea madawati au vifaa vya zahanati walivyowenda kuomba kwa wafadhili na marafiki huko ulaya na Marekani kama si michango kutoka kwa marafiki.

Maswali hayo yakiulizwa kila siku bila woga, yatawaweka Wabunge na Watendaji kiti moto wachape kazi na kuifanya Seikali Kuu ianze kulazimika kupeleka na kuratibu maendeleo kwa ufanisi kila siku na si kusubiri kila baada ya miaka mitano na ahadi hewa.

CCM hawawezi kubadilika, wenye uwezo wa kuwawabasilisha ni CHADEMA< CUF, TLP na sisi kama jamii!

Leo tunaweza kubadilisha mtawala na chama, lakini kama hatutabasilisha mfumo ambao utatuletea viongozi waadilifu, wachapakazi na wenye ufanisi, tatizo letu bado liko pale pale, hapatakuwa na nafasi ya kuunda na kutunga sheria achilia mbali kuhakikisha zinafanya kazi ambazo zitawabana Mafisadi na kutuondolea upuuzi wa EPA, RICHMOND na Ufisadi wote ambao hadi leo hii inaonnekanza wazi kuwa tumekuwa tukipigia gitaa mbuzi, iwe ni kwa Watanzania au Serikali.

Ikiwa leo hii Watanzania wanaridhika kukosa maji na umeme (nasema wameridhika maana hawajakasirika na kuifanya Serikali iamke) au hata hili suala la mgomo tunaona wanapoozwa na kuna wanaoridhika jamani twende Ikulu tukajadiliane, na huku kila mtu anajua ataambiwa kuwa Mishahara mipya au suluhisho litakuwa 2012, lakini msisahu kutupigia kura, je tukiimba kama Mbilia Bell au Papa Wemba na Mr. Nice kuhusu Ufisadi wataelewa au Watanzania watasubiri matokeo 2012?

Mbinu za Medani zinabidi kubadilika, hichi ndicho ninachojaribu kuwashawishi CHADEMA, lakini wanajiamini sana kwa mbinu zao ambazo leo hii miaka 18 tangu waanzishwe, tumeyaona matunda yake!

Ndugu Reverand Kishoka;

Kwenye ile thread yangu ya wapi tumekwama,ndugu Miner alikuwa na mawazo kama hayo,kuwa tatizo ni mfumo period,na kwamba tukibadili mfumo na viongozi hao watabadilika!

Siamini hilo hata chembe,at least kwasasa,ila tunaweza kuwa na compromise on this one kwasababu tunataka tufikie conclusion kwamba what we should do,mambo yaazie hapa JF,we've everything we want ideas wise,pia hata facts on the ground....Compromise naona itakuwa kwamba lazima mfumo mpya na viongozi wapya viende hand to hand,kwamba we just cant have only one by itslef and expect to fix dis mess!

Ndugu Reverand Kishoka;

Nasema hayo kwasababu swlowly but surely,hata pale mfumo ulipokuwa na strengths,ie maadili ya uongozi kwenye AD nk,viongozi hao ambao mnadai kwamba mfumo umewaangusha ndiyo walizimalizia kabisa zile some strenghts ambazo zilitumiwa na viongozi wazalendo kama Sokoine na Mwalimu kuushughulikia ufisadi na viongozi mafisadi,ulikuwa ni mwanzo mzuri,ilkuwa ni nyota njema ya asubuhi tuliyoamua kuipa kisogo either kwa kujua ama kutokujua,je are we poised to repeat the same mistakes?Kwamba ni mfumo tu ndo tatizo?

Ndugu Reverand Kishoka;

Mfumo hauharibiki wenyewe,rather unaharibiwa,kuwabadilishia wanaouharibu ni jambo la busara kweli?naweza kuwa wrong....However, hilo ndio mantiki halisi ya mijadala kama hii,kukosoana na kumove forward kwa manufaa ya Taifa letu!

