Nini mtazamo wako kuhusu mama wa kambo

Sijalelewa na mama wa kambo na bado sijawahi kuwa mama wa kambo ila nimekuwa mama wa yatima.
Ila mama yangu keshalea mama wa kambo.

Kuna kipindi ilibaki kidogo tuletewe mama wa kambo wakati baba na mama walivyotengana.
Nakumbuka kaka zangu walikuwa wakiambizana jinsi gani watakavyomfanyia visa huyo mama akiletwa. Thank God it never happened.

Ninachoweza sema, kuna aina 2 ambazo zinamchango mkubwa sana wa mahusiano ya watoto na step parents zao.
1: watoto uliowakuta, mara nyingi chuki kwa watoto hawa huwa si kubwa sana unless the wife is a real monster.
2: watoto wakiokukuta, ingawa watoto ni honest hawana kosa lkn ni wamama wachache sana (mine included) wanaoweza ishi nao vizuri.

Sasa ni nini keinachochangia (in either cases) mama akamtreat vibaya mtoto wa mumewe.
1: mume kutukuwa na uwezo wa kuiongoza familia
2: mume kuabuse mkewe ambaye naye hutafuta mnyonge wake
3: mume kuwa malaya na kutoitimizia familia mahitaji
4: mawifi kuingilia na mara nyingi kuwapenda watoto wa kambo kuliko wa ndoa
5: tabia au roho mbaya ya mke.

Sasa nini cha kufanya.
Kabla ya kumuintroduce mtoto kwa mke na mke kwa mtoto, baba ongea nao kwa undani na kwa kutulia.

Baba uwe na muda wa kutosha na familia ikiwezekana hakikisha mnasali pamoja jioni.

Mtrust mkeo, na mwambie amlee mwanao kama wake; asiache kumkanya kisa si mwanaye.

Ongea na mtoto, amuone mama wa kambo kama mama yake na amuheshimu.

Msigombane mbele za watoto na muwashirikishe wote ktk mipango yenu ya maendeleo.

Onesheni upendo kwa maneno na matendo.

Ni hayo tu Ablessed
Dah umeongea kiundani sana , kiukweli hiki ulichoandika ni sehemu ya ukweli dear. Ina maana mume anapaswa kuwajibika vema/ kutimiza wajibu wake. Unajua mimi nimeishi na mama wa kambo tulifanya kila lililojema juu ya mama huyu lkn alichoturudishia ni maumivu tu. Hata wanae walikua wakitusogelea basi wanapigwa utadhani wamesogelea kifo. Kumbuka yeye alitukuta pale home. Baada ya kua na maisha yetu tumemsomeshea watoto wake wote na sasa wengine wanafanya kazi. Nae alikuja na mwanae pia tulimtendea wema wote ikiwa pamoja na kumsomesha kwani tulijifunza kuwa usilipize kisasi. Sasa naelewa kumbe matatizo mengine yanasababishwa na baba kuwa either kumuamini sana mkewe na kutowafuatilia watoto.

Kwa mtazamo wangu , sintakua mbali sana na wewe ni kwamba wababa muwe karibu na watoto wenu . Na hili la kua karibu na watoto lifanyike kwa hekima sana ili mama asijione kua anadharaulika. Pia si kila anacholalamika mtoto juu ya mama wa kambo/ mama basi kinakua cha kweli la hasha vingine vinachanganyika na utoto/chuki. So baba ajaribu kubalance.
 
Ablessed my dear, l feel for you lkn l more proud of you kwamba malezi yako badala ya kukuathiri negatively, umekuwa strong on the positive side. Salute!

Kuna insecurity fulani ambayo huwakumba wamama ambao wanawakuta watoto tayari, n jinsi ya kudeal na hiyo insecurity ndipo makosa makubwa hufanyika.

I pray that if l am to be a step mom, Mungu anipe busara, upendo na understanding.

Lkn vipi kuhusu step dads?
 
Last edited by a moderator:
sikatai inawezekana na hilo lipo kibaiolojia zaidi kuwapenda wanae zaidi ila wangu atawalea the same way i raised her.
yeye atazaa na senior bachelor awe na patent right
So naye atazaa na waume za watu? Still kuna uwezekano wa kuwapenda wanae zaidi ya wanako.
 
