Nimshaurije huyu baba?

Nov 19, 2011
69
11
Vipi wadau wa hapa ndani, leo nimekuja kwenu kuomba msaada juu ya hili. Nina baba yangu ambaye mambo yake yamemwendea kombo sana mwaka huu, haswa kwa swala la kifedha. Na ameniambia anataka kuuza nyumba pamoja na kiwanja alicho nacho ambamo ndiko anakoishi na familia yake ili warudi kijiji walipotoka na kufanya biashara na fedha atakayopata. Je hii itasaidia ama ndio muendelezo wa matatizo endapo biashara itazorota?
 
labda auze kiwanja kwanza akanunue shamba na kulima aone mwelekeo wa hiyo biashara huku akiishi hapo kwenye hiyo nyumba, mara nyingi watu waliokaa mjini wakienda shamba sio lazima wafanikiwe, Kilimo sio kwa kila mtu, pili kilimo gani na wapi anakoenda inategemea, bora aanze kidogokidogo mambo yakiwa mazuri aweza uza au hata pangisha akapata pa kufikia akija uza mazao yake uku mjini.
 
Hapana! Mimi ningeshauri aangalie alternative nyingine, biashara ya kulima sio rahisi kiasi hicho, japo wimbo wa sasa kwa serikali ni Kilimo kwanza! watu wamekuwa wakilima miaka mingi na hawajafanikiwa hata chembe. Kwa sasa watu wanafanya kilimo kama mazowea tu ili kuwatosheleza kwa mahitaji ya chakula tu, wanaofanya kilimo kama biashara wamewekeza mtaji wa kutosha kwa hiyo suala la kuuza malia alizonazo sasahivi na kuenda kuanza kilimo mimi sikushauri kwa sasa.
 
Vipi wadau wa hapa ndani, leo nimekuja kwenu kuomba msaada juu ya hili. Nina baba yangu ambaye mambo yake yamemwendea kombo sana mwaka huu, haswa kwa swala la kifedha. Na ameniambia anataka kuuza nyumba pamoja na kiwanja alicho nacho ambamo ndiko anakoishi na familia yake ili warudi kijiji walipotoka na kufanya biashara na fedha atakayopata. Je hii itasaidia ama ndio muendelezo wa matatizo endapo biashara itazorota?

Unaomba ushauri ili ukatoe ushauri!

Huna uwezo wa kutoa ushauri, huna ushauri. Hata ukipewa ushauri hapa huwezi kuufikisha ipasavyo na pengine lengo lisitimie.

Cha msingi tafuta washauri wamshauri 'huyo baba'.
 
Mwambie nyumba asiuze bora kiwanja,na pia asifanye biashara yakuiga,afanye biashara aliona uzoefu nayo..kilimo ni sawa lakini sidhani kama anapesa zakutosha kuweze kulima akapata bidhaa nzuri zakuuza nje ya nchi sana atapata chakula chakula yeye mwenyewe...
 
Aisee si bora ungenyamaza, kwani amefanya kosa gani kuomba ushauri!!!

yeye si mtaalam wa kutoa ushauri, hivyo hata akipewa ushauri mzuri kuna mashaka kama ataweza kuufikisha ipasavyo. Atafute mshauri akaongee na baba na sio vinginevyo...
 
Kwenye hilo tatizo kuna options nyingi za kufuata.

1. Katika ulimwengu wa biashara kuna vitu viwili. Asset na liability. Asset ni mali yoyote inayokupatia pesa na liability ni inayochukua pesa kutoka kwako. Ili kufanikiwa katika biashara yoyote ni lazima katika uwiano wa asset na liability, uwe na asset nyingi zaidi ya liabilities. Kama nyumba na kiwanja unavilipia kodi kutoka mfukoni mwako hiyo ni liability ila kama ungekuwa umeikodisha kwa watu na wanakulipa kodi then inakuwa asset. So cha kufanya kama mna sehemu nyingine mnaweza kuishi kwa muda, ikodisheni nyumba yenu kwa watu ili mpate pesa itakayoweza kuanzishia biashara nyingine na baada ya biashara kukua mnarudi kukaa kwenye nyumba yenu. Kama hamna sehemu ya kukaa kwa muda then inakuja option ya piuli,

2. Itumieni hiyo nyumba kama collateral kuchukulia mkopo benki then mnafanyia biashara hiyo hela. Ishu ni kwamba hiyo biashara ikibuma then nyumba yenu inachukuliwa. Inabidi huo mkopo mkiupata muutumie vizuri kujenga biashara itakayo lipa.

3. Mwambiemzee wako ajenge utamaduni wa ku save kila kiasi cha pesa anachopata hata wakati wa kipindi kigumu kipesa unakuwa na uwezo wa kusurvive. Next time make sure that una asset ambayo inakuingizia hela muda wote nfano biashara yoyte, kumiliki hisa mahali n.k. Kuna watu duniani hawana physical biashara ila wanaishi kwa kununua na kuuza hisa kwenye soko la hisa. Huo ni mfano nakupa

4. Halafu kwa huyo jamaa anayekushambulia kwamba eti unakuja kuchukua ushauri na kwenda kumshauri baba yako, yeye amekupa ushauri gani? Watu wengine huwa ni wasen'' sana.
 