Pi umezungumzia kuwa mfumo mpya ndiyo utatuletea vingozi wapya na wachapa kazi,how is that possible? Nia za watu hupimwa kwa matokea ya matendo yaliyotokana na nia hizo! Nia inaweza kuwa nzuri lakini matokea yakawa mabaya,hapo tatizo linaweza kuwa mfumo,hata hivyo on the other hand,nia mbaya haijalishi ni mfumo gani ulioko maana sheria za maadili ya uongozi ziliondolewa kwa nia mbaya....Ili kuweza kulikomboa taifa ni lazima tuwe aware on that,tusicheze kwenye tope la kisiasa linalotupotezea muda...Ukweli ni dawa ya uongo,uongo umetawala kwenye siasa za kifisadi,hatuwezi kuushinda ufisadi bila ya kuushinda uongo....Na pia hatuwezi kuushinda uongo kama tukiendelea kukubali kudanganywa!

Na hata kama wananchi walio wengi hawajui kuwa wanadanganywa,basi ni lazima wawepo waliojitolea kupambana kwa niaba ya wananchi na maslahi ya Taifa na kuhakikisha kuwa uongo is defeated,tukushawapata hao wenye nia ya kuushinda uongo ili tuondokane na ile dhana ya "Wadanganyika" na "Ndivyo tulivyo mentalities" then we can build on it ie kuufanyia kazi mfumo nk.

Hivyo basi ningefurahi kama ungenielewesha ni kivipi tutatoka tulipokwama kwa kubadili mfumo peke yake na kuwaacha viongozi wale wale.....Kwasababu naelewa kuivalisha maiti suti mpya hakutaifufua maiti hiyo! Nasubiri kutoka kwako.

Natanguliza shukrani za dhati!
 
All in all naamini Operesheni Sangara ina Mafanikio na Mapangufu. Sasa ni jambo kuangalia ni wapi kuna Mapungufu na kuwashauri nini wafanye ili kuboresha. Je Katika Operesheni Sangara wanahamasisha vipi watu kujiandikisha kupiga kura? Je katika watu wanaokuja kwenye mikutano can they estimate ni wangapi wamejiandikisha na wangapi watapiga Kura. Ingefaa wawaambie wananchi kuhudhuria kwenye mkutano pasi na kuwa umejiandikisha ni Kazi Bure
 
Watanzania tunapenda majibu rahisi na ya mkato sana.
Mmh, haya tuendelee, may be you are right, we will soon see.

Umasikini wa Tanzania si ufisadi, japo ni kweli ufisadi unachangia lakini asilimia yake ni neglegible.
Hakuna anayesema umasikini wa Tanzania ni ufisadi, unachangiwa na ufisadi. Kwa asilimia ngapi ? Inategemea wewe kwako ufisadi ni nini, kwangu ufisadi ni njama zozote zinazozorotesha maendeleo ya nchi kwa ujumla wake huku wanaonufaika ni watu au kundi fulani tu katika jamii.

Na hata hivyo basically, kila mtanzania ni fisadi na ndiyo maana mnaolia kubadili chama kwa nia ya kukombati ufisadi naweza kusema hesabu zenu ni butu.
Hili ndilo mimi naweza kuliita jibu rahisi. Ufisadi unalimwa, unapandwa, na unashamiri chini ya mfumo unaodumishwa na kulindwa na mamlaka. Mamlaka zina hiari ya kuupiga vita ufisadi na kuutokomeza au kuukumbatia kwa kuwa zinafaidika nao.Chama tawala kimeonyesha kuwa hakina nia wala sababu ya kuutokomeza na huo ndio ukweli.

Mtanishambulia, nakusema wale sio sisi hiyo ni kweli kama utarusha juu DICE mara kumi, lakini ukiirusha DICE hiyohiyo mara milioni ni hakika uta converge palepale
Hapana, hapa unataka kupingana na ukweli wa kisayansi. Dice unavyozidi kuirusha mara nyingi ndivyo kila upande unakuwa na nafasi sawa na hata siku moja huwezi kudai eti uta converge pale pale.

kama, wao na hao si wengine, ni wakenya kumwondosha MOI na KANU yake ufisadi kule umeongezeka, wameuana hata kumeingia virtual serikali (MUNGIKI)
.