Oooh kwa hiyo kumbe tatizo wakati mwingine linakua kwa watoto. Najua dear kua kuna baadhi ya wamama wa kambo wazuri mno lkn kwanini hawa wengine wanakua na roho mbaya hivi.

kama nilivyotangulia kusema ni roho ya mtu kweli kwa bahati wapo wazuri sana tu hadi huwezi tofautisha lakini machache ........kuhusu watoto wengine wanakuwa wanapandakizwa chuki labda na ndugu wa mke wa kwanza au hata majirani na watu mbali2 kuna mama wa kambo alikuwa anakwenda hadi kwa waganga wa kienyeji watoto ili wasiweze kufanikiwa wakwake ndio wawe safi walimwengu wabaya sana aise waone hivyo
 
Kaunga,
Baba wa kambo wana nafuu kiasi flani . Unajua mama ndio hasa mtunza familia so mtoto wake hawezi pata tabu sababu wababa wengi huwa na shughuli nyingi zinazowasababishia kurudi home night kali. Kuteseka kwa mtoto anayeishi na b/kambo kunategemea sana msimamo wa mama . Kuna wamama huwasahau watoto wao na kuzamisha mapenzi yao yote kwa huyu baba mpya na hata wengine wanadiriki kuwaneglect watoto wao sijui inasababishwa na maumivu ya previous relationship.
 
Last edited by a moderator:
Mama wa kambo anafungua makucha anapojua kuwa baba yuko upande wa watoto wa kambo
vinginevyo mama wa kambo huwa wako poa tu mbona.
 
roho mbaya ni mtu mwenyewe tu,maana kuna kina mama wengine wanaroho mbaya kwa watoto wao wa kuwazaa nina mfano hai.
 
Sipendi kabisa kitu hicho kije kinitokee maishani kwa watoto wangu .. mama wa kambo alinitesa simpendi hadi leo namsalimia kinafiki tu jamani ... umenikumbusha mbali sana wewe
 
Sipendi kabisa kitu hicho kije kinitokee maishani kwa watoto wangu .. mama wa kambo alinitesa simpendi hadi leo namsalimia kinafiki tu jamani ... umenikumbusha mbali sana wewe
Rafiki pole sana. Time is a great healer Mungu atakupa neema utapona na kumuona wa kawaida. Binadamu hawafanani dear ni kweli hawa watu wanasababisha maumivu makali.
 
ha haaa, Ablessed umenikumbusha siku moja katika michapo na hubby tukajikuta tunaongelea familia ya rafiki yake mmoja aliyesusiwa mtoto huko nje ikabidi amlete kwa mkewe. basi mbele ya story akaniuliza wewe ungefanyaje ndo ningekuletea mtoto kama huyo?
nikamwambia ningehakikisha mlo wako unaofwata mboga itakuwa huyo mwanao......halafu hapo nipo serious sina utani....... yaani aliniangalia kwa mshangao mkubwa sana, hakutegemea kama ningeweza kujibu hivyo....... nimemtisha vibaya sana
 
Last edited by a moderator:
My dear, na madigirii yoote sijui na umjini, mimi naamini katika mume kuwa kichwa cha familia (japo akiamua kuwa kiuno sitakaa kushangaa maghorofa. Nitakuwa mumewe abaki anashangaa yeye).

Baba akiwa failure aisee hakuna linaloenda. Ndo maana mtoto akikataa kula anaambiwa ntakusemea kwa baba! Nina rafiki mumewe kazaa twins huko kaleta kawabwaga hapo. Mbaya ni kuwa wana extended ama sijui tuite stretche family yenye mawifi na watoto wao na wajukuu na mama mkwe! Baba akirudi anatukana watu wote mbele ya watoto. mtoto analia mama wa kambo anaenda kuuliza unalia nini twin wake anasema hataki kuvalishwa socks. Mama anamgombeza na akitoka mtoto analia upya. Baba akija twin mtu anasema ana kidonda wanamlazimisha viatu. Yaani vitoto vina hila wanagombana nyumba nzima. Baba anatukana mnanijazia vyoo hela natafuta kwa ajili ya wanangu tuuu. Hivi kesho baba amesanda huyu mama atanunua viatu vya hao wanae wa kambo?

Nasisitiza, mamangu alikuwa mama wa kambo bora sana kwa sababu alipata full support ya baba na ndugu zake baba. Mama wa kambo hana tofauti na mke wa pili. You need to work extra hard to prove that you are better. Kama watu wana attitude na kuhesabu makosa, hakuna litakalowezekana. My cousin was the worst step father ever to his wife's kids hadi aibu!
Kaunga,
Baba wa kambo wana nafuu kiasi flani . Unajua mama ndio hasa mtunza familia so mtoto wake hawezi pata tabu sababu wababa wengi huwa na shughuli nyingi zinazowasababishia kurudi home night kali. Kuteseka kwa mtoto anayeishi na b/kambo kunategemea sana msimamo wa mama . Kuna wamama huwasahau watoto wao na kuzamisha mapenzi yao yote kwa huyu baba mpya na hata wengine wanadiriki kuwaneglect watoto wao sijui inasababishwa na maumivu ya previous relationship.
 
