Mali ikipotea mwenye mali anaumia sio kwamba mwenye mali akipotea mali inaumia.mimi huwa nashangaa sana! hapa jf akija mdada anaomba ushauri mumewe anamsaliti, watu mnamshauri chondechonde amsamehe kisa watoto, nk! lakini mbona uyu mnakomaa naye kuwa amuache? kwanini naye asisamehewe? mkuki kwa nguruwe.....wanaume huwa wanaumia sana wake zao wakiwacheat ila wao aaaah, wacheat tu wanaona kama sisi tuna mioyo ya chuma na sio nyama humu katika miili yetu!! inaniuma sana!
Pole sanaWana JF nimeoa na nina mtoto mmoja ana miaka minne, nimemfunia mke wangu anafanya mambo na kijana fulani wa mtaani hapa hapa.
Nimemrudisha kwao ila naona kama adhabu haitoshi kuna muda natamani kama nimkatekate vipande vidogo vidogo vya nyama au hata niende kwa mganga amfanye chizi.
Bado wazazi wamekutana wanasema nimsamehe.
Naomba busara zenu wanaJF ila pia nawapeni somo msiwaamini wanawake anaweza kukugeuka siku yoyote, mimi mke wangu nimetoka nae shule ya msingi mpaka mwaka huu ni zaidi ya miaka 13