Ni kweli waliuana na siku zote mabadiliko ya msingi yanakuwa na gharama zake. Ulidai hapo nyuma kuwa Watanzania tunapenda majibu rahisi lakini hapa unaonyesha wazi kuwa wewe ndio hasa kio cha hao Watanzania. Kenya karibu wanapata katiba mpya - sasa hayo ndio matunda ya kujitoa mhanga kupigania haki.

Nikirudi hapa tena, Kipindi cha Nyerere haukuwepo ufisadi na kama ulikuwepo basi kwa asilimia ambazo ni ndogo sana,lakini nakumbuka enzi hizo umasikini kwa watanzania ulikuwa sugu,

Yawezekana tulikuwa masikini lakini tulipata elimu, tulipata huduma za afya na tuliweza kumpiga adui aliyetaka kuivamia ardhi yetu. Mali zetu za asili tuliweza kuzilinda mpaka hapo walipotokea manyang'au wakaamua kuziteketeza kama hazina mwenyewe. Hivi sasa tumekuwa kama wakimbizi ndani ya ardhi hiyo hiyo tuliyotoa damu zetu kuilinda.

nakumbuka sana ile mifuko ya kaki mzee alipokuwa ananunua sukari kilo moja kwa miezi na sababuni za magwaji na hasa zile shati za juliana bila kusahau ile kitu pima kwa mwaga na kiatu fulani ile kuwa na sole ndefu sana.Kifupi hapa nasema hakukuwa na ufisadi lakini umasikini ulikuwa umeshamili.
Ndio ni kweli, we made a sacrfice kuilinda nchi yetu na heshima yetu hata kama kwa kufanya hivyo ilibidi tununue kilo moja ya sukari kwa mwezi. Kama hujui hata hadithi ya viatu vya sole ndefu au suruali za miguu mipana ni bora ukae kimya ndugu yangu.

Ukiangalia trends za wapinzani wetu, mie naamini hawana malengo tofauti na waliopo madarakani yani kupata upenyo na huo upenyo kuutumia inavyowezekana ili wapate kufisadi kwa bidii ile ile
.
Utaonaje trend za wapinzani huku unakula kuku kwa mrija. Trend tunayoitaka ni kwamba ukipewa madaraka ukavurunda ukae pembeni uwapishe na wengine. Wao nao wakija wakavurunda, wawekwe pembeni waingie wengine. Ni kwa njia hiyo tu atakayepewa madaraka atawaheshimu waliompa hayo madaraka. Lakini kwa mtindo wako wa kuwakumbatia hao hao kwa miaka hamsini, hatutaweza kuwa na nia, sababu wala uwezo wa kuwawajibisha .

Hawana njia wala hawajui kwa nini sie ni masikini ,wanatumia njia ambazo ni availlable lakini zisizo-solve tatizo kwa vile mawindo yao ni yale yale. kama Mamba atowapo tabasamu akiona mawindo yanafanikiwa.
Huwezi kudai hawajui kwa nini sisi ni masikini. Watu wenye mawazo kama yako ndio maadui wakubwa wa taifa hili na hasa ndio kiini cha matatizo pamoja na umasikini wetu. Haya nayo yanatosha kabisa kuitwa mawazo ya kifisadi kulingana na maelezo niliyoyatoa mapema kabisa.

Bahati mbaya ama nzuri karibu wote walio ktk politiks ktk vyama vyote wamepata kuwepo ktk awamu zote.Sasa unapata kuwashangaa kama wanapokuja na suluhisho rahisi kabisa kwamba umasikini wetu ni ufisadi na mikataba mibovu.

Tanzania ina watu zaidi ya milioni arobaini na katika watu hawa inadaiwa milioni nne ni wana CCM. Hivi unataka tuamini kuwa katika milioni thelathini na sita hakuna ambao hawajawahi kujihusisha na CCM mimi nikiwa moja wao. Umasikini wetu unatokana na uongozi na uongozi mbovu ni zao la ufisadi na chama kinachotoa viongozi hao ni cha kifisadi pia, alamsiki.
 
Back
Top Bottom