Last edited by a moderator:
Mimi mtazamo wangu ni kama wako aisee. Watoto watakaonikuta kwenye ndoa sina neno nao ila walelewe na mama zao. Kila mwanamke anaeweza kukuzalia mtoto na ajue kukulelea pia. Kama unajali sana hamia huko ukalee mwanao. Ila mtoto anakaribishwa kuja kuona ndugu zake na sio kuhamia. Na akifika full majuisi na wenzie bila ubaguzi. Manake safari moja huanzisha nyingine, ukichekacheka hukawii kuanzishiwa nursery skuli!
ha haaa, Ablessed umenikumbusha siku moja katika michapo na hubby tukajikuta tunaongelea familia ya rafiki yake mmoja aliyesusiwa mtoto huko nje ikabidi amlete kwa mkewe. basi mbele ya story akaniuliza wewe ungefanyaje ndo ningekuletea mtoto kama huyo?
nikamwambia ningehakikisha mlo wako unaofwata mboga itakuwa huyo mwanao......halafu hapo nipo serious sina utani....... yaani aliniangalia kwa mshangao mkubwa sana, hakutegemea kama ningeweza kujibu hivyo....... nimemtisha vibaya sana
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri ni Watu wanavyowafikiria.Wa mama wakambo ni wazuri tu sema it depends alivyoingia Kwenye uhusiano wa baba yenu .Kama huyo mama ndio sababu ya ndoa ya wazazi Wenu kuvunjika well hata Mie sitompenda.kama ni gold digger na mdogo kiumri Mpaka mnakuuliza kulikoni .kwa ujumla msifananishe Woote .Mie naekewana na mama mkwe wangu wa kambo ( mama wa kambo wa mume wangu ) .
 
My dear, na madigirii yoote sijui na umjini, mimi naamini katika mume kuwa kichwa cha familia (japo akiamua kuwa kiuno sitakaa kushangaa maghorofa. Nitakuwa mumewe abaki anashangaa yeye).

Baba akiwa failure aisee hakuna linaloenda. Ndo maana mtoto akikataa kula anaambiwa ntakusemea kwa baba! Nina rafiki mumewe kazaa twins huko kaleta kawabwaga hapo. Mbaya ni kuwa wana extended ama sijui tuite stretche family yenye mawifi na watoto wao na wajukuu na mama mkwe! Baba akirudi anatukana watu wote mbele ya watoto. mtoto analia mama wa kambo anaenda kuuliza unalia nini twin wake anasema hataki kuvalishwa socks. Mama anamgombeza na akitoka mtoto analia upya. Baba akija twin mtu anasema ana kidonda wanamlazimisha viatu. Yaani vitoto vina hila wanagombana nyumba nzima. Baba anatukana mnanijazia vyoo hela natafuta kwa ajili ya wanangu tuuu. Hivi kesho baba amesanda huyu mama atanunua viatu vya hao wanae wa kambo?

Nasisitiza, mamangu alikuwa mama wa kambo bora sana kwa sababu alipata full support ya baba na ndugu zake baba. Mama wa kambo hana tofauti na mke wa pili. You need to work extra hard to prove that you are better. Kama watu wana attitude na kuhesabu makosa, hakuna litakalowezekana. My cousin was the worst step father ever to his wife's kids hadi aibu!
Ni kweli dear wapo wamama wazuri na mambo mengine watoto na jamii inachangia kwa kiasi flani. Nasikitika juu ya hiyo familia ya rafiki .Cha msingi wahusika wajitahidi kufanya mabadiliko ili maisha yawe ya furaha kwa kila pande. Kwa bahati mbaya yeyote anaeamua kuachia feeling zake mbovu juu ya mtoto ambae si wake ni vema akajifunza kuzicontrol maana wanaoumia ni hao watoto hata kama nao ni tatizo.
 
