Pole sana Tete.
Kufiwa ni kitu kigumu sana. Ila Mungu atakupa nguvu.
Safari njema na natumaini mazishi na mipango mingine itaenda vizuri mumpumzishe mama yenu salama
Pole kwa msiba mzito wa kufiwa na mama mzazi.Mtihani ulioko mbele yako ni ule wa kumkosa na kukumbuka malezi yake na mapenzi yake.
Mimi nakuombea dua Mungu akujaze subira na kukupa moyo wa uvumilivu.Mwenyezi Mungu sisi wote ni waja wake na kwake tutarejea.alale mahali pema peponi mama huyu mpendwa.Amin.
Wana jfs nimefiwa na mama yangu mzazi leo kcmc bado nipo dar nataraji kuondoka kesho kuelekea moshi naomben sala zenu ktk kipindi hiki kigumu
My number 0719354556
pole sana ndugu yetu TaT!
Ni tukio la kustua na kuhuzunisha sana kufiwa na mzazi. Mungu akupe nguvu kuhimili majonzi, simanzi na ombwe utakalolisikia.
RIP mama....
Kwakweli msiba ni usikie tu umetokea lakini ukikufika ni Balaa.Pole sana tete kwa kuondekewa na NGUZO kuu ya Kidunia..yote hayo ni mapenzi yake mungu.Roho ya Marehemu mama Ipumzike kwa Amani...Amen..Pole sana naomba maulana akutie nguvu katika mapito haya magumu ya kidunia
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.