Unaomba ushauri ili ukatoe ushauri!

Huna uwezo wa kutoa ushauri, huna ushauri. Hata ukipewa ushauri hapa huwezi kuufikisha ipasavyo na pengine lengo lisitimie.

Cha msingi tafuta washauri wamshauri 'huyo baba'.

iv kwani we ni malaika unajua kila kitu?acha kumshambulia mwenzio.jamaa kaona hapa ni kisima cha maarifa ndo mana kaamua aombe ushauri amsaidie baba yake alie ktk kpnd kigumu.uwe na busara!!
 
Vipi wadau wa hapa ndani, leo nimekuja kwenu kuomba msaada juu ya hili. Nina baba yangu ambaye mambo yake yamemwendea kombo sana mwaka huu, haswa kwa swala la kifedha. Na ameniambia anataka kuuza nyumba pamoja na kiwanja alicho nacho ambamo ndiko anakoishi na familia yake ili warudi kijiji walipotoka na kufanya biashara na fedha atakayopata. Je hii itasaidia ama ndio muendelezo wa matatizo endapo biashara itazorota?

Samahani,
Mkuu unaweza kuweka hadharani mazingira ya kijiji chenu. Maana kuna vijiji vingine kwa mtu aliye toka mjini ni kaburi wazi na vingine ni neema tele.
 
Samahani,
Mkuu unaweza kuweka hadharani mazingira ya kijiji chenu. Maana kuna vijiji vingine kwa mtu aliye toka mjini ni kaburi wazi na vingine ni neema tele.

ni moja ya vijiji vilivyopo Kilimanjaro, ila maendeleo yake sii mazuri sana mkuu!
 
ni moja ya vijiji vilivyopo Kilimanjaro, ila maendeleo yake sii mazuri sana mkuu!

Kiasi Kilimanjaro naifahamu, si vizuri akarudi huko, anaweza akaishia kupata presha bure. Ingekuwa vijiji vya Iringa/mby au Ruvuma ningeweza kusema akajaribu. Kwa hapo KLM tafuteni option ya pili.
 
Ushauri wangu....... Auze kiwanja akajenge kijijini. Nyumba ya kijijini ikiwa tayari wahame mji na kupangisha nyumba. income ya pango ya nyumba ya mjini itamwezesha kuishi kijijini na kujaribu biashara tofauti tofauti bila kuwa na pressure ya mikopo ya bank.
 
Elewa siku zote maisha yanapokuwa magumu sana cha msingi usikate tamaa mwana, mambo yatakuwa safi tu. Haimaanishi kwamba kwa sababu sasa hivi mna hali ngumu basi itakuwa hivyo milele. Siku zote dawa ya kulitatua tatizo lolote ni hii: Unapopatwa na tatizo lolote badala ya kufikiri zile negative outcomes zitakazofuata, unafikiria hivi, ntafanya nini kulitatua hili tatizo nililonalo? Hata kama huna jibu kwa wakati huo, majibu yanaanza kuja kutoka kila direction. Hiyo ndo sayansi ya laifu.
 
Pia kujua background ya biashara au shughuli alizokuwa anafanya inasaidia kutoa ushauri bora kwa mlengwa, maana inasaidia kujua strong point yake na weakeness zake.

Kurudi kijijini tu ghafla na kuanza kilimo sio rahisi sana kufanikiwa, pia inatokana na majukumu yake kwa familia maana kama anawatu wengi wanamtegemea inakuwa tabu kidogo kufikia malengo.

Kuuza kitu kutokana una matatizo ya fedha sio vizuri mara nyingi watu hupata hasara.
 
Ni biashara ya uuzaji wa nyama.
Pia kujua background ya biashara au shughuli alizokuwa anafanya inasaidia kutoa ushauri bora kwa mlengwa, maana inasaidia kujua strong point yake na weakeness zake.

Kurudi kijijini tu ghafla na kuanza kilimo sio rahisi sana kufanikiwa, pia inatokana na majukumu yake kwa familia maana kama anawatu wengi wanamtegemea inakuwa tabu kidogo kufikia malengo.

Kuuza kitu kutokana una matatizo ya fedha sio vizuri mara nyingi watu hupata hasara.
 
Ni biashara ya uuzaji wa nyama.
Kwnza zingatia kwamba turnover ya kilimo ni ndogo sana na ya kusua kusua cost zake ni kubwa na output is totally unpredictable....utangoja weee mpaka mazao yaote ndo utazidi ku sanda.....cha msingi think of a simple business yenye turnover kubwa meaning that there should be a good circulation of stock. kwa ushauri wangu kama ana kama million 2....anaweza kufungua vibanda vya chips kama 10 hivi...hiyo biashara inalipa sanaaa kama ukiwa serious
 
Back
Top Bottom