Nafikiri ni Watu wanavyowafikiria.Wa mama wakambo ni wazuri tu sema it depends alivyoingia Kwenye uhusiano wa baba yenu .Kama huyo mama ndio sababu ya ndoa ya wazazi Wenu kuvunjika well hata Mie sitompenda.kama ni gold digger na mdogo kiumri Mpaka mnakuuliza kulikoni .kwa ujumla msifananishe Woote .Mie naekewana na mama mkwe wangu wa kambo ( mama wa kambo wa mume wangu ) .
Upo sawa dear hata mimi sikugeneralize maana najua kuna walio wema wengi tu. Lkn najua unafahamu kuwa wapo wengine sio wema. Na hao ndio waliosababisha hili jina kua baya kitu ambacho si kizuri kama nilivyoainisha kuwa hakuna mwanamke anaependa kua mama wa kambo bali inatokea tu kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake . Hivyo nakubali kabisa wapo walio wema na ninawapongeza na kuwatia moyo wasirudishwe nyuma wala kukatio
shwa tamaa na kundi dogo .
 
Sijawahi kusikia wala kuona story nzuri kuhusu mama wa kambo....zote ni za kuniwasha masikio tu. Sijui labda ninavozidi kuishi nipate uzoefu chanya kuhusu hawa viumbe. Nitabaki kuamini kwamba Mama wa kambo si mama hadi hapo nitakapopata cases mpya ili ni re-frame theory yangu. Hao wanawake wengi wanaojifanya kuwapenda watoto wa kambo mara nyingi unakuta ni kimaslahi zaidi (mara nyingi lazima kuna kitu kinachomfanya afanye hivyo na si bure) na unafiki tu mbele za umma ila mioyo yao inasuta.

Na wanaume ambao hamjaoa na ambao mmeoa jihadharini sana kuzaa nje na kutarajia mje muwalee watoto wenu mkiwa na wake zenu ambao si mama wa watoto husika. Mnawasababishia watoto mateso wasiyostahili. Starehe zenu wawili zinakuja kuwa dhahama kwa viumbe wasio na hatia. Story zingine ukizisikia ni za kusikitisha sana. Mama wa kambo si mama na hataweza kuwa mama sababu always sisi binadamu ni egoistic na lazima tunalinda maslahi yetu kwanza.
 
Hua mara nyingi tatito linakua kwa mama halisi wa mtoto na ndugu zake kwa kutaka kumwonyesha mtoto kua wanamjali kuliko mama mlezi wakati ukweli ni kua mara nyingi unakuta hawana uwezo wa kifedha (kumsomesha n.k). Mimi nimelelewa na mama wa kambo baada ya mama kufariki nikiwa na miaka 13 kusema ukweli alinilea zaidi ya mwanawe. nadhani hivi ndivyo inavyokua mara nyingi sababu hua wanaogopa kusemwa na jamii endapo watamnyanyasa mtoto wa kambo. Nilipoanza Sekondari nilishuhudia sasa malezi aliyokua anayatoa kwa wanawe, niliwaonea huruma wadogo zangu na nilijisikia kupendelewa zaidi kimalezi.

Ningependa niwaase kina dada na wanaume wenzangu hawa watoto tunaowaita "wa nje" Mungu ana mipango nao na msiwadhihaki na kuwatesa. Mimi kwa sasa nafanya kazi nzuri, nampenda sana mama yangu (nashindwa kumwita mama wa kambo), na kwa sasa nimechukua jukumu la kuwalea na kuwasomesha wadogo zangu sababu uwezo wa baba kifedha sio kama wakati ule nilipokua nasoma.



PakaJimmy, nimekua na kaka ambae sithubutu kumuita wa kambo. Na yeye pamoja na sisi hatukujua kama ana mama yake na siku tunaambiwa (nikiwa std 5 hivi) i was like what do you mean ni mamake kaka?!?!?!.

Mama wa kambo, kama alivyo baba wa kambo anaweza kukupa treatment nzuri tu! Mama wa kambo anahitaji ushirikiano kutoka kwa familia nzima ili awe mama.

Roho mbaya ni tabia ya mtu.Lakini mama wa kambo anaweza kukataa kwa njia nyingi kutokuwa mama wa kambo. Mfano mdogo tu ni pale unapomsapraizi mkeo na mtoto wa nje tena mdogo kuliko wanae na ukamlazimishia awe mama wa kambo. Hapo inakuwa ngumu kumesa. Na ndoa ikiwa haina amani tumeshuhudia humu watu wakisema; they took it out on the kids. Huenda mtoto wa kambo anaweza kuwa an easy victim?
 
Mama angu wa kambo angekuwa hai ningehakikisha anaishi kama queen. Nilikuwa mtoro shule ile mbaya. Nikitoroka shule alikuwa ananipa kichapo cha kufa mtu, ananifunga kamba ananipeleka shule. Nikitazama nyuma naona bila yeye hata primary singemaliza, but now am a Doctor of Philosophy.
 
Back
Top